VURUGU ARUSHA-Waandishi wa Habari Arusha watoa siku 7 kwa Polisi kuomba radhi

Mathias Byabato

JF-Expert Member
Nov 24, 2010
1,020
691
Tumetumiwa kwenye email zetu



Ndugu Waandishi wa Habari

CHAMA cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Arusha (APC), kinalaani,kwa
nguvu zake zote, matukio ya askari polisi mkoani Arusha kuendeleza
tabia ya kuwazuia na kuwapiga, waandishi wa habari wakati
wakitekeleza majukumu yao halali.

Mfano wa hivi karibuni ni tukio la Januari 5 mwaka huu, ambapo
waanidishi wa habari habari mkoani Arusha wakiwa katika majukumu yao
halali ya kufuatilia maandamano na mkutano wa Chama cha Demokrasia na
Maendeleo(CHADEMA), walikumbana na kipigo kutoka kwa Polisi waliokuwa
wakijaribu kuzuia vurugu zilizotokea.

Pamoja na waandishi kujaribu kujitambulisha kwa kuonyesha vitambulisho
halali,hakuna askari aliyejaribu kuwasikiliza na matokeo yake
walikumbana na kipigo na wengine kuwekwa ndani kama vile ni wahalifu

Hatua ya waandishi kufuatilia tukio hilo ilikuwa katika kutimiza
majukumu yao ya msingi kabisa ya kuwahabatisha wananchi wnegine
nchini ambao kwa namna moja au nyinbgine wasingeweza kufika au kuwa
Arusha kwa wakati huo.

Huo ni wajibu wa kwanza unaotambulika kikatiba na kila chombo
kinapaswa kuuheshimu kama kweli nchi yetu inataka kujenga demokrasia
ya kweli katika mfumo wa siasa uliopo nchini.


Hata hivyo katika hali ambayo APC haikubaliani nayo askari polisi
waliokuwa katika kulinda amani ikiwa ni pamoja na kuzuia maandamano
hayo yasifanyike walianza kuwatisha waandishi wa habari wakiwa nje ya
Hoteli ya Mount Meru. Hali ambayo ilionyesha kana kwamba waandishi wa
habari nao walikuwa sehemu ya wanachama wa CHADEMA kitendo ambacho si
kweli.

Pamoja na maandamano hayo kufanyika kwa takribani kilomita mbili hivi
waandishi wa habari waliendelea kupiga picha na kukusanya taarifa zao
ikiwa ni pamoja na kufuatilia kwa karibu nyendo zote za maandamano
hayo. Lakini katika mazingira ya yaliyoleta utata pamoja na kwamba
askari polisi walikuwa wakiowana waandishi wa habari mbele ya
maandamano wakiwa na zana zao za kazi.

Pamoja na hali hiyo bado askari polisi walidiriki kuanza kuwapiga
waandishi wa habari huku wakiwatishia kuwanyang’anya kamera na vitabu
vyao. Hata hivyo hali bado iliendelea kujitokeza kwa waandishi wa
habari waliokuwa wakisubiria mkutano wa viongozi wa CHADEMA ktaika
hoteli moja, ambapo bado askari polisi waliwakamata kwa tuhuma za
kupiga picha wakati Dk. Slaa akiwa anakamatwa.

Waandishi hao walikamatwa na kufikishwa kituoni na kamera zao
kuchukuliwa kisha kufutwa picha zote zilizokuwa zimepigwa,

MSIMAMO WA APC

Kutoka na mazingira hayo Chama cha Waandishi wa habari mkoani wa
Arusha kinatambua na kuheshimu kwamba jeshi la polisi ni moja ya
vyanzo vikubwa vya upatikanaji kwa taarifa kwa waandishi wa habari.

Pamoja na kutambua hilo APC inaelewa mahusiano mazuri yaliyopo,kwa
muda mrefu kati ya Jeshi la Polisi na Waandishi wa habari mkoani
Arusha na ushirikiano uliodumu kwa muda mrefu sasa.

Hata hivyo, kutokana na mazingira hayo ya Januari 5, 2011 ya kuonyesha
kukamiana yaliyofanywa na baadhi ya askari polisi, APC inatoa muda wa
wiki moja kwa jeshi hilo mkoani Arusha kuchukua hatua za haraka za
kurekebisha kasoro zote hizo.

Hatua ambazo Jeshi hilo linapaswa kuchukua ni pamoja na kuwaomba radhi
waandishi wa habari kwa usumbufu na maumivu ya kupigwa waliyoyapata
wakati wakiwa wanafanya kazi zao halali.

Pili APC, inatoa tamko kuwa endapo msamaha huo hautatolewa katika
kipindi hicho basi tutalazimika kuangalia upya mahusiano na
ushirikiano wetu na Jeshi la Polisi na ikiwezekana kusitisha kabisa
ushirikiano wa aina yoyote mpaka kila upande utakapozingatia umuhimu
wa mwenzake.

Tatu,tungependa kuona askari waliohusika kwa makusudi katika
kuwadhalilisha waandishi wa habari,ambao wanafahamika hata kwa majina,
wanachukuliwa hatua zinazostahili ikiwa ni pamoja na kulipa fidia
waandishi waliodhurika na kuharibiwa vifaa vyao vya kazi.

Ni utamaduni wa APC wa kuepuka kulumbana au kutofautiana kwa namna
yoyote na wadau wetu Jeshi la Polisi likiwamo, lakini kamwe hatutakaa
kimya tukiona tunadharauliwa na kunyanyaswa mbela ya jamii wakati
tunatekeleza majukumu yetu

tuko tayari kushirikiana na mdau yeyote anayejali kazi zetu
tunazofanya kwa weledi na kamwe hatutamwogopa mtu, taasisi au mdau
yoyote mwenye nia ya kutunyamazisha kwa sababu zake binafsi.

Inawezekana iwapo kila mmoja atatimiza wajibu wake.


Imetolewa na

ARUSHA PRESS CLUB

6th January,2011
 
Tumetumiwa kwenye email zetu



Ndugu Waandishi wa Habari

CHAMA cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Arusha (APC), kinalaani,kwa
nguvu zake zote, matukio ya askari polisi mkoani Arusha kuendeleza
tabia ya kuwazuia na kuwapiga, waandishi wa habari wakati
wakitekeleza majukumu yao halali.

Mfano wa hivi karibuni ni tukio la Januari 5 mwaka huu, ambapo
waanidishi wa habari habari mkoani Arusha wakiwa katika majukumu yao
halali ya kufuatilia maandamano na mkutano wa Chama cha Demokrasia na
Maendeleo(CHADEMA), walikumbana na kipigo kutoka kwa Polisi waliokuwa
wakijaribu kuzuia vurugu zilizotokea.

Pamoja na waandishi kujaribu kujitambulisha kwa kuonyesha vitambulisho
halali,hakuna askari aliyejaribu kuwasikiliza na matokeo yake
walikumbana na kipigo na wengine kuwekwa ndani kama vile ni wahalifu

Hatua ya waandishi kufuatilia tukio hilo ilikuwa katika kutimiza
majukumu yao ya msingi kabisa ya kuwahabatisha wananchi wnegine
nchini ambao kwa namna moja au nyinbgine wasingeweza kufika au kuwa
Arusha kwa wakati huo.

Huo ni wajibu wa kwanza unaotambulika kikatiba na kila chombo
kinapaswa kuuheshimu kama kweli nchi yetu inataka kujenga demokrasia
ya kweli katika mfumo wa siasa uliopo nchini.


Hata hivyo katika hali ambayo APC haikubaliani nayo askari polisi
waliokuwa katika kulinda amani ikiwa ni pamoja na kuzuia maandamano
hayo yasifanyike walianza kuwatisha waandishi wa habari wakiwa nje ya
Hoteli ya Mount Meru. Hali ambayo ilionyesha kana kwamba waandishi wa
habari nao walikuwa sehemu ya wanachama wa CHADEMA kitendo ambacho si
kweli.

Pamoja na maandamano hayo kufanyika kwa takribani kilomita mbili hivi
waandishi wa habari waliendelea kupiga picha na kukusanya taarifa zao
ikiwa ni pamoja na kufuatilia kwa karibu nyendo zote za maandamano
hayo. Lakini katika mazingira ya yaliyoleta utata pamoja na kwamba
askari polisi walikuwa wakiowana waandishi wa habari mbele ya
maandamano wakiwa na zana zao za kazi.

Pamoja na hali hiyo bado askari polisi walidiriki kuanza kuwapiga
waandishi wa habari huku wakiwatishia kuwanyang'anya kamera na vitabu
vyao. Hata hivyo hali bado iliendelea kujitokeza kwa waandishi wa
habari waliokuwa wakisubiria mkutano wa viongozi wa CHADEMA ktaika
hoteli moja, ambapo bado askari polisi waliwakamata kwa tuhuma za
kupiga picha wakati Dk. Slaa akiwa anakamatwa.

Waandishi hao walikamatwa na kufikishwa kituoni na kamera zao
kuchukuliwa kisha kufutwa picha zote zilizokuwa zimepigwa,

MSIMAMO WA APC

Kutoka na mazingira hayo Chama cha Waandishi wa habari mkoani wa
Arusha kinatambua na kuheshimu kwamba jeshi la polisi ni moja ya
vyanzo vikubwa vya upatikanaji kwa taarifa kwa waandishi wa habari.

Pamoja na kutambua hilo APC inaelewa mahusiano mazuri yaliyopo,kwa
muda mrefu kati ya Jeshi la Polisi na Waandishi wa habari mkoani
Arusha na ushirikiano uliodumu kwa muda mrefu sasa.

Hata hivyo, kutokana na mazingira hayo ya Januari 5, 2011 ya kuonyesha
kukamiana yaliyofanywa na baadhi ya askari polisi, APC inatoa muda wa
wiki moja kwa jeshi hilo mkoani Arusha kuchukua hatua za haraka za
kurekebisha kasoro zote hizo.

Hatua ambazo Jeshi hilo linapaswa kuchukua ni pamoja na kuwaomba radhi
waandishi wa habari kwa usumbufu na maumivu ya kupigwa waliyoyapata
wakati wakiwa wanafanya kazi zao halali.

Pili APC, inatoa tamko kuwa endapo msamaha huo hautatolewa katika
kipindi hicho basi tutalazimika kuangalia upya mahusiano na
ushirikiano wetu na Jeshi la Polisi na ikiwezekana kusitisha kabisa
ushirikiano wa aina yoyote mpaka kila upande utakapozingatia umuhimu
wa mwenzake.

Tatu,tungependa kuona askari waliohusika kwa makusudi katika
kuwadhalilisha waandishi wa habari,ambao wanafahamika hata kwa majina,
wanachukuliwa hatua zinazostahili ikiwa ni pamoja na kulipa fidia
waandishi waliodhurika na kuharibiwa vifaa vyao vya kazi.

Ni utamaduni wa APC wa kuepuka kulumbana au kutofautiana kwa namna
yoyote na wadau wetu Jeshi la Polisi likiwamo, lakini kamwe hatutakaa
kimya tukiona tunadharauliwa na kunyanyaswa mbela ya jamii wakati
tunatekeleza majukumu yetu

tuko tayari kushirikiana na mdau yeyote anayejali kazi zetu
tunazofanya kwa weledi na kamwe hatutamwogopa mtu, taasisi au mdau
yoyote mwenye nia ya kutunyamazisha kwa sababu zake binafsi.

Inawezekana iwapo kila mmoja atatimiza wajibu wake.


Imetolewa na

ARUSHA PRESS CLUB

6th January,2011

Wamwulize yule WAZIRI aliyegombana na waandishi wa habari siku za nyuma! Waandishi wa habari wakiamua kuandika tu negatives za askari, watajijimbia. Utakuta picha zao wakikojoa, wakijisaidia, wakifanya ngono, nk. Zingine nzuri hazitaandikwa....

Mbona POLISI mmefikia/kufikishwa hapo?

Hii nayo iongezwe kwa OKAMPO
 
Poleni waandishi.
Yaliyowapata kwa vyovyote yalifanywa na askari wachache.
Mnastahili kuombwa radhi.
Polisi wetu ni wasikivu, watawasikiliza na kumaliza tofauti zilizojitokeza.
Tuko pamoja nanyi.
 
Back
Top Bottom