Mwana Mpotevu
Platinum Member
- Sep 7, 2011
- 3,295
- 2,500
JK amekana kuwa Tanzania haijapeleka majeshi mpakani na Malawi kama Amiri Jeshi mtarajiwa Edward Lowasa alivyoeleza. Soma Habari hii kwa kina
Tanzania haitapigana na Malawi, asema JK
Tausi Mbowe
RAIS Jakaya Kikwete amesema kuwa, Tanzania haina mpango wala nia ya kuingia katika vita na nchi jirani ya Malawi kufuatia tofauti zao kuhusu mpaka katika Ziwa Nyasa.Rais Kikwete alisema hayo jana alipokutana na Rais wa Malawi, Joyce Banda mjini Maputo Msumbiji.
"Namhakikishia dada yangu (Joyce Banda) na watu wote Malawi kwamba, hatuna nia wala mpango wa kuingia vitani. Hatuna matayarisho ya jeshi wala jeshi alijasogea popote kwa vile hakuna sababu ya kufanya hivyo,
"Mimi ndiye amiri Mkuu wa Majeshi ya Tanzania na sijapanga wala kutoa maelekezo ya vita."Kauli hiyo inapingana na iliyowahi kutolewa hivi karibuni na Edward Lowassa ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, aliyesema kuwa Tanzania iko tayari kwa vita iwapo Malawi itaendelea kushikilia msimamo wake kuwa eneo hilo ni la Malawi.
Katika mkutano wake na waandishi wa habari mjini Dodoma hivi karibuni, Lowassa alisema kuwa Tanzania imejiandaa kiakili na kivifaa kuingia vitani na Malawi kama italazimika kufanya hivyo na kwamba kamati yake imeridhishwa na maandalizi ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Rais Kikwete, alisema kwa muda mrefu kumekuwa na utata kuhusu suala la mpaka na tayari maofisa wa pande zote mbili wameanza kulizungumzia kwa nia ya kulitatua kwa amani.
Rais Kikwete aliwalaumu wanasiasa kwa kulikuza suala hilo na kuwataka waandishi wa habari kujiepusha na maneno yanayoleta taharuki na chokochoko baina ya nchi hizo mbili.
"Tuviachie vyombo vyetu vya umma vifanye kazi. Hebu tuvipe nafasi na wanasiasa na waandishi wa habari wajiepushe na maneno haya yanayosababisha taharuki na chokochoko, kwani hayana maana yoyote katika kujenga uhusiano wetu, Kikwete alisisitiza na kuongeza:
Naomba wanasiasa na waandishi wa habari waiache diplomasia ifanye kazi yake."
Rais Kikwete yuko mjini Maputo, Msumbiji kuhudhuria mkutano wa viongozi wa
Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), uliofunguliwa juzi na ulitarajiwa kumalizika jana jioni.
Kutokana na kauli hiyo, Rais Banda alisema kuwa, amefurahishwa na kufarijika kwa Rais Kikwete kumhakikishia kuwa hakuna vita.
"Nimefarijika sana, suala hili limetusumbua sana," alisema Rais Banda na kuvishukuru vyombo vya habari vya Malawi kwa kuonyesha uzalendo na ukomavu katika suala hilo.
MY TAKE;
1: Ni kweli jeshi letu lilisogea mpakani au la?
2: Je, Joyce Banda anastahili kuaminika au la?
3: Je, nani mungo? EL kwa kutwambia Jeshi letu limejiandaa kuingia vitani na Malawi, au JK anayetutangazia kuwa hata jeshi halijasogea mpakani na hakuna mpango wa kupigana?
Tanzania haitapigana na Malawi, asema JK
Tausi Mbowe
RAIS Jakaya Kikwete amesema kuwa, Tanzania haina mpango wala nia ya kuingia katika vita na nchi jirani ya Malawi kufuatia tofauti zao kuhusu mpaka katika Ziwa Nyasa.Rais Kikwete alisema hayo jana alipokutana na Rais wa Malawi, Joyce Banda mjini Maputo Msumbiji.
"Namhakikishia dada yangu (Joyce Banda) na watu wote Malawi kwamba, hatuna nia wala mpango wa kuingia vitani. Hatuna matayarisho ya jeshi wala jeshi alijasogea popote kwa vile hakuna sababu ya kufanya hivyo,
"Mimi ndiye amiri Mkuu wa Majeshi ya Tanzania na sijapanga wala kutoa maelekezo ya vita."Kauli hiyo inapingana na iliyowahi kutolewa hivi karibuni na Edward Lowassa ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, aliyesema kuwa Tanzania iko tayari kwa vita iwapo Malawi itaendelea kushikilia msimamo wake kuwa eneo hilo ni la Malawi.
Katika mkutano wake na waandishi wa habari mjini Dodoma hivi karibuni, Lowassa alisema kuwa Tanzania imejiandaa kiakili na kivifaa kuingia vitani na Malawi kama italazimika kufanya hivyo na kwamba kamati yake imeridhishwa na maandalizi ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Rais Kikwete, alisema kwa muda mrefu kumekuwa na utata kuhusu suala la mpaka na tayari maofisa wa pande zote mbili wameanza kulizungumzia kwa nia ya kulitatua kwa amani.
Rais Kikwete aliwalaumu wanasiasa kwa kulikuza suala hilo na kuwataka waandishi wa habari kujiepusha na maneno yanayoleta taharuki na chokochoko baina ya nchi hizo mbili.
"Tuviachie vyombo vyetu vya umma vifanye kazi. Hebu tuvipe nafasi na wanasiasa na waandishi wa habari wajiepushe na maneno haya yanayosababisha taharuki na chokochoko, kwani hayana maana yoyote katika kujenga uhusiano wetu, Kikwete alisisitiza na kuongeza:
Naomba wanasiasa na waandishi wa habari waiache diplomasia ifanye kazi yake."
Rais Kikwete yuko mjini Maputo, Msumbiji kuhudhuria mkutano wa viongozi wa
Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), uliofunguliwa juzi na ulitarajiwa kumalizika jana jioni.
Kutokana na kauli hiyo, Rais Banda alisema kuwa, amefurahishwa na kufarijika kwa Rais Kikwete kumhakikishia kuwa hakuna vita.
"Nimefarijika sana, suala hili limetusumbua sana," alisema Rais Banda na kuvishukuru vyombo vya habari vya Malawi kwa kuonyesha uzalendo na ukomavu katika suala hilo.
MY TAKE;
1: Ni kweli jeshi letu lilisogea mpakani au la?
2: Je, Joyce Banda anastahili kuaminika au la?
3: Je, nani mungo? EL kwa kutwambia Jeshi letu limejiandaa kuingia vitani na Malawi, au JK anayetutangazia kuwa hata jeshi halijasogea mpakani na hakuna mpango wa kupigana?