Vita vya Kagera tulipigana na Libya (Gadafi)

There is a universally accepted wisdom " Treat others the same way as you will like to be treated". I find it is all right by some in this web to set out just to attack Arabs or to throw hate words in this forum and they get away with it!- This is racialist.

Kuna msemo kuwa watendee wenzako kama unavyotaka kutendewa wewe! - Nimegundua kama inkubalika kwa baadhi ya watu kutukana na kukashifu au kutupa maneno ya chuki , ubaguzi dhidi ya Waarabu.

Je huo mpira ungekuwa dhidi ya Waafrika mgelalamika kiasi gani?

This is not a civilized way or how people build respect among nations or people!!
 
There is a universally accepted wisdom " Treat others the same way as you will like to be treated". I find it is all right by some in this web to set out just to attack Arabs or to throw hate words in this forum and they get away with it!- This is racialist.

Kuna msemo kuwa watendee wenzako kama unavyotaka kutendewa wewe! - Nimegundua kama inkubalika kwa baadhi ya watu kutukana na kukashifu au kutupa maneno ya chuki , ubaguzi dhidi ya Waarabu.

Je huo mpira ungekuwa dhidi ya Waafrika mgelalamika kiasi gani?

This is not a civilized way or how people build respect among nations or people!!
Ni kweli kabisa hapa panaonekana ni ubaguzi mtupu,hivi mnataka usema Tanzania haikuwa imesaidiwa katika vile ? Kama haitoshi ni nani alikuwa akiwaonyesha WaTz njia,wakati tuliingia kule Uganda hata njia na ramani za tunakokwenda hatuna ? Ulizeni msiwe mnafuata propaganda za mpiga picha,maana vita ile nilikuwemo ndani kama mtu wa mawasiliano kuna wakati tulizachapa wenyewe kwa wenyewe kwenye nyasi ndefu,friendly fighting not fire,kama kuna kusaidiwa wakati wa ile vita basi tukubali hata Tz walikuwa na msaidizi ,tuwache ubaguzi ,kwanza tukubalianeni kuwa vita vilipiganwa kati ya Tz na Uganda maana mkisema sana wengine tunaweza kuja na hoja nzito hapa ,ili kuonyesha kuwa vita ile ilianzishwa na Tanzania na hakuna sehemu ambayo ilivamiwa na Uganda au mtabisha ?

Kama zilivyokuwa propaganda za kuivamia Iraqi ndivyo zilivyosukwa propaganda za kuivamia Uganda !! Mnashangaa kitu gani ? Au mnataka kupinga hapa tuanze kufundishana ni nani alipanga vita ile ? Afu kama mlizunguka na kuivaa Uganda mpaka kwenye mipaka ya Sudan na Zaire mbona mpaka leo kuna rasta yule mlokole Joseph Kony anatesa na hakuna anaemuingilia katika anga zake,semeni alianza 1986 ,hivi mlisafisha kitu gani zaidi ya kuweka utawala alioutaka Nyerere pale Kampala nao ukatimuliwa na kuchawanyika hata wale mliowaweka leo hii hawajulikani wapo wapi ?

Vita ile msitake kuipamba sana maana kusema kweli hakuna sababu hata moja ya kupigana au kushiriki ila siasa za ujamaa ndizo zilizowapeleka ndugu na jamaa zetu wengi tu kupoteza maisha ,hivi kuna mtu alihoji ni waTanzania wangapi walipoteza maisha katika vita ile ? Je Serikali iliwafanyia nini wafiwa ? Je mnajua mpaka leo kuna watu hawajalipwa chochote ? Ni nani amewaulizia na kuwadaia chochote kutoka kwa serikali zinazopokezana vijiti za CCM ,wait & see once CUF ikikamata dola itahakikisha wale wote ambao hawajalipwa wanalipwa na wale ambao ndugu na jamaa zao walifariki nao wanapewa chochote ,ndio mashujaa wanavyokumbukwa sio kukaa na kuwakusanya uwanja wa Taifa mkiwacheza kwata na wengine kuwapeleka nchi za nje eti kwenda kusimamia amani na wanapopata maafa huko hakuna anaewakumbuka zaidi ya siku mbili za mwanzo ,zaidi ya viongozi tulio nao ni kujikurupusha na wakiendewa kudaiwa malipo hupiga watu tarehe.
 
13uganda.600.jpg

The leader of the Lord’s Resistance Army, Joseph Kony, far left, met with Jan Egeland of the United Nations ,he is against serikali ya mafisadi na anasema mafisadi wataondoka kwa mtutu wa bunduki sijui hapa Tz kama wazee wa machakani wanaweza kuivalia njuga serikali inayowahifadhi mafisadi mpaka kieleweke.
 
13uganda.600.jpg

The leader of the Lord’s Resistance Army, Joseph Kony, far left, met with Jan Egeland of the United Nations ,he is against serikali ya mafisadi na anasema mafisadi wataondoka kwa mtutu wa bunduki sijui hapa Tz kama wazee wa machakani wanaweza kuivalia njuga serikali inayowahifadhi mafisadi mpaka kieleweke.

No mkuu, hapa ninaungana na mkuu Companero kulipongeza jeshi letu, unajua mambo ambayo Kony anayowafanyia raia wa Uganda lakini ? Kama ni kupinga ufisadi siyo kihivyo, labda ungemtaja late Thomas Sankara kidogo ningekuelewa.
 
enzi za cold war ambapo mnapewa silaha bure zimekwisha,sasa hivi ni pesa yako,wataalam wa mambo ya kijeshi wanatazama % ya national product inayokwenda kwenye ulinzi,in that case sisi tanzania net national product yetu tayari ndogo hivyo basi we cannot afford to buy any weapons ndiyo maana hata choppers za kiraia zinatumiwa jeshini

SOA:

Inabidi uwe unatokea mara kwa mara hapa. Wakati wa vita vya baridi waMarekani na waRusi waligawa zana za kivita kama vile Kikwete alivyogawa pipi.

Na sababu moja ya Tanzania kushinda hile vita ilikuwa ni waRusi ku-supply zana pande zote mbili. Lakini kama waMarekani wangehamua kum-support Idd Amin basi vita vile vingechukua sura ya vita vya Mozambique au Angola.
 
nini drone,tomhawk cruise missile lilikuwa linaelekea baghdad,likawa limepotea jangwani,bahati nzuri likawaona mabedui wanachunga mbuzi,likapunguza mwendo na kuwauliza kwa kiarabu,baghdad iko wapi?kuelekezwa tu likageuza njia na kuelekea baghdad.hii kitu ikiwa usawa wa ardhi inaheshimu hata traffic lights by stopping at red lights

hahahahhaha
hii ni ya mwaka sasa
 
Elewa maelezo kwanza kabla haujanukuu, nimeandika wana teknolojia. hiyo, na uwezo pia wanao,lakini hawana silaha hiyo, Mandela alifuta program hiyo alipochukua nchi,haina maana kwamba walichoma moto program yote. Ni tofauti na North Korea sasa hivi, au Iran wao ndiyo wanakimbilia huko. SA waliishafika huko tayari.

Acha kucheza mchezo anaouita Nyani Ngabu semantics. Posti yako kaisome tena. Inasema wakishindwa wanaweza ku-pull Nagasaki. Kwa taarifa yako hawawezi. Mmarekani hataki kabisa Mwafrika awe na uwezo huo. Ndio maana walihakikisha wanamuondolea Msauzi uwezo huo kabla ya uchaguzi wa uhuru wa 1994. Kapitie nyaraka za CIA uone walizifanya nini nyuklia za wasauzi na wataalamu wake. Sauzi hata kwa Angola hakanyagi!
 
Si ndio hapo. Afu Maroketi yaliyoitwa sabasaba (Kaytusha rockets), wapalestina na Izbollah wanategeneza kwenye garage za uchochoroni. AK47, inatengenezwa na watu wasiokwenda shule Pakistani.

Wezetu south afrika wanatengeneza umkhoto misssiles (hizi mpaka wanauza ulaya- ni makini sana hizi) angalia www.denel.co.za wanatengeneza helikopta za kivita, drones, bongo sijui tunatengeneza silaha zozote?
 
Ni kweli kabisa hapa panaonekana ni ubaguzi mtupu,hivi mnataka usema Tanzania haikuwa imesaidiwa katika vile ? Kama haitoshi ni nani alikuwa akiwaonyesha WaTz njia,wakati tuliingia kule Uganda hata njia na ramani za tunakokwenda hatuna ? Ulizeni msiwe mnafuata propaganda za mpiga picha,maana vita ile nilikuwemo ndani kama mtu wa mawasiliano kuna wakati tulizachapa wenyewe kwa wenyewe kwenye nyasi ndefu,friendly fighting not fire,kama kuna kusaidiwa wakati wa ile vita basi tukubali hata Tz walikuwa na msaidizi ,tuwache ubaguzi ,kwanza tukubalianeni kuwa vita vilipiganwa kati ya Tz na Uganda maana mkisema sana wengine tunaweza kuja na hoja nzito hapa ,ili kuonyesha kuwa vita ile ilianzishwa na Tanzania na hakuna sehemu ambayo ilivamiwa na Uganda au mtabisha ?

Kama zilivyokuwa propaganda za kuivamia Iraqi ndivyo zilivyosukwa propaganda za kuivamia Uganda !! Mnashangaa kitu gani ? Au mnataka kupinga hapa tuanze kufundishana ni nani alipanga vita ile ? Afu kama mlizunguka na kuivaa Uganda mpaka kwenye mipaka ya Sudan na Zaire mbona mpaka leo kuna rasta yule mlokole Joseph Kony anatesa na hakuna anaemuingilia katika anga zake,semeni alianza 1986 ,hivi mlisafisha kitu gani zaidi ya kuweka utawala alioutaka Nyerere pale Kampala nao ukatimuliwa na kuchawanyika hata wale mliowaweka leo hii hawajulikani wapo wapi ?

Vita ile msitake kuipamba sana maana kusema kweli hakuna sababu hata moja ya kupigana au kushiriki ila siasa za ujamaa ndizo zilizowapeleka ndugu na jamaa zetu wengi tu kupoteza maisha ,hivi kuna mtu alihoji ni waTanzania wangapi walipoteza maisha katika vita ile ? Je Serikali iliwafanyia nini wafiwa ? Je mnajua mpaka leo kuna watu hawajalipwa chochote ? Ni nani amewaulizia na kuwadaia chochote kutoka kwa serikali zinazopokezana vijiti za CCM ,wait & see once CUF ikikamata dola itahakikisha wale wote ambao hawajalipwa wanalipwa na wale ambao ndugu na jamaa zao walifariki nao wanapewa chochote ,ndio mashujaa wanavyokumbukwa sio kukaa na kuwakusanya uwanja wa Taifa mkiwacheza kwata na wengine kuwapeleka nchi za nje eti kwenda kusimamia amani na wanapopata maafa huko hakuna anaewakumbuka zaidi ya siku mbili za mwanzo ,zaidi ya viongozi tulio nao ni kujikurupusha na wakiendewa kudaiwa malipo hupiga watu tarehe.

CUF kuchukua nchi?????hapa ndipo mzee unaota ndoto zako za mchana....hii nchi ni bora hata ije ikose mtawala kuliko kuwa chini ya vibaraka CUF.Na tena ni bora CCM itawale milele kuliko hawa CUF.
...........ndio hio.
 
MBONA,idi amin nae alidai kwamba tanzania ilikuwa inasaidiwa na mercenaries na akaonyesha maiti ya mwanajeshi mzungu!!!!

Huyu alikuwa Mtanzania, Hans Pope, ambaye ngozi yake ni nyeupe! Idi Amin Dada alitumia propaganda ku-justify matumizi ya mamluki wake wa kiarabu/kiislamu!
 
hapa ndipo nionapo mawazo ya WaTanzania yanapoishia ,hivi vyuo vyote hivi vikubwa vikubwa tulivyonavyo tunashindwa kuwapa chalenji wasomi wetu kubuni mbinu za kutumia maji ya ziwa victoria na maziwa mengine yaliyotusheheni kila pembe mbali ya utaalamu wa kutumia maji ya bahari ?

Ikiwa tutaendelea kuwa omba omba huoni tutarudi palepale kuwakaribisha mafisadi wa ndani na nje kuweza kuendeleza dili za kifisadi ?

Na zaidi itatubidi tufunge vyuo vyote tulivyonavyo maana miaka zaidi ya arubaini hatujatoa msomi awezae kubuni hata miradi ya maji ,tuvifunge hivi vyuo ili kuendeleza kuleta waisraeli na wachina.

Mimi huwa naona aibu sana panaposemwa mambo haya ya kiufundi kuombwa nchi za nje ?
Na tujiulize tumewatumia vipi wananchi wetu wasomi ambao wanazunguka na mashahada kutoka ofisi moja kwenda nyingine kutafuta kuajiriwa ,hawa tumewafundisha na tumewapatia elimu ya juu kabisa kiasi ya kuwashinda baadhi ya hao wanaokwenda kuombwa ,sasa kujaribu kuwashirikisha katika mambo haya ,hamuoni kama kwamba tutakuwa tunajenga utamaduni wa kuwatumia ,iangalieni Irani,iangalieni India iangalieni Pakistani ,wate hawa wamefikia walipofikia kwa kuwatumia wasomi wake kiasi cha kuwafanya wawe wanahitajika katika mataifa makubwa kwa bei yeyote ile.
Hebu kamtafuteni Doctor Kadeer ,huyo ni mpakistani ambae ndie aneitesa Amerika katika mambo ya kiufundi ya silaha za nyuklia aliondoka Amerika kwa Buibui na kurudi nchini kwake hadi hii leo Wamerikani wanamhitajia lakini amejichimbia kwao na kila siku tunasikia Pakistan wakifanya majaribio ya kinyuklia ,sisi hapa Uranium tunaikanyaga na tunao wataalamu wa mambo ya nyuklia.

Nasema wasomi tulio nao wanadharauliwa sana na hawapewi kipau mbele na bajeti inanyimwa kuwapa mwanya wa kujitanua katika elimu yao ,leo hii kama wataalamu wetu wangekuwa wanathaminiwa tusingefika kutafuta makandarasi wa kutandaza reli ya kisasa Tanzania nzima,tusingeshindwa kutandaza barabara za lami Tz nzima ,mawe yametujalia,cement kila sehemu vyuma vinatuozea ,nguvu kazi imekaa haina la kufanya inacheza bao tu.

Wasomi tulio nao ni hazina kubwa sana lakini wamenyimwa sehemu katika serikali hizi za CCM zinazopokezana vijiti kuongoza nchi hii.

Somo ambalo lipo mbele yetu na kila mmoja wetu analiona ni kuanguka kwa uchumi wa dunia ,athari zake zinazidi kusonga mbele na kupanda kila siku ,na kila nchi inajibana kivyake ,hivyo kutafuta sababu za kuombaomba na kukubaliwa zinazidi kuwa ngumu ,kila nchi hivi sasa inabana matumizi na inajaribu kutumia wasomi wake katika kujikwamua na kubuni mbinu za kusonga mbele bila ya kutegemea nchi nyengine kuna siku jawabu tutakalopata kutoka nchi tunazo ombaomba ni kutwambia mtajiju !!

Mawazo yako mazuri alikuwa nayo Nyerere hasa kwa upande wa kujenga miundombinu ya reli, barabara na viwanda ambavyo karibu vyote vimesambaratika. Pia kwa kulinda bidhaa za ndani alizuia bidhaa toka nje ya nchi! Azimio la Arusha ndilo lilikuwa kikomo cha mafisadi! Pamoja na hayo yote, kwa hali ilivyo, hatutakwepa misaada ya kitaalamu, kifedha na mingineyo.
 
Basi, either kwa sababu ya ufisadi, mipango mibovu na sababu kadha wa kadha, jeshi letu siyo imara kama unavyotaka tufikirie. Jeshi haliwezi kununua helikopta za kiraia na kuwa za kivita. Hata mounted machine guns zinaizidi uzito !!

Harufu ya inferiority complex! Beware of somebody who is ashamed of himself! Hili jeshi, JWTZ, ni imara asikudanganye mtu! Amin ambaye alimkejeli Nyerere kwamba kwa kuwa yeye nduli alikuwa heavy weight boxer, hakukuwa na haja ya kuendelea kupoteza maisha ya wanajeshi, bali waingie ulingoni huku yeye Amin akiwa amefungwa mkono mmoja nyuma akiwa anapambana naye kwa mkono mmoja na atamshinda! Anyway, kejeli zake hazikuwa lolote, kwani "UWEZO WA KUMPIGA TUNAO!"
 
Harufu ya inferiority complex! Beware of somebody who is ashamed of himself! Hili jeshi, JWTZ, ni imara asikudanganye mtu! Amin ambaye alimkejeli Nyerere kwamba kwa kuwa yeye nduli alikuwa heavy weight boxer, hakukuwa na haja ya kuendelea kupoteza maisha ya wanajeshi, bali waingie ulingoni huku yeye Amin akiwa amefungwa mkono mmoja nyuma akiwa anapambana naye kwa mkono mmoja na atamshinda! Anyway, kejeli zake hazikuwa lolote, kwani "UWEZO WA KUMPIGA TUNAO!"
Hakika JW ni imara. Nami nakubaliana nawe. Nakumbuka miaka 2 iliyipita nilikuwa naongea na askari mmoja (kepteni) alinisimulia kwamba JW ni moja ya majeshi bora barani Afrika. Aliniambia baadhi ya sifa zao ni uwezo wa kujifunza silaha mpya kwa haraka sana na kuzitumia kwa usahihi unaostahili bila jazba. Pia alisema wao ni magwiji wa mbinu za kivita, yaani mbinu za medani - wana uwezo wa kujipanga kwa haraka na kwa makini na kumuwahi adui kabla yeye hajaamuka na kummaliza. Wana spidi na ujasiri.

Katika kulinganisha uwezo wa kijeshi jamaa alidai kwamba JW wanaweza kukabilina na majeshi ya nchi kama Afrika ya Kusini, Angola, Zimbabwe. Majeshi ya nchi zingine alisema hayana kitu. Nilipomtajia Nigeria jamaa alisema wale wana masilaha mazito mazito tu lakini kwa mbinu za kivita hawana kitu. Akanichekesha kwa kusema kwamba wanigeria anaweza kumwona adui mmoja na kuamua kumfuata na kummaliza kwa kifaru badala ya kutumia bunduki ya kawaida. Kwa kweli nilicheka!

Kumbe jamaa wanaolidharau jeshi letu, bado hawalijui kisawasawa. Jamaa ni wakali sana kimbinu, kimafunzo na matumizi ya silaha walizonazo.
 
babuyao,tunakubali tanzania jeshi zuri,but the art of modern warfare has taken a diffrent turn,hivi sasa AERIAL SUPERIORITY ni neccesity,and its on this basis TPDF will be found wanting-trust me tukipigana na nchi yenye ndege,our infantry will be sitting ducks
 
babuyao,tunakubali tanzania jeshi zuri,but the art of modern warfare has taken a diffrent turn,hivi sasa AERIAL SUPERIORITY ni neccesity,and its on this basis TPDF will be found wanting-trust me tukipigana na nchi yenye ndege,our infantry will be sitting ducks
Mkuu, nakubaliana nawe kwamba vita ya sasa inapiganwa kiteknolojia. Mkuu wa nchi naona kwa kutambua hilo ameahidi kuwaongezea vifaa vya kisasa vya kijeshi. Kumbe kama ahadi hiyo ataitimiza basi JW litakuwa jeshi la kisasa kabisa licha ya mbinu za medani walizosheheni.
 
Harufu ya inferiority complex! Beware of somebody who is ashamed of himself! Hili jeshi, JWTZ, ni imara asikudanganye mtu! Amin ambaye alimkejeli Nyerere kwamba kwa kuwa yeye nduli alikuwa heavy weight boxer, hakukuwa na haja ya kuendelea kupoteza maisha ya wanajeshi, bali waingie ulingoni huku yeye Amin akiwa amefungwa mkono mmoja nyuma akiwa anapambana naye kwa mkono mmoja na atamshinda! Anyway, kejeli zake hazikuwa lolote, kwani "UWEZO WA KUMPIGA TUNAO!"

Hebu fafanua tafadhali. JWTZ ni imara kivipi? Jee, kiutawala, idadi ya professional soldiers, kiuzoefu, kisilaha na zana nyinginezo za kijeshi/kivita unalinganisha vipi JWTZ na majeshi ya nchi jirani au hata nyingine za Kiafrika?

Vita iliyomalizika miaka 30 iliyopita, na ushindi uliopatikana kwa ku-recruit wakulima na watu wa kawaida wasio na kazi waliopitia crash course ya mgambo kwa wiki chache tu halafu kupelekwa en masse kwenye frontline kama cannon fodder - isiwe sababu ya kuita JWTZ "jeshi imara"?
 
Hamna kikwazo kwa Africa Kusini in the whole of Africa, Siyo Black Africa tu. Kidogo Egypt wanaweza kupigana lakini nao watalazwa chali. Angola wana F18 lakini they are no match to SA. Tusisahau kwama SA wana teknolojia ya nyuklia kutoka miaka ya 70. Wakishindwa kabisa they might pull a Nagasaki on their enemy.
sio kweli, pamoja na jeuri yote ya SA hawezi kutia mguu hata kidogo kwa jeshi la Zimbabwe, usisikie maneno ya vijiweni, cha pili unapashwa kujua vita ni moyo na ukakamavu wa wanajeshi na wala sio vifaa bila kuwa ngangali, ebu kaangalie jeshi la SA lilivyojaa wanajeshi dhaifu na walevi kupindukia,
pamoja na nguvu hizo zote lakini alishindwa kabisa kuingia bongo hili hali akijua kuwa bongo ndio ilikuwa kitofu cha vita ya ukombozi wa nchi hiyo
 
sio kweli, pamoja na jeuri yote ya SA hawezi kutia mguu hata kidogo kwa jeshi la Zimbabwe, usisikie maneno ya vijiweni, cha pili unapashwa kujua vita ni moyo na ukakamavu wa wanajeshi na wala sio vifaa bila kuwa ngangali, ebu kaangalie jeshi la SA lilivyojaa wanajeshi dhaifu na walevi kupindukia,
pamoja na nguvu hizo zote lakini alishindwa kabisa kuingia bongo hili hali akijua kuwa bongo ndio ilikuwa kitofu cha vita ya ukombozi wa nchi hiyo
mi naona huu mjadala tuufunge,duh!!!! south africa jeshi bovu na walishindwa kuingia bongo,hizi data kali sana
 
babuyao,tunakubali tanzania jeshi zuri,but the art of modern warfare has taken a diffrent turn,hivi sasa AERIAL SUPERIORITY ni neccesity,and its on this basis TPDF will be found wanting-trust me tukipigana na nchi yenye ndege,our infantry will be sitting ducks

Sio kweli huo ni woga tu,kama utakumbuka vita ya kwanza ya Iraqi na dunia nzima walishindwa kumg'oa yule mzee alieidhibiti Iraq na kama unakumbuka Mrusi alionya kuwa vita ile hata ikimalizika hakuna tena atakaeweza kuidhibiti Nchi ya Iraq maana kama utafuatilia historia yake kivita basi utaona kweli Saddam aliweza kuidhibiti ,sasa ukiangalia hadi hii leo mambo huko Iraqi si shuari tena. Madege na maroketi ya mbali ya mmarekani hayakufua dafu.

Kama haitoshi majeshi mingine pale kwa wakulima wa hashishi na cocci hadi leo hakuna cha midege wala askari wa mievuli ,wanakusanyana aafu wanakimbia si wamirekani wala waingereza na hata NATO nao wamebwaga manyanga na sasa wanaona ni bora wakubaliane na Talabani na kukaa meza moja ,wamesema ikiwa talabani anaweza kuikantrol ncho basi bora yeye aachiwe ila Karzai ndio bado anatamaa ,ukiangalia kumbe karzai utawala wake ni palepale ndani ya Kabul kwengineko kote hakutawaliki ,hivyo jiulize midege ya kivita imeishia wapi ,kuna starageic za kivita ,ila midege si ya kutegemea ushindi kila pahala.

Historia inaonyesha Mmarekani alitoka baru kule Vietnam na alikuwa na midege ya kila aina ,hakuna filamu inayoonyesha mmarekani amepigana kule na kushinda ,karibu filamu zote inaonekana wanakimbia na helikopta ,hata hapa jirani SOmalia waliingia na mahelkopta kilichowakuta natumai mnakielewa. Maana walitambua kuwa bangi si mboga. Ila pale Somali jamaa wanatumia mirungi.
 
Back
Top Bottom