queen matara
Member
- Apr 29, 2011
- 40
- 61
Natumia jukwaa hili la kufikiri na kutafakari ili niweze kutoa mchango wangu wa mawazo niliyoyapata katika kufikiri kwangu kuhusu hili jambo lililo sababisha uvunjifu wa amani huko Mbagala.
Tunaelezwa kuwa chanzo ni watoto wawili,{mmoja mkristu na wa pili muislamu}, waliokuwa wakibishana kuhusu kuutia najis Msahafu na matokeo ya laana fulani itakayompata mara moja mtendaji wa tukio hilo.
Kinachosikitisha hapa ni mtazamo wa upande mmoja tu. Mtoto Mkristu kautia najis msahafu. Pamoja na utukutu wake wa kupinga kuwa hawezi kugeuka kuwa mjusi ama panya, hicho hakikuwa kitendo cha busara kwake. Mtoto Emmanuel alipaswa kujua kuwa kile ni kitabu Kitukufu cha imani ya dini ya yule mwenzie.
Upande wa pili ambao ungepaswa kutazamwa ni wa yule mtoto muislamu. Hii ni dini yake na Msahafu ni kitabu Kitukufu cha dini yake.Kitendo cha yeye kuwa tayari kushuhudia kitabu hiki kikitiwa najis, tena na mtoto mwenzie ambaye ni wa dini tofauti na yake, ni kufru kubwa sana kwake na kwa Waislamu wenzake. Huyu mtoto kwa ridhaa yake amechukuwa Msahafu akauweka chini ukojolewe na mtoto mwenzie, hata kama mtoto huyo angekuwa ni muislamu mwenzie, kitendo hiki ni cha utovu mkubwa sana wa maadili ya kidini, tabia na malezi pia. Sijui kwa nini watu wazima na busara zao hawataki kuliona hili. Emmanuel anastahili kukaripiwa kwa kukizalilisha kitabu Kitukufu cha dini ya mwenzie, lakini huyu mtoto mwenye dini yake anatakiwa kupata karipio kubwa zaidi kwa kuizalilisha dini yake, kuwazalilisha wazazi wake, waalimu wake wa Madrasa, na Waislamu wenzake.
Tunaelezwa kuwa chanzo ni watoto wawili,{mmoja mkristu na wa pili muislamu}, waliokuwa wakibishana kuhusu kuutia najis Msahafu na matokeo ya laana fulani itakayompata mara moja mtendaji wa tukio hilo.
Kinachosikitisha hapa ni mtazamo wa upande mmoja tu. Mtoto Mkristu kautia najis msahafu. Pamoja na utukutu wake wa kupinga kuwa hawezi kugeuka kuwa mjusi ama panya, hicho hakikuwa kitendo cha busara kwake. Mtoto Emmanuel alipaswa kujua kuwa kile ni kitabu Kitukufu cha imani ya dini ya yule mwenzie.
Upande wa pili ambao ungepaswa kutazamwa ni wa yule mtoto muislamu. Hii ni dini yake na Msahafu ni kitabu Kitukufu cha dini yake.Kitendo cha yeye kuwa tayari kushuhudia kitabu hiki kikitiwa najis, tena na mtoto mwenzie ambaye ni wa dini tofauti na yake, ni kufru kubwa sana kwake na kwa Waislamu wenzake. Huyu mtoto kwa ridhaa yake amechukuwa Msahafu akauweka chini ukojolewe na mtoto mwenzie, hata kama mtoto huyo angekuwa ni muislamu mwenzie, kitendo hiki ni cha utovu mkubwa sana wa maadili ya kidini, tabia na malezi pia. Sijui kwa nini watu wazima na busara zao hawataki kuliona hili. Emmanuel anastahili kukaripiwa kwa kukizalilisha kitabu Kitukufu cha dini ya mwenzie, lakini huyu mtoto mwenye dini yake anatakiwa kupata karipio kubwa zaidi kwa kuizalilisha dini yake, kuwazalilisha wazazi wake, waalimu wake wa Madrasa, na Waislamu wenzake.