Visasi vya JK kwa watu wa Arusha? Ahamishia mkutano wa wakuu wa EAC Dar

Ni kelele za mfa maji, iko siku atajiona hata yeye kuwa hajui anachokifanya, mbona kwenye kikombe alienda kwa miguu yake, sasa anashindwa nini. One day YES!
 
Huyo JK " WENU " alitoa sababu gani?......nadhani washauri wake mtakuwa mlimuambia kuwa tayari anapewa za uso huku JF

Heshima kwako Phillemon Mikeal,

Mkuu JF iko juu sana washauri wake watakuwa wamemwambia jana TBC1 walikuwa wakimwonyesha JK akiifungua MT Meru Hotel ndani ya hotuba yake aliusifia mji wa Arusha kwamba ni mji wa kimataifa kwasababu mikutano mingi ya kimataifa inafanyika hapa pia alisisitiza serekali yake itaendelea kutoa support ili mikutano mingi mkubwa ifanyike jijini Arusha.

Niligundua tayari sisimizi wake wamemtonya juhudi zikafanyika TBC1 ikatumika kutujibu habari ndiyo hiyo.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
kisasi cha JK kwa Arusha kilianza mara baada ya uchaguzi mkuu na alianzia na mgao wa umeme ambao unaendelea hata sasa kwa makali makubwa katika vkata ambazo CHADEMA ilikinyima chama cha CCM na wagombea wake akiwemo rais kura. Maeneo ya Kimandolu na vitongoji vyake mgao wa umeme ulianza tarehe 5/11/2010 hadi leo huku wakitoa visingizio mara transformer imeharibika Singida , mara maji Mtera n.k hadi sasa. Mgao ni mkali wa zaidi ya masaa 10 hadi 14 siku nne kwa wiki.

Sisi tuligundua hizi ni chuki na siasa za visasi za CCM dhidi ya wananchi wa Arusha. Wakati wa Kampeni barabara zilianza kutengenezwa ila baada ya matokeo ya uchaguzi zoezi hilo lilitoweka ghafla hivyo kuacha barabara za pembezoni mwa manispaa ya Arusha zikiwa milima na mabonde.


Ila tunamwambia RAIS AHAMISHE NA JENGO LA ICC NA MBUGA ZA WANYAMA APELEKE MSOGA NA HATA MLIMA KILIMANJARO AONDOKE NAO ILA HATA AKIGOMBEA KESHO HAKUNA MWANANCHI WA ARUSHA MWENYE KURA ZA KUPOTEZA KUWAPA
MAFISADI WA CCM
.

Akitaka kujua asiruke Arusha arudi baada ya miaka 10 atashangaa kuona mabadiliko kwani watu wa kanda za kaskazini hatujazoea spoon fed ni watu wa kujituma tu hata kama rais atasusa. Tena hatuhitaji wacheza viduku hapa. Kwanza JK ameikuta Arusha ikiwa hivihivi na ataiacha ikiwa hivi hivi , hana cha kuiongezea wala hataweza kupunguza kitu chochote.
 
Namhurumia rais kama yuko hivi basi ana mambo ya kiswahili sana na ndo maana hakui kabisa ; akiendelea hivi itabidi wakuu tuwavike ccm gauni
 
Ni kweli,ni mtu hatari kwa visasi. Alipoambiwa asubiri mwaka 1995 na Baba wa Taifa, marehemu Mwl JK Nyerere tangu hapo hajatumia neno "Baba wa Taifa" anapomrefer Mwalimu badala yake anamwita mzee.
Tusimkatalie, nae anasoma kinachoandikwa humu.Na hili la kisasi kwa Arusha is a serious alegation,mwache atajibu kwa njia moja au nyingine hasa tega sikio kwa Rweyenyamu.
 
Heshima kwako Phillemon Mikeal,

Mkuu JF iko juu sana washauri wake watakuwa wamemwambia jana TBC1 walikuwa wakimwonyesha JK akiifungua MT Meru Hotel ndani ya hotuba yake aliusifia mji wa Arusha kwamba ni mji wa kimataifa kwasababu mikutano mingi ya kimataifa inafanyika hapa pia alisisitiza serekali yake itaendelea kutoa support ili mikutano mingi mkubwa ifanyike jijini Arusha.

Niligundua tayari sisimizi wake wamemtonya juhudi zikafanyika TBC1 ikatumika kutujibu habari ndiyo hiyo.


Safi tulijuwa lazima atajitetea tu...nawashangaa watu waliokuwa wanakebehi hii thread walifikiri tulikurupuka......
Ukweli ni kuwa kwenye kikao cha concil of ministers kilichofanyika Arusha ...kikiwashirikisha mawaziri wa jumuia na wasaidizi wa usalama wa nchi husika[protocal]....walipingana na vikali na kushangazwa na serikali kulazimisha mkutano ujue dar....hii inatokana na miundombinu ya dar kutokuwa rafiki ......na inaonyesha mara zote wakiwa dar wanaopata tabu ni wasaidizi wa hao viongozi...malalamiko yalikuwa dhahiri....Arusha imeshapata kupokea marais 77 kwa mpigo na kinachosaidia ni kuwa pamoja na jiji kuwa dogo tatizo la msongamano ni dogo......na hoteli wanazofikia ziko at a walking distance toka ukumbini...

NARUDIA tena ..jiji la dar tukitaka lijipange kimikutano we have to take initiative kama ya kampala ..wao kuelekea Commonwealth ..walijenga Convetion center na village ..ambayo ili accomodate wakuu wa nchi na wasaidizi wao....offcourse village ya kwanza ya viongozi East Africa alijenga Mwalimu Nyeree pale Arusha yaani 77 hotel...ile ilikuwa mahsusi kwa ajili ya kuwapokea wakuu wa nchi 77 walifika Arusha miaka hiyo...ni masikitiko makubwa pia kuwa ile hoteli iliachwa ikafa na hata aliyeuziwa mbia wake Kikwete wa Kempsiki anasua sua kuifufua ...na inatia shaka kama anataka kubadili matumizi ya eneo la 77 au atajenga hoteli nyingine itakayosaidia kuboresha utalii wa mikutano Arusha...kama nayo ameisusa tujuwe!!!
 
Heshima kwako Phillemon Mikeal,

Mkuu JF iko juu sana washauri wake watakuwa wamemwambia jana TBC1 walikuwa wakimwonyesha JK akiifungua MT Meru Hotel ndani ya hotuba yake aliusifia mji wa Arusha kwamba ni mji wa kimataifa kwasababu mikutano mingi ya kimataifa inafanyika hapa pia alisisitiza serekali yake itaendelea kutoa support ili mikutano mingi mkubwa ifanyike jijini Arusha.

Niligundua tayari sisimizi wake wamemtonya juhudi zikafanyika TBC1 ikatumika kutujibu habari ndiyo hiyo.

Kwa hiyo amemeza matamshi yake aliyoyatoa hadharani kwenye mkutano wa hadhara wa miaka 34 ya ccm pale dodoma ..kuwa angependa ofisi za kimataifa Arusha zihamishwe......kama amebadili mawazo AWAOMBE RADHI WATANZANIA hadharani na sio kwa kuzunguka zunguka....kwa kitendo cha kudhamiria kuwabagua sehemu ya wananchi anaowaongoza...shame ..shame ..shame!!!

 
Du kama hili ni kweli basi hatuna kiongozi hapa na matatizo mwanzo mwisho,we need solutions not vendetta. sasa na dar wakimuuzi atahamisha ikulu?
 
Hili la mkutano kufanyika Dar badala ya Arusha ni vigumu kulihusisha na ajenda binafsi ya Jakaya. Mikutano ya Wakuu wa Nchi za Afrika Mashariki huwa inafanyika katika nchi mbalimbali na kwa mara ya mwisho nakumbuka mkutano kama huu ulifanyika Bujumbura. Summit moja kwa mwaka ambayo ni ya kawaida (Ordinary) ni lazima ifanyike Arusha yalipo Makao Makuu ya Jumuia. Hii ya sasa si ya kawaida (Extra ordinary) na hivyo inaweza kufanyika sehemu yoyote kama nchi inayoomba kuhost itachukua sehemu kubwa ya gharama. Hii inaongeza visibility ya Jumuia kwa watu wa Afrika Mashariki. Kuna mmoja ametolea mfano wa East Africa Legislative Assembly ambao kila mkutano huwa wanazunguka katika miji tofauti ya Jumuia. Siupendi sana huu mfano kwani binafsi nadhani kitendo cha EALA hakinufaishi jumuia bali ni kutaka kuvuja fedha za Jumuia bila sababu. Kikao hiki cha sasa kimefanyika Dar es Salaam kwa sababu kulikuwa na Mkutano mwingine wa Uwekezaji wa Afrika ambao wakuu wa nchi walikuwa wanahudhuria na hivyo ikaonekana ni vyema ikaungana. Ndiyo maana napata kigugumizi kuhusisha suala hili na ubaguzi wa wazi wa JK. Hata hivyo, anything is possible.

Thanks for this clarification!
 
Tumechoka na mambo ya uvumi na ya kufikirika yasiyo hata na msingi. Kwanza kama kupingana na JK ndiyo uadui basi Mwandosya, Mwakyembe, Mary Nagu, Magufuli, Kagasheki na wengine wengi wasingekuwa mawaziri au Njoolay asingekuwa RC, maana hao wote walipinga ugombea wake. Haya ni mambo yasiyo na msingi na hata hili la kuhamisha mkutano kutoka arusha kuja dar es salaam ni porojo zisizostahili hata kutupotezea muda. Kama ingekuwa hivyo basi hata vikao vya Council of Ministers ambavyo vimekuwa vikifanyika mpaka mwisho wa wiki iliyopita vingekuwa vimehamishwa. Suala la mkutano ufanyikie wapi ni suala la convenience na ingewezekana kufanyikia hata Tabora. Hivi Arusha kuna nini cha ajabu alichofanyiwa JK ,mpaka awalipizie visasi maana kama ni wabunge wa upinzani basi Mkoa wa Mwanza una wapinzani wengi kuliko Arusha. Hoja nyingine ni potofu mpaka inakera.

BUT the message is home, you elected CRAPPPP!! for the highest office of the country!!!!!!!!
 
ivi cdm mbna mko kama was*** kwani mkutano kufanyikia dar badala ya arusha kuna tatzo gani?sio lazima arusha,,na mtataapika nyongo mwaka huu,leteni hoja za msingi kama kweli nyie ni wanasiasa mlio timamu,acheni majungu ya kinafiki fanyeni kazi .

KUTUKANA ni dalili ya kuishiwa HOJA....na why do you generalise and call all of us here CHADEMA ....i wish you knew...!!!....always JF ni kijiwe cha watu wenye uchungu na nchi hii ...na wanaopenda kutoa mawazo yao kwa huru..ambayo kwa kiasi kikubwa yameendelea kuisaidia nchi hii!!!...sasa kama watu wakiwa na uchungu na nchi jina lao ni CHADEMA basi ....no wounder hiyo CHADEMA inaimarika!!!!....mimi binafsi ukifuatilia thread zangu utagundua huwa nawasifia watu wengi tu ndani ya ccm na ccm yenyewe pale wanapofanya mema!
 
Philemon Mikael,

..hivi Raisi alipowaambia wananchi wa Mwanga-Kilimanjaro wasifikirie kuhamia mkoa wa Pwani akidai hakuna ardhi ni kutokana na magomvi yake na Nicodemus Banduka?

..Raisi alitoa kauli hiyo wakati anatembelea jimbo la Mwanga ambako ndiko alikozaliwa Nicodemus Banduka.
 
Jamani mimi siwalaumu ccm, huo ndio uwezo wao wa kufikiri na wa kutenda umeishia hapo. Jk anasahau kuwa dhana ya visasi cku hizi hailipi anaiga tu. Matokeo yake ndo yaliyowakuta mwaka jana, walipigwa danganya toto na wananchi wakati wa kampeni kwa kuweka bendera za ccm kwenye maeneo yao ya makazi na biashara especially arusha,mbeya na iringa ili wasibughudhiwe kwenye kura wakapigwa knock out. Kwisha kazi!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Philemon Mikael,

..hivi Raisi alipowaambia wananchi wa Mwanga-Kilimanjaro wasifikirie kuhamia mkoa wa Pwani akidai hakuna ardhi ni kutokana na magomvi yake na Nicodemus Banduka?

..Raisi alitoa kauli hiyo wakati anatembelea jimbo la Mwanga ambako ndiko alikozaliwa Nicodemus Banduka.

Du hiii nayo kali Ameshawahi kutoa kauli kama hiii?? ....Mimi kali nyingine ninayokumbuka ni ile aliyoitoa kwenye ziara yake Bagamoyo ...ALIKEMEA KITENDO CHA WATU WANAONUNUA MASHAMBA WILAYANI KWAKE...NA KUNA AMBAO WALIONUNUA PALE CHALINZE WAKO MBIONI KUONDOLEWA ..NA WANAKIJIJI AMEWAAMBIA WAACHE KUUZIA "WAGENI" ..hivi kuna wakati anajisahau kuwa yeye ni RAIS na kujiona kama mzee wa kawaida pale msoga.....that is too low indeed....maana as far as i know ...katiba ya nchi inasema mtu ana haki ya kuishi mahali popote ndani ya jamuhuri hii..na pia kulikuwa na presidential decree wakati wa mwalimu iliyompa nguvu rais kuanzisha new settlement hi ililenga kuwasaidia Wananchi ambao kwa bahati mbaya sehemu zao za asili ni kama au zimejaa ....serikali inatakiwa IWAPE SETTLEMENY MPYA BILA KUHARIBU SILKA NA MILA ZAO KWENYE SEHEMU NYINGINE NDANI YA JAMUHURI HII ZENYE NAFASI......kwa fursa hii kuna watu walipelekwa Morogoro....na pia kulikuwa na wazo la kuwaahamishia wakimbizi waliopewa uraia toka mikoa ya pembezoni na rwanda ,burundi na kuwapeleka mikoa ya kati nyanda za juu au kusini...ili kuondoa uwezekano wa raia hao wapya kuendelea kushirikiana na nchi walizotoka kwa nia mbaya dhidi ya jamuhuri...ie of recent mmeona namna Banyamulenge upande wa Congo walivyooendelea kushirikiana na serikali ya Rwanda badala ya kutii ya Congo...hii ndio sababu kuu ya kufikiri wakimbizi waliopewa uraia mikoa ya kigoma na bukoba waingizwe ndani zaidi ya nchi.....na ndio maana mwalimu Nyerere wale wa mwanzo waliopewa uraia kuna ambao walipewa settlement Tabora.
 
Hata kama siwezi hata kuotea next president ni nani ila siwezi kusubiri JK AMALIZE URAISI..Ameyumbisha sana nchi huyu kiumbe!!
 
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom