EasyFit
JF-Expert Member
- Jul 4, 2011
- 1,269
- 1,082
Chadema kimetangaza kuandaa awamu mpya ya operesheni zake, ambayo safari hii kitapeleka nguvu zake katika mikoa ya Kanda ya Kusini, Lindi na Mtwara, ili kuuhamasisha umma kuleta mabadiliko na uwajibikaji serikalini. Hayo yalisemwa na Katibu wa Habari na Uenezi wa Chadema, John Mnyika.
Amesema operesheni hiyo imelenga kushughulikia mambo matatu;
Amesema operesheni hiyo imelenga kushughulikia mambo matatu;
- kusimamia uwajibikaji katika ngazi zote za serikali, ili kuhakikisha changamoto zote zinazolikabili taifa zinashughulikiwa.
- kutoa elimu ya kisiasa kwa umma kuhusu mchakato wa mabadiliko ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
- kujenga organaizesheni ya chama mijini na vijijini.