Kiby
JF-Expert Member
- Nov 16, 2009
- 6,899
- 4,623
Mawazo yangu nilikuwa nafikiri maandamano ni mpaka yapangwe na kutangazwa siku ndio yafanyike, kumbe sivyo.
Jana wanafunzi wa shule mbili za msingi wilayani Temeka waliandamana , wakitaka kupeleka kilio chao ikilu. Hii ni baada ya wenzao wawili kugongwa na pikipiki na gari hapo jana. Walikuwa wakiimba peoples power na kuitikiwa na wenzao mpaka kieleweke, tunataka matuta. Achilia mbali wabongo tunachofahamu ni matuta barabarani kupunguza speed ya magari tofauti na nchi za wenzetu wanaajiri watu maalumu katika vivuko vya mashule ama wanajenga madaraja ya juu ama ya under ground, hapa kwetu hata hilo la matuta halitekelezeki. Kilichonifurahisha sana kwenye hii habari ni pale kuona gazeti la majira limetoa picha ya police wakiwa wamewashikilia vitoto vitatu kuvipeleka kwenye karandinga eti hao ndio vinara wa maandamano. Tanzania tunaelekea wapi?
Natumia simu siwezi rusha picha iliyopo katika gazeti la majira, naomba yeyote atusaidie kuiweka hiyo picha hapa maana ndio utamu wenyewe.
.
Jana wanafunzi wa shule mbili za msingi wilayani Temeka waliandamana , wakitaka kupeleka kilio chao ikilu. Hii ni baada ya wenzao wawili kugongwa na pikipiki na gari hapo jana. Walikuwa wakiimba peoples power na kuitikiwa na wenzao mpaka kieleweke, tunataka matuta. Achilia mbali wabongo tunachofahamu ni matuta barabarani kupunguza speed ya magari tofauti na nchi za wenzetu wanaajiri watu maalumu katika vivuko vya mashule ama wanajenga madaraja ya juu ama ya under ground, hapa kwetu hata hilo la matuta halitekelezeki. Kilichonifurahisha sana kwenye hii habari ni pale kuona gazeti la majira limetoa picha ya police wakiwa wamewashikilia vitoto vitatu kuvipeleka kwenye karandinga eti hao ndio vinara wa maandamano. Tanzania tunaelekea wapi?
Natumia simu siwezi rusha picha iliyopo katika gazeti la majira, naomba yeyote atusaidie kuiweka hiyo picha hapa maana ndio utamu wenyewe.
.