Viwango Hivi Vya Elimu Vimepitwa na Wakati!

Ni vizuri bunge letu likawa na wabunge wasomi lakini sipendi kuwepo na sheria ya kukataza wasiosoma kuwa na haki ya kugombea ubunge,ningependa zaidi wananchi waachiwe nafasi ya kuamua wenyewe wanataka kuwakilishwa na mtu wa namana gani.

Rorya wamemkataa Profesor Sarungi wakamchgua mtu wa darasa la saba,sipendi kuwahukumu vibaya wapiga kura wa Rorya yamkini wamebaini mapungufu ya kuwakilishwa na Mzee Sarungi.Moja kubwa mara nyingi hawa wasomi kama Professor Sarungi hawakai kwenye majimbo yao sana sana wanaishi Dar es Salaam Ostabay na Masaki wapiga kura wanaona hakuna haja ya kumchagua msomi ataeishia kuishi Dar ni bora kumchagua darasa la saba atakaishi na kushiriki kutatua kero za vijijini.Wasomi wa aina ya Professor Sarungi wanawawakilisha wasomi wengi sana ambao mara nyingi wanaenda vijijini wakati wa mchakato wa kuomba kura wakishapata ubunge hawaonekana tena mpaka uchaguzi mwingine.Nadhani hii ni sababu moja kubwa kwanini wananchi siku hizi hawapendi kuwakilishwa na wasomi.
 
Wandugu, ubunge ni uongozi (leadership), sio lazima kuwa na elimu ili uwe kiongozi bora. Elimu inahitajika kwenye utawala (management). John Major hakuwa na elimu kubwa (Form Six) lakini alikuwa kiongozi mzuri. Kagame (elimu yake ya kuungaunga, hiyo mnayosema formal education), ni bora kuliko hawa wenye shahada na wala rushwa. Viongozi weu zamani hawakuwa na elimu kubwa lakini walikuwa wazuri na rushwa kwao ilikuwa mwiko. (Tatizo mishahara yao ilikuwa haitoshi). Shughuli za mbunge ni nyingi ikiwa ni pamoja na kuangalia eneo lake kama lina miundombinu bora kwa maendeleo ya watu wake.
Mimi nawasifu sana hao watu ambao ni darasa la saba lakini wameweza kufikia hatua hiyo zama hizi. Kwa habari nilizonazo wengi wao ni watu ambao wameajiri watu katika makampuni yao na yanaendelea vizuri sana. Mchukulie Lamek Airo au Jah People ni watu ambao wana biashara za kimataifa hivyo sioni kama wanaweza kuongoza makampuni yao kwa ufanisi wasiweze kuongoza wanachi kwa shughuli za kibunge.
Kama suala ni lugha tukumbuke lugha rasmi ya Serikali ya Tanzania ni Kiswahili. Tusiwabeze.
La mwisho, katiba yetu inasema wazi kuwa (kifungu cha 67 (1) a) kuwa mbunge ni Mtanzania aliyefikisha miaka 21 ambaye atakuwa anajua kusoma na kuandika Kiswahili na Kiingereza. Kama hawajui kusoma kiingereza kawaekeeni pingamizi!
 
Kwa kweli kuna haja ya kuweka viwango vya elimu vinavyoeleweka kwa mtu kuweza kugombea ubunge. Hivi hawa wataenda kuchambua mikataba ya madini bungeni wataielewa? Au miswaada inayoletwa bungeni imeandikwa kwa kiingereza, hawa watakuwa wanachangia nini?

Kuna sababu ya kubadilika kwa kweli.


Naungana na wewe Lukolo, elimu ni jambo la kuzingatiwa hasa linapokuja swala la kuwa mbunge, umegusia mikataba ya madini na kadhalika ila hata kwenye swala la kutetea hoja kwa manufaa ya taifa au jimbo lake ni muhimu sana kwani elimu humpa mtu upeo mpana wa kujua mambo mbalimbali yanayohusu maendeleo ya nchi.Kwa hili inabidi tuwe makini licha ya kwamba hata hao wasomi nao wana matatizo yao, mfano Prof Sarungi ameondolewa kwenye kura za maoni na mtu mwenye elimu ndogo sana, labda alikuwa busy na ishu za consultation upande wa afya nk badala ya kuendeleza jimbo lake, lakini bado faida ni kubwa za kuwa na mbunge angalau form four sio mbumbu au std 7.Hii inaonyesha jinsi gani sisiemu wanakotaka kutupeleka kubaya.
 
Kwa kulijadili hili kwa upande mwingine hebu tuangalie hii dhana ya UDUMAVU kama ilivyotambulishwa na Iddi Simba kwenye kongamano moja hivi alisema ...

"Kuna watalaamu wamenieleza asilimia 51 ya watoto wenye umri chini ya miaka mitano nchini wamedumaa akili na asilimia 53 ya wenye udumavu wa akili wamevuka umri wa miaka mitano. Kwa bahati mbaya, hatuna shule za kutenganisha wenye udumavu wa akili na wasio na tatizo hilo. Kwa hiyo wote wanasoma pamoja. Katika hali ya kawaida, si kawaida kwa wasio na udumavu wa akili kuwaambukiza kitabia wenye udumavu wa akili,"

"Ilivyo ni wenye udumavu wa akili huambukiza kitabia wasio na udumavu huo. Sasa nimesema asilimia 53 ni watu wazima lakini wenye udumavu wa akili, wamesoma pamoja na wengine, hao hao wamo serikalini ni viongozi. Yaani hiyo asilimia 53 inajumuisha viongozi wadumavu wa akili, ambao pia wameambukiza wenzao na hasa wasomi waliomo kwenye uongozi kwa sasa ..ni dhana ya mtapanyo," alisema Iddi Simba

Je hawa darasa la Saba ndio chanzo cha muambukizo wa UDUMAVU bungeni kwa kuwanyima Wabunge wasomi changamoto stahiki..!??
 
You can use any language you want but, formal education is quite important especially these dayz ambapo dunia ni kijiji. Kazi ya mbunge kwa sasa haihitaji kujua mazingira ya eneo lake tu ili awe mtunga sheria na mwakilishi mzuri wa wapiga kura wake. Ufahamu wa zaidi ya local environment unahitajika na unapatikana kila mahali sasa but access yake tukubaliane inahitaji formal education. Nakubali kuwa na formal education haitoshelezi pekee kuwa mwakilishi mzuri but it is a good starting point.
 
Kwa kweli kuna haja ya kuweka viwango vya elimu vinavyoeleweka kwa mtu kuweza kugombea ubunge. Hivi hawa wataenda kuchambua mikataba ya madini bungeni wataielewa? Au miswaada inayoletwa bungeni imeandikwa kwa kiingereza, hawa watakuwa wanachangia nini?

Kuna sababu ya kubadilika kwa kweli.

Kosa ni wanaoileta katika lugha hiyo, kwani Bungeni China wanatumia kiingereza au UK na US wanatumia Kiswahili? Tatizo litakuwa la msingi ikiwa hata Kiswahili hawajui
 
Ni muhimu kwa bunge letu kuwa cross-section ya population. Lisiwe exclusive country club ya watu wa kuanzia elimu fulani tu.
 
Navyojua mimi bunge ni sehemu ambayo sheria zetu upitishwa na mwelekeo wa matumizi yetu (policies on spending, allocating our resources, to please many and all other political ideas) kitaifa.

Since these decisions are coined by a few executives each appointed by Mr. President, legislatures act as a watchdogs to their reps and that is their number one concern. Hizo policies au sheria zina affect watu wote kama wakisema si sawa mtu kuwa na zaidi la gari moja hivyo wananchi wenye zaidi awana budi bali kuuza au kufanya wajuavyo hili wabakie na moja regardless of their wealthy na mara nyingi huwa kuna penalties kwa wale wanaovunja sheria, au policy ikija ambayo imewekewa budget ndogo mfano kama elimu ujue kutakua akuna hela ya kulipa walimu, shule zitakua uchwara na pengine under baobab trees.

Hivyo ni muhimu watu wanaoingia mjengoni wawe na ufahamu kwa kuwa kuna moral decisions that are made there (mfano issue ya sasa mahakama ya khadi), economical decisions (hasara tunazopata na contract za uchimbaji to make matters worse kuna conditions from the IMF za misaada ambazo zinataka turuhusu wanyonyaji hili tupewe misaada ambayo mara nyingine tunahitaji), kujua umuhimu wa priorities zetu kama taifa ni nini.

Yaani bunge kwa kweli alitakiwi kuwa na akina MC wala majaa sijui nani, naweza kuelewa serikali kuweza kutumia hawa watu kama 'social patners' hili kujua matatizo ya jamii. Hila kuna technicals ambazo mtu ambae ana elimu au niseme mvivu hata kusoma vitabu atojua namna ya kuuliza au kubisha zaidi ya kutoa au kupewa simple expalnations tuu.

Hivi atushangai kwanini sisi ni maskini ajabu wakati policies zote upitia bungeni na upigiwa kura na hawa wabunge it reflects ni jinsi gani tulivyojaza wasomi wezi wanaojua kuwa peleka mabozzo waliopo bungeni. Na CCM inapenda kuwaweka percent fulani ya hawa hili wizi uendelee at our cost.

Mara tu watu wanachukua mapanga kutaka kuchukua ardhi yao wakati kuna sheria mbovu ambazo zimepita bungeni kuruhusu upuuzi in the first place. talk about zero utendaji pelekeni tu hawa jamaa wenu.
 
Again, elimu ni nini? elimu inapimwaje ? Je elimu ni madarasa uliyopitia? Inapimwa kwa ma certificate uliyopata ?

Kiranga,

Nimeona niazime tafsiri ya wakongwe kama Hill, N (1937) aliyesema maneno haya kuhusu maana sahihi ya neno Education and Educate "That word is derived from the Latin word "educo", meaning to educe, to dfraw out, to DEVELOP FROM WITHIN. An educated man is not, necessariry, one who has an abundance of general or specialized knowledge. An educated man is one who has so developed the faculties of his mind tha he may acquire anything he wants, or its equivalent, wothout violating the rights of others."

Mkongwe mwingine ambaye utakubaliana nami hakuwa mvivu wa kufikiri wakati anazindua "The Declaration of Dar es Salaam" J.K. Nyerere alisema hivi kuhusu Education "Education is thus intensely personal. In the sense that it has to be a personal experience- no one cam have his consciousness developed by proxy. But it is also am activity of great social significance, because the man whom education liberates is a man in society, and his society will be affected by the change which education creates in him."

Natumai majibu hayo ya wakongwe wawili yatakuwa yamesaidia kutoa jibu la swali lako. Wakongwe wote wawili wanakubaliana kuwa matokea ya Elimu ni lazima yaonekane kwenye jamii husika.

Nakubaliana na wewe kabisa kuwa vyeti sio hoja, infact vyeti havina maana yoyote iwapo mwenye vyeti hivyo hajafanya vitendo vinavyoonyesha na vinavyokubalika kwenye jamii husika.
 
Kwa kulijadili hili kwa upande mwingine hebu tuangalie hii dhana ya UDUMAVU kama ilivyotambulishwa na Iddi Simba kwenye kongamano moja hivi alisema ...

"Kuna watalaamu wamenieleza asilimia 51 ya watoto wenye umri chini ya miaka mitano nchini wamedumaa akili na asilimia 53 ya wenye udumavu wa akili wamevuka umri wa miaka mitano. Kwa bahati mbaya, hatuna shule za kutenganisha wenye udumavu wa akili na wasio na tatizo hilo. Kwa hiyo wote wanasoma pamoja. Katika hali ya kawaida, si kawaida kwa wasio na udumavu wa akili kuwaambukiza kitabia wenye udumavu wa akili,"

"Ilivyo ni wenye udumavu wa akili huambukiza kitabia wasio na udumavu huo. Sasa nimesema asilimia 53 ni watu wazima lakini wenye udumavu wa akili, wamesoma pamoja na wengine, hao hao wamo serikalini ni viongozi. Yaani hiyo asilimia 53 inajumuisha viongozi wadumavu wa akili, ambao pia wameambukiza wenzao na hasa wasomi waliomo kwenye uongozi kwa sasa ..ni dhana ya mtapanyo," alisema Iddi Simba

Je hawa darasa la Saba ndio chanzo cha muambukizo wa UDUMAVU bungeni kwa kuwanyima Wabunge wasomi changamoto stahiki..!??

Hivi sasa ughaibuni , msisitizo ni kuwachanganya watoto wenye matatizo ( unaowaita wadumavu) na wale ambao bila shaka wewe na Iddi Simba mtawaona wa kawaida. Hii inasaidia kupunguza fikra mbovu dhidi ya hao wenye matatizo na imeonekana kusaidia pande zote, wenye matatizo wanakuwa na confidence baada ya kukubalika na hao wengine kugundua kuwa hao wenzao bado ni binadamu kama wao. Wanaotengwa ni wale ambao matatizo yao ni extreme kiasi cha kuweza kuhatarisha usalama wake mwenyewe au wa watu wengine.

Amandla....
 
Napingana na wote mnaokataa kwamba elimu rasmi (kwa maana ya vidato vya sekondari na elimu ya taasisi za juu) si lazima na mnadai msingi mkubwa ni mtu kuwa ana elimu (informal au formal). Mbuge anayo majukumu yanayolazimisha awe na elimu rasmi. Elimu, kwa mtazamo wangu, haina maana ya kusoma na kuandika kiingereza bali ni, pamoja na mengine, kuwa na uwezo wa kuchambua na kutathmini mambo mbali mbali. Mtu ambaye hana hata elimu ya kidato cha nne itakuwa tabu:

1) Kutumia angalau saa moja kupitia mswada

2) Kuchambua mswada wenyewe maana kwanza hawezi kuusoma na kuulewa...hana mazoea ya kusoma

3) Atadharauliwa na wenzake hata kama ana 'points' zenye mantiki (At university level, kwa mfano, ni kawaida Profesa kumdharau Daktari licha ya wote kuwa sawa at least academically speaking).

4)Watu hawa (wasio na formal education) hufanikiwa kwa vile tu wanatoka kwenye koo kubwa, wanapesa nyingi au ni jamii inatoa tu adhabu kwa wagombea wengine kwa sababu kadha wa kadha...si wazuri hivyo!

5) n.k.
 
Mbunge na mpinga kura kupata elimu inayojitoshereza ni muhimu.Mbunge wa kuchaguliwa anapatikana kwenye jimbo kwa kupigiwa kura na wanajimbo lake,lakini kwa bahati mbaya sio majimbo yote yana watu wana elimu ya kujitoshereza.Hivyo kwa wakati mwingine mwenye chongo ndio mfalme.
Lakini waheshimiwa wabunge wenye viwango tofauti vya elimu wanapojadiri miswaada mbali mbali bungeni hutumia dakika karibu saba kati ya dakika 15 alizopewa kuchangia hoja akisifu mkewe,mumewe,mawaziri,Raisi,Chama cha mapinduzi nk.na kutumia dakika hizo 8 tu kuchangia mswaada.Kwa lugha nyingine wote hao wanalitania bunge tukufu licha ya tofauti ya elimu. Takwimu za Wabunge wasomi wenye shahada zinazidi kuongezeka na Idadi ya wabunge wasio na shahada inazidi kupungua.Lakini wananchi haturidhiki na ufanisi wa Bunge.
 
Lakini kwenye uchaguzi mdogo alishinda, una uhakika gani kwamba mwezi Oktoba atashindwa kupita?

I know common sense is not common; ndio alishinda kwenye uchaguzi mdogo kwasababu tu mgombea wa Chadema alienguliwa!! Ukichukua idadi ya waliojiandikisha kwenye ile by-election na wale waliopiga kura, inaonesha wananchi wengi walisusia ule uchaguzi. Wale waliosusuia wangepiga kura huyu jamaa asingeshinda na hivyo ndivyo itakavyokuwa October iwapo Chadema itamsimamisha mgombea wao yule yule. Ccm wanalijua hilo!!
 
Napingana na wote mnaokataa kwamba elimu rasmi (kwa maana ya vidato vya sekondari na elimu ya taasisi za juu) si lazima na mnadai msingi mkubwa ni mtu kuwa ana elimu (informal au formal). Mbuge anayo majukumu yanayolazimisha awe na elimu rasmi. Elimu, kwa mtazamo wangu, haina maana ya kusoma na kuandika kiingereza bali ni, pamoja na mengine, kuwa na uwezo wa kuchambua na kutathmini mambo mbali mbali. Mtu ambaye hana hata elimu ya kidato cha nne itakuwa tabu:

1) Kutumia angalau saa moja kupitia mswada

2) Kuchambua mswada wenyewe maana kwanza hawezi kuusoma na kuulewa...hana mazoea ya kusoma

3) Atadharauliwa na wenzake hata kama ana 'points' zenye mantiki (At university level, kwa mfano, ni kawaida Profesa kumdharau Daktari licha ya wote kuwa sawa at least academically speaking).

4)Watu hawa (wasio na formal education) hufanikiwa kwa vile tu wanatoka kwenye koo kubwa, wanapesa nyingi au ni jamii inatoa tu adhabu kwa wagombea wengine kwa sababu kadha wa kadha...si wazuri hivyo!

5) n.k.

Point hizo mbili hapo juu zina ji contradict.

Kwanza unasema,

Napingana na wote mnaokataa kwamba elimu rasmi (kwa maana ya vidato vya sekondari na elimu ya taasisi za juu) si lazima na mnadai msingi mkubwa ni mtu kuwa ana elimu (informal au formal).

Halafu baada ya hapo unaema

Elimu, kwa mtazamo wangu, haina maana ya kusoma na kuandika kiingereza bali ni, pamoja na mengine, kuwa na uwezo wa kuchambua na kutathmini mambo mbali mbali.

Kwa hiyo unaonekana either unaji contradict au huelewi kwamba uwezo wa kuchambua na kutathmini mambo si lazima upatikane darasani. Kuna watu wamechungulia darasani wakaona kuna wapotezea muda tu, wanaweza kufanya yote ya darasani na kuongeza vingine wenyewe, sasa hata nao utawazuia wasiwe wabunge?

Hivi Brazil wangesema hawataki mtu ambaye hana formal education mtu kama Lula Da Silva ambaye anasifiwa kwa kuiongoza Brazil vizuri sana angefika wapi? Inawezekana "msomi" asingeweza kuifikisha Brazil ilipo.

Tusichanganye "formal education" na usomi, unaweza kupata formal education lakini usiwe msomi, na unaweza usipate formal eduction ukawa msomi. Wamarekani ambao wamesoma hiyo "formal education" kutupita sisi wanaelewa hili, ndiyo maana rais Truman mpaka leo ni mmoja wa marais wanaoheshimiwa sana Marekani, lakini hakuwa na formal education bali elimu yake ya maisha kutoka jeshini mpaka kazi katika TANROADS ya Missouri, mpaka local politics zao at the state level, mpaka kuwa senator, mpaka vice president zimemfundisha. Sasa utasema tukiwa na mtu amepanda ngazi zote hizo anaelewa serikali inavyokwenda na uzoefu wa miaka mingi lakini hana formal education tumkatae kwa sababu hana degree tu ? Degree zenyewe hizi wanapata watoto hata kuandika hawajui siku hizi ?

I am sorry, kwangu mimi wananchi waachiwe wafanye maamuzi, kuweka vikwazo vya elimu ni kuiminya demokrasia.

Hizi points zako nne zote weak, hebu tuziangalie.

Mtu ambaye hana hata elimu ya kidato cha nne itakuwa tabu:

1) Kutumia angalau saa moja kupitia mswada

Unasema haya kwa kutumia kigezo gani ? Mtu anaweza kumaliza kidato cha nne na division 0 asiweze hata kusoma vizuri, na mwingine wa darasa la saba akawa na jitihada zake binafsi kuwa na uchanganuzi mzuri zaidi, tena ambao haujajikita katika usomi -ambao unaweza kuwa theoretical zaidi- bali uliojikita katika matatizo real ya wananchi.

2) Kuchambua mswada wenyewe maana kwanza hawezi kuusoma na kuulewa...hana mazoea ya kusoma

Mazoea ya kusoma hayana uhusiano wowote na kiwango cha elimu, watu kibao wanaenda mpaka chuo kikuu na hawana mazoea ya kusoma, wanasoma pale tu wanapolazimika ili kupasi mitihani. Na kuna watu kibao hawajasoma rasmi shule lakini ni wapenzi sana wa kusoma na kuandika.Hivi Shaaban Robert alisoma chuo gani ? Hivi hao wanaoandika na kuachia madudu kwenye website ya Chuo Kikuu hawajasoma hao?

3) Atadharauliwa na wenzake hata kama ana 'points' zenye mantiki (At university level, kwa mfano, ni kawaida Profesa kumdharau Daktari licha ya wote kuwa sawa at least academically speaking).

Kama mtu anamdharau mwenzake kwa sababu ya "formal education" yake, bila kujali points, nani kaelimika na nani hajaelimika hapa? Wewe unajali perception au reality? Ukijali watu watakaokudharau unaweza kufanya chochote duniani hapa? Kila kitu utakachofanya utadharauliwa na watu fulani. Hivi wewe unajiamini wewe mwenyewe au unangojea kupata approval ya watu ?

4)Watu hawa (wasio na formal education) hufanikiwa kwa vile tu wanatoka kwenye koo kubwa, wanapesa nyingi au ni jamii inatoa tu adhabu kwa wagombea wengine kwa sababu kadha wa kadha...si wazuri hivyo!

Unaweza kutupa mifano? Lula da Silva niliyemtolea mfano katoka katika familia maskini kabisa, na kafanikiwa beyond any dreams, utasemaje hapo?
 
ELIMU SI KIGEZO CHA UZALENDO........! TUCHAGUE MZALENDO......!AANGALIAYE MASLAHI YA TAIFA KWANZA HALAFU MASLAHI MENGINE BAADAYE!.....akilipenda taifa lake hawezi hongwa apitishe sheria ya kuuza kila kilcho chetu kwa kuwa tu amejengewa nyumba au anasomeshewa watoto ulaya na kadha wa kadha, linapohitajika suala la utaalamu katika kutunga sheria husika wapo wataalmu wa sheria toka vitengo husika. MATHALANI...UHAMIAJI,ARDHI,MAJI,MADINI N.K.
 
Point hizo mbili hapo juu zina ji contradict.

Kwanza unasema,



Halafu baada ya hapo unaema



Kwa hiyo unaonekana either unaji contradict au huelewi kwamba uwezo wa kuchambua na kutathmini mambo si lazima upatikane darasani. Kuna watu wamechungulia darasani wakaona kuna wapotezea muda tu, wanaweza kufanya yote ya darasani na kuongeza vingine wenyewe, sasa hata nao utawazuia wasiwe wabunge?

Hivi Brazil wangesema hawataki mtu ambaye hana formal education mtu kama Lula Da Silva ambaye anasifiwa kwa kuiongoza Brazil vizuri sana angefika wapi? Inawezekana "msomi" asingeweza kuifikisha Brazil ilipo.

Tusichanganye "formal education" na usomi, unaweza kupata formal education lakini usiwe msomi, na unaweza usipate formal eduction ukawa msomi. Wamarekani ambao wamesoma hiyo "formal education" kutupita sisi wanaelewa hili, ndiyo maana rais Truman mpaka leo ni mmoja wa marais wanaoheshimiwa sana Marekani, lakini hakuwa na formal education bali elimu yake ya maisha kutoka jeshini mpaka kazi katika TANROADS ya Missouri, mpaka local politics zao at the state level, mpaka kuwa senator, mpaka vice president zimemfundisha. Sasa utasema tukiwa na mtu amepanda ngazi zote hizo anaelewa serikali inavyokwenda na uzoefu wa miaka mingi lakini hana formal education tumkatae kwa sababu hana degree tu ? Degree zenyewe hizi wanapata watoto hata kuandika hawajui siku hizi ?

I am sorry, kwangu mimi wananchi waachiwe wafanye maamuzi, kuweka vikwazo vya elimu ni kuiminya demokrasia.

Hizi points zako nne zote weak, hebu tuziangalie.



Unasema haya kwa kutumia kigezo gani ? Mtu anaweza kumaliza kidato cha nne na division 0 asiweze hata kusoma vizuri, na mwingine wa darasa la saba akawa na jitihada zake binafsi kuwa na uchanganuzi mzuri zaidi, tena ambao haujajikita katika usomi -ambao unaweza kuwa theoretical zaidi- bali uliojikita katika matatizo real ya wananchi.



Mazoea ya kusoma hayana uhusiano wowote na kiwango cha elimu, watu kibao wanaenda mpaka chuo kikuu na hawana mazoea ya kusoma, wanasoma pale tu wanapolazimika ili kupasi mitihani. Na kuna watu kibao hawajasoma rasmi shule lakini ni wapenzi sana wa kusoma na kuandika.Hivi Shaaban Robert alisoma chuo gani ? Hivi hao wanaoandika na kuachia madudu kwenye website ya Chuo Kikuu hawajasoma hao?



Kama mtu anamdharau mwenzake kwa sababu ya "formal education" yake, bila kujali points, nani kaelimika na nani hajaelimika hapa? Wewe unajali perception au reality? Ukijali watu watakaokudharau unaweza kufanya chochote duniani hapa? Kila kitu utakachofanya utadharauliwa na watu fulani. Hivi wewe unajiamini wewe mwenyewe au unangojea kupata approval ya watu ?



Unaweza kutupa mifano? Lula da Silva niliyemtolea mfano katoka katika familia maskini kabisa, na kafanikiwa beyond any dreams, utasemaje hapo?

Dear Kiranga,

Nashukuru kwa mawazo yako. Ila tungefanya random sampling ya watu wasomi (kwa maana ya formal education) na wasio wasomi (kwa maana ya informal education) na tukastudy ni kundi lipi lina nafasi ya kuwa na uelewa mkubwa wa kufanya kazi inayohitaji utaalamu (eg kutunga sheria), sina shaka guys with formal education watakuwa na nafasi (probability) nzuri ya kufanya vyema. Kwa hiyo, kama nachagua nipo kwenye issue ya probability na nitaavoid risk kwa kujaribu msomi.

Pamoja na kuasassinate point zangu zote, ukweli unabaki kwamba highly educated (learned?) fellows tend to have more confidence as compared to those who lack formal education. Lula Da Silva and Shaaban Robert are rare cases and may be referred to as "extreemes" or outliers.

Ama kuhusu kudharauliwa, unaweza kukubali au kukataa lakini mimi hapa nimeongelea fact. Iam not speculating or surmising. Nimetolea mfano wa university kwa vile najua hali halisi hapo.
 
Dear Kiranga,

Nashukuru kwa mawazo yako. Ila tungefanya random sampling ya watu wasomi (kwa maana ya formal education) na wasio wasomi (kwa maana ya informal education) na tukastudy ni kundi lipi lina nafasi ya kuwa na uelewa mkubwa wa kufanya kazi inayohitaji utaalamu (eg kutunga sheria), sina shaka guys with formal education watakuwa na nafasi (probability) nzuri ya kufanya vyema. Kwa hiyo, kama nachagua nipo kwenye issue ya probability na nitaavoid risk kwa kujaribu msomi.

Tafadhali usifanye assumption kabla ya kupata evidence, fanya hiyo study kwanza, halafu ukipata supporting evidence utaweza kuongea.

Ndiyo usomi wenyewe tunaoutaka huu? Wa ku conclude vitu bila evidence ?

Pamoja na kuasassinate point zangu zote, ukweli unabaki kwamba highly educated (learned?) fellows tend to have more confidence as compared to those who lack formal education. Lula Da Silva and Shaaban Robert are rare cases and may be referred to as "extreemes" or outliers.

Katika mfumo wa demokrasia, tukiweka kikwazo cha kumzuia Lula Da Silva au Shaaban Robert mmoja tu, kikwazo hiki hakitufai. Kwa sababu inawezekana huyu Lula au Shaaban Robert ndiye angetuletea mabadiliko nchini mwetu.

Kwa hiyo mimi naona badala ya kufunga mlango kwa watu wasio na formal education, ni muhimu zaidi kuwaelimisha wananchi wenyewe wajue kitu gani cha kuangalia katika wagombea, ili kusudi waweze kuchuja mgombea gani asiye na formal education hafai, na nani ni Lula Da Silva na Shaaban Robert.

Ama kuhusu kudharauliwa, unaweza kukubali au kukataa lakini mimi hapa nimeongelea fact. Iam not speculating or surmising. Nimetolea mfano wa university kwa vile najua hali halisi hapo.

Fact gani? Inatokana na study gani? Mwenyewe umesema kwamba ume conclude kabla ya kufanya any study, sasa fact inatoka wapi?

Wewe sema hizi ni personal prejudices zako, kwamba una kawaida ya kudharau watu wasiosoma.

Let me tell you a story about these snobbish prejudices, kulikuwa na Katibu mkuu wizara ya ujenzi, Dr. George Mlingwa, huyu bwana ana PhD, akasema yeye hawezi kuongea na mtu yeyote ambaye hana degree, alikuwa na nyodo sana pale wizarani, kama kuna wanaomfahamu watatueleza hapa. Siku zikaenda akawa implicated kwenye issue ya scandals za rushwa za ujenzi (pamoja na Nalaila Kiula) Mzee Mlingwa akaswekwa ndani, wafanyakazi wa ujenzi ambao hawakuwa na kinyongo naye wakawa wanaenda kumtembelea lupango, mbona mwenyewe alitia adabu akawa anaongea nao vizuri tu.

Hivi Tanzania tuna watu wangapi wenye kusoma formally mpaka tujitie kuwa na masharti haya? Mbona Marekani wenye kusoma zaidi yetu hawana upuuzi huu ? Wenzetu wanaelewa demokrasia ni nini, na wanaelewa "formal education" ni sehemu ndogo tu ya education, na wanaelewa ukishaanza kuweka vikwazo vya kielimu unatengeneza "guilds" za kufungia uongozi kuwa katika class fulani ya watu tu, unaua demokrasia.

Mwisho tutaenda kusema watu ambao hawana nasaba na familia za kichifu wasiruhusiwe kugombea uongozi, maana hawana historia ya uongozi, si ndiyo line ile ile ya kutumia credentials ku block a segment fulani ya population kupata nafasi yao ya kikatiba.

Tunachotaka sasa hivi ni kuondoa barriers kwa haki za kikatiba, kama vile kuruhusu private candidacy na kuondoa barrier ya kuhitaji vyama. Hatutakiwi kuongelea kuongeza barriers za watu kupata constitutional rights.

Hizi restrictions zikiwekwa zitakuwa unconstitutional. Hata mahakama haiwezi kuziruhusu unless tubadilishe katiba.
 
Kiranga

LET US AGREE TO DISAGREE!

Agreeing to disagreeing is a politically correct logical tautology linguistic mess carrying an unnecessary redundancy, you can be more precise by saying "Let us disagree".

Even "extremes" and "outliers" have constitutional rights too.Let's uphold that right and not bow under uncollected and unverifiable "statistics".

Tatizo letu wala si "formal education" ingekuwa hivyo tungeona tofauti kubwa baina ya majimbo, this barking for "formal education" is barking under the wrong tree. Tuna matatizo kibao makubwa zaidi ya formal edcation ambayo tunaweza kuya address mapema zaidi na kwa kupitia katiba yetu iliyopo.

Ni kawaida yetu kutafuta quick fixes na majibu rahisi kwa maswali magumu, badala ya kutaka kupandisha elimu ya wananchi kwa ujumla, tunafikiri tutatatua tatizo kwa kuweka educational restrictions kwa wabunge. Badala ya kukubali kwamba zaidi ya masuala ya elimu, tuna maswala ya utamaduni yanayosababisha hata hawa "wasomi" wa formal education wasifanye chochote cha maana, tunabaki kusujudu mivyeti, mpaka hata hao wenye vyeti wanaenda kununua vyeti vya kuongezea Almeda, chuo kinachotoa vyeti hata kwa mbwa.

Kusujudia usomi wa elimu rasmi sio utatuzi wa matatizo yetu, kusujudia usomi rasmi ni moja ya matatizo ya taifa letu.
 
Even "extremes" and "outliers" have constitutional rights too.Let's uphold that right and not bow under uncollected and unverifiable "statistics".

Nilifikiri wewe ni mathematician (going by your signature). Issue hapa siyo constitutional right (unaleta mambo ya Obama juu ya Ground Zero Mosque anapesama ametetea haki na hafanyi comment juu ya busara-wisdom). Nimeargue mathematically kwamba probability kwamba formally educated person will perform better than a standard seven leaver is higher. Kwa vile uko unshakable in what you believe hutaki kukubali opinion za wenzako bila kujali mantiki yake. Huwezi kutuambia hata nchi moja isiyo amini in formal education. I tell you, even those guys you are defending (wasio na vidato) wanajua ni kiasi gani wangekuwa more efficient and effective kama wangekuwa na formal education! You're the only guy (outlier) who dont see the necessity of formal educ.
 
Back
Top Bottom