Vitabu vya Willy Gamba (Elvis Musiba)

mi nimesoma vitabu vyote vya james hadley chase na erle stanley gardner. Nimesoma pia vitabu vya musiba. Kwa kifupi sidhani kam vitabu vya chase vinafanana hata kidogo na vya musiba. Chase ni 3w- women, wealth and wine. Vitabu vyote vya chase vinafanana. Mwanamke mzuri anasababisha mtu afanye mambo ya kipuuzi ikiwepo kuiba pesa na mwisho anakamatwa. Willy gamba ni tofauti vitabu vyote ni kuhusus hujuma ya mabeberu wa kimagharibi.sidhani kama anaiga hata kidogo, ila kuna jambo muhimu moja. Ukiwa unasoma vitabu vingi unajikuta unakuwa mkosoaji sana wa vitabu na iyo ndo njia inaweza kukufanya kuandika vizuri au kuwa na mawazo mapana. Kwa mfano tanzania nani mtunzi mzuri kati ya musiba, mtobwa au shingongo? Ntampa asilimia kubwa musiba kwa kuwa anjua namna ya kuvutia msomaji kila mara awe anajikuta ameingia kimawazo, mtobwa na joram kiango wake kwa kiasi anajitahidi ila ana tatizo moja la kuchanganya mambo mengi. Kuhusus shingongo, kwanza hana kipaji cha kuandika, analazimisha uku akisaidiwa na majarida yake, ila upeo wake ni mdogo wa ubunifu, na watu wataofurahia uandishi wake hawajasoma vitabu vya waandishi wazuri kama grisham. Shingongo ana tabia ya uandishi wa kuandika maneno mengi akifikiri kuandika sana ndo uzuri ila hawezi kuunganisha matukio kwa njia itakayo vutia msomaji
hapo jyfranca umenikumbusha uhondoo wa grisham ana novel inaitwa the client hakika ilinifurahisha mno
 
Jamani hizo hadithi za Willy Gamba nilikuwa nasafiri kijiji kilomita 20 nikiambiwa mtua anacho...naazima kwa siku mbili....hata kula inakuwa napoteza muda. Nakumbuka mama alituma kwenda kuchota maji nikawa naendelea kuchapa novel, duh alikishika akakichanachana....nililia kinoma mpaka akashangaa lidume la darasa la sita linalia hivyo! aliona huruma mpaka kasafiri kwenda kuniombea masamaha kwa niliyemuazima.

Ule uandishi wa Elvis ulikuwa kiboko!
 
Kweli nyinyi vijana wa zamani...vijana wa sasa tunavutiwa na series zilizotungwa kwa kutumia akili nyingi kama 24 Hrs,The Unit,Lost,Prison Break N.K Ninapotizama filamu hizi usingizi uniruka na ujikuta nina uwezo wa kukaa mbele ya "kideo" hata kwa zaid ya masaa 20
 
Navyo jua mimi hivyo vitabu vilipigwa marufuku na serikali kwasababu vilielekea kuwaharibu kisaikolojia vijana wa taifa hili,maana vijana walivisoma wakapandwa na mizuka! wakataka kuiga yanayoelezwa mule vitabuni,vikapigwa marufuku ndo maana havionekani,hata mie enzi hizo nilikuwa bado kinda lakini nimesikia historia kuhusu hivyo vitabu nilipojaribu kuvitafuta nakaambiwa vilizuiliwa.
 
hakika msiba kwa enz yetu alikuwa mtunz alie vuta hisia mi ni mmoja wa watu walioshndwa kufanya mengne kwa kuvnj ratba zingne il nisome hivyo vtb kabla muda nilopewa kwisha.nilibahatka kusoma vingi na ksha nilipata kununua viwil niko navyo hata leo sijathubtu kuuza ila kwa wale ninaowafahamu huwa nawaazma kuna NJAMA NA HOFU.Vngnd nilvysoma ni k.k kikomo nk malazote mpelelez maalfu wa afrk wily gamb hurudi na ushndi ktk mazngra magumu.(RIP a.e.musiba)
 
wakuu naombeni msaada wenu kama kuna anayejua ninakoweza kupata hivi vitabu ya Elvis Musiba, vikiwa na stellingi Willy Gamba.

Vitabu hivyo ni kama vile:
1.Kikosi cha Kisasi
2.Kufa na Kupona
3.Hofu.
4.Njama
5.Uchu

na vinginevyo. nimevisoma baadhi zamani lakini sasa hivi sina nakala tena ningependa kujua ninakoweza kuvipata.

shukrani!

Mzee Elvis Musiba kafariki mwishoni mwa 2011, nilikua naishi na mjuu wake geto moja akati twasaka kazi. Hivyo nilipata hata kuhudhulia msiba hata kusafirishwa kwa mazishi.
 
Kweli nyinyi vijana wa zamani...vijana wa sasa tunavutiwa na series zilizotungwa kwa kutumia akili nyingi kama 24 Hrs,The Unit,Lost,Prison Break N.K Ninapotizama filamu hizi usingizi uniruka na ujikuta nina uwezo wa kukaa mbele ya "kideo" hata kwa zaid ya masaa 20

ndg yangu na mimi,ni kijana wa sasa lkn mzee kwenye shelf yake ya vitabu nilikuta vitabu hivyo 2005 cha njama na kufa na kupona,ukisoma huo upelelezi wa humo kwenye hivyo vitabu.Basi yaani kama Musiba angekuwa marekani na Jack Bauer yuko bongo.Tungesema 24 wamegandamizia kwenye hivyo vitabu kunaupelezi wa hatari acha wa Jack Bauer!...
 
ndg yangu na mimi,ni kijana wa sasa lkn mzee kwenye shelf yake ya vitabu nilikuta vitabu hivyo 2005 cha njama na kufa na kupona,ukisoma huo upelelezi wa humo kwenye hivyo vitabu.Basi yaani kama Musiba angekuwa marekani na Jack Bauer yuko bongo.Tungesema 24 wamegandamizia kwenye hivyo vitabu kunaupelezi wa hatari acha wa Jack Bauer!...

Bora umeliona hili watunzi wengi wanajikuta wanagongana idea kutokana na ukweli kwamba wote wanazungumzia mambo yanayotokea duniani hapa hapa namanisha hakuna jipya nashangazwa na watu kumsema bwana msiba anacopy kisa tu kajisehemu kadogo tu kumatch na hadith za watu wa mbele.
 
ndg yangu na mimi,ni kijana wa sasa lkn mzee kwenye shelf yake ya vitabu nilikuta vitabu hivyo 2005 cha njama na kufa na kupona,ukisoma huo upelelezi wa humo kwenye hivyo vitabu.Basi yaani kama Musiba angekuwa marekani na Jack Bauer yuko bongo.Tungesema 24 wamegandamizia kwenye hivyo vitabu kunaupelezi wa hatari acha wa Jack Bauer!...


Kwanza kabisa RIP mzee MUSIBA.

Mkuu umenena vema.....kama ukisoma vitabu vya watuzni wetu wa enzi za mwalimu ....

Bwanaee walikuwa wakali mno!! dah naweza kukubaliana na wewe 100% ilikuwa ukikishika kitabu kile basi siku hiyo ni balaa ....na korobai mafuta ..unapangiwa ...basi unatamani kuche uanze hekaheka za Wlly...

Lakini nadhani baadhi ya vijana wasiku hizi sio wadadisi mie kijana wangu mmoja anamiaka 18 nilimpa asome vitabu viwili tu..... lkn keshasoma vinne hadi sasa vingine katafuta mwenyewe!!
 
mwenye hivi vitabu aniazime
salam toka kuzimu
Tumerudi na roho zetu
Nilikuwa nikisome naona kama kweli vile
 
Mkuu, kama kweli unaweza kuvipata vitabu hivi please tuwasiliane, Kikosi cha Kisasi, Kikomo, Kufa na Kupona, na Njama. Au nielekeze vizuri kwa jamaa na mawasiliano yake ni mpigie nivipate hivyo vitabu kaka!

Aristablus Elvis Musiba ni marehemu
 
Mwandika vitabu pekee ambaye alikuwa akinakili neno kwa neno, ni yule aliyekuwa akitumia jina la ... J. M S. Simbamwene.
 
Back
Top Bottom