Vitabu tu au kuna vingine? ushauri plzzz

Thats what my daddy always used to say those days.

yes na ndio ilitufanya tukawa hivi tulivo and the vice versa,huwezi kuwa unaniletea ujinga wa bf zako kuja nyumbani kwangu na kuleza upuuzi wa kuchoma vitabu niliyvonunua kwa pesa zangu nisikuulize eti kisa umemaliza chuo kikuu!never!kama mleta mada anadhani kumaliza chuo kikuu ndio kukua she has to say it again!chini ya paa la nyumba ya wazazi wake yeye bado ni mtoto na anahitaji kuelezwa.
 
being it uko nyumbani kwangu,under the very roof of my own!u will always be mtoto!

Ukiweza hivyo hongera sana
kuna wazazi wanakuja kuteseka mno kwa sababu ya 'kudekeza watoto'
mtoto anamka asubuhi anachukua gari la mzazi na kwenda kwenye mishe mishe
mzazi anakuta gari haipo,anapanda daladala...
gari ikipata hata pancha,toto linapiga simu nyumbani
kudai pesa ya kuziba au kutengeneza,hata akikamatwa na trafiki
atapiga simu nyumbani,

toto halitumwi bila kwenda na gari......
nyumbani mitoto inaamua chakula kipi kipikwe na ku demand mara kuku,mara
hiki while toka wazaliwe hawajawahi kupata pesa ya jasho lao...

toto linatafutiwa kazi,unakuta hata barua halijui kuandika..na limetoka Univeersity
likipewa kazi kwanza linauliza mshahara...na utasikia ahh hiyo kazi mshahara mdogo,sifanyi...

wazazi wanalazimika kubembeleza likubali job......hii dunia hiii...acha tu
 
yani we acha tu!hivi mzazi anakwambia uache kitu miaka ile unathubutu kumjibu!nini kumjibu mi mamangu alikuwa akikuona umekunja sura tu utafinywa mapajani we mpaka ukojoe.

siku hizi wazazi wengine ni kama
wamekuwa watoto wa watoto wao
nyumba zinaendeshwa na watoto
 
ndio hapo!yani mtoto nizae mwenyewe hawezi kuniendesha kiasi hiki,hataki OFF HE GOES!haya mamabo ya kulea watoto kama wao ndo wametuzaa haya yanatutokea puani hatujui tu ndo mana hawaogopi yeyote barabarani,chukua mfano wanavobehave ukipanda kwenye daladala af uwe umesimama wao wamekaa utapata picha ni kizazi cha aina gani tunkikuza,hawako responsible na chochote si mali,si heshima si imani zao angalia ni vijana wangapi wanakwenda nyumba za ibada,utaona nazungumza nini,yani utakuta ni jumapili au ijumaa hakuna anyeshtuka kusali wala kuswali.mi sijui ungemweleza nini mzee K akubalie ulale nyumbani bila kwenda kanisani!
 
Nilitaka kuuliza umri na darasa kwa mtoa mada naona kakimbia
Lakini ujumbe aupata toka kwa wanaJF, hawa watoto watatuuwa kwa presha.
Kwani shule zinafunguliwa lini?
 
dah!unanikumbusha enzi zile za mkoloni wetu acha kabisa yale yalikuwa maisha bana. mtoto nyumbani unajua huyu ni baba na huyu ni mama mtalima mboga na mashamba kama kubota akikupeleka shule anachagua shule yenye kazi eti kisa ukirud home uwe na akili ya kazi.

jamani nilisoma weruweru huko kazi mtido mmoja hadi kuosha ng'ombe ukirud home hakuna kupumzika tena kama kuonsha ng'ombe uje na skills ulizo pata shule ukienda kupanda mahindi uje na skills ulizopewa shule yaani hadi unahisi duia si yako tena. leo hii mpe mtoto bustani ya hatua 4 tu uone cha mtema kuni lol!
uwiiiiiiiii ulisoma weruweru kumbe...........hata mimi nilisoma hapo A'level lakini.
jamani ile shule acha tu nilikuwa nalia kila siku juu ya kazi ambazo tulikuwa tunafanyishwa mana shule niliyotoka ni ya private full kubembelezwa dah kwenda weruweru nilihisi wazazi hawanipendi na nikawaomba waniamishe wazee wakagoma ingawa uwezo wa kufanya hivyo walikuwa nao kumbe walinisaidia sana..............nimelima mimi, nimechimba mtaro wa kupitisha bomba, mashimo ya kutupa taka, tumezibua vyoo, nimefyeka jamani, kusugua corridor kwa majivu tena matron anakwambia mpaka sura yangu niione,kusukuma gari tena walikuwa wanaliita scandnavia etc............na kila wiki kuna test na unabidi ufaulu..............ila niliweza kumanage hayo yote na nikafaulu nikaenda zangu chuo kikuu kiulaini.
 
wee acha tu nakumbuka kuna siku tulikuwa tumetoka shamba kuchuma kahawa kisha tukatakiwa kutwaga ili kupata pishi moja la mchele tupike tule. miye nikajidi kuchoka nikasingizia naumwa tumbo nikaenda chooni nikakaa huko muda mrefu kweli hadi wakamaliza kutwanga. mama hakunisemesha kitu. imefika msosi umepikwa miye nikajisahau nikawa nkachangamka as if siumwi. muda msosi uko tayari mezani maza akapakulia kila mtu kwenye sahan yake si unajua kijijini hakuna self service? basi alichokifanya Mungu hatak alichukua mpunga akaweka mboga akanipa akasema hakuna mtumwa hapa kila mtu ale kwa jasho lol! niliishia kula mboga tu nikalala usingizi haukujakabisa kisa njaa. toka siku hiyo uvivu niliachana nao.
loh mimi nakumbuka niligoma kupika chapati asubuhi kisa dada yupo basi mama akamwambia dada pika muda wa kula mama akasema share yako haipo ila nenda jikoni kuna unga na mafuta kule upike..............wakanywa chai mimi si nikajidai kususa jamani mama akunipa chakula siku mbili.............na nikawa naosha vyombo walivyolia wenzangu...........sikurudia tena kususa na wala kukataa kupika na wala akuna mtu aliyediriki kususa tangu siku hiyo.
 
kiukweli hii ishu imekakaa kitoto sana lakini anyway ngoja tumshamuri, Mi nadhani usipaparike ye kama kakusemea kwa mzazi wako we tuliza 'ball', mama akikuuliza simply mwambie ni kweli ulianza mahusiano nae lakini soon ukagundua kuwa unafanya makosa so umemwaga ili urejee kundini, nadhani mama atawaka kidogo but ataona umekomaa ndo mana umeacha upuuzi
 
unajua kila siku nilikuwa naiskip hii post leo nkasema ngoja nifungue, nikakusanya nguvu kuisoma, dah kadiri ninnavyosogea sielewi...aghrr nakuja kumaliza na habari za mamdogo nitamwambia nini...dah :yawn:
 
Ukiweza hivyo hongera sana
kuna wazazi wanakuja kuteseka mno kwa sababu ya 'kudekeza watoto'
mtoto anamka asubuhi anachukua gari la mzazi na kwenda kwenye mishe mishe
mzazi anakuta gari haipo,anapanda daladala...
gari ikipata hata pancha,toto linapiga simu nyumbani
kudai pesa ya kuziba au kutengeneza,hata akikamatwa na trafiki
atapiga simu nyumbani,

toto halitumwi bila kwenda na gari......
nyumbani mitoto inaamua chakula kipi kipikwe na ku demand mara kuku,mara
hiki while toka wazaliwe hawajawahi kupata pesa ya jasho lao...

toto linatafutiwa kazi,unakuta hata barua halijui kuandika..na limetoka Univeersity
likipewa kazi kwanza linauliza mshahara...na utasikia ahh hiyo kazi mshahara mdogo,sifanyi...

wazazi wanalazimika kubembeleza likubali job......hii dunia hiii...acha tu

it all has to do with a permissive sort of parenting...watoto wanalelewa kwa design ya kutotaka waexperience pain...forgetting kwamba without experiencing some degree of hustles u won't be able to appreciate pleasure since it's kinda always around u...rubbish kweli!
 
Habari wanajf
Mimi niko na tatizo , mpenzi wangu tuliyeachana hivi karibuni ameenda kudai vitabu hom, sijui ana maana gani na malengo gani kwangu coz si heshima mtu kwenda kichwakichwa kwa wazazi wa x-gal wako kujieleza ili iweje? hapa nilipo nimechanganyikiwa coz mazingira ninayoishi it is not easy for them kuichukulia hiyo issue kawaida, hapa tayari nimeulizwa maswali kadhaa na mama mdogo anayenilea najua itakuwa vigumu sana kwa yeye kuchukulia hiyo issue kawaida. Ushauri plz, tatizo pia kajieleza kuwa tulikuwa na uhusiano na hiyo kitu kwa jinsi ninavyomfahamu mama ni msala mtupu. Plz naihitaji ushauri wenu nifanyeje coz sijui amemueleza nini mama. nahitaji ushauri wenu coz sina mwingine wa kumuomba ushauri.
N.B
Vitabu alinipa mimi na kutokana na hasira zake aliniambia nivichome hivyo alivyovifuata kwangu nikamjibu nimevichoma kwahiyo ili anichomee akaona aende kunisemea hom na huko ameeleza sijui nini kwa mama mdogo.

Labda niulize upo kidato cha ngapi maana tunaweza kukupa ushauri kumbe unahitaji viboko.
 
Back
Top Bottom