Vita dhidi ya Ufisadi: Tujiadhari na kina Marando!

jmushi1

Platinum Member
Nov 2, 2007
24,967
22,476
CCM wezi, adai Mabere Marando

na Prisca Nsemwa

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimezidi kutuhumiwa kuwa kinashinda chaguzi mbalimbali kwa kuiba kura.

Baada ya viongozi kadhaa wa kambi ya upinzani kutoa tuhuma hizo kwa nyakati tofauti, hususan baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2005, tuhuma za hivi karibuni zimetolewa na wakili maarufu hapa nchini ambaye pia ni muasisi wa mageuzi, Mabere Marando.

Akizungumza jana katika kongamano la kutathimini hali na mwelekeo wa vyama vya siasa kwa kipindi cha miaka mitatu baada ya uchaguzi mkuu wa 2005, lililoandaliwa na Asasi ya Maendeleo Tanzania (TADIP), Marando alisema udanganyifu na wizi wa kura unaofanywa na CCM wakati wa uchaguzi, ni suala linalosababisha kuwepo kwa mchafuko wa kisiasa visiwani Zanzibar.

Marando ambaye aliwahi kuwa Mbunge wa Rorya kwa tiketi ya NCCR-Mageuzi, alisema bila kuwepo ukweli na uwazi wakati wa kuhesabu kura, CCM itaendelea kuiba kura na kupata ushindi usio halali jambo ambalo litazidisha mgogoro wa kisiasa hapa nchini, hasa visiwani Zanzibar.

Alitahadharisha kuwa mgogoro wa kisiasa Zanzíbar unahatarisha usalama wa wananchi wa visiwani humo na pia unachafua sifa nzuri ya Tanzania kuwa ni nchi yenye amani katika Bara la Afrika.

Alisisitiza kuwa, tuhuma zinazoiandama CCM kuiba kura za urais Zanzíbar hazina ubishi na kwamba viongozi wa serikali iliyopo madarakani wanatambua ukweli huo, lakini wanashindwa kuweka wazi.

“Ni kweli kilichofanyika Zanzibar kipindi cha uchaguzi mwaka 2005 ni wizi wa kura, hakuna mtu ambaye anaweza kubisha na hata serikali inalifahamu hilo ila haiwezi kuwa wazi,” alisema Marando.

Akizungumza kuhusu madai ya kuwepo kwa mabadiliko ya katiba, alisema hayatasaidia kubadili matokeo ya chaguzi zinazofanyika hapa nchini kwa sababu wizi wa kura katika chaguzi mbalimbali utaendelea kwa kuwa serikali hutumia zaidi fedha ili kushinda.

Alisema, vyombo vya usalama wa taifa kwa kushirikiana na serikali vinaongoza kuiba kura ili kukisaidia chama kilichopo madarakani kiendelee kutawala.

Marando aliwataka wanasiasa wa kambi ya upinzani kufahamu kuwa suala la wizi wa kura kwa serikali iliyopo madarakani si jambo la kushangaza tena, hivyo hoja za msingi kwa vyama vya upinzani ni kujipanga na kujadili mbinu thabiti za kukabiliana na wizi huo.

Aidha, alivitaka vyama vya upinzani kuwa na hoja nzito zitakazokubalika kwa wananchi ili kuwajengea imani badala ya kudai kuendelea kulilia katiba mpya ama mabadiliko ya sheria.

“Vyama vya upinzani tusikate tamaa kwa kuibiwa kura, suala hapa ni kujipanga kwa kuwa na hoja nzito ili kuweza kufanikiwa katika chaguzi zijazo,” alisema.

Aidha, alivishauri vyama vya upinzani kuelekeza nguvu zake vijijini ili kujiwekea misingi bora kwa wananchi wa huko ambao wengi wao ndio wapigakura.

Alisema, yaliyotokea Kenya wakati wa uchaguzi mkuu hadi kusababisha machafuko ni zaidi ya wizi wa kura na kuongeza kuwa uporaji wa kura uliofanyika Kenya ndio unaofanyika sasa Zimbabwe, mambo ambayo yanaweza kusababisha kuibuka machufuko yanayohatarisha maisha ya wananchi wa kawaida.

Naye Mhadhiri kutoka Idara ya Sayansi ya Siasa na Utawala Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Bashiru Ally, alisema tatizo la Tanzania si sheria wala katiba bali matumizi mabaya ya pesa za walipakodi wakati wa uchaguzi yanayofanywa na serikali.

“Tatizo lipo kwenye uchaguzi, wagombea wote si wasafi hata kidogo, wanakuwa na matumizi mabaya ya pesa, wanawalaghai wananchi na hili nina uhakika nalo,” alisema Ally. Katika mjadala huo, zaidi ya wadu 120 kutoka asasi mbalimbali, taasisi za serikali na vijana walishiriki. Huo ni mjadala wa tatu kufanywa na TADIP ambako mwaka jana ulizungumzia tathimini ya miaka 15 ya vyama vingi hapa nchini.
 
Akizungumza kuhusu madai ya kuwepo kwa mabadiliko ya katiba, alisema hayatasaidia kubadili matokeo ya chaguzi zinazofanyika hapa nchini kwa sababu wizi wa kura katika chaguzi mbalimbali utaendelea kwa kuwa serikali hutumia zaidi fedha ili kushinda.

Alisema, vyombo vya usalama wa taifa kwa kushirikiana na serikali vinaongoza kuiba kura ili kukisaidia chama kilichopo madarakani kiendelee kutawala.

Marando aliwataka wanasiasa wa kambi ya upinzani kufahamu kuwa suala la wizi wa kura kwa serikali iliyopo madarakani si jambo la kushangaza tena, hivyo hoja za msingi kwa vyama vya upinzani ni kujipanga na kujadili mbinu thabiti za kukabiliana na wizi huo.

Aidha, alivitaka vyama vya upinzani kuwa na hoja nzito zitakazokubalika kwa wananchi ili kuwajengea imani badala ya kudai kuendelea kulilia katiba mpya ama mabadiliko ya sheria.

“Vyama vya upinzani tusikate tamaa kwa kuibiwa kura, suala hapa ni kujipanga kwa kuwa na hoja nzito ili kuweza kufanikiwa katika chaguzi zijazo,” alisema.
Ni muhimu tujiadhari na watu kama kina Marando ambao licha ya kwamba wana ujuzi wa kisheria bado wanadai katiba haina haja ya mabadiliko!Ni Nyaucho huyu huyu aliyeu uwa upinzani wakati wa vurugu zake na Mrema huko NCCR-Mageuzi..na baadae kupewa madaraka na CCM...na sasa kutumia taaluma yake bila msimamo kwa kuzungumza maneno ambayo si rahisi kujua kama ni mpinzani ama CCM lakini ni mwenye kujali tumbo tu!Kama yeye na kina Lamwai!Hatutaki walete vurugu!Kwani wao wamesha expire na sasa tuna wakina tundu lissu na kina Slaa upande wa upinzani na watu wengine wenye nia nzuri na wazalendo ambao bado wamebaki kwenye mtego wa chama bila ya kujua kuwa ni hatua gani waichukue!Tunawatakia kila la kheri..either kufanya mabadiliko makubwa ndani ya chama chao..ama kujiunga na wapinzani na kuleta chachu ya uwajibikaji na maendeleo!Marando yeye akae pembeni kwanza!
 
JMushi,
Katika dunia ya leo hakuna haja ya kuogopa mawazo tofauti cha msingi ni kujadili hoja kwa kueleza yale unayodhani ni kwanini katiba ibadilishwe na si kuhadharisha watu na kina Marando.

Hoja yako hii ni dhaifu sana.
 
Ni kweli ni hoja dhaifu
Sio hoja dhaifu kwasababu Marando alishiriki kikamilifu kuumaliza upinzani yeye na Lamwai kwa kutumia usomi wao..hawakutaka kuwa upande wa haki..na ndio maana wamelipwa fadhila!Marando akapewa ubunge wa East Africa kwa kura nyingi za CCM huko bungeni dhidi ya kura chache za upinzani ambao waliona kuwa ni msaliti!Mimi sina chama ila ninaamini kuwa upinzani na utofauti wetu wa kimawazo ni namna za tofauti na mitizamo ya tofauti ya namna ya kuwatumikia wananchi na kuwaletea maendeleo na sio kuwa wajali matumbo na mafuska wa kisiasa kama walivyoonyesha Marando na mwenzake Lamwai!
 
JMushi,
Katika dunia ya leo hakuna haja ya kuogopa mawazo tofauti cha msingi ni kujadili hoja kwa kueleza yale unayodhani ni kwanini katiba ibadilishwe na si kuhadharisha watu na kina Marando.

Hoja yako hii ni dhaifu sana.
Katiba ni lazima ibadilishwe kama kweli tunataka viongozi wawe wawajibikaji na maslahi ya taifa kusimamiwa kikamilifu na mwananchi wa kawaida kulindwa na katiba hiyo!Kwa maoni yangu hivi sasa siasa za vyama zinawekwa mbele zaidi ya maslahi ya taifa!Maamuzi magumu yanayowagusa raia wote bila kujali itikadi zao hayahitaji mwongozo wa chama..bali mwongozo wa katiba!Ni wakati wa kuiangalia katiba ya nchi yetu ambayo ndio kimbilio la mwisho la myonge!kutumia katiba inayomlinda kudai haki na mabadiliko!
 
damn this puppet amerudi tena?the guy is dishonest to the core na politician kama huyu is like a poison in any democracy,hawa ndio wameweka base ya siasa za kitapeli Tanzania na ndio maana tuna suffer
 
damn this puppet amerudi tena?the guy is dishonest to the core na politician kama huyu is like a poison in any democracy,hawa ndio wameweka base ya siasa za kitapeli Tanzania na ndio maana tuna suffer
Wanatayarishwa/Kujitayarisha..wanaanza kujipanga ili kuleta tafrani nyingine ambayo itapelekea nothing to be done!Wanaibukia kipembeni pembeni ili kuanza kujikita mawazoni mwa wananchi!wanaona kuna ulaji zaidi unakuja kwenye hayo makesi ya ufisadi!Usishangae akiwa anajipanga kwenye timu ili na yeye aendelee kulijaza tumbo!na Lamwai we subiri tu utamsikia!So ndio maana natoa taadhari kwasababu anaanza kuyapima maji!Halafu Tanzania Daima inadiriki kumpa cheo cha uasisi wa upinzani?!KWA MAONI YANGU MABERE NYAUCHO MARANDO NI MWENYE MURDER CASE YA UPINZANI!AKAE MBALI NA AENDELEE KULIJAZA TUMBO LAKE KWENYE HUO UBUNGE ALIOPEWA NA CCM..NA AWAACHE WAHANGA WAIPIGANIE NCHI YAO!
 
Binafsi sina sababu ya kumwogopa Marando et al,Kwani Marando kapewa cheo gani tena kwenye chama cha kijani mpaka tujihadhari naye?Kama walivunja upinzani zamani zile basi ijulikane leo wana inji si bendera fuata upepo kwa kununuliwa kwa kuongwa kanga na kofia na fulana.Hata wasipobadili katiba tutapambana kwa silaha tulizo nazo.NO RETREAT NO SURRENDER
 
Binafsi sina sababu ya kumwogopa Marando et al,Kwani Marando kapewa cheo gani tena kwenye chama cha kijani mpaka tujihadhari naye?Kama walivunja upinzani zamani zile basi ijulikane leo wana inji si bendera fuata upepo kwa kununuliwa kwa kuongwa kanga na kofia na fulana.Hata wasipobadili katiba tutapambana kwa silaha tulizo nazo.NO RETREAT NO SURRENDER

Kweli kabisa SingleD,

kuna haja gani ya kumuogopa Marando ambaye tayari yuko kijani kama kina Lamwai na wengine? Ngoja aseme anachopenda lakini for the rest of us maisha ni kwenda mbele.

You go to war with the army you have - Donald Rumsfeld
 
Kweli kabisa SingleD,

kuna haja gani ya kumuogopa Marando ambaye tayari yuko kijani kama kina Lamwai na wengine? Ngoja aseme anachopenda lakini for the rest of us maisha ni kwenda mbele.

You go to war with the army you have - Donald Rumsfeld

...hakuna mtu anamwogopa marando ila asitupe lecture ya wizi wa kura wakati huo huo anatuambia tatizo sio katiba,wakati ukiangalia vizuri matatizo yote ya wizi wa kura yako rooted kutokana na hiyo katiba,marando njaa yake na tabia zake za kitapeli zilisaidia sana kurudisha nyuma upinzani.
 
Kweli kabisa SingleD,

kuna haja gani ya kumuogopa Marando ambaye tayari yuko kijani kama kina Lamwai na wengine? Ngoja aseme anachopenda lakini for the rest of us maisha ni kwenda mbele.

You go to war with the army you have - Donald Rumsfeld
Kuwa kijani haina maana kwamba hawatakuwa na uwezo wa kuleta mikanganyiko kwa kauli zao tata ambazo zinaonyesha ufuska wa kisiasa kwa kuwa mguu mmoja nadani na mwingine nje..they're distractive and divisive evil forces able and ready to once again disrupt the freedom movement!Kwa kujidai kuwa wana sympathize na ku ushauri upinzani wakakti ni wao walioshiriki ku uua..hilo kwangu lina mashaka!
Cheo alichopewa ni pale alipopigiwa kura za fadhila na wabunge wa CCM pale walipomchagua huko bungeni kuwa mwakilishi wa Tanzania kwenye bunge la east Africa!Wapinzani wao walikuwa na chaguo jingine lakini CCM kwa kusaidiana na pandikizi lao Marando waliwazidi nguvu upinzani!
Ni wazi kuwa hawana nia nzuri popote pale wanapopeleka pua zao!
 
...hakuna mtu anamwogopa marando ila asitupe lecture ya wizi wa kura wakati huo huo anatuambia tatizo sio katiba,wakati ukiangalia vizuri matatizo yote ya wizi wa kura yako rooted kutokana na hiyo katiba,marando njaa yake na tabia zake za kitapeli zilisaidia sana kurudisha nyuma upinzani.
Ni kweli kabisa mkuu Koba!Mrando amesahau kuwa wizi wa kura na wa wanasiasa ni kitu kimoja!KWANI NANI ASIYEJUA KUWA MARANDO ALINUNULIWA YEYE PAMOJA NA KURA?Akae pembeni asituletee kichefu chefu!Anajua sheria lakini bado ana yale mawazo ya kukandamiza haki za wananchi kwa maslahi ya tumbo lake!Mwasisi wa upinzani?!Marando..these guys must be kidding!
 
Kuwa kijani haina maana kwamba hawatakuwa na uwezo wa kuleta mikanganyiko kwa kauli zao tata ambazo zinaonyesha ufuska wa kisiasa kwa kuwa mguu mmoja nadani na mwingine nje..they're distractive and divisive evil forces able and ready to once again disrupt the freedom movement!Kwa kujidai kuwa wana sympathize na ku ushauri upinzani wakakti ni wao walioshiriki ku uua..hilo kwangu lina mashaka!
Cheo alichopewa ni pale alipopigiwa kura za fadhila na wabunge wa CCM pale walipomchagua huko bungeni kuwa mwakilishi wa Tanzania kwenye bunge la east Africa!Wapinzani wao walikuwa na chaguo jingine lakini CCM kwa kusaidiana na pandikizi lao Marando waliwazidi nguvu upinzani!
Ni wazi kuwa hawana nia nzuri popote pale wanapopeleka pua zao!

Alichosema je kina ukweli?
 
Alichosema je kina ukweli?
Kuhusu wizi wa kura ni kweli..lakini yeye haja qualify kutueleza kuhusu wizi wa kura!Yeye mwenyewe aliibwa ama alinunuliwa!sasa anataka kutueleza kuhusu wizi wa kura!Yeye ni mwanasheria mzuri tu..lakini he can't have it both ways!abaki huko aliko aendelee kula tu..nafikiri uanasheria na uzalendo ni vitu viwili proven to be far away from each other during this man's courier!
 
Kuhusu wizi wa kura ni kweli..lakini yeye haja qualify kutueleza kuhusu wizi wa kura!Yeye mwenyewe aliibwa ama alinunuliwa!sasa anataka kutueleza kuhusu wizi wa kura!Yeye ni mwanasheria mzuri tu..lakini he can't have it both ways!abaki huko aliko aendelee kula tu..nafikiri uanasheria na uzalendo ni vitu viwili proven to be far away from each other during this man's courier!

Mimi nakubaliana nawewe katika hili. Labda kama ungeungana naye katika hoja yake na kisha umpinge yeye binafsi pembeni. Au wewe unaonaje?
 
Mimi nakubaliana nawewe katika hili. Labda kama ungeungana naye katika hoja yake na kisha umpinge yeye binafsi pembeni. Au wewe unaonaje?
Nisawa tu ila mimi nimefanya utafiti na uzoefu wa kisiasa unaonyesha kuwa anataka kurudi mawazoni mwa watu!Kumbuka makala hiyo imemtaja kuwa ni mwasisi wa upinzani!Hapo ndio nilipojua kuwa ana agenda maybe kamtumia mwandishi..lakini nia ya huyu jamaa siyo nzuri!Narudia tena jamaa anayapima maji na anajitayarisha kurudi kwenye ulingo wake wa kawaida wa divisive and destruction!Sawa tu tsikilize kwani ni haki yake kutoa maoni..lakini tahadhari ni lazima!
 
Huyu Mabere Marando alikuwa mwanasiasa machachari sana nchi ya Tanzania ilipoingia kwenye mfumo wa vyama vingi vya siasa.
Hivi yuko wapi siku hizi?
Ni nini kimemaliza umaarufu wake katika uwanja wa siasa hapa TZ?
 
Huyu Mabere Marando alikuwa mwanasiasa machachari sana nchi ya Tanzania ilipoingia kwenye mfumo wa vyama vingi vya siasa.
Hivi yuko wapi siku hizi?
Ni nini kimemaliza umaarufu wake katika uwanja wa siasa hapa TZ?

Mabere Marando sasa hivi ni Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki kama sikosei. Katulizwa huko! In fact NCCR Mageuzi chini ya Mrema iliyumba sana kutokana na Mrema kuwa mropokaji majukwaani mara kwa mara na kina Marando na Lamwai kujikuta kila siku wako Mahakamani kumtetea mwenyekiti wao badala ya kufanya kazi zao za Kibunge na Kichama!

Pia inasemekana ni mbinu za CCM zilizotumika kukisambaratisha Chama, kumweka Lamwai benchi bila kazi yoyote na kisha kumrudisha CCM na kumpa kazi. Tangu hapo wote wakawa kimya kabisa!

Pia CCM mwaka 2005 waliweka nguvu nyingi sana kwenye majimbo yote ya uchaguzi ambayo wabunge wake walikuwa wa vyama vya Upinzani. Kwa mfano kwenye jimbo la Benedicto Mutungirehi ambaye alikuwa machachari bungeni kuliko Zitto Kabwe. Lakini la kuvunda halina ubani, wakamwekea nguvu nyingi Mutungirehi, akaibuka Zitto Kabwe!

Sijui kwa sasa Mutungirehi anafanya nini, lakini nina imani 2010 atagombea tena ubunge! Akirudi bungeni na kuongeza nguvu kwa kina Zitto na Slaa, na tukaapata wabunge wengine kama watano tu walio machachari, nchi itakwenda na bunge litakaa sawa!

Hawa kina Mramba, Yona, Patel, Mgonja na wenzao mnaowaona wana kesi mahakamani ni juhudi za wabunge wachache (na za JF pia), matunda yanaonekana na wanatakiwa kupewa moyona kuongezewa nguvu zaidi!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom