Balantanda
JF-Expert Member
- Jul 13, 2008
- 12,476
- 4,754
HALMASHAURI Kuu ya Taifa ya CCM imesema kuanzia sasa ukomo wa viti maalumu vya ubunge, uwakilishi na udiwani ni vipindi viwili, baada ya hapo watatakiwa kwenda majimboni kugombea.
Uamuzi huo ulitangazwa jana mjini hapa na Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama katika Mkutano wa Baraza Kuu la Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT), katika makao makuu ya CCM. Kuanzia sasa wanaojiona wametumikia vipindi viwili, ifikapo uchaguzi mkuu wa 2015 waanze kujiandaa kwenda majimboni kugombea, alisema.
Aliongeza kuwa, NEC imefikia kuwa na ukomo katika uongozi wa viti maalumu kutokana na uamuzi wa Baraza Kuu la UWT katika mkutano wake uliopita. Mukama alisema uamuzi huo ni mzuri, kwani wabunge wanapotumikia vipindi viwili, tayari wanakuwa na ujasiri, uzoefu na wanaweza kusimama majimboni kugombea.
Watakuwa na uzoefu ni vizuri wakasimama majimboni kugombea au kufanya kazi za kuimarisha chama, alisema.
Mukama alisema hata hivyo, Kamati ya Wabunge wa CCM ilikataa uamuzi huo na kutaka utazamwe upya na akaurudisha Baraza Kuu la Wanawake ili waujadili tena. Baada ya kauli hiyo, wajumbe wa mkutano huo walipiga kelele wakisema uamuzi huo ni msimamo wao na hawataubadilisha.
Hapana hatutaki na sisi tunataka iwe vivyo hivyo wakagombee majimboni, walisema baadhi ya wajumbe ambao walimfanya Mukama kusitisha kuzungumza hadi walipomaliza kauli zao.
Aidha, Mukama alisema wakati umefika kwa UWT kutumia vitegauchumi walivyonavyo ili kuwa na ufanisi. Alisema ni muhimu wakawa na mipango ya mapema kuendeleza viwanja vya UWT kwani ni rasilimali yenye thamani kubwa kwa sasa.
Tuimarishe mali tulizonazo, tuhakikishe zinakuwa na hati, hasa ardhi zikiwa na hati ni vizuri zaidi, alisema na kuongeza: Huwezi kuendesha uongozi bila kuwa na timu ya wanawake kwani hata kwenye familia mama asipokuwa imara familia itayumba na watoto watahangaika.
Awali, Mwenyekiti wa UWT, Sofia Simba, alisema mkutano huo una mambo mazito ya kuzungumza kutokana na kuwa kwenye maandalizi ya uchaguzi na ya mabadiliko ya Katiba na tayari kuwa vikundi vimeanza kupitapita kupotosha.
Alisema wapinzani wana mbinu nyingi, kwani wanapandikiza maneno na mtu kuonekana wa CCM kumbe wamempandikiza kwani wanatafuta mbinu ya kutuvuruga. Tuwe makini na wapinzani kwani wanaweza kutuletea mapandikizi, alisema.
Chanzo: Gazeti la Habari Leo
Uamuzi huo ulitangazwa jana mjini hapa na Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama katika Mkutano wa Baraza Kuu la Jumuiya ya Wanawake Tanzania (UWT), katika makao makuu ya CCM. Kuanzia sasa wanaojiona wametumikia vipindi viwili, ifikapo uchaguzi mkuu wa 2015 waanze kujiandaa kwenda majimboni kugombea, alisema.
Aliongeza kuwa, NEC imefikia kuwa na ukomo katika uongozi wa viti maalumu kutokana na uamuzi wa Baraza Kuu la UWT katika mkutano wake uliopita. Mukama alisema uamuzi huo ni mzuri, kwani wabunge wanapotumikia vipindi viwili, tayari wanakuwa na ujasiri, uzoefu na wanaweza kusimama majimboni kugombea.
Watakuwa na uzoefu ni vizuri wakasimama majimboni kugombea au kufanya kazi za kuimarisha chama, alisema.
Mukama alisema hata hivyo, Kamati ya Wabunge wa CCM ilikataa uamuzi huo na kutaka utazamwe upya na akaurudisha Baraza Kuu la Wanawake ili waujadili tena. Baada ya kauli hiyo, wajumbe wa mkutano huo walipiga kelele wakisema uamuzi huo ni msimamo wao na hawataubadilisha.
Hapana hatutaki na sisi tunataka iwe vivyo hivyo wakagombee majimboni, walisema baadhi ya wajumbe ambao walimfanya Mukama kusitisha kuzungumza hadi walipomaliza kauli zao.
Aidha, Mukama alisema wakati umefika kwa UWT kutumia vitegauchumi walivyonavyo ili kuwa na ufanisi. Alisema ni muhimu wakawa na mipango ya mapema kuendeleza viwanja vya UWT kwani ni rasilimali yenye thamani kubwa kwa sasa.
Tuimarishe mali tulizonazo, tuhakikishe zinakuwa na hati, hasa ardhi zikiwa na hati ni vizuri zaidi, alisema na kuongeza: Huwezi kuendesha uongozi bila kuwa na timu ya wanawake kwani hata kwenye familia mama asipokuwa imara familia itayumba na watoto watahangaika.
Awali, Mwenyekiti wa UWT, Sofia Simba, alisema mkutano huo una mambo mazito ya kuzungumza kutokana na kuwa kwenye maandalizi ya uchaguzi na ya mabadiliko ya Katiba na tayari kuwa vikundi vimeanza kupitapita kupotosha.
Alisema wapinzani wana mbinu nyingi, kwani wanapandikiza maneno na mtu kuonekana wa CCM kumbe wamempandikiza kwani wanatafuta mbinu ya kutuvuruga. Tuwe makini na wapinzani kwani wanaweza kutuletea mapandikizi, alisema.
Chanzo: Gazeti la Habari Leo