Vita mpya mji wa Mosul nchini Irak, kuwaondoa ISIS yaanza

Richard

JF-Expert Member
Oct 23, 2006
14,939
20,399
Cu9k3eIWEAAFgeL.jpg:large


UPDATES

========

- Ndege za kivita za Marekani zimeteketeza kiwanda cha kuunda magari ya kutumia kwenye vita kichokuwa kikitumiwa na magaodo wa ISIS na hakuna kilichosalimika.

- Magaidi wa ISIS wamenza kutumia mabomu ya kujitoa mhanga na kuwashambulia majeshi ya kikurdi.

- Kuna uwezekano mkuwa magaidi wa ISIS wakatumia silaha za kikemikali pamoja na mabomu ya kujitoa mhanga.

- Tayari vijiji kadhaa vimekwishakombolewa na vikosi vya Peshmerger ambavyo vinasogea kuelekea katikati ya mji wa Mosul, bado hakuna majehi yaloingia ndani ya mji.

Operesheni mpya kubwa kabisa kufanywa ndani ya nchi ya Iraq inaanza leo na majeshi ya Iraq yanajianda kwa vita tarakitu ndani ya mji wa Mosul iliopo magharibi mwa nchi hiyo.

Peresheni hiyo inahusisha vikosi vya majeshi visivyopungua 30,000 vikiwa ni vikosi vya waasi wa kikurdi kiitwacho Peshmerga, vile vya mgambo vya Iraq na jeshi lenyewe la Iraq.

Lengo kuu la operesheni hii ni kuwandoa wapiganaji wa ISIS ambao wanakisiwa kuwa kati ya 8,000 na 10,000 mbao waliuteka mji huo mwaka 2014 mji wenye wakazi wanaokisiwa kuwa ni milioni 1.5

Mji wa Mosul ni mji wa kimkakati na unapakana na nchi ya Syria kwa upande wa mashariki operesheni hiyo itahusisha ndege za kivita za Marekani, Australia, Itali, Ufaransa na Uingereza pamoja na vikosi maalum vya ardhini vikiwemo vile vya majini vya Marekani, vikosi maalum vya Italia na Uingereza, Ujerumani na Canada.

Usiku wa jana vipeperushi vilikuwa vikiangushwa kwa wakazi wa mji huo kuonywa kujiandaa na vita hiyo ambayo haijawahi kutokea kwenye miaka ya hivi karibuni.

Lengo kuu ni kuwashambulia ISIS kadari inavyowezekana kwa mashambulizi yanayotokea kusini, mashariki na kaskazini ambapo upande wa magharibi utaachwa wazi ili kuwaruhusu magaidi wa ISIS kuelekea huko.

39753E7800000578-3842016-image-a-52_1476705828284.jpg

Upande wa magharibi mwa mji wa Mosul utaachwa wazi ili kuwanusuru magaidi wa ISIS ambao watataka kuelekea upande huo.

Mkuu wa majeshi ya nchi shirikishi Luteni jenerali Stephen Townsend amesisitiza kwamba vikosi vya ardhini vya Iraq ndivyo vitakavyokuwa vikiendesha operesheni hiyo.

Inaaaminika kwamba Marekani na nchi wahisani watatumia ndege zisizo na abiria yaani drones na ndege zeingine za kawaida za kivita kusaidia operesheni hiyo.

Waziri mkuu wa Iraq bwana Heider- al- Abadi alitangaza juu ya operesheni hiyo jana jioni nchi humo na kuwataka wananchi wawe watulivu kusubiri mji huo wa Msul kukombolewa.

111347342_TOPSHOT_-_Iraqi_forces_deploy_in_the_area_of_al-Shourah_some_45_kms_south_of_Mosul_as-large_trans++-QHDtkn10EVHquJjKACpq3MG2_Cj9ELhbl7QWEQvwH8.jpg
 
hawa mbwa wanatesa sana raia na watoto, jitihada zaidi zifanyike kukifuta hiki kikundi asibaki hata mmoja japokuwa kutakuwa na consequences zitakazoifanya dunia itahayari lakini hamna jinsi
 
Wakuu, hiyo ndiyo vita inatengenezwa kati ya nchi za magharibi na Russia/ Syria kwani hiyo njia ya kukimbilia iliyopo upande wa magharibi inaelekea nchini Syria.
sasa huko watakuwa wamemuachia mrusi awasambaratishe, Europe si salama tena, PUTIN kasababisha ISIS wa kutosha huko kwa hawa jamaa kwa kipigo anachotoa
 
Mkuu wewe ndio umejua lengo liko wap...hakuna vita hapo, kinachoangaliwa hapo ni syria tu ndio mtafutwaji hapo

Inaonekana hizi taarifa ni za kipropaganda na ukweli ni kwamba serikali ya Iraq sasa hivi inawasikiliza wanajeshi wa Hizbollah kutoka Iran ambao wamegawanyika katika makundi matatu yaani Hasbi Al- Shaabi, Badr na Kataib.

Sidhani kama hii operesheni itawapata ISIS wote, maana wengine watakimbilia Uturuki na wengine mashariki mwa Syria, hawa wa Iraq wataleta matatizo makubwa ya kiusalama nchini Uturuki.

Kama unakumbuka kwenye mdahamo wa kwanza kati ya Donald Trump na Hillary Clinton. mama Clinton alisema kwamba magadi wa ISIS watasogezwa wakimbilie kwemye mji wa Raqqa nchini Syria, ambako watatumika pamoja na waasi wa Al Nusra ambao wapo magharibi mwa Syria, kuleta tabu kwa majeshi ya Syria na Russia.

Baada ya hapo UN watatoa tamko la kusimamisha mapigano ili kuwanusuru ISIS na Al Nusra wasiuwawe na majeshi ya Syria na Russia, hivyo kuendelea kulinda upande wa mashariki mwa Syria hadi hapo uchaguzi wa Marekani utakapokamilika.
 
marekan na washirika wake wameleta balaa kubwa,vita hivi ni matokeo ya ubabe wao
 
Inaonekana hizi taarifa ni za kipropaganda na ukweli ni kwamba serikali ya Iraq sasa hivi inawasikiliza wanajeshi wa Hizbollah kutoka Iran ambao wamegawanyika katika makundi matatu yaani Hasbi Al- Shaabi, Badr na Kataib.

Sidhani kama hii operesheni itawapata ISIS wote, maana wengine watakimbilia Uturuki na wengine mashariki mwa Syria, hawa wa Iraq wataleta matatizo makubwa ya kiusalama nchini Uturuki.

Kama unakumbuka kwenye mdahamo wa kwanza kati ya Donald Trump na Hillary Clinton. mama Clinton alisema kwamba magadi wa ISIS watasogezwa wakimbilie kwemye mji wa Raqqa nchini Syria, ambako watatumika pamoja na waasi wa Al Nusra ambao wapo magharibi mwa Syria, kuleta tabu kwa majeshi ya Syria na Russia.

Baada ya hapo UN watatoa tamko la kusimamisha mapigano ili kuwanusuru ISIS na Al Nusra wasiuwawe na majeshi ya Syria na Russia, hivyo kuendelea kulinda upande wa mashariki mwa Syria hadi hapo uchaguzi wa Marekani utakapokamilika.
watashangaa jamaa wanaweka ushia na usunni pembeni na kuanza kumsaidia Assad na Mrusi.
 
Napata ukakasi sana nchi za magharibi style yao vita.. haiwezekani gaidi mmoja lakini mji mzima mnaangamiza kwa mabomu matokeo yake wanakufa watu wasio hatia...!
 
Richard nimemsikiliza Sergei Lavrov leo mchana kasema hili shambulio wanakubaliana nalo lakini bado linaleta ukakasi. Kwasababu kama shambulio litaendelea ina maana kutakuwa na wakimbizi wengi ambao mpaka sasa Shirika la msalaba mwekundu (ICRC) linasema wanaweza kufika zaidi ya laki tatu.
Ukiangalia ramani sehemu ambayo wakimbizi wanaweza kufika kwa urahisi sana ni Uturuki na Syria. Japo kuingia nchini Uturuki ni ngumu kwasababu hali ya hewa ya kisiasa haijakaa vizuri baada ya jaribio la uasi; hivyo wakimbizi watapata vikwazo vingi sana.

Hapo njia rahisi kwa wakimbizi itakuwa ni kuingia nchini Syria, na hili linawezekana kwasababu maeneo mengi ya mipaka hayapo chini ya uangalizi mzuri. Sasa wakimbizi zaidi ya laki moja wanapoingia kwenye nchi huwezi kujua mbaya ni yupi na mwema na yupi. Magaidi wanaweza wakajichanganya humo humo pamoja na wakimbizi. Na kinachotatiza zaidi ni kwamba mpaka sasa inasemekana Marekani kapeleka wakufunzi wa kijeshi kama 5000 nchini Iraq ambao humo ndani unweza kuta nao wakajichanganya na wakimbizi na kwenda kuongeza nguvu huko Syria.

Hapa anayetafutwa ni Urusi na Syria,
Tena kuna fununu zinasema kwamba Saudi Arabia imewaambia Magaidi wakimbie Mosul na kuelekea Syria. Huko watendelea kulindwa na kupewa silaha. Binafsi naamini huu uvumi kwasababu kwenye E-Mail za Clinton zilizovujishwa na Wiki-Leaks wiki lililopita zinaonyesha Hillary akikubali kwamba silaha zinafika kwa magaidi kupitia Saudi Arabia. Marekani anajifanya anawauzia waarabu kumbe wao wanazipeleka kwa magaidi huko Syria na Iraq. Sasa hapa lazima ujiulize sana kama kweli wanamapenzi mema na kuikomboa Mosul kama wanavyosema.
 
Waislam tumeruhusiwa jihad lkn sio hii inayoendeshwa na isis
 
Nia ni kuwasafisha ISIS from Iraq lakini long term plan target ni Russia and Assad, Russia watafunga virago tuu kama ilivyowatokea Afghanistan, is a long term game plan kumtia hasara Russia mpaka agundue NOT WORTH IT to defend Syria...oil price drop , heavy spending, causalities na kuwapa silaha waasi na wakorofi wa ISIS,hii vita Russia atajikuta anapigana with unknown enemy na atakimbia tuu VITA NI HELA!
 
Back
Top Bottom