Vita kubwa ya ardhi yaja tanzania

sammosses

JF-Expert Member
Jan 24, 2011
1,682
1,110
Vita kubwa ambayo itagharimu maisha ya wananchi ni migogoro ya ardhi iliyoshika kasi kubwa kwa sasa hapa nchini mwetu.Utendaji mbovu na tamu inayosababishwa na njaa za watendaji waliopewa dhamana hiyo,inapelekea taifa letu kuingia kwenye mgogoro mkubwa.Limekuwa sasa ni jambo la kawaida kwa watendaji wa serikali kupitia wizara hiyo kuwagawia wananchi viwanja bila kufuata utaratibu.Hali hiyo iliwahi kumtokea hata mkuu wa nchi kugaiwa kiwanja ambacho tayari alikwisha pewa mtu.Kama si hekima ya mheshimiwa rais,tayari ulikuwa mgogoro uliopandikizwa na wachumia tumbo wachache ambao ungechafua heshima ya rais.Sheria zipo wazi kabisa,tatizo nini linalosababisha kiwanja kugawanywa kwa watu zaidi ya watatu.Watendaji hao tunawajua,serikali nayo inawajua lakini hakuna sheria zinazochukuliwa dhidi yao.


Hali ni mbaya kwa nchi yenye kufuata utawala bora,ikiwa hali hii itaachiwa kama ilivyo sasa bila kuwawajibisha watendaji hawa.Yanayo jiri huko Mbarari ni matokeo ya wasomi wetu tuliowaamini lakini wakashindwa kujua kuwa cheo ni dhamana.Waatalamu hawa waliosomeshwa kwa kodi za Watanzania leo hii wamekuwa wachonganishi kati ya serikali na wananchi wake,kwa kugawa maeneo yaliyokuwa yana milikiwa na wananchi.Migogoro mingi tumeiona huko Babati kati ya mwekezaji na wazawa.Serikali imenyamaza kimya kwa kujua kuwa watendaji wake ndiyo waliotufikisha hapa tulipo.Machafuko haya yakizidi kushika kasi itakuwa zaidi ya Zimbabwe.


Tunabinafsisha ardhi yetu bila kunufaika na chochote,ardhi ipo chini ya wageni,nchi inakabiliwa na njaa kubwa.Hatuna miundo mbinu ya kuinua kilimo chetu ili kuwawezesha wananchi wasitegemee mvua na kuepukana na janga la njaa linalotukumba kila mwaka.Maandalizi haya ya zimamoto kwa serikali yetu kukabiliana na baa hili haina tija kwa wananchi wake,kiasi cha kauli mbiu ya kilimo kwanza kuwekwa kwenye makaratasi bila kufanyiwa kazi.Ukitazama hata vipau mbele katika bajeti yetu iliyopita,kilimo hakikupewa kimbau mbele cha kwanza kama ambavyo tunaaminishwa na wanasiasa hawa.Hatupendi kulalamika kwa kila jambo ila tumechoshwa na mipango mibovu ya serikali kwa kuwalinda watendaji wake bila sababu za msingi.


Ardhi yetu leo hii imekuwa sababu ya kuwatanguliza wazawa mbele ya haki kabla ya muda uliopangwa na Mungu.Nasema hivyo nikimaanisha kuwa wawekezaji waliohodhi ardhi yetu wanatumia nguvu kubwa kuwauwa wazawa kwa kisingizio cha wazawa kuingilia maeneo yao.Wakati mwingine chombo chetu cha dola kinawasidia wawekezaji hawa kufupisha maisha ya wazawa kwa kuwapiga risasi za moto kama yaliyokwishatokea huko Nyamongo.Serikali mpaka leo imekuwa ikishirikiana na wageni hawa kiasi cha kushindwa kutolea maamuzi.Mbaya zaidi zinaundwa tume kwa kutumia kodi za walalahoi matokeo yake ripoti zake zinaliwa panya kwenye makabrasha.

Serikali isipokuwa makini kwa hali inajionyesha sasa ni hatari kwa mustakabali wa amani yetu.Wananchi wamechoshwa kugombanishwa kwa kupambanishwa viwanja.Ipo siku watakuja lipa deni la usaliti.Wananchi wamechoshwa kinachofuata ni kujichukulia sheria mkononi,kwani wamekosa mtu wa kuwatetea ilichobaki watajitetea wenyewe kwa njia watakazoona zinafaa.Ardhi ni rasilimali ndiyo maana hata mwalimu alitoa kipau mbele cha pili kitakacho muwezesha mtu apige hatua za kimaendeleo.Rasilimali watu ni kubwa lakini maendeleo hayo yatapatikana vipi ikiwa ardhi inaporwa na wageni kwa kisingizio cha uwekazaji.Zama za mwalimu tuliamini kilimo ni uti wa mgongo wa maendeleo ya nchi yetu.Zilionekana juhudi binafsi kuhakikisha ardhi inatumika vizuri kwa manufaa ya wote,tena mbaya zaidi hata zana tulizotumia zilikuwa duni lakini kilimo kilikuwa na tija,kilichomuwezesha mlalahoi kukidhi matakwa yake na kumuwezesha kulipa kodi ya maendeleo.

Vyama vya ushirika vilikuwa nguzo kuu na muhimu kilichotumika kama soko na chombo cha kumkomboa mkulima huyo wa jembe la mkono.Hata kama serikali ikitumia nguvu kubwa kuvisimamisha viwe na nguvu kama zamani bado tatizo lipo kwa wanachama wake ambao ndiyo wakulima.Tunaitaka serikali iliangalie suala hili la ardhi kwa mapana na marefu vinginevyo vita kubwa nchi mwetu ni vita ya ardhi.




Mnyonge mnyongeni kilicho chake abaki nacho,na ndicho atakachojitetea nacho.
 
ninachokiona siku izi sheria ya ardhi na mipango ya matumiz bora ya ardhi haifatwi, watendaji wa wizara ya ardhi na halmashauri za wilaya wangekuwa wanafanya wajibu wao haki ingetendeka
 
Suala la ardhi ni issue toka enzi na enzi!
Migogoro yake huwa inakuwa minimized tuu ila huwa haiishi!
 
Vita kubwa ambayo itagharimu maisha ya wananchi ni migogoro ya ardhi iliyoshika kasi kubwa kwa sasa hapa nchini mwetu.Utendaji mbovu na tamu inayosababishwa na njaa za watendaji waliopewa dhamana hiyo,inapelekea taifa letu kuingia kwenye mgogoro mkubwa.Limekuwa sasa ni jambo la kawaida kwa watendaji wa serikali kupitia wizara hiyo kuwagawia wananchi viwanja bila kufuata utaratibu.Hali hiyo iliwahi kumtokea hata mkuu wa nchi kugaiwa kiwanja ambacho tayari alikwisha pewa mtu.Kama si hekima ya mheshimiwa rais,tayari ulikuwa mgogoro uliopandikizwa na wachumia tumbo wachache ambao ungechafua heshima ya rais.Sheria zipo wazi kabisa,tatizo nini linalosababisha kiwanja kugawanywa kwa watu zaidi ya watatu.Watendaji hao tunawajua,serikali nayo inawajua lakini hakuna sheria zinazochukuliwa dhidi yao.

Mnyonge mnyongeni kilicho chake abaki nacho,na ndicho atakachojitetea nacho.

Angekua na hekima migogoro isingekuwepo kabisa. Hekima hii inaishia kutatua migogoro inayomkuta yeye tu ???
 
tufanye nini sasa Watanzania wenzangu ili kuondokana na janga hili.Nafikiri tatizo hapa lipo kimfumo zaidi ndiyo maana kila tunapobadili viongozi katika kila kipindi cha miaka mitano tunaowachagua ni wale wale waliotokana na mfumo mbovu na ndiyo maana hata ile kasi ya yule mama wa makazi aliyeheshimika sana alipokuwa UN sasa imegubikwa na wimbi la wasiwasi kiutendaji ama kutokana na mfumo dume alioukuta au ana mashinikizo ya wakubwa katika kazi zake.

Ukijaribu kutafakari kwa kina utaona hata zile open space zilizotengwa kwaajili ya watoto wetu nazo zimeingilia na vigogo wenye mikono mirefu ndani ya serikali.Hali hii ya migogoro ya ardhi ni janga kubwa la kitaifa na jamii ya wapenda amani.Wakati wa Mwalimu tulijivunia mashamba yetu ya ngano ambayo ilitosheleza mahitaji ya wakati huo,na si kweli kwamba hapakuwa na upungufu wa chakula la hasha bali juhudi za dhati za kupambana katika kujikwamua kutokana na janga hilo zilionekana dhahiri tofauti na hivi sasa,ambapo kila mmoja anajichukulia chake mapema,

Hofu kuu inayotanda siku hadi kutokana na kukosekana juhudi za makusudi kutokomeza hali hii ya kugawa ardhi yetu kwa wageni inapelekea watu kukosa imani na serikali yao waliyoiamini.Imefikia watu kudhani hata wao wapo hatarini ama kuuzwa au wameshauzwa ila wanasubiri kukabidhiwa kwa mnunuzi.Wananchi wa Zimbabwe angalau walinufaika kwa mashamba yao yaliyokuwa yameshikiliwa na wakoloni wale kwa kukidhi haja zao za chakula tofauti na sisi hapa kwetu.Ardhi imekwenda,chakula hakuna unategemea nini kama si ulofa kwa kila Mtanzania unawezekana.

Mapinduzi ya kijani hayaonekani kama dhana nzima inavyotaka tuelewe.Kilimo kwanza kimekuwa kisiasa zaidi kuliko kivitendo hali inayoonekana ni uchakachuaji wa sera na ufundi wa kauli mbiu kila kukicha.Haingi akilini serikali kunadi kauli mbiu yake hiyo ya kilimo kwanza wakati hakuna mikakati inayoonyesha utekelezaji kwa vitendo wa dhana nzima.Usanii huo tunauona kwa vitendo kwa serikali yetu kutuletea mashine(power tiller) za kulimia zisizo na tija kutokana na asili ya ardhi yetu.Yawezekana ukawa ni mradi wa mkubwa mmoja kutumia mwamvuli huo wa kilimo kwanza kuweza kufanikisha malengo yake ya kibiashara kwa kuuza power tiller.Mapinduzi hayo ya kijani yalitakiwa yaenda sanjari na utumiaji wa kilimo cha umwagiliaji.Mathalani ukiangalia nchi kama Libya ilionyesha mapinduzi ya kweli ya kijani kwa kuweza kulibadilisha jangwa na kuweza kujipatia chakula.Tusiwe wepesi wa kuandika kwenye makaratasi vitu ambavyo tuna imani hatuwezi kuvisimamia utekelezaji wake.
 
tufanye nini sasa Watanzania wenzangu ili kuondokana na janga hili.Nafikiri tatizo hapa lipo kimfumo zaidi ndiyo maana kila tunapobadili viongozi katika kila kipindi cha miaka mitano tunaowachagua ni wale wale waliotokana na mfumo mbovu na ndiyo maana hata ile kasi ya yule mama wa makazi aliyeheshimika sana alipokuwa UN sasa imegubikwa na wimbi la wasiwasi kiutendaji ama kutokana na mfumo dume alioukuta au ana mashinikizo ya wakubwa katika kazi zake.

Ukijaribu kutafakari kwa kina utaona hata zile open space zilizotengwa kwaajili ya watoto wetu nazo zimeingilia na vigogo wenye mikono mirefu ndani ya serikali.Hali hii ya migogoro ya ardhi ni janga kubwa la kitaifa na jamii ya wapenda amani.Wakati wa Mwalimu tulijivunia mashamba yetu ya ngano ambayo ilitosheleza mahitaji ya wakati huo,na si kweli kwamba hapakuwa na upungufu wa chakula la hasha bali juhudi za dhati za kupambana katika kujikwamua kutokana na janga hilo zilionekana dhahiri tofauti na hivi sasa,ambapo kila mmoja anajichukulia chake mapema,

Hofu kuu inayotanda siku hadi kutokana na kukosekana juhudi za makusudi kutokomeza hali hii ya kugawa ardhi yetu kwa wageni inapelekea watu kukosa imani na serikali yao waliyoiamini.Imefikia watu kudhani hata wao wapo hatarini ama kuuzwa au wameshauzwa ila wanasubiri kukabidhiwa kwa mnunuzi.Wananchi wa Zimbabwe angalau walinufaika kwa mashamba yao yaliyokuwa yameshikiliwa na wakoloni wale kwa kukidhi haja zao za chakula tofauti na sisi hapa kwetu.Ardhi imekwenda,chakula hakuna unategemea nini kama si ulofa kwa kila Mtanzania unawezekana.

Mapinduzi ya kijani hayaonekani kama dhana nzima inavyotaka tuelewe.Kilimo kwanza kimekuwa kisiasa zaidi kuliko kivitendo hali inayoonekana ni uchakachuaji wa sera na ufundi wa kauli mbiu kila kukicha.Haingi akilini serikali kunadi kauli mbiu yake hiyo ya kilimo kwanza wakati hakuna mikakati inayoonyesha utekelezaji kwa vitendo wa dhana nzima.Usanii huo tunauona kwa vitendo kwa serikali yetu kutuletea mashine(power tiller) za kulimia zisizo na tija kutokana na asili ya ardhi yetu.Yawezekana ukawa ni mradi wa mkubwa mmoja kutumia mwamvuli huo wa kilimo kwanza kuweza kufanikisha malengo yake ya kibiashara kwa kuuza power tiller.Mapinduzi hayo ya kijani yalitakiwa yaenda sanjari na utumiaji wa kilimo cha umwagiliaji.Mathalani ukiangalia nchi kama Libya ilionyesha mapinduzi ya kweli ya kijani kwa kuweza kulibadilisha jangwa na kuweza kujipatia chakula.Tusiwe wepesi wa kuandika kwenye makaratasi vitu ambavyo tuna imani hatuwezi kuvisimamia utekelezaji wake.







migogoro ya ardhi kamwe hata kama angekuja nani haiwez kuisha cha msingi tu ni kuipunguza. kila mtu anapigania kupata ardhi hivo migogoro haiepukiki!
 
Ni vizuri kama ingeonekana nia ya dhati ya kuipunguza,tatizo si kila mtu kugombea ardhi,tatizo hapa ni uchonganishi unaofanywa na watendaji wa wizara hiyo.Jambo hili linahitaji uzalendo wa kweli kulitatua kuliko kuogozwa zaidi na njaa zetu.
 
Back
Top Bottom