Vitabu vya Willy Gamba (Elvis Musiba)

hapo nakuunga mguuu mkuuu Hussein Chuwa anafata nyayo za akina Musiba na Kiango nimekisoma hicho kitabu kizuri sana , jamaniiiii shigongo anabore na hadithi zake zinazofanana na picha za kinigeria na kisha kujirudiarudia nilikuwa mpenzi wa hadithi zake lakini baada ya kusoma nne tu nikajua jamaaa amefulia huyuuuuu mpaka leo sijagusa hata moja maana naona uzushi tu bora niangalie 24hrs kuliko kuangalia tafsiri za movie za kinigeria

Hiki cha Hussein ni kile chenye msichana mwenye jina gumu sijui alikuwa akiitwa Tiganini sijui ? alikuwa anafanya kazi kwenye makumbusho sijui au siyo huyo? Wenzie waliuliwa walipokwenda field na yeye peke yake akabakia akiwa na mkanda unaoonyesha mauaji yalivyofanyika mle msituni? Kama ni hicho nakubaliana nanyi ni kizuri nilifanikiwa kukisoma kwa siku mbili kwani utamu wake haukuruhusu nikiweke chini kivivu!
 
Nakumbuka shambulio lilofanyika pale Butiama hotel shinyanga, nakumbuka kuna mtu alikuwa anaitwa Skazwe, nakumbuka kuna mtu alikua anaitwa Kabwe makanika au Jitu kumbuka, nakumbuka kuna dada alikua anaitwa Amanda si mchezo kabisa bila kumsahau Inspector wa Polisi, nakumbuka ile ajari ambapo treni iligonga gari ambalo Gmaba alikuwa amekodi kisha yule mtu akalipwa toka serikalini. vile vitabu havisahauliki.ila kwa ufupi mmiliki wa vitabu vile sijui sio mjasiliamali? kwa sababu akivirudisha kwenye market vitalipa sana.

Kabwe Makanika alikuwa ni Zahir Ally Baba yake Banana Zorroh, mzee wa Ma- POUDAAA!!
Sikulaumu mzee ni sikunyingi mno! na vichwa navyo huwa vinapata kutu...sometimes!

Bwana wee, enzi hizo, enzi za mwalimu Daftari likiisha Mwalimu analichana kidogo unapewa jipyaa!! Mshahara wa mwalimu wa shule ya msingi ulikuwa unatosha kulisha familia ya watu kumi na zaidi tena misosi yanguvu na maziwa ya B&B!!......
....Hebu mwalimu ajaribu sasa hivi hata kukaa na watu wanne tu, wataugua utapiamlo, na vitovu kugusa migingo!!
 
Nadhani wote mli koment humu ni watu wa nje.huyu mtunzi alifariki dunia nadhani mwaka jana
mkuuu hiyo sentensi yako ni nzito sasa tunaomba usidhani ila uwe na uhakikaaaaaaaaaaa na source utupe kwasababu huyo ni mtu anayependwa na watu wengi , kwangu mimi haingiii akilini afe kisha isitangazwe na tusijueee na karne yetu hiii ya mitandao sembuse amekufa Nasma Hamisi Kidogo tu watu wote tumejua wapenzi na wasio wapenzi wake sembuse kubwa la makachero??????
 
Nadhani wote mli koment humu ni watu wa nje.huyu mtunzi alifariki dunia nadhani mwaka jana
mkuuu hiyo sentensi yako ni nzito sasa tunaomba usidhani ila uwe na uhakikaaaaaaaaaaa na source utupe kwasababu huyo ni mtu anayependwa na watu wengi , kwangu mimi haingiii akilini afe kisha isitangazwe na tusijueee na karne yetu hiii ya mitandao sembuse amekufa Nasma Hamisi Kidogo tu watu wote tumejua wapenzi na wasio wapenzi wake sembuse kubwa la makachero??????
 
hapo nakukubali mkuuu mie nilikuwa obsessed na Gamba hadi nikawa na ndoto za kuwa mpelelezi nikiwa mkubwa nikaanza mpaka mazoezi ya kareti......... hahahaha nilivyokuwa mkubwa nikagundua hata kujipeleleza mwenyewe siwezi..

Du ebwana nimecheka sana,maana watu wengi baada ya kusoma vitabu vya willy Gamba walijiona na wao wanaweza kuwa wapelelezi siku za usoni ..du si mchezo,namkumbuka rafiki yangu enzi za o level Mwanza sec,alijiona ashakuwa kama willy gamba.
 
Nakumbuka shambulio lilofanyika pale Butiama hotel shinyanga, nakumbuka kuna mtu alikuwa anaitwa Skazwe, nakumbuka kuna mtu alikua anaitwa Kabwe makanika au Jitu kumbuka, nakumbuka kuna dada alikua anaitwa Amanda si mchezo kabisa bila kumsahau Inspector wa Polisi, nakumbuka ile ajari ambapo treni iligonga gari ambalo Gmaba alikuwa amekodi kisha yule mtu akalipwa toka serikalini. vile vitabu havisahauliki.ila kwa ufupi mmiliki wa vitabu vile sijui sio mjasiliamali? kwa sababu akivirudisha kwenye market vitalipa sana.
Inaonekana unakumbuka kinyumenyume,huyo kabwe makanika hakuwepo kwenye kikomo,labda unamzungumzia pweke au Elungata.
 
Hakika vilikuwa vitabu vizuri sana vya kipelelezi.

Nilikipenda sana Kikosi cha kisasi ( Gamba, Robert, Ozu na kofi bila kumsahau Mwadi na TETE, huku kuna muteba na papa.

Vile vile NJAMA ambako kuna Gamba, Sharif, Veronika ,Edi na zawadi.

Vile vile kuna KIKOMO, ambacho kilichezewa kule mwanza na shinyanga maeneo ya maganzo.

Vitabu ni vizuri saaaaaaaaaaaaaana
 
Hahaha! mimi nilivutiwa zaidi na Njama, si mnakumbuka kile kikundi kilichokuwa kinajiita KULFURT au GONGO LA CHUMA, kilikuwa na wakala wake Nairobi na Arusha, siwezi sahau kikosi cha kisasi kilivyo sambaratisha wale mawakala wa makaburu waliokuwa wanamiliki magereji makubwa kule Zaire (sasa Congo), aah masikini Kofi aliuwawa! lakni nakumbuka Willy Gamba alivyokuwa makali wa watoto! alimuanza tete kwa kumuambia 'sango nini" hahah tete alijibu "malamu" aaaha enzi hizo bwana. lakini hata Joram Kiango alikuwa mkali mnakumbuka story kama Tutarudi na Roho zetu, Malaika wa Shetani!
 
Hivi na yule mtunzi aliyekuwa akitunga vitabu vya Inspekta Fog, alikuwa nani vile, nakumbuka kitabu kimoja Sukuma namba nane!
 
Nani kasoma Operesheni Pata Potea?simkumbuki mtunzi lakini kile kiliandikwa kwa ustadi mkubwa
 
Nadhani wote mli koment humu ni watu wa nje.huyu mtunzi alifariki dunia nadhani mwaka jana
ANGALIA ISIJEKUWA WEWE UKO NDANI YA BOX, kuwa nje haimaanishi watu hawana ISSUE za mAHOME


Musiba yuko somewhere kwenye serikali hii hii ya tanzania. ana wadhifa unaokaribiana au kufanana na ule wa Tido Mhando

ELVIS MUSIBA mara ya mwisho nilimsikia TCI Tanzania Chamber of Indusry...
Sijui yuko wapi sasa hivi....
 
honestly I don't want to take the shine away from the author.......but i always suspected that the author copied some foreign novels and translated them in Swahili!

2 cents, mine!
 
Kazinja uko china? haya kaka ntakutumia namba yangu bana tuone tunavipataje hivyo vitabu...
 
....
Bytheway, Huyu muandishi wa Riwaya hizi yupo wapi siku hizi, na anafanya kazi gani?
Nilizipenda sana kazi zake kama hizo ulizozitaja, lakini iliyonisisimua zaidi ni ile ya KIKOMO.

Bw Musiba yuko na taasisi ya Tanzania Chamber of Commerce Industry and Agriculture (TCCIA) kama CEO. Pia ni mjumbe wa bodi ya Ngrongoro.
Nakumbuka sana akina Pierre na Jean katika kitabu chake cha kikosi cha Kisasi (KK).
 
Bw Musiba yuko na taasisi ya Tanzania Chamber of Commerce Industry and Agriculture (TCCIA) kama CEO. Pia ni mjumbe wa bodi ya Ngrongoro.
Nakumbuka sana akina Pierre na Jean katika kitabu chake cha kikosi cha Kisasi (KK).
Ningependa pia kuhusishwa kati ya watakao pata vitabu hivyo, kuna washiriki ka Vicky, nammisi sana.
Pia alifanya nizijue barabara za Dar kabla sijafika mjini; mitaa kama Samora, Sokoine, Livingstone, Lumumba aliipenda sana jamaa.
 
...nakumbuka kipande hiki kama sikosei kwenye kufa na kupona 'nenda rudi salama umefanikiwa, kwenda na mwoneshaji wa mavazi, leo usiku toka uaduini tunamofikiri' acha kabisa novo zile.

hata kama kuna baadhi wanasema alikuwa anakopi kwenye chase, then he is also smart... he knows streets za mwadui, nairobi, kinshasa na dar. hv zote ziliandikwa kwa Chase zile? BIG UP ELVIS MUSIBA.
 
Back
Top Bottom