Vituko vya Raila..Jaza mwenyewe!!!

Ab-Titchaz

JF-Expert Member
Jan 30, 2008
14,631
4,225
Haya nduguzanguni, jamaa huyo kashakua mlokole eti!!!


news050509_03.jpg


Prime Minister Raila Odinga (centre) after being baptised by Prophet David Owuor (left), of the Ministry of Repentance and Holiness in Nairobi, on Monday.







 
hongera raila kwa kuchagua njia hii......!
imani uilinde ulete amani na uwe kioo kuwa UKRISTO SI CHUKI NA VISASI KAMA DINI NYINGINE bali ni misamaha, mapatano, amani na maendeleo...!
KEEP GOING......!
 
Kwani mtu huwa anaingia ukristo mara 2? Nadhani hii ni ukiukaji wa miongozo ninavyofahamu kubatizwa ni kuingizwa katika ukristo, ina maana alikuwa hajabatizwa kabla?
 
Wanasiasa wa kiafrica wanaona mbali, they will do anything to get what they want!! Naamini ni mapema sana kumpongeza Mh. Raila!

Ni mtizamo tu!!
 
Whether unampongeza or not...hii ni issue yake na Mungu wake. Swala la kuhusisha imani yake na kazi yake ya kisiasa ni upotoshaji.
 
Mapapa wa kuiba kura (Bwana Kibaki, Mikuki, etc.) wafuate nyayo.
 
Haya nduguzanguni, jamaa huyo kashakua mlokole eti!!!


news050509_03.jpg


Prime Minister Raila Odinga (centre) after being baptised by Prophet David Owuor (left), of the Ministry of Repentance and Holiness in Nairobi, on Monday.







Kwa nini unaita vituko? Mtu kuamua kumgeukia Mungu ni vituko? mbona tunakua negative sana kwa wayafanyao wengine?

Nina amini kuwa mtu yeyote anaweza mgeukia Mungu atakapoijua kweli. Huyu jamaa alikua mkristo asiyeeleweka na ndio mana alikua anaweka hata mafungamano na watu fulani wakati wa kugombea urais kwa lengo la kutetea imani zao. Nina amini amekutana na kweli na ameamua kuifuata. Tumuombee kua asonge mbele na amaanishe alichoamua kukifuta. Yeye siyo kiongozi wa kwanza kuyafanya haya. Kule malawi raisi alikubali kubatizwa na kumgeukia Mungu baada ya kuona uchawi wa ajabu ulikua ikulu. Kule Zambia pia, raisi aliyefariki mwaka jana alimgeukia Mungu na alisimama katika zamu yake vizuri zaidi.

Hata Raila damu ya Yesu ilimwagika kwa ajili yake na anaweza kubadilishwa. Mungu msaidie kiongozi huyu asonge mbele kwa imani akiyaacha yaliyopita na kusonga mbele katika mwenendo mpya. Hata kama kaokoka kwa hila, basi akutane na nguvu ya wokovu itakayoibadilisha hila yake kuwa sababu ya ukombozi.

Glory to you Jesus
 
Mind you, wanasiasa ni watu wajanja sana. Nadhani hata wewe pia umeweka wasiwasi kuwa huenda ameokoka kwa hila. Je alikuwa hawezi kutenda matendo mema akiwa kwenye dhehebu lake la awali? Kuokoka ni matendo.
 
Big up Hr Raila,
that is right decision for human been who living under the sun,

Songa mbele kwa uamnifu Bwana atakutetea kwa kuwa umekuwa miongoni mwa familia ya Mungu mwenyewe,na mamlaka ya nchi mungu anapenda kuwa chini ya mtu mwenye kumjuwa.
 
Mind you, wanasiasa ni watu wajanja sana. Nadhani hata wewe pia umeweka wasiwasi kuwa huenda ameokoka kwa hila. Je alikuwa hawezi kutenda matendo mema akiwa kwenye dhehebu lake la awali? Kuokoka ni matendo.
sina hakika unasoma biblia ipi inayosema kuokoka ni matendo...ila ninayosoma mimi inasema mwanadamu haokolewi kwa matendo ya sheria (dos and donts)...anaokolewa kwa neema kwa imani katika Kristo Yesu....mimi sijaongelea swala la dhehebbu wala sijui alikua ana dhehebu gani.....ninachokiona cha msingi ni kuwa kaamua kumgeukia Yesu...kama ameamua kuhama alipokua anasali (iwapo alikau nako) anajua yeye ni kwa nini na huenda hapakumasaidia kumjua Mungu. ana haki kabisa ya ku-renew maisha yake. mara nyingine inatulazimu kuhama tulipokuwepo ili mabadiliko yetu yawe dhahiri na tupate malisho ya kutuwezesha kukua katika imani....

Kuhusu kuokoka kwa hila, nataka tu nikujulishe kuwa wako wengi walioingia kwenye wokovu kwa sababu fulani na sio kwa misingi ya kuishi sawasawa na mapenzi ya Mungu...na walipoingia tu, Mungu aliwakamatia humohumo na wakabadilishwa mtazamo wao wa awali....kwa uapnde wangu, sioni chochote cha kisiasa kwa maamuzi ya Odinga kuokoka...tena ninapotazama jina la ministry/dhehebu alilokwenda, sioni kama ni dhehebu lenye ushawishi wowote kwa wakenya....

Ni tabia mbaya kuangalia imani za wengine katika mtazamo negative. tunasimama kwenye nafasi za Mungu kuwa wahukumu wa yaliyo ndani ya mioyo ya watu ambayo hatuyajui....ni bora tungejihukumu sisi kwanza.....pia kumbuka hutapata dhambi iwapo utamfikiria mtu mema ingawa yeye amekusudia mabaya, ila ni dhambi kumkusudia mtu mabaya wakati yeye amakusudia mema au hata kama amekusudia mabaya. Tuwe na nia ya Kristi ndani yetu...Alituona tunafaaa ingawa tulikua katika hali ya dhambi na kupotea akajitoa kwa ajili yetu. Huwezi kumsaida mwingine kumjua Mungu na kumuombea iwapo unamuawazia mabaya.

Asante Bwana Yesu kwa kumuokoa Odinga. Tunaomba UMUOKOE NA ROSTAM AZIZ, SOMAIYA, JEETU, LOWASA NA WENGINE WOTE AMBAO KATIKA MACHO YA WANADAMU WANAONEKANA KUWA HAWAFAI TENA. WAPE TOBA YA KWELI NA WAUNGAME JUU YA NCHI WALIYOIKOSEA NA KWA RAIA WAKE.

Najua bado unawapenda sana na kwa vile bado wanaishi, basi unawapa nafasi nyingine ya kutafakari njia zao na kubadilisha maisha yao. waoenshe kuwa bila wewe hawatafika popote.

Liokoe taifa letu na uiponye nchi yetu
 
Mind you, wanasiasa ni watu wajanja sana. Nadhani hata wewe pia umeweka wasiwasi kuwa huenda ameokoka kwa hila. Je alikuwa hawezi kutenda matendo mema akiwa kwenye dhehebu lake la awali? Kuokoka ni matendo.
sina hakika unasoma biblia ipi inayosema kuokoka ni matendo...ila ninayosoma mimi inasema mwanadamu haokolewi kwa matendo ya sheria (dos and donts)...anaokolewa kwa neema kwa imani katika Kristo Yesu....mimi sijaongelea swala la dhehebbu wala sijui alikua ana dhehebu gani.....ninachokiona cha msingi ni kuwa kaamua kumgeukia Yesu...kama ameamua kuhama alipokua anasali (iwapo alikau nako) anajua yeye ni kwa nini na huenda hapakumasaidia kumjua Mungu. ana haki kabisa ya ku-renew maisha yake. mara nyingine inatulazimu kuhama tulipokuwepo ili mabadiliko yetu yawe dhahiri na tupate malisho ya kutuwezesha kukua katika imani....

Kuhusu kuokoka kwa hila, nataka tu nikujulishe kuwa wako wengi walioingia kwenye wokovu kwa sababu fulani na sio kwa misingi ya kuishi sawasawa na mapenzi ya Mungu...na walipoingia tu, Mungu aliwakamatia humohumo na wakabadilishwa mtazamo wao wa awali....kwa uapnde wangu, sioni chochote cha kisiasa kwa maamuzi ya Odinga kuokoka...tena ninapotazama jina la ministry/dhehebu alilokwenda, sioni kama ni dhehebu lenye ushawishi wowote kwa wakenya....

Ni tabia mbaya kuangalia imani za wengine katika mtazamo negative. tunasimama kwenye nafasi za Mungu kuwa wahukumu wa yaliyo ndani ya mioyo ya watu ambayo hatuyajui....ni bora tungejihukumu sisi kwanza.....pia kumbuka hutapata dhambi iwapo utamfikiria mtu mema ingawa yeye amekusudia mabaya, ila ni dhambi kumkusudia mtu mabaya wakati yeye amakusudia mema au hata kama amekusudia mabaya. Tuwe na nia ya Kristi ndani yetu...Alituona tunafaaa ingawa tulikua katika hali ya dhambi na kupotea akajitoa kwa ajili yetu. Huwezi kumsaida mwingine kumjua Mungu na kumuombea iwapo unamuawazia mabaya.

Asante Bwana Yesu kwa kumuokoa Odinga. Tunaomba UMUOKOE NA ROSTAM AZIZ, SOMAIYA, JEETU, LOWASA NA WENGINE WOTE AMBAO KATIKA MACHO YA WANADAMU WANAONEKANA KUWA HAWAFAI TENA. WAPE TOBA YA KWELI NA WAUNGAME JUU YA NCHI WALIYOIKOSEA NA KWA RAIA WAKE.

Najua bado unawapenda sana na kwa vile bado wanaishi, basi unawapa nafasi nyingine ya kutafakari njia zao na kubadilisha maisha yao. waoenshe kuwa bila wewe hawatafika popote.

Liokoe taifa letu na uiponye nchi yetu
 
hivi siyo vituko kwani mtu kuamua kumrudia Mungu wake na kutubu dhambi zake ni vituko jamani.
nampongezza sana amechukua uamuzi wa busara na amechagua lililo jema, kuanzi sasa Mungu atampigania kwenye kila jambo, anacontrol kila kitu kwenye maisha yake kuanzi sasa, asome neno, alishike na alitende
 
Hili ni suala binafsi halina uhusiano wowote na utendaji wake wa kisiasa.....ingawa tunaamini atakuwa safi na kutenda haki.....maana anafuata haki na anasimama kwenye neno....la Mungu.hongera sana Raila,maana unaokoa nafsi yako.
 
hongera raila kwa kuchagua njia hii......!
imani uilinde ulete amani na uwe kioo kuwa UKRISTO SI CHUKI NA VISASI KAMA DINI NYINGINE bali ni misamaha, mapatano, amani na maendeleo...!
KEEP GOING......!

Tafadhali onyesha moyo wa Kikristo, usihukumu. Tabia ya ukristo wako iwe mfan wa kuigwa na hata wale wenye imani zingine, ili nao waone utukufu wa imani yako kama ulivyosema kuwa Ukristo ni kuwa na misamaha, mapatano, amani na maendeleo. Mimi naongelea pia ni kuwa na upendo.
 
Big up Kosamfe, utanijuaje kuwa nimeokoka? Kwa kuwa muumini wa kadhehebu fulani? Hapana, angalia matendo yangu, Petro alijaribu kumsaliti Yesu lakini matendo yalimsuta, sio kadhehebu...
 
Back
Top Bottom