R.B
JF-Expert Member
- May 10, 2012
- 6,296
- 2,573
Halmashauri ya Manispaa ya Temeke imepima viwanja 1,800 katika eneo la Gezaulole ikiwa ni mwendelezo wa utekelezaji wa Mradi wa Upimaji viwanja. Katika awamu hii ya pili, inatarajiwa kuuza fomu za maombi ya viwanja vyenye ukubwa na matumizi mbalimbali kwa utaratibu ufuatao:-
i) Fomu za maombi ya kununua kiwanja zitaanza kutolewa tarehe ...11.06.2012 hadi tarehe 15.06.2012 katika ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke.
ii) Kila Mwombaji atapaswa kulipia ada ya maombi ya kiasi cha shilingi elfu thelathini (Tshs 30,000/=) katika ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke iliyopo mkabala na Uwanja Taifa. Fedha hizo hazitarejeshwa.
iii) Mwombaji atajaza nakala 2 za fomu ya maombi na kuzirejesha zikiwa zimebandikwa picha 3 za ukubwa wa pasipoti. Mwisho wa kurudisha fomu hizo ni tarehe 18.06.2012 saa 8 mchana.
iv) Wakazi wenye nyumba na mashamba ndani ya eneo la Mradi ambao walitambuliwa kabla ya zoezi la upimaji kuanza, nao wanatakiwa kununua fomu za maombi kwa utaratibu uleule ulioainishwa hapo juu.
v) Orodha ya majina ya waombaji watakaouziwa viwanja itabandikwa katika Mbao za Matangazo za Manispaa za Temeke, Ilala na Kinondoni na pia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuanzia tarehe 29.6.2012:help:
vi) Utaratibu wa kulipia Ankara za malipo ya viwanja pamoja na muda wa kulipia utatolewa sambamba na tangazo la orodha ya waliofanikiwa kuuziwa viwanja na litakalobandikwa katika mbao za Matangazo zilizotajwa hapo juu.
JEDWALI: VIWANGO VYA GHARAMA YA VIWANJA:banplease:
Na. Aina ya matumizi Gharama kwa kila Mita ya mraba
Imetolewa na,
MKURUGENZI W MANISPAA:tea:
TEMEKE
i) Fomu za maombi ya kununua kiwanja zitaanza kutolewa tarehe ...11.06.2012 hadi tarehe 15.06.2012 katika ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke.
ii) Kila Mwombaji atapaswa kulipia ada ya maombi ya kiasi cha shilingi elfu thelathini (Tshs 30,000/=) katika ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Temeke iliyopo mkabala na Uwanja Taifa. Fedha hizo hazitarejeshwa.
iii) Mwombaji atajaza nakala 2 za fomu ya maombi na kuzirejesha zikiwa zimebandikwa picha 3 za ukubwa wa pasipoti. Mwisho wa kurudisha fomu hizo ni tarehe 18.06.2012 saa 8 mchana.
iv) Wakazi wenye nyumba na mashamba ndani ya eneo la Mradi ambao walitambuliwa kabla ya zoezi la upimaji kuanza, nao wanatakiwa kununua fomu za maombi kwa utaratibu uleule ulioainishwa hapo juu.
v) Orodha ya majina ya waombaji watakaouziwa viwanja itabandikwa katika Mbao za Matangazo za Manispaa za Temeke, Ilala na Kinondoni na pia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuanzia tarehe 29.6.2012:help:
vi) Utaratibu wa kulipia Ankara za malipo ya viwanja pamoja na muda wa kulipia utatolewa sambamba na tangazo la orodha ya waliofanikiwa kuuziwa viwanja na litakalobandikwa katika mbao za Matangazo zilizotajwa hapo juu.
JEDWALI: VIWANGO VYA GHARAMA YA VIWANJA:banplease:
Na. Aina ya matumizi Gharama kwa kila Mita ya mraba
- Makazi pekee (Ujazo wa juu, kati na chini) 8,000
- Makazi na Biashara 9,000
- Biashara 20,000
- Huduma za Jamii 8,000
- Ibada/kuabudu 8,000
- Viwanda vidogo vidogo (Service trade) 15,000
- Makazi maalumu(Housing Estate) 10,000
- Viwanja Vyenye nyumba (kwa wenye nyumba waliotambuliwa kabla ya upimaji na walioko ndani ya eneo la viwanja) 3,000
Imetolewa na,
MKURUGENZI W MANISPAA:tea:
TEMEKE