Gaijin
JF-Expert Member
- Aug 21, 2007
- 11,812
- 5,284
Kinachokutisha wewe ni mzimu wake sio kitu kingine, kifo cha huyu ndugu hakikuwa msiba kwa familia yake tu, ni msiba kwa watanzania wote wanaoheshimu democrasia na utawala unaofuata sheria.
Hii ni kumbukumbu ya ukatili wa serikali dhidi ya watu wake chini ya uongozi wa chama cha mapinduzi, ni lazma tukumbushane historia hii sababu tunajijua sisi kama binaadamu ni wepesi sana kusahau.
tutaendelea kukumbushia kifo hiki na vingine vyote vya namna hii hata baada ya kukiondoa chama hiki madarakani, hata wakati wa kikomo cha furaha katika Taifa letu, tutakumbushana kwa picha hizi kwamba tulikotoka hapakuwa salama, hakukuwa na amani wala utulivu ili tusijetukaruhusu wauaji wengine kutuongoza.
Ni rahisi kujitia utukufu na kukosea wengine heshima kwa vile huna vinasaba nae
Angelikuwa baba yako usingethubutu kutamka haya