Fahamu kupika Vitumbua vya aina mbalimbali

X-PASTER

JF-Expert Member
Feb 12, 2007
11,610
1,810
1603635041641.png


Mchanganuo wa jinsi ya kupika vitumbua
Vitumbua ni aina ya vitafunwa vya chai ambavyo hutengenezwa kwa kutumia unga wa mchele,nyama,samaki,tambi,mtama nk.

Kiasili vitumbua ni chakula ambacho hupendelewa sana na watu wa pwani. Na mara nyingi wamekuwa wakipika kwa kuchanganya na nazi au maziwa nk ili kuvifanya viwe na ladha nzuri zaidi

Mahitaji

1. Mchele wa vip vikombe 2
2.Hamira kijiko cha chai 1
3. Tui la nazi kikombe 1
4. Ute wa mayai 2 (ukipenda)
5. Sukari kikombe 1
6. Unga wa ngano kijiko cha chakula 1
7. Hiriki kijiko cha chai

Maandalizi

1. Loweka mchele katika maji usiku mzima.
2. Chuja maji yote kisha utie mchele katika blender pamoja na tui la nazi, unga wa ngano, hiriki na hamira.
3. Saga hadi uwe laini, mimina katika bakuli, funikia acha sehemu yenye joto ufure hadi ujae mara mbili.
4. Tia sukari na ute wa yai, koroga vizuri.
Choma vitumbua vyako katika moto wa kiasi hadi vipate rangi ya kahawia pande zote mbili.

Tayari kwa kuliwa.
--------

Au

Mahitaji


Unga wa mchele ½ kg
Sukari vijiko 4 vya mezani
Tui bubu la nazi
Mafuta ya kupikia
Unga wa hiliki ½ kijiko cha chai
Hamira kijiko 1 cha chai

Jinsi ya kuandaa na kupika

Chukua unga wa mchele na weka kwenye bakuli au sufuria ya kilo moja
Weka hamira kisha weka sukari kisha miminia tui katika mchanganyiko wako
Weka hiliki koroga hadi Uwe uji mzito.

Acha uji huo kwa muda wa saa moja hadi uumuke, mara nyingi kuumuka kunategemea na hali ya hewa Yani joto au baridi.

Baada unga kuumuka
Washa jiko weka chuma Cha vitumbua kisha weka mafuta kijiko kimoja cha chakula kila kishimo acha yapate moto Kisha mimina mchanganyiko kiasi kwenye kikarai maalumu cha kuchomea vitumbua.

Hakikisha Moto sio mkali kitumbuai kikiiva upande mmoja, geuza upande wa pili mpaka kiwe tayari.

Ukimaliza kuchoma panga kwenye sahani. unaweza kula vitumbua vikiwa moto au vikipowa. Kinywaji utachagua mwenyewe kama ni chau nk.

Michango ya wadau
Vitumbua (Aina Ya 1)

Vipimo

  • 1 Kikombe cha mchele.
  • 1 Kijiko cha kulia cha unga wa ngano.
  • 3/4-1 Kikombe cha tui la nazi zito.
  • 2 Mayai.
  • 1 Kijiko cha chai cha hamira.
  • 1/2- 3/4 kikombe cha sukari.
  • Iliki kiasi upendacho.

Naman Ya Kutayarisha Na Kupika

  1. Osha na kuroweka mchele ndani ya maji ya baridi masaa manane au siku moja.
  2. Mimina vifaa vyote ispokuwa sukari, ndani ya blender na usage mpaka mchele uwe umesagika kabisa.
  3. Mimina sukari ndani ya mchanganyiko na usage tena kidogo tu.
  4. Mimina mchanganyiko ndani ya bakuli na ufinike. Weka bakuli mahali penye joto ili mchanganyiko uuumuke.
  5. Mchanganyiko ukisha umuka, weka karai kwenye moto.
  6. Tumia kama kijiko 1-2 cha chai cha samli kwa kukaangia kila kitumbua.
  7. Mimina mchanganyiko kiasi kwenye karai kulingana na kikarai unachotumia.
  8. Kitumbua kikiiva upande mmoja, geuza upande wa pili mpaka kiwe tayari.
  9. Panga kwenye sahani. unaweza kula vitumbua vikiwa moto au vikipowa.
----
Vitumbua Vya Mchele

View attachment 1606887
Mahitaji
Mchele ......2cups
Tui zito ......1cup
Ute wa yai ......1
Unga wa Sembe ...1 table spoon
Unga wa Ngano …1table spoon
Hamira.........…1 table spoon
Hiliki ..........1 table spoon
Sukari .......½ Cup

Jinsi Ya Kupika
Saga mchele na tui kwenye blender mpaka uwe laini uhakikishe hauna chenga hata kidogo tia yai, hamira na hiliki endelea kusaga. Tia sukari endelea kusaga na mwisho utatia unga wa ngano na wa sembe, saga tena kidogo toa weka kwenye bakuli, acha uumuke.

Ukishaumuka weka kwenye chuma cha vitumbua na uanze kuchoma kwa mafuta pole pole, mpaka uone vimebadilika rangi.
-----

Wapendwa..amani iwe juu yenu!!
I hope u have a great weekend.

Unga wa mchele glass 2 na nusu
Maziwa glass 2
Sukari vijiko 10 vya kulia
Iliki vijiko 2
Hamira vijiko 2
Yai 1

Jinsi ya kutayarisha
Changanya vitu vyote kwenye blender..
Saga kwa dkk 4-6
Mimina kwenye bakuli safi
Wacha viumuke na uchome.
Vitumbua tayari kwa kuliwa
 
Vitumbua Vya Mchele

85A4B6B6-600E-4188-A899-5838D89FADCE.jpeg
Mahitaji
Mchele ......2cups
Tui zito ......1cup
Ute wa yai ......1
Unga wa Sembe ...1 table spoon
Unga wa Ngano …1table spoon
Hamira.........…1 table spoon
Hiliki ..........1 table spoon
Sukari .......½ Cup

Jinsi Ya Kupika
Saga mchele na tui kwenye blender mpaka uwe laini uhakikishe hauna chenga hata kidogo tia yai, hamira na hiliki endelea kusaga. Tia sukari endelea kusaga na mwisho utatia unga wa ngano na wa sembe, saga tena kidogo toa weka kwenye bakuli, acha uumuke.

Ukishaumuka weka kwenye chuma cha vitumbua na uanze kuchoma kwa mafuta pole pole, mpaka uone vimebadilika rangi.
 
Jinsi Ya Kupika


Saga mchele na tuwi kwenye blender mpaka uwe laini uhakikishe hauna chenga hata kidogo tia yai, hamira na hiliki endelea kusaga tia sukari endelea kusaga na mwisho utatia unga wa ngano na wa sembe saga tena kidogo towa weka kwenye bakuli wacha uumuke.

Ukisha umuka teleka chuma cha vitumbuwa na uwanze kuchoma kwa mafuta pole pole, mpaka uone vimebadirika rangi.
Dakika ngapi kuumuka mkuu?
 
Salaaale,nnavyopenda vitumbua,kila siku najiuliza ntapata wapi unga wa mchele! kesho naenda kusaka chuma cha kuchomea! sasa baba, kwanini yai tunatia ute tu? mchele hauhitaji kulowekwa b4 blending?
Dakika 15 - 25 mkuu, na hata hivyo utaona tu unga ukija juu.
 
salaaale,nnavyopenda vitumbua,kila siku najiuliza ntapata wapi unga wa mchele! kesho naenda kusaka chuma cha kuchomea! sasa baba, kwanini yai tunatia ute tu? mchele hauhitaji kulowekwa b4 blending?
Mchele unaitajika kulowekwa mpaka uone umebadirika rangi na kuwa mweupe, almost 6hrs.

Kutia ute wa yai kunasaidia pia kwenye kuumuka na kushikana kwa unga.
 
Vitumbua (Aina Ya 1)

Vipimo

  • 1 Kikombe cha mchele.
  • 1 Kijiko cha kulia cha unga wa ngano.
  • 3/4-1 Kikombe cha tui la nazi zito.
  • 2 Mayai.
  • 1 Kijiko cha chai cha hamira.
  • 1/2- 3/4 kikombe cha sukari.
  • Iliki kiasi upendacho.

Naman Ya Kutayarisha Na Kupika

  1. Osha na kuroweka mchele ndani ya maji ya baridi masaa manane au siku moja.
  2. Mimina vifaa vyote ispokuwa sukari, ndani ya blender na usage mpaka mchele uwe umesagika kabisa.
  3. Mimina sukari ndani ya mchanganyiko na usage tena kidogo tu.
  4. Mimina mchanganyiko ndani ya bakuli na ufinike. Weka bakuli mahali penye joto ili mchanganyiko uuumuke.
  5. Mchanganyiko ukisha umuka, weka karai kwenye moto.
  6. Tumia kama kijiko 1-2 cha chai cha samli kwa kukaangia kila kitumbua.
    kuumuka ni kwa muda gani ndugu, na huko kuumuka ni bila amira amira?
 
Wapendwa..amani iwe juu yenu!!
I hope u have a great weekend.

Unga wa mchele glass 2 na nusu
Maziwa glass 2
Sukari vijiko 10 vya kulia
Iliki vijiko 2
Hamira vijiko 2
Yai 1

Jinsi ya kutayarisha
Changanya vitu vyote kwenye blender..
Saga kwa dkk 4-6
Mimina kwenye bakuli safi
Wacha viumuke na uchome.
Vitumbua tayari kwa kuliwa
 

Attachments

  • 1401546347954.jpg
    1401546347954.jpg
    47.2 KB · Views: 1,058
Mrs Kharusy hizi picha za misosi mingine humu zinafanya mtu kutoa order ya vitumbua lol!!!!! Mie vitafunio hivi viwili vitumbua na chapati navipenda sana kuliko vitafunio vingine vyovyote vile, sasa upate na mchuzi mzito wa kuku uliotiwa giligilani na vikolombwezo vingine na chai ya maziwa iliyotiwa hiliki weeee hahahahahah :):):)

Wapendwa..amani iwe juu yenu!!
I hope u have a great weekend.

Unga wa mchele glass 2 na nusu
Maziwa glass 2
Sukari vijiko 10 vya kulia
Iliki vijiko 2
Hamira vijiko 2
Yai 1

Jinsi ya kutayarisha
Changanya vitu vyote kwenye blender..
Saga kwa dkk 4-6
Mimina kwenye bakuli safi
Wacha viumuke na uchome.
Vitumbua tayari kwa kuliwa
 
Last edited by a moderator:
Mrs Kharusy hizi picha za misosi mingine humu zinafanya mtu kutoa order ya vitumbua lol!!!!! Mie vitafunio hivi viwili vitumbua na chapati navipenda sana kuliko vitafunio vingine vyovyote vile, sasa upate na mchuzi mzito wa kuku uliotiwa giligilani na vikolombwezo vingine na chai ya maziwa iliyotiwa hiliki weeee hahahahahah :):):)

Nipe order nikutengezee..lol
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: BAK

Similar Discussions

Back
Top Bottom