MAMA POROJO
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 4,976
- 784
Mbinu chafu za serikali zashindikana Mwanza, idadi kubwa ya wananchi wa jiji la Mwanza jana walienda uwanjani kusikiliza sera za CHADEMA baada ya jeshi la polisi kuwarushia raia mabomu 8 yaliyojeruhi baadhi ya raia. Mbinu hii ambayo pia itatumika siku ya uchanguzi kuzuia raia kwa vitisho kutoka majumbani kwao kupiga kura, imekuwa ikiandaliwa kwa muda mrefu sasa, ambapo mafunzo ya kutoa vitisho, na kununua vifaa, magari aina mbalimbali ya zana za kivita yakiwa ni maandalizi ya vitisho vitavyotawala siku ya jumapili ya tarehe 31/10/2010.
Serikali sasa inawaza ifanye nini baada ya jaribio lao la jana kugonga mwamba, baada ya kipigo walichopigwa raia kwa mabomu wamebaki wakishangaa ujasiri walio nao hawa watu wanapigwa lakini hawakubali kurudi nyuma.
CHADEMA wanarushiwa mabomu, lakini hawakurudi nyuma, wamemfuata kamanda wao SLAA
CCM bila pesa, khanga, malori kamanda wao hapati mtu.
JUMAPILI ni mbele kwa mbele Watanzania mabomu, risasi zitalia lakini hakikisha unapiga kura yako kwa CHADEMA