Katika kuendelea kueneza elimu ya Uraia, kuimarisha Chama na kueneza dhana ya Vuguvugu la Mabadiliko(M4C), na kuzindua Ofisi ya Chama Kata, viongozi waandamizi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) wikiendi hii watafanya mkutano mkubwa wa hadhara katika Mji Mdogo wa Mto wa Mbu ulipo jimboni Monduli.
Mkutano huo utakaoongozwa na Wabunge (Wah. Mch. Natse, Nassari na Gekul) na Viongozi wengine, unategemewa kuufanya mji huo na kata zake jirani za Esilalei, Makuyuni na Majengo kuwa ngome ya CHADEMA jimboni humo.
Wananchi wengi wamejaa hamasa ya kutaka kusikia ujumbe huu wa mabadiliko na nyumba nyingi za maeneo ya Korea, Kisutu, NHC(Shirika), Sabato, Jangwani, Magadini na Kigongoni zimeonekana kupambwa kwa bendera za CHADEMA.
Hata hivyo, kuna habari kwamba vijana kadhaa wanaoendesha Bodaboda ambao walijipanga kuupokea msafara wa viongozi wa Chama kutoka Kata ya Makuyuni(umbali wa Kilometa 35) wamezuiliwa kufanya hivyo.
Nitawapasheni kinachojiri LIVE kutoka mkutano huo na kuwawekeeni picha.
NGUVU YA UMMA
Mkutano huo utakaoongozwa na Wabunge (Wah. Mch. Natse, Nassari na Gekul) na Viongozi wengine, unategemewa kuufanya mji huo na kata zake jirani za Esilalei, Makuyuni na Majengo kuwa ngome ya CHADEMA jimboni humo.
Wananchi wengi wamejaa hamasa ya kutaka kusikia ujumbe huu wa mabadiliko na nyumba nyingi za maeneo ya Korea, Kisutu, NHC(Shirika), Sabato, Jangwani, Magadini na Kigongoni zimeonekana kupambwa kwa bendera za CHADEMA.
Hata hivyo, kuna habari kwamba vijana kadhaa wanaoendesha Bodaboda ambao walijipanga kuupokea msafara wa viongozi wa Chama kutoka Kata ya Makuyuni(umbali wa Kilometa 35) wamezuiliwa kufanya hivyo.
Nitawapasheni kinachojiri LIVE kutoka mkutano huo na kuwawekeeni picha.
NGUVU YA UMMA