18 SEPTEMBER 2012
Na Mwandishi Wetu, Ludewa
VITA ya ubunge Jimbo la Ludewa, mkoani Njombe, kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu ujao 2015, imeanza kujionesha wazi baada ya Mjumbe wa Kamati Kuu (CC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bw. Pindi Chana, kudaiwa kufanya jitihada za kumpigia debe mgombea wa nafasi ya Mwenyekiti wa UWT, wilayani humo.
Baadhi ya wanachama na viongozi wa CCM jimboni humo, wanadai jitihada za Bw. Chana kumpigia debe mgombea huyo ni maandalizi ya kunyakua jimbo hilo ambalo hivi sasa lipo chini ya mbunge wake Bw. Deo Filikunjombe.
Hata hivyo, mgombea aliyekuwa akipigiwa debe na Bw. Chana, alianguka vibaya katika uchaguzi huo na yule aliyekuwa akiungwa mkono na Bw. Filikunjombe, alipata ushindi wa kishindo.
Kwa upande wake, Bw. Filikunjombe alikiri kuwepo kwa taflani hiyo na kudai kuwa, haukuwa mgogoro kati yake na Bw. Chana bali ulihusisha kwa kiasi kikubwa wagombea wa kiti hicho.
"Si kwamba tulizozana ana kwa ana na Bw. Chana hapana, Kilichotokea ni kwamba mwenzangu alikuwa na mgombea anayemuunga mkono na akina mama wa Ludewa walikuwa na mgombea wao.
"Yeye alitaka kutumia nguvu kama Mjumbe wa Kamati Kuu kupindisha sheria ili mgombea wake ashinde, lakini sisi tulisimama kidete kuhakikisha kanuni za chama zinazingatiwa kumpata mshindi halali.
"Kwa mfano, alama alizowekewa Bi. Mlowe hakuna kikao chochote kuanzia Kamati ya Utekelezaji ya Wanawake Wilaya, Baraza la Wanawake Wilaya na Kamati ya Siasa Wilaya waliohusika kuziweka, Bw. Chana alitaka haya yote yapuuzwe na viongozi walipomweleza yeye akaleta ubabe," alisema Bw. Filikunjombe.
Huyu mwandishi sijui kama anamfahamu huyo Pindi Chana ama amefanya kwa makusudi!
Second to my beloved Pindi Chana: Kama kweli unajitambulisha unampenda Yesu mtegemee yeye naye atakusaidia hizo cris cros hazitakufikisha popote zaidi ya kukuangusha big tyme! Let your light so shine that those in dark might see and glorify your heavenly father...At your age ukianza kujipeleka katika uovu mpaka uzeeni utakuwa na majeraha mengi sana!