Vita ya Gazeti la Mwananchi na Joshua Nassari- Limekosa hoja

Kuna waziri aliwahi kusema TUTANUNUA NDEGE YA RAISI HATA KAMA KUNA WATU WATAKULA MAJANI. Mwingine waalimu walipolalamikia mishahara midogo akasema ASIETAKA KAZI YA UALIMU AIACHE AKAFANYE KAZI NYINGINE.

Hiyo ni mifano michache tu.
 
kwenye thread hii unaweza kuona tofauti kubwa ya washabiki, wazalendo na wapenzi!! mpenzi huwa kipofu, shabiki anafuata mkumbo na mzalendo anaangalia ukweli

nani hakosei? Dogo alikosea yet ni mbunge na ana bright future!! anakosea Obama iwe nassari? anakosolewa obama iwe nassari??
 
Unajua kinchotokea ni nini wandugu, ni ulimbukeni wa mawazo na upungufu wa fikra endelevu
kwa sababu jana wakati mweshimiwa Dogo Janja mbunge wa majimbo mawili ya kaskazini alipo
fika kuhojiwa baadhi ya maafisa police wenye kuaminika kuwa na vyeo vyao walisikika wakidhubutu kusema
eti, ndio ivyo sasa wao wana msikiliza aliyeko madarkani kwa hiyo kwa kuwa chadema ni chama
kinacholenga kuchukua dola wakiwa na wao madarakani nao wata watesa hao c.c.m....! Hii inatosha kuonyesha
umma na jamii nzima yakuwa isije ika kubaliana na ulimbukeni ulio jaa uchuro ndani yake kwa kuamini mia ya mia
vyombo vya habari, kwani kama hata walio kula viapo sio watu waadilifu kwa ujumla wao.....!
 
kwenye thread hii unaweza kuona tofauti kubwa ya washabiki, wazalendo na wapenzi!! mpenzi huwa kipofu, shabiki anafuata mkumbo na mzalendo anaangalia ukweli

nani hakosei? Dogo alikosea yet ni mbunge na ana bright future!! anakosea Obama iwe nassari? anakosolewa obama iwe nassari??

Hilo ndilo la msingi cha ajabu watu wanabaki kupiga kelele waache utaratibu ufuate mkondo wake
 
Usifikiri kwa gazeti kuandika ndo kumsaidia Nassari ili aweze kuwa mbunge mwadilifu na competent. Alishaelewa aliteleza na akakiri then iweje mhariri kwa uroho tu wa kuuza gazeti anaanza kufufua habari ambayo mwenye kuitoa alisha clarify.
Mbaya zaidi kusema Nassari hana uzoefu ni sawa na kusema newly wed couple wapate uzoefu kwanza ndo waoane. Huku ni kuwakashifu watu wa Arumeru ambao tangu 2010 walitaka kumchagua.

Walichokifanya Mwananchi Com. nikutimiza wajibu wa habari na ilipaswa kuwa hivyo. Kilichohitajika si Nasari kutolea ufafanuzi kauli yake maana hapakuwepo mkanganyiko katika kuilelewa. Alipaswa kuomba radhi.

Pili kwenye sijazungumzia swala la uzoefu kwenye nukuu uliyofanya
 
Tido anatekeleza kazi alotumwa na EL. Mtindo huu huu wa kutumia magezeti ambayo yanaaminika kuwa makini ndo walotumia kumchafua Salim wakati wa mbio za uraisi mwaka 2005 kutumia Rai.
 
Tatizo watanzania hatutaki kukubali udhaifu!!
Tanzania kama wewe upo tofauti na mwenzio au kumkosoa basi wewe unatumika..
 
1. He need to be advised on how to adress the mass independently...................he is just growing and unfortunately through turmoils...........so even if you/we admire and support young politicians as well we need to tell them to be kean on tress passing, to adress before the public effectively and efficiently you need either skills or charisma or the combination.....he need to check his score sheets for his benefit particularly and the general community

2. His chairman Hon Mbowe noticed it instantly but the history has it that .....the words uttered, time spoiled...........Josh's case stands to be the living example.......distinction between an error and a mistake has to be bolded thus

3. Despite salutation and hon. status vested in Him (Nassari), love and appreciation among us....... still he is not experienced as most of us would like the case to be ..... he has his homework still ahead of him...........to learn from the experienced and not necessarily to share the threshold with them

This is for us all....who wishes to be vocal and vibrant......cautious practice makes it perfect......politics always is a a game of opportunity...hunting for a weakness to capitalise on.....thus more opportunities you give the weaker you become

Hapo mkubwa hiyo ni conciouse talk bro, besides samaki anakunjika angali mmbichi na huyu bwana Nassari na amini bado mmbichi na asipo chafuka ata jifunzaje...? Hivo basi i believe your so ryt. Mistakes do show the proper way...!
 
Tido Mhando alikuwa hana mahali baada ya kupigwa stop TBC. Kapata kibarua sasa anakipamba na kukilinda. Siku zote wanasema "Adui yako muombee njaa usiwe na haja ya kutafuta silaha ya kumpiga. Acha atimize matakwa kwa mabosi, M4C mwendo mdundo.


Soma Habari kamili maoni ya Mwananchi kuhusu JOSHUA NASSARI:

Vyama vya siasa viwafunde, viwalee wabunge vijana
Send to a friend
Tuesday, 08 May 2012 21:25
0diggsdigg

mwananchi-logo.jpg
KWA siku tatu mfululizo, Jeshi la Polisi nchini limekuwa likimsaka Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari kwa udi na uvumba kwa kile jeshi hilo linachodai kauli za uchochezi na uhaini ambazo yeye na baadhi ya viongozi wa Chadema wanadaiwa kuzitoa katika mkutano wa hadhara ulioandaliwa na chama hicho jijini Arusha mwishoni mwa wiki iliyopita katika mwendelezo wa kampeni ya chama hicho inayojulikana kama ‘Vua Gamba Vaa Gwanda'.

Naibu Kamishna wa jeshi hilo, Isaya Mngulu alidai kwamba mbunge huyo na wenzake ambao tayari wamekamatwa na polisi walitoa matamshi ya kashfa na uchochezi katika mkutano huo, zikiwamo za kumpiga marufuku Rais Jakaya Kikwete asikanyage katika Jimbo la Arumeru Mashariki na Kanda ya Ziwa kwa madai kwamba maeneo hayo ni ya Chadema. Habari zinasema mbunge huyo alijisalimisha polisi jana mchana mjini Arusha.

Polisi wanasema matamshi ya vijana hao hayana maana yoyote kwa jamii na kusisitiza kwamba yana lengo la kuleta migongano kati ya Serikali na wananchi. Hata hivyo, maelezo kuhusu matamshi ya vijana hao yanatofautiana kutegemeana na misimamo kinzani ya kisiasa na kiitikadi ya watu wanayoyatoa. Lakini inadaiwa kuwa, mara tu baada ya matamshi hayo kutolewa jukwaani, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisimama na kuyakana kwa kusema huo siyo msimamo wa chama hicho na kwamba ni kauli binafsi za vijana hao aliosema wana damu iliyochemshwa kwenye moto wa gesi.

Itakumbukwa kwamba tangu aingie bungeni miezi michache iliyopita , mbunge huyo kijana amekuwa akitoa baadhi ya kauli siyo tu zinazotatanisha, bali pia zinazothibitisha kwamba pengine alipata ubunge kabla hajajiandaa au kuandaliwa kisaikolojia kubeba majukumu mazito ya ubunge. Nassari ana umri wa miaka 26 tu na tungetegemea chama chake kingemfunda kuhusu kauli zinazofaa na zisizofaa kutolewa hadharani. Kauli zake nyingi zimekuwa zikihusu tatizo la ardhi katika jimbo lake ambazo zimeonekana kuwahamasisha wananchi kuvamia mashamba ya wawekezaji.

Lakini hoja yetu hapa siyo kumuhukumu mbunge huyo kijana au wenzake ambao wanadaiwa kutoa maneno ya uchochezi katika mkutano wa Arusha. Hatuwezi kufanya hivyo kwa sababu ya kuhofia kuingilia upelelezi wa polisi, hasa pia tukitilia maanani ukweli kwamba watuhumiwa hawajapata nafasi ya kuelezea upande mwingine wa shilingi. Hayo ndiyo matakwa ya maadili yanayosimamia taaluma yetu ya uandishi wa habari.

Hata hivyo, tunachotaka kueleza hapa ni kwamba matatizo yanayowakumba wabunge vijana katika vyama vya siasa nchini hivi sasa yanatokana na viongozi wa vyama hivyo kushindwa kujenga mifumo ndani ya vyama vyao kwa lengo la kuwatayarisha vijana chipukizi na kuwajengea uwezo wa kubeba majukumu ya uongozi katika vyama hivyo katika ngazi zote za uongozi, yakiwamo ya ubunge. Viongozi hao wameshindwa kutambua kwamba uwezo wa vijana kuongea bungeni au kuvuta hisia za wananchi katika majukwaa ya kisiasa pekee hautoshi kuwafanya vijana hao wakidhi vigezo vya ubunge na kukubalika ndani na nje ya Bunge.

Duniani kote vyama vya siasa vilivyo makini huanzisha taasisi na vyuo vya kuwajengea vijana uwezo wa kuongoza na kada hao ndiyo hutwaa uongozi wa nchi zao katika siku za baadaye. Hapa Tanzania hilo liliwezekana wakati chama cha TANU kilipoanzisha Chuo cha Kivukoni ambacho kilikuwa tanuru ya kupika viongozi wa baadaye tunaowaona hivi sasa. Bahati mbaya chuo hicho kilikufa na kuzikwa sawia na Azimio la Arusha


Hii ni changamoto kubwa na pengine ni vyema vyama vya siasa vikatambua kwamba, vijana wakipikwa vizuri na kupata ujuzi katika uongozi, wakajua umuhimu wa maadili ya uongozi na uadilifu na wakaelewa itikadi za vyama vyao na wapinzani wao watakuwa tayari kushika hatamu za uongozi. Vinginevyo tutabakia kuwalaumu kina Joshua Nassari kwa kauli za uchochezi, huku tukikwepa kuondoa kiini cha tatizo.

My take:

Kama kweli Mwananchi wanataka kutuaminisha hii habari yao basi WANGEANZIA NA CHAMA TWAWALA-CCM. Mwananchi ni mashahidi wa KAULI CHAFU,MATUSI NA UCHOCHEZI AMBAZO MARA KWA MARA ZIMEKUWA ZIKITOLEWA NA VIONGOZI WA CCM (WAZEE KWA VIJANA)WAKIWEMO MAWAZIRI NA WABUNGE.Nitatoa mifano michache:

  1. LIVINGSTONE LUSINDE: Katika Kampeni za Uchaguzi mdogo wa Jimbo la Arumeru Mashariki Mbunge huyu kijana toka MTERA kwa tiketi ya CCM ALIPOROMOSHA MATUSI AMBAYO HAYAJWAHI KUSIKIKA POPOTE KATIKA SIASA ZA NCHI HII. Je,POLISI WALIKWA WAPI KUMKAMATA NA KUMFUNGULIA MASHTAKA KAMA AMBAVYO WAMEFANYA SASA KWA MH.NASSARI???Je, Mwananchi mlikuwa wapi KUWAAMBIA CCM JU YA KUMFUNDA LIVINGSTONE LUSINDE ILI ASIWE ANAPAYUKA NA KUTUKANA WATU HOVYO?IWEJE LEO KWA CHADEMA NDIYO MYASEME HAYA.TUNAWAHESHIMU SANA.PSE ACHENI UNAFIKI NA UZANDIKI Tunajua Polisi wako kwa ajili ya CCM na siyo upinzani. Lakini wajue kuwa kuna siku wataelewa somo.
  2. STEVEN WASSIRA-WAZIRI WA USINGIZI BUNGENI: Kwenye kampeni hizihizi za A.Masahariki huyu MZEE KIKONGWE,ambaye mimi nilianza kumsikia akiwa kiongozi wa Serikali tangu nikiwa shule za msingi lakini mpaka leo ni Waziri naye ALIONGEA MANENO YA UCHOCHEZI DHIDI YA KANISA KATOLIKI,WAFUASI WAKE NA VATICAN! Wassira alisema kwamba DR.SLAA ALIIBA FEDHA YA MICHANGO YA ZIARA YA BABA MTAKATIFU ALIPOTEMBELEA TANZANIA MIAKA YA 90 NDIYO MAANA AKAFUKUZWA UPADRE! Je,Polisi walikuwa wapi kumkata huyu kizee mropokaji na kumfungulia mashtaka ya Uchochezi??Nawauliza Mwananchi: Huyu BABU WASSIRA ANAHITAJI KUFUNDWA KITU GANI MTU AMBAYE YUKO KWENYE SYSTEM KWA ZAIDI YA NUSU KARNE??Mwananchi acheni unafiki.Naona gazeti lenu linaanza kupoteza dira,mwelekeo na heshima ambayo limejijengea kwa Watanzania
 
Hoja ya Gazeti la Mwananchi:

1. Nimefurahi kuona leo asilimia kubwa ya wanajamvi tumejikita kukipa CDM upande wake wa pili kwa 'nia nzuri' ya kukijenga na kukiimarisha kwa kuwa ndicho chama 'makini' kinachoelekea kuchukua dola. Tusiogope kujadili mapungufu ya CDM yatakisaidia na kukifanya kuendelea kuwa bora ukilinganisha na CCM chenye serikali na dola na vile vingine vya upinzani.

2. Tanzania Daima, gazeti pia ambalo limejimbambanua kwa kiasi kikubwa ni la itikadi za CDM nalo kwa busara limechapisha makala kwenye ukurasa wake wa 19, nayo nimeona lengo lake ni katika kukijenga CDM. Ni vizuri tukasoma na tukazidi kuhakikisha 'kazi yetu si bure' kwa maana halisi ya kwamba makamanda walio mstari wa mbele kama kina Josh Nassari wasije 'wakaouwawa' before we accomplish our mission. Kwa makamanda wowote ninachojua ni hiki '...till the mission is accomplished'. we have a mission. Josh Nassar kama kateleza ni kwamba hajafa tunyanyue tumtibu aendelee na mapambano. Sidhani unaenda vitani ati unaogopa majeraha. Tupo nyuma yao hata kwa ushauri.

3. Mimi namshukuru Mhariri wa Mwananchi na timu yake nzima ya uhariri. Najua ni makini na weledi. Jambo linapoletwa linaweza kuwa na mapokeo tofauti kama kamanda mwenzetu alivyolipokea. Nawashukuru kwa sababu hata tahariri yenu haijajikita kwenye kuhukumu bali inaonyesha kwa undani lengo la mhariri ni kukitahaadharisha CDM. Sasa ni kazi ya kitengo cha UTAFITI,MAMBO YA BUNGE NA WAPUNGE,SIASA,PROPAGANDA NA ITIKADI za CDM kulichukua na kulifanyia kazi accordingly. Ni muhimu sana.

4. Narudia tena kuna harufu ya CDM kushika serikali na dola 2015. Kazi si ndogo ni kubwa. Mimi si mwanasiasa, ni Mhandisi lakini si lelemama, tutegemee mengi zaidi, kazi yeyote ngumu na muhimu inahitaji ku-establish a degree of precicion, so ni kweli CDM wawe makini kuhesabu kila neno na matendo wafanyayo kwa sababu CCM wanafanya kazi sasa kwa kufuata CDM kimesema nini. On other terms 'They're reactive to CDM issues,' as for now they're not in position to come with new ideas.

5. The only opportunity CDM can use ni kuelewa kwamba CCM kina 'frustration', while in frustration they find themselves working on CDM agendas, wakati watajigundua wanatekeleza agenda za chadema watataka kurudi kwenye agenda zao, while watakuwa wameipaisha CDM, so really this an opportunity comrades,Lets don worry

VIVA CDM,Aluta Continua Josh Nasari
 
Unajua kinchotokea ni nini wandugu, ni ulimbukeni wa mawazo na upungufu wa fikra endelevu
kwa sababu jana wakati mweshimiwa Dogo Janja mbunge wa majimbo mawili ya kaskazini alipo
fika kuhojiwa baadhi ya maafisa police wenye kuaminika kuwa na vyeo vyao walisikika wakidhubutu kusema
eti, ndio ivyo sasa wao wana msikiliza aliyeko madarkani kwa hiyo kwa kuwa chadema ni chama
kinacholenga kuchukua dola wakiwa na wao madarakani nao wata watesa hao c.c.m....! Hii inatosha kuonyesha
umma na jamii nzima yakuwa isije ika kubaliana na ulimbukeni ulio jaa uchuro ndani yake kwa kuamini mia ya mia
vyombo vya habari, kwani kama hata walio kula viapo sio watu waadilifu kwa ujumla wao.....!

Na ndiyo maana sasa hivi gazeti mwananchi linajikomba kwa watawala kwa kutenga kurasa za gazeti lake kutukana wapinzani.
 
. Huu ni unafiki mkubwa na chuki binafsi kwani the same gazeti kwa kipindi chote karibu mwenzi mzima wa Kampeni za ubunge huko Arumeru liliweza kusikiliza na kuripoti kampeni za Nassari vizuri kabisa na wakati mwingi kumsifia.

Hii inaonesha kwamba hawapo biased, kipindi anafanya mazuri walimsifia na sasa wanamuona anaboronga ndio wanampa haki yake. Na hiyo ndio maana ya uandishi wa habari.

Kama mnaona hawajatenda haki basi waiteni na Mwananchi "MAGAMBA" kama ambavyo nyie hufanya.
 
Tido anatekeleza kazi alotumwa na EL. Mtindo huu huu wa kutumia magezeti ambayo yanaaminika kuwa makini ndo walotumia kumchafua Salim wakati wa mbio za uraisi mwaka 2005 kutumia Rai.

There you are.Na ndicho wanachofanya gazeti mwananchi kwa sasa kutenga kurasa za gazeti lake maalum kutukana wapinzani ili wananchi wakose imani nao
 
yaani imefikia hatua binadamu anakuwa kama robot, anakuwa programmed kurespond vile ambavyo programmer anataka1

programmer akiset ushabikie chadema basi unafanya hivyo mpaka wakati ule ambao hata utu wako unadhalilika, programmer akisema ushabikie CCM basi uko tayari kufanya hivyo hata kama kila mtu akikuona mjinga!!

I am not sure when and how we will be able to use our own unique and wonderful brains in almaost everything we do or think!

we are depicting very serious problems that African have been accused to possess since then.

Nassari is very very wrong, he mad mistake and no exuce on this

1. amekirudisha nyuma chama chake ambacho tuhuma za ukaskazini umekitanda
2. anaharibu umoja wa kitaifa

All I can say he was not serious na ndio maana Mbowe alimuonya palepale kuwa hizi ni fikra za KITOTO, Mbowe kasema hivyo tukimsikia kwa nywele na macho yetu!

sasa wanavyokuja hawa wakisema hivi mbona is just okay? povu la nini?

Hivi kitengo cha propaganda cha wapinzani wa CDM wakishikia bango hili mbona ni kubwa sana

ona ambavyo ingewekwa


''Nassari avujisha siri za chadema''........!!!!! HALAFU kingeandikwa kisichokuwepo kuwa CDM wana mpango wa kuigawa taifa, unafikiri hata kama ni hoja ya uongo itawaaminisha wangapi??

Mwananchi siku zote wako neutral....me too
 
Magamba wote wamevamia jukwaa leo kuunga mkono mashambulizi ya gazeti mwananchi kwa CDM.You can smell something here
 
AMA kweli mkuki kwa nguruwe kwa binadamu mchungu. Hii ni Mara ya kwanza kusoma washabiki wa Chadema wakishambulia gazetii la mwananchi. Hii imetokea kwa sababu kwa kawaida gazeti la mwananchi hushabikia sana kwa kuandika habari za Chadema mpaka wasomaji wanapata tabu kutofautisha kati Mwanacni na Tanzania Daima ambalo ni gazeti la Chadema . Leo gazeti hili limeandika ukweli kuhusu kauli ya mbunge wa Chadema Joshua Nassari akizungumzia. Kuundwa kwa jamhuri ya kaskazini na kumpiga maerufuku Rais aw jamhuri ya muungano asikanyage Arusha . Kinachonishangaza ni kwa nini Chadema hawataki kukubali ukweli kwamba mbunge au amepotoka au ametoka siri ya Chama chao kabla ya Wakati . Kwa namna yeyote, watanzania wapenda umoja na amani. Ni lazima tutafakari kauli hiyo ya Nassari kwa akili ya kulinda mustabhari aw taifa letu. Afrika ni bara la makabila. Ukabila na udini ndiyo umekuwa chanzo cha machafuko katika Africa. Migogoro wa Ivory coast imetokana na ukabila na udini. Migogoro uliosababisha Sudan kugawanyika na kuundwa kwa taifa hip ya la Sudan kusini ni ukabila rangi na udini. Haiwezekani kauli ya Nassari iwe ni yake peke yake. Lazima ndiyo msimamo aw Chama Chake . Wote tunajua, Chadema wana hamuwezi sana ya kutawala Tanzania .. Lakini wakishindwa hii Hoja ya Nassari unaweza kuwa ndiyo plan B. tatizo linaweza kuwa ni Wakati gani amesema. Historia ni mwalimu mzuri na Mara nyingi historia hujirudia. Mwaka1961 baadhi ya viongozi aw nudge zebu aw Kilimanjaro walioahidiwa kugombea eneo linazunguka mzima Kilimanjaro Lowe seems ya Kenya. Mwalimu Julius k Nyerere akiwa waziri mkuu Wakati huo alisema kwa vile aliamini kuwa Africa ni moja, Hana tatizo kama wananchi aw Kilimanjaro wataamua kutamka Kenya ili maradi mipaka ya Kenya na Tanzania inabaki ile ile inaouweka mlima Kilimanjaro unabaki Tanzania . Nassari ni mwanasiasa wa kizazi kipya kupitia Chama Chenye sera ya majimbo, si vizuri kupuuza mawazo haya ya kihitler kwani yanaweza huko tuendako yanaweza kuliangamiza taifa.
 
Back
Top Bottom