Lekanjobe Kubinika
JF-Expert Member
- Dec 6, 2006
- 3,020
- 577
Jamani, nawaza kila wakati sipati jibu.
Mwalimu JKN alithubutu kuanzisha utengenezaji wa magari ya NYATI hapa nchini akiwatumia wanajeshi kwa kuamini kwamba ni waaminifu zaidi na wanajituma kazi, tena kwamba labda wataweza kuwa wabunifu wakatengeneza na magari mbalimbali ya kivita na kupunguza ununuaji wa magari kutoka nje ya nchi. Nyati miaka yote hii ukibahatika utaambiwa imepita lakini ni ya jeshi. Technologia haijasambazwa na wala sidhani kama kuna mpango huo.
Afrika kusini wanatengeneza magari aina zote ya kijapani, kijeremani na kadhalika na kujipatia ajira na vipuri kinafuu sana kiasi kwamba kuwa na gari kuu kuu sio tija kule. Botswana nao wanatengeneza magari. India ni third word pia na hata China lakini hata ndege zinatengenezwa kule.
Kwa nini Tanzania haichukui hatua za makusudi kulobby makampuni makubwa yanayotengeneza magari Japan, China, India, German nk kuja kuwekeza nchini ambapo tunalo ardhi kubwa kabisa isiyofaa kwa kilimo lakini ingetumika kwa kazi za viwanda hivyo, nasi tukawa kama Japan siku moja kiviwanda kwa kununua au hata kuiba technologia zao na kuzikarabati ili kutengeneza made in TZ hapa hapa, badala yake tumeshupaza shingo kuleta magari ambayo ni mikweche tu kuja kujaza kama vyuma chakavu nchini, kama dumping area?
Hivi hatuna wataalam wa kulobby uwekezaji mkubwa wa aina hiyo, ila wa kubangaiza wachimba madini ambao wanatuachia mashimo tu? Nadhani uzalendo ni tatizo kubwa TZ. Imekaa vipi hapo?
Mwalimu JKN alithubutu kuanzisha utengenezaji wa magari ya NYATI hapa nchini akiwatumia wanajeshi kwa kuamini kwamba ni waaminifu zaidi na wanajituma kazi, tena kwamba labda wataweza kuwa wabunifu wakatengeneza na magari mbalimbali ya kivita na kupunguza ununuaji wa magari kutoka nje ya nchi. Nyati miaka yote hii ukibahatika utaambiwa imepita lakini ni ya jeshi. Technologia haijasambazwa na wala sidhani kama kuna mpango huo.
Afrika kusini wanatengeneza magari aina zote ya kijapani, kijeremani na kadhalika na kujipatia ajira na vipuri kinafuu sana kiasi kwamba kuwa na gari kuu kuu sio tija kule. Botswana nao wanatengeneza magari. India ni third word pia na hata China lakini hata ndege zinatengenezwa kule.
Kwa nini Tanzania haichukui hatua za makusudi kulobby makampuni makubwa yanayotengeneza magari Japan, China, India, German nk kuja kuwekeza nchini ambapo tunalo ardhi kubwa kabisa isiyofaa kwa kilimo lakini ingetumika kwa kazi za viwanda hivyo, nasi tukawa kama Japan siku moja kiviwanda kwa kununua au hata kuiba technologia zao na kuzikarabati ili kutengeneza made in TZ hapa hapa, badala yake tumeshupaza shingo kuleta magari ambayo ni mikweche tu kuja kujaza kama vyuma chakavu nchini, kama dumping area?
Hivi hatuna wataalam wa kulobby uwekezaji mkubwa wa aina hiyo, ila wa kubangaiza wachimba madini ambao wanatuachia mashimo tu? Nadhani uzalendo ni tatizo kubwa TZ. Imekaa vipi hapo?