Vitambulisho vya Taifa vyakamilika!

Michael Amon

JF-Expert Member
Dec 22, 2008
8,775
3,610
kitambulisho.jpg


Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), imesema awamu ya kwanza ya Vitambulisho vya Taifa imekamilika na vitaanza kutolewa mapema mwezi ujao (May).

Imesema kuwa uzinduzi wa kutoa vitambulisho hivyo ulikuwa ufanyike jana katika maadhimisho ya sherehe za miaka 48 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, lakini ilishindikana kutokana na shughuli nyingi na ukubwa wa tukio hilo.

Ofisa Habari wa NIDA, Rose Mdami alisema uzinduzi huo unatarajiwa kufanywa na Rais Jakaya Kikwete ambapo wiki ijayo watazungumza na waandishi wa habari na kuelezea utaratibu mzima utakavyokuwa.

Katika utekelezaji wa mradi huo, Mamlaka itatoa vitambulisho katika makundi matatu; Watanzania, wageni wakazi na wakimbizi.

Alisema baada ya wafanyakazi wa Serikali, watafuatiwa wanafunzi, wafanyabiashara na hatimaye Watanzania wote watafikiwa na huduma hiyo muhimu kwa Taifa bila gharama yoyote.

Hata hivyo, imeelezwa kuwa, pamoja na kuwa huduma hiyo ni bure, lakini mwananchi atakayepoteza kitambulisho chake atalazimika kukilipia.
 
China wanavyo hivi.. nakumbuka nilikuwa train station! polisi anakuwa pale anapita randomly ku scan .. kina info zako zote!!! kama ni wanted man imekula kwako... kama haunacho ule muda imekula kwako... sijui hivi navyo itakuwa hivo... !
 
China wanavyo hivi.. nakumbuka nilikuwa train station! polisi anakuwa pale anapita randomly ku scan .. kina info zako zote!!! kama ni wanted man imekula kwako... kama haunacho ule muda imekula kwako... sijui hivi navyo itakuwa hivo... !

Duh! Lets hope itakuwa hivyo.
 
Lakini Mi ningependa sana kila Mtanzania angekuwa nayo kwn ingependeza sana!

kweli mkuu wenzetu zambia wanavyo tokea zamani wakati huo sisi tunatumia vya ccm vilikua vinatolewa na wenyeviti wa vijiji kama sikosei.!
 
Dah, sasa me nikajua nivizuri zaidi, mbona inaonekana sio Digitally hivi nikama vya wagambo au vya kupigia Kura, ndo nini sasa mpaka Wanyasa wanavyo.
 
Dah, sasa me nikajua ni vizuri zaidi, mbona inaonekana sio Digitally hivi nikama vya wagambo au vya kupigia Kura, ndo nini sasa mpaka Wanyasa wanavyo.
Hivi si kama vya Kura, hivi vina Chip kama vile ATM ambayo itakua na info zako zote.
 
mie nabeba kinachonipa mkate hivi vya kwenu ym...hongereni hatimaye mmefanikiwa
 
Back
Top Bottom