Vodacom tz kwafukuta..

Serikali yenyewe hipi haswa ya kuwatetea na kulinda ajira ya waTanzania? Serikali hii ya rais kuongwa vipande vya suti!!!!.waongwa

Mkuu naamini wabongo wakisimama kidete na kila kampuni kupaza sauti about huu muongezeko wa wageni non-professional lazima itachuka hatua, tatizo hao wafabyakazi wenyewe wauza sura tu kazi kulalamika tuu basi. Huu Ujinga hata Kenya hawawezi kukubali, only kwa waajiriwa wa Tanzania(waoga sana). Heri ya sisi tuliojiajiri kwa kilimo kuliko manyanyaso ya wahindi njaa wa bongo
 
NSN mbona sio Vodacom? Hii ni separate company

Ishu ipo hivi...
makampuni mengi ya simu yameoutsource dept zao za technical(maintanance na operation), si Tanzania tu bali hata sehemu nyingine duniani..Vodacom Tanzania ni mfano mmoja wapo na wana mkataba na NokiaSiemens.
Hivyo mwenye jukumu la kuajiri wafanyakazi wa Technical mostly ni upande unaohusu telecom network ni NSN...using that advantage ndio huwa wanalundika wataalam wengi kutoka nje.
 
Yasemekana hali si shwari ndani ya Vodacom Tz hususan baada ya mkataba kati yake na Nokia Siemens Networks (NSN) kitengo cha Operations.

Labda Dr. Slaa akiwa rais...lakini nikiangalia waliokopiwa kwenye hiyo barua wote ni wale waleee!!..hosea, manumba,..tumeshawazoea..hakuna kitakachofanyika
 
Vodacom wamekuwepo Tanzania kwa zaidi ya miaka 10 sasa, ina maana muda wote huo hawaja-train watanzania kushika hizo nafasi? Hivi kweli inaingia akili hata 'Human resource manager anatoka nje ya nchi? Hakuna mtanzania anaweza kufanya hiyo kazi?

Pia bado sijaelewa ni kwanini hadi leo hii Vodacom hawana jengo lao wenyewe, bado wanakodisha! Are they planning to leave the country? Commitment yao Tanzania iko wapi? Wana wateja zaidi ya 10 million (simu) na hatujagusa M-pesa. Lakini bado wanapanga office!
 
Ukweli ni kuwa wabongo tunajua kazi ila ni wavivu na wezi kupindukia ndicho kinachowasukuma kutumia gharama kubwa kuleta expatriates toka nje ya nchi
 
Ukweli ni kuwa wabongo tunajua kazi ila ni wavivu na wezi kupindukia ndicho kinachowasukuma kutumia gharama kubwa kuleta expatriates toka nje ya nchi

Deal na kutajirika haraka haraka...halafu wenye mali waliamua vingine tunawaona wanga. Kitu cha msingi ni kwa muajiri kufuata taratibu zote za kisheria...ila duka la mtu ni la kwake tu. Anaweza kuamua lolote analotaka.
 
Ishu ipo hivi...
makampuni mengi ya simu yameoutsource dept zao za technical(maintanance na operation), si Tanzania tu bali hata sehemu nyingine duniani..Vodacom Tanzania ni mfano mmoja wapo na wana mkataba na NokiaSiemens.
Hivyo mwenye jukumu la kuajiri wafanyakazi wa Technical mostly ni upande unaohusu telecom network ni NSN...using that advantage ndio huwa wanalundika wataalam wengi kutoka nje.

umetoa jibu la kueleweka. nyongeza,hatuna budi tukiri na tuone kama janga la taifa vijana wetu wengi kukosa uaminifu makazini na ni wavivu,na baadhi ni mabingwa wa vyeti vya kughushi.
 
Tatizo la kuzoea mfumo wa sisi wote ni sawa na Afrika ni moja ndio inakotupeleka huku. Matokeo yake ni kulalama mwanzo mwisho. Inawezekana ni bado hatujaweza kukabiliana na mfumo wa ushindani. Tena mmesahau sio wahindi tu, kuna wakenya, Wa-Nigeria, Wa ghana, Wa Afrika- Kusini, Wa-Senegali, Wanyarwanda, Wa Congo n.k Suala ni sifa na uwezo wa kukabiliana na ushiindani. Kamwe usitarajie kwamba utapata favor kutoka kwa mtu katika hili kama hujitumi.Matokeo ya kupendeleana na ushikaji ndio yanayotucost mpaka kesho. Bora hata ya wageni ambao wanapiga kazi wakijua siku yoyote wakiambiwa wasepe wanasepa kwingine na siri kwao ni kujituma na sio ubabaishaji wa kijinga wa kujiamini kwamba nikiharibu fulani yupo wa kunilinda. HABARI NDIO HIYO
 
Hili suala si la Vodacom tu. Ni nchi yote imeoza. Serikali haifanyi kiti chochote cha maana katika hili. Tulishakosa imani na serikali yetu. Watu mtalizungumzia lakini hakuna mabadiliko yoyote. Wizara ya Mambo ya Ndani, Wizara ya Kazi sioni wanachokifanya katika hili. Wenzetu wageni hawana nafasi hata kidogo. Wengine hata sifa hawana.

Hapa bila miujiza ya MUNGU hakuna kitakachoendelea.:eek2:
 
Acheni na nyinyi NSN kudanganya watanzania. Watu wanawafahamu fika mlivyo wezi na wavivu. Ni kweli mlikuwa Vodacom na Vodacom ikawauza muwe ndani ya NSN.

Lakini hebu kumbukeni mliyofanya mkiwa katika ulimwengu wa Vodacom. Mlikuwa na watu wafuatao.

Naanza kwa kumtaja Erasto Haule. Huyu na wenzake walikuwa wakifanya biashara ya kupangisha minara ya Vodaco. Kupangisha kwa maana ya kwamba unapokuwepo mnara yeye na wenzake wanaandikisha kiwanja jina la ndugu ili kodi ya kiwanja inayolipwa na Vodacom iende kwa ndugu na huko mnagawana. Idara ya huyu bwana wametajirika hakuna mfano kwa wizi wa aina hii. Haule mwenyewe nasikia ameshaondoka hapo na amefungua shule kubwa ya sekondari huko Njombe na kama si NJombe basi ni moja ya sehemu za huko kusini. Usishangae miaka ijayo Haule akaja kuwa mbunge kwa hela alizokwiba kwa staili hii. Si Haule tu wengi tu mlioko Vodacom mmefanya mchezo huu.

Vijana wengi tu ndani ya Vodacom mmeanzisha kampuni kubwa za ujenzi wa minara. Mmepata wapi fedha wakati mishahara na matumizi yenu vinajulikana?

Kilichotokea ni kwamba kwa siku nyingi wazungu wa Vodacom wamewagundu mchezo huu lakini hawakuwa na njia ya kufanya. Sasa hii njia ndiyo iliyoonekana inawafaa kuwaondokana na nyinyi.

Mimi nafanya kazi Wizara ya Ardhi mpangaji wangu wa mwaka 2002 nimemuona live akiingia Vodacom kama fundi lakini miaka nane baadaye ana nyumba zaidi ya tatu kama zangu, tena za gharama. Unadhani watu hawaoni haya.

Nasikia wenzenu wengine wamejenga hostel za wanafunzi huko Mwanza ambazo zinakaliwa na student wa SAUT. Mwingine alianzisha kampuni kubwa inaitwa JR Communication jina kamili sikufanikiwa kulipata. JR ni kampuni ile inayohusika na hizi mita za LUKU. Mmevipataje hivi?

Bado nazidi kupeleleza na nikipata data zaidi nitazimwaga humu. Watanzania tuwe waangalifu na watu wanaotaka wakati mwingine kutushirikisha tuwatetee kwenye mitandao wakati walipokuwa wanafaulu kufanya wizi wao kwenye makampuni ya wazungu hawakutaka tujue mianya ya wizi wao.

Msitudanganye enyi watanzania mlioko Vodacom au NSN. Nyinyi ni wezi wa kutupwa na hamfai hata kuongoza kijiji. Nyinyi ni mafisadi kuliko hata Lowasa! Acheni za kuleta. Kinachowatokea ndiyo dawa yenu. Tena kimechelewa kuja!!

Jamani serikali iwasaidie hata kwa hili? Naona mkuu umeyamaliza. Hawa ndiyo wanaopiga kelele. kama kuna mtu anayefikiria kuwa alichokisema MdogoWenu ni uongo tafuta watu aliyo wataja waulizeni.

Hata Vodacom wenyewe wanayajua haya fika kabisa.

Nafikiri hao walio andikiwa barua wafanye utafiti wa kina, siyo tu kwamba ni Voda wanashida makampuni mengi yanajikuta yanatamani kuwafukuza watanzania kwa sababu za udokozi kama huu.

Jamani tutafanya wadogo zetu wakose kazi kula kidogo.
 
na wewe mshamba kweli. Nenda internet cafe yoyote toa elfu moja tu kisha funguka kwa kadiri unavyoweza. Eleza kila kitu.

Najua ofisi zenu ziko pale Mlimani City. Sasa usirogwe kwenda kwenye ile internet cafe iliyomo mle maana ni rahisi kuwagonga staff wa hiyo cafe ili kuwatambua wafanyakazi wa Vodacom au NSN wanaoingia cafe hiyo na wakitoka humo history inaonyesha kwamba umesoma Jamii Forum.

Ukitaka kufanya hivyo nenda internet cafe iliyo mbali na hapo Mlimani City yaani nenda mjini kabisa kama kule Gongo la Mboto, Tabata nk.

Ukifika huko andika unvyoweza, wala hakuna atakayejua. Mimi huwa nafanya hivyohivyo. Sifungui JF au mtandao wowote nikiwa karibu na maeneo ya karibu na ofisini mwetu.

Kuwepo kwa ukweli katika haya uliyoandika, hakuondoi uhalali wa madai ya hawa wafanyakazi wa NSN.Serikali itumie Busara katika kutunza soko la AJIRA nchini,kwani kama mfumo unaotumia na NSN ukifanikiwa,wawekezaji wote watautumia,na muda si mrefu utaambiwa na wataalam wa ARDHI hapo WIZARANI hawahitajiki kwani muwekezaji ameleta WATAALAM wake wanaoweza kufanya kazi bila kuiba.

Kuiba ni tatizo linalotakiwa kutatuliwa kwa njia tofauti,sio ya kuwanyima wafanyakazi waliokuwepo haki zao za msingi,na kudumaza soko la ajira nchini
 
Wizi unaondoa uhalali wa kila kitu. Dawa ya mwizi ni kurudisha kile alichoiba bila kujali ana madai gani mengine halali.

Kupitia mpangaji wangu nilikuwa nasikia mengi ndani ya Vodacom. Kuna mwaka mfanyakazi wa Vodacom alitekwa na gari huko Shinyanga na kidogo auawe. Watekaji naambiwa wakamwacha wakaenda na gari.

Kuna namna minara yenu ilikuwa inamulika gari hilo lilivyokuwa linakata mbuga kati ya Shinyanga na Mwanza na hatimaye kwa kutumia usalama wa Taifa mkalipata gari na watekaji. Kiongozi wa watekaji alikuwa anaitwa somebody Kisusi. Huyu Kisusi namfahamau wakati nimeishi Shinyanga na alikuwa ni mwanajamii mzuri pale Shinyanga na mchangiaji namba moja wa CCM. Tena si CCM tu, bali alikuw amchangiaji mzuri wa Kanisani.

Kumbe hela ile alikuwa anipata kwa biashara ile. Mbona Vodacom mlikasirika na mlitaka apewe adhabu ya kutosha bila kujali mchango wake katika jamii.

Wezi wa EPA hadi leo tanang'ang'ania wakamatwe waswekwe ndani. Hatusemi eti kwamba wezi wale tuwatetee madai yao mengine na tunajua wengine kama KAGODA tunasikia ni ma-shareholders wenu huko. Mwizi akishatoka gerezani ndipo na yeye afuatilie madai yake wengine.

Hivyo, huwezi kusema eti sasa kampuni inawashughulikia Vodacom na NSN kwa wizi wenu wa muda mrefu mtutake tuwatee wakati tukijua mnatuletea hoja mitandaoni ili kututumia tu ili muendelee kujineemesha na utajiri wa wizi mnaoufanya hapo Vodacom.

Wala msitudanganye mnatetea ajira za watanzania bali mnatetea ajira zenu tu. Hebu nikumbusheni. Ni lini ajira za Vodacom zilitangazwa magazetini? Maana yake inawezekana ajira zipo lakini nyinyi mliomo kwa ujanja hamtaki zitangazwe na mnachukuana ndugu zenu watakaowasaidia kufanikisha huo wizi wenu wa kuandikisha majina ya ndugu zenu kama wamiliki wa minara na kuiba mafuta ya magari ya kampuni hadi nasikia kwamba mnanyang'anywa magari yaliyokuwa yamejaa kama utitiri, bila kusahau wizi mwingi tele mnaoufanya hapo Vodacom.

Wanafiki wakubwa nyinyi? Ni lini Vodacom mmeshiriki katika mitando ya jamii katika masuala ya nchi? Kampuni yenu inapandisha gharama za simu kila leo lakini hatuwaoni wafanyakazi wa Vodacom mkijitokea kuetetea. Mko kimya ili muendelee kujenga majumba Mbezi Beach, mfungue shule za sekondari na hata chekechea.

Kama ninabisha basi tuleteeni list ya wenye viwanja vya minara ya Vodacom halafu tutaweka list ya wafanyakazi wa Vodacom wa zamani na waliomo sasa hivi halafu uone majina yanavyofanana baadhi.

Hivyo kinachofanyika ni kuondokana na uvivu na wizi wenu na wala si kuwaonea kwamba hakuna ajira. Kuna hotel hapa nchini zimeandikwa mlangoni kwamba BEWARE NOW YOUR IN AFRICA KEEP THE DOOR LOCKED. Maana yake ni kwamba ukiwa hapa Tanzania jiahadhari na ni kweli mnaonyesha.

Hebu semeni nyie wenyewe ni wangapi hapo wanatimuliwa kwa wizi wa mabilioni hapo Vodacom. Acheni za kuleta kujifanya mnatetea ajira za watanzania bali mnatetea ajira zenu.

Tena mnavyoodoka hapo kama mnavyoondolewa sasa basi kila mwajiri hapa nchini anatakiwa kuwa macho na wafanyakazi waliopitia Vodacom na hasa waliopitia ngazi za juu. Ni vijana wa juzijuzi tu, wamejifunza kuendesha gari juzijuzi tu ajabu haijapita miaka 10 lakini wana utajiri kuliko wa Lowasa. Wameupata wapi?

Si ni afadhali kuliko hata Lowasa ambaye hata alipokuwa hapa Wizarani hakuna rekodi inayoonyesha alifukuzwa au kuiba hata senti.

Keep it up NSN and Vodacom. FUkuza hawa mafisadi wadogo ili serikali ijifunze kufukuza mafisadi wakubwa.

Mheshimiwa sifanyi kazi NSN wala VODACOM,sijawahi kufanya kazi kwenye makampuni hayo mawili,nimeandika kwa kutazama uhalisia wa tatizo na sio kwa kuegemea upande wowote.
Umeandika kama mtu mwenye hasira kali na wafanyakazi wa vodacom,kutokana na mafanikio ya muda mfupi waliyoyapata,kutokana na hilo itakuwa ngumu kuijadili mada hii kwa mtazamo huru.
Sijaandika matukio ya wizi yasifanyiwe kazi,nimeandika kuwa kama NSN wanavunja sheria za nchi suala hilo lishughuikiwe mara moja,kwani baada ya muda waajiri wa kigeni watajifunza kutokana na yanayotokea NSN na kuendelea kuwakandamiza waajiriwa watanzania.
 
majungu haya...kma haina signature za wahusika waliondika then ni majungu...kwanza kuna foreign expatriates??? sijaelewa au kuna local expatriates pia...hahaaa
 
Back
Top Bottom