Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Vita umeya CCM moto
Thursday, 09 December 2010 20:55
Ramadhan Semtawa na
Raymond Kaminyoge
KAMATI Kuu (CC) ya CCM leo itakutana kujadili majina ya wagombea nafasi za umeya wa majiji na manispaa, huku kambi mbili za watuhumiwa wa ufisadi na wapambanaji zikiumana kila moja kutaka kusimika washirika wao kisiasa.
Tayari mchuano huo umekwishapandisha joto katika hatua ya mchujo wa awali, huku kwa upande wa meya wa Jiji la Dar es Salaam kambi hizo zikionekana kuvutana zaidi.
Katibu Mkuu wa CCM Yusuph Makamba, jana aliliambia gazeti hili kwamba CC itakutana Ikulu chini ya uenyekiti wa Rais Jakaya Kikwete, kwa ajili ya kupitisha majina yasiyopungua matatu kupeleka kikao cha chama cha madiwani.
Makamba alifafanua kwamba, kwa mujibu wa kanuni za chama hicho kikao hicho cha madiwani ndicho cha mwisho chenye mamlaka ya kupigia kura jina moja litakalowakilisha chama.
"Kesho (leo) kamati kuu itakutana Ikulu kuanzia asubuhi chini ya uenyekiti wa Rais Jakaya Kikwete, ajenda kuu ni moja tu kujadili na kupitisha majina yasiyopungua matatu ya wagombea ambayo yatapelekwa katika kikao cha chama cha madiwani," aliweka bayana Makamba.
Mtendaji mkuu huyo wa CCM aliongeza kwamba, majina yanayojadiliwa na kupitishwa ni ya mameya wa majiji na manispaa huku majina ya wenyeviti wa halmashauri yakiishia katika ngazi ya siasa ya mkoa.
Kauli hiyo ya mtendaji mkuu wa CCM inakuja wakati zikiwepo taarifa za genge la watuhumiwa wa ufisadi likianza kutoa fedha kiasi cha Sh 500,000 kwa kila diwani anayeingia katika vikao vya chama vya madiwani ambavyo vitatoa majina yasiyopungua matatu yatakayopendekezwa na Kamati kuu ili washirika wao washinde.
Genge hilo ambalo linatuhumiwa kujilimbikizia mabilioni ya fedha chafu, linatajwa na duru mbalimbali za kisiasa ndani na nje ya CCM, kwamba zimekuwa zikifanya kampeni kubwa katika kiti cha umeya wa jiji la Dares Salaam.
Dar es Salaam imekuwa ikichukuliwa kama kitovu kikuu cha shughuli mbalimbali za kiserikali, kidiplomasia na kibiashara, hivyo vita kubwa ya umeya imekuwa ikielekezwa katika kiti cha meya huyo na wenzake wa manispaa zake tatu.
Mchuano mkali katika umeya wa jiji la Dar es Salaam unatarajiwa kuwa kati ya Dk Didadas Masaburi, Jerry Slaa na Hashim Sagaf huku wengine ni Abuu Jumaa, na Bisalala Salum.
Vikumbo hivyo vya kambi hizo vikiendelea, tayari baadhi ya madiwani wilayani Ilala, wameomba CC ya CCM kupendeleza watu wenye uwezo na siyo wapiga porojo.
Hatua hiyo inatokana na baadhi ya wagombea hasa wenye nguvu za mafisadi, kuanza kutumia baadhi ya vyombo vya habari kuwapaka matope wenzao ili waonekane hawafai kushika nafasi hiyo.
Wakizungumza na Mwananchi jana jijini Dar es Salaam, kwa sharti la kutotajwa majina yao, madiwani hao walisema, kuna baadhi ya wagombea ambao wanawapaka matope wenzao ambao wanahisi ni watu wenye uwezo ili waenguliwe kwenye kamati kuu na wao kuwa na uwezekano mkubwa wa kushinda.
Halmashauri yetu ndiyo imejaa fitina, majungu, kuna mgombea mmoja ambaye anahangaika kuchafua wenzie kwenye vyombo vya habari, kwa nini anafanya hivyo sasa na si zamani, huyu anachafua wenzie ili kujenga mazingira ya kuteuliwa na kamati kuu, alilalamika mmoja wa madiwani.
Aliongeza, Tunaiomba kamati kuu ifanye maamuzi yake kwa kufuata vigezo vilivyowekwa na siyo kuangalia propaganda zinazoenezwa kuwachafua wagombea, vinginevyo tutapata meya hatari,
Diwani mwingine, alisema kamati ya maadili ifanye kazi ya ziada kuwaibua baadhi ya wagombea waliowekwa na matajiri ili kulinda maslahi kwenye biashara zao.
Unajua Ilala, ndiyo Dar es Salaam, kuna shughuli nyingi za kiuchumi ambazo zinafanyika, kamati kuu ipendekeze majina ya wagombea wenye uwezo ili waweze kusimamia ipasavyo rasilimali zilizopo, alisema
Alisema inashangaza mara nyingi propaganda chafu zinaenezwa kupitia vyombo vya habari kuhusu halmashauri hii hali inayoonyesha kuna baadhi ya wagombea hawajiamini kutokana na uwezo wao kuwa mdogo.
Hivi karibuni madiwani wengine katika halmashauri hiyo waliitahadharisha kamati kuu, kuwa makini wakati wakupendekeza mameya kutokana na baadhi ya wagombea kufadhiliwa na matajiri ili waweze kulinda maslahi yao.
CCM itapita katika hatua hiyo ngumu kisiasa baada ya kutikiswa na mbio za uspika ambazo genge la mafisadi lilituhumiwa kuweka mkakati wa kumwangusha Spika aliyejijengea umaarufu mkubwa kwa umma, Samuel Sitta.
Thursday, 09 December 2010 20:55
Ramadhan Semtawa na
Raymond Kaminyoge
KAMATI Kuu (CC) ya CCM leo itakutana kujadili majina ya wagombea nafasi za umeya wa majiji na manispaa, huku kambi mbili za watuhumiwa wa ufisadi na wapambanaji zikiumana kila moja kutaka kusimika washirika wao kisiasa.
Tayari mchuano huo umekwishapandisha joto katika hatua ya mchujo wa awali, huku kwa upande wa meya wa Jiji la Dar es Salaam kambi hizo zikionekana kuvutana zaidi.
Katibu Mkuu wa CCM Yusuph Makamba, jana aliliambia gazeti hili kwamba CC itakutana Ikulu chini ya uenyekiti wa Rais Jakaya Kikwete, kwa ajili ya kupitisha majina yasiyopungua matatu kupeleka kikao cha chama cha madiwani.
Makamba alifafanua kwamba, kwa mujibu wa kanuni za chama hicho kikao hicho cha madiwani ndicho cha mwisho chenye mamlaka ya kupigia kura jina moja litakalowakilisha chama.
"Kesho (leo) kamati kuu itakutana Ikulu kuanzia asubuhi chini ya uenyekiti wa Rais Jakaya Kikwete, ajenda kuu ni moja tu kujadili na kupitisha majina yasiyopungua matatu ya wagombea ambayo yatapelekwa katika kikao cha chama cha madiwani," aliweka bayana Makamba.
Mtendaji mkuu huyo wa CCM aliongeza kwamba, majina yanayojadiliwa na kupitishwa ni ya mameya wa majiji na manispaa huku majina ya wenyeviti wa halmashauri yakiishia katika ngazi ya siasa ya mkoa.
Kauli hiyo ya mtendaji mkuu wa CCM inakuja wakati zikiwepo taarifa za genge la watuhumiwa wa ufisadi likianza kutoa fedha kiasi cha Sh 500,000 kwa kila diwani anayeingia katika vikao vya chama vya madiwani ambavyo vitatoa majina yasiyopungua matatu yatakayopendekezwa na Kamati kuu ili washirika wao washinde.
Genge hilo ambalo linatuhumiwa kujilimbikizia mabilioni ya fedha chafu, linatajwa na duru mbalimbali za kisiasa ndani na nje ya CCM, kwamba zimekuwa zikifanya kampeni kubwa katika kiti cha umeya wa jiji la Dares Salaam.
Dar es Salaam imekuwa ikichukuliwa kama kitovu kikuu cha shughuli mbalimbali za kiserikali, kidiplomasia na kibiashara, hivyo vita kubwa ya umeya imekuwa ikielekezwa katika kiti cha meya huyo na wenzake wa manispaa zake tatu.
Mchuano mkali katika umeya wa jiji la Dar es Salaam unatarajiwa kuwa kati ya Dk Didadas Masaburi, Jerry Slaa na Hashim Sagaf huku wengine ni Abuu Jumaa, na Bisalala Salum.
Vikumbo hivyo vya kambi hizo vikiendelea, tayari baadhi ya madiwani wilayani Ilala, wameomba CC ya CCM kupendeleza watu wenye uwezo na siyo wapiga porojo.
Hatua hiyo inatokana na baadhi ya wagombea hasa wenye nguvu za mafisadi, kuanza kutumia baadhi ya vyombo vya habari kuwapaka matope wenzao ili waonekane hawafai kushika nafasi hiyo.
Wakizungumza na Mwananchi jana jijini Dar es Salaam, kwa sharti la kutotajwa majina yao, madiwani hao walisema, kuna baadhi ya wagombea ambao wanawapaka matope wenzao ambao wanahisi ni watu wenye uwezo ili waenguliwe kwenye kamati kuu na wao kuwa na uwezekano mkubwa wa kushinda.
Halmashauri yetu ndiyo imejaa fitina, majungu, kuna mgombea mmoja ambaye anahangaika kuchafua wenzie kwenye vyombo vya habari, kwa nini anafanya hivyo sasa na si zamani, huyu anachafua wenzie ili kujenga mazingira ya kuteuliwa na kamati kuu, alilalamika mmoja wa madiwani.
Aliongeza, Tunaiomba kamati kuu ifanye maamuzi yake kwa kufuata vigezo vilivyowekwa na siyo kuangalia propaganda zinazoenezwa kuwachafua wagombea, vinginevyo tutapata meya hatari,
Diwani mwingine, alisema kamati ya maadili ifanye kazi ya ziada kuwaibua baadhi ya wagombea waliowekwa na matajiri ili kulinda maslahi kwenye biashara zao.
Unajua Ilala, ndiyo Dar es Salaam, kuna shughuli nyingi za kiuchumi ambazo zinafanyika, kamati kuu ipendekeze majina ya wagombea wenye uwezo ili waweze kusimamia ipasavyo rasilimali zilizopo, alisema
Alisema inashangaza mara nyingi propaganda chafu zinaenezwa kupitia vyombo vya habari kuhusu halmashauri hii hali inayoonyesha kuna baadhi ya wagombea hawajiamini kutokana na uwezo wao kuwa mdogo.
Hivi karibuni madiwani wengine katika halmashauri hiyo waliitahadharisha kamati kuu, kuwa makini wakati wakupendekeza mameya kutokana na baadhi ya wagombea kufadhiliwa na matajiri ili waweze kulinda maslahi yao.
CCM itapita katika hatua hiyo ngumu kisiasa baada ya kutikiswa na mbio za uspika ambazo genge la mafisadi lilituhumiwa kuweka mkakati wa kumwangusha Spika aliyejijengea umaarufu mkubwa kwa umma, Samuel Sitta.