Mwawado
JF-Expert Member
- Nov 2, 2006
- 993
- 252
Ndugu Wanabodi,
Katika Mchakato wa kutafuta wagombea Ubunge kupitia Chama Tawala (CCM), kumetokea mwamko mkubwa kutoka kwa wananchi wa kawaida kutaka ridhaa ya kuwawakilisha wenzao Bungeni. Katika Mchakato huo kumetokea watu wa rika, rangi, dini na makabila tofauti. Utofauti huo wa wagombea unaonyesha ni kiasi gani demokrasia inakuwa Nchini kwetu.
Kilichonishangaza Mimi,ni kiwango cha Elimu cha baadhi ya Wagombea waliopitishwa katika kazi hiyo muhimu ya Kutunga Sheria. Naomba nisionekane mbaguzi hapa, lakini ni ukweli usiopingika kuwa ni vyema tuchague watu wenye kiwango kizuri cha Elimu ili kuweza kukimbizana na mwendokasi huu wa maendeleo. Kiwango cha Elimu ya Msingi si kiwango kizuri kwa kazi ngumu ya mijadala na Utungaji sheria.
Naomba Tume ya Uchaguzi (NEC) iweke utaratibu wa kutangaza angalau kiwango cha Elimu ya Kidato cha sita. Vinginevyo tutakuwa na kundi la Watunga sheria wasio na uelewa wa wanachosimamia.
Hapa chini nimejaribu kuweka Majina ya Wagombea Ubunge waliopitishwa na NEC/CC ambao kiwango chao cha Elimu ni shule ya Msingi na kuna mmojawapo hana kabisa Elimu ya darasani.
1; Deo Sanga (Jah People) (Njombe Kaskazini)
2; Jamal A Tamim (Muhambwe - Kigoma)
3; Lameck O Airo (Rolya - Mara)
4; Moshi S Kakoso (Mpanda Vijijini - Rukwa)
5; Stephen Ngonyani (Korogwe Vijijini - Tanga)
6; Livingstone J. Lusinde ( Mtera - Dodoma)
7; Hussein Nassoro Amar (Nyang'wale - Mwanza)
8; Luckson Ndaga Mwanjale (Mbeya Vijijini) - Hana Formal Education.
9; Mahmood Abuu Juma (Kibaha Vijijini - Pwani)
10;Aeshi Khalfany Hillary (Sumbawanga mjini - Rukwa).
Mniwie radhi kama nitakuwa nimewakwaza baadhi ya watu/wagombea katika bandiko langu hili.Lakini kwa mustakabali wa Taifa letu naomba tujadilane kwa hili.
Katika Mchakato wa kutafuta wagombea Ubunge kupitia Chama Tawala (CCM), kumetokea mwamko mkubwa kutoka kwa wananchi wa kawaida kutaka ridhaa ya kuwawakilisha wenzao Bungeni. Katika Mchakato huo kumetokea watu wa rika, rangi, dini na makabila tofauti. Utofauti huo wa wagombea unaonyesha ni kiasi gani demokrasia inakuwa Nchini kwetu.
Kilichonishangaza Mimi,ni kiwango cha Elimu cha baadhi ya Wagombea waliopitishwa katika kazi hiyo muhimu ya Kutunga Sheria. Naomba nisionekane mbaguzi hapa, lakini ni ukweli usiopingika kuwa ni vyema tuchague watu wenye kiwango kizuri cha Elimu ili kuweza kukimbizana na mwendokasi huu wa maendeleo. Kiwango cha Elimu ya Msingi si kiwango kizuri kwa kazi ngumu ya mijadala na Utungaji sheria.
Naomba Tume ya Uchaguzi (NEC) iweke utaratibu wa kutangaza angalau kiwango cha Elimu ya Kidato cha sita. Vinginevyo tutakuwa na kundi la Watunga sheria wasio na uelewa wa wanachosimamia.
Hapa chini nimejaribu kuweka Majina ya Wagombea Ubunge waliopitishwa na NEC/CC ambao kiwango chao cha Elimu ni shule ya Msingi na kuna mmojawapo hana kabisa Elimu ya darasani.
1; Deo Sanga (Jah People) (Njombe Kaskazini)
2; Jamal A Tamim (Muhambwe - Kigoma)
3; Lameck O Airo (Rolya - Mara)
4; Moshi S Kakoso (Mpanda Vijijini - Rukwa)
5; Stephen Ngonyani (Korogwe Vijijini - Tanga)
6; Livingstone J. Lusinde ( Mtera - Dodoma)
7; Hussein Nassoro Amar (Nyang'wale - Mwanza)
8; Luckson Ndaga Mwanjale (Mbeya Vijijini) - Hana Formal Education.
9; Mahmood Abuu Juma (Kibaha Vijijini - Pwani)
10;Aeshi Khalfany Hillary (Sumbawanga mjini - Rukwa).
Mniwie radhi kama nitakuwa nimewakwaza baadhi ya watu/wagombea katika bandiko langu hili.Lakini kwa mustakabali wa Taifa letu naomba tujadilane kwa hili.