Vurugu Tegeta, msafara wa JK waathirika pia (Dar)

Mambo mengine mleta Mada kachanganya habari. Mosi kulikuwa na Uvunjaji wa nyumba hapo Namanga- Tegeta kwa hiyo kulikuwa na Mabaunsa waliokuwa wakifanya fujo ndipo Polisi wakaingilia kati. Kupita kwa Rais hakuna uhusiano na tukio hilo
Pale Namanga kuna sheli ya BigBon iko barabarani kwa nyuma yake amepakana na nyumba za wanakijiji, sasa yeye anadai kanunua hilo eneo lote na anamiliki hati wanakijiji wamesema hawamtambui wala hawajawahi kuuza kwa mtu eneo hilo, kesi ilikwenda baraza la ardhi kwa mbinu na hila akafanikiwa kushinda kwani baraza hilo halina haki kisheria ya kusikiliza kesi hiyo.

Wananchi wameamua kuipeleka kesi mahakama kuu na wameshatoa notisi ya siku 90 kwa mwanasheria mkuu wa serikali ili kuishitaki wizara ya ardhi, kuna kesi nyingine ya madai ameshtakiwa mahakama kuu kitengo cha ardhi na mzee mmoja amepakana nae kwenye hilo eneo kwa kumuingilia na kuharibu mali zake zote kwa kudai (BigBon) kuwa eneo hilo ni lake. kesi imepangwa kusikilizwa July.

Leo hii BigBon akijua fika kua kuna kesi mahakamani na hazijasikilizwa bado amepeleka kikundi cha mabaunsa kwenda kuvamia kwa nguvu eneo hilo la wanakijiji kwa lengo la kuwatoa, ndipo vita kali baina ya mabaunsa hao na wanakijiji ilipozuka kwa taarifa nilizozipata, zaidi ya mabaunsa wanne wameuliwa na wanakijiji ila kwasasa hali imetulia.

Wakati vurugu hizo zikiendelea na msafara wa rais ulikuwa ukipita maeneo hayo hakuna uhusiano wowote kati ya vurugu hizo na msafara huo, ila ilikua ni jambo la heri kwani msafara huo ulisaidia kuzima vurugu hizo baada ya askari wa FFU kufika katika eneo hilo na kuanza kutawanya watu...


Source: taarifa kutoka kwa mzee mmoja mwanakijiji ambae nae ni mmojawapo kati ya wanakijiji wanaogombania eneo na BigBon

 
Source: RADIO ONE
WANANCH WALIKUWA WANAGOMBANA WAKILALAMIKA NYUMBA ZAO KUVUNJWA NA ENEO KUUZIWA MMILIK MMOJA WA MAFUTA

VURUGU ZILIANZA KABLA HATA YA MSAFARA WA RAIS KUFIKA ENEO LILE

KWAHYO SI KWAMBA WANANCH WALIJIPANGA KUZUIA MSAFARA BALI WALIKUA NAVURUGU ZA HAPANAPALE KUZUIA NYUMBA ZAO ZISIVUNJWE.
 
Nikweli kabisa,Ni eneo la Tageta-Namanga ni mbele kidogo baada ya kutoka njiapanda ya kwenda wazo kama unaenda bunju,kuna maeneo kuna petrol station,ndipo JK kaonja chungu ya watanzania.

Thanx for Clarification Mkuu. Sasa inabidi kile aendako iwe hivyo hivyo mshenzi mkubwa huyu!!
 
mbona laisi tu!,umesahau mbeya?Watu hufanya taiming ikisha pita kile king'ola watu wanaingia barabarani na ndicho walichofanya leo.
Mbeya waliupopoa na si kuuzuia. Halafu baada ya king'ora huwa yanafuata magari kadhaa ya polisi pamoja na yale ya wanausalama kabla ya gari la rais. Zaidi ya yote ili hilo liwezekane ni lazima watu wajue kwamba Rais atapita hapo mahali na wajipange kwa ajili ya kuuteka huo msafara. But is not easy man.
 
Kilahunja, hapa alichouliza ni kuwa msafara utazuiwa vipi? nilichojibu ni namna ambavyo unaweza kuzuiwa... ni lazima kuwa hao waliotaka kuzuia walikuwa wame ji organize, yaani kwa akili yako Kilahunja inaweza tokea tu from nowhere watu wakazuia msafara bila kuamua kwa pamoja kufanya hivyo? acha udwanzi bana!!
Wee lijamaa kumbe hamnazo kabisa! Mbona unauliza swali lilelile nililouliza mimi? Mimi nimeuliza ni nani aliwaambia kama rais atapita hapo? Na wewe unauliza wangeanzaje bila kujiorganize? Hofu yangu ilikuwa ni namna gani wamejiorganize kiasi cha kuweza kujipanga kufanya hayo, na wangewezaje kufanya hayo bila vyombo vya usalama kujua? Sometimes tupunguze ukurupukaji.
 
Hivi msafara wa rais mnauzuiaje? Hapa bado nahitaji technical explanations za namna ambavyo hili limefanyika.

udaku street hiyo kuzuia msafara wa Rais ni jambo linalowezekana pengine walikuwa na shida ya kumweleza Rais lakini JF tunachukulia kuwa wamezuia kumpopoa mawe...... stupid thinking
 
Mmmh, sijui maana kwa ule msafara wa Rais unavyokuwaga, sioni kabisa hiyo nafasi ya wananchi kuweza kusimama tu barabarani na kuzuia, otherwise waliambiwa kwamba Rais angepita maeneo hayo. Na sijui wakati wa kuzuia barabara walianzaje, ina maana walizuia na magari ya kawaida? Anyway sijui, but nafikiri ni jambo gumu sana, bora mngesema wameupopoa kwa mawe, lakini si kuzuia.

Haingii akilini labda kama kuna agenda ya siasa ndani ya thread hii
 
Back
Top Bottom