MwanajamiiOne
Platinum Member
- Jul 24, 2008
- 10,470
- 6,562
hapo nakuunga mguuu mkuuu Hussein Chuwa anafata nyayo za akina Musiba na Kiango nimekisoma hicho kitabu kizuri sana , jamaniiiii shigongo anabore na hadithi zake zinazofanana na picha za kinigeria na kisha kujirudiarudia nilikuwa mpenzi wa hadithi zake lakini baada ya kusoma nne tu nikajua jamaaa amefulia huyuuuuu mpaka leo sijagusa hata moja maana naona uzushi tu bora niangalie 24hrs kuliko kuangalia tafsiri za movie za kinigeria
Hiki cha Hussein ni kile chenye msichana mwenye jina gumu sijui alikuwa akiitwa Tiganini sijui ? alikuwa anafanya kazi kwenye makumbusho sijui au siyo huyo? Wenzie waliuliwa walipokwenda field na yeye peke yake akabakia akiwa na mkanda unaoonyesha mauaji yalivyofanyika mle msituni? Kama ni hicho nakubaliana nanyi ni kizuri nilifanikiwa kukisoma kwa siku mbili kwani utamu wake haukuruhusu nikiweke chini kivivu!