Nilikuwa nasafiri kutoka Msata - Pwani kuja Dar, Tulipofika Kongowe, alipanda jamaa mmoja akiwa ameongozana na mwanamke mmoja mrefu kiasi na unene kiasi. Walipokaa kwenye siti wakawa wanaendelea na stori zao na kuonyeshana mapenzi na kutufanya wengine tuvutiwe na kuanza kugeuza shingo zetu huku kama mimi nikisema moyoni mh! kuna wengine wamejaliwa kipawa cha kupendana kama ni mke wake basi wamependelewa ndoa si ndio hii. kwa ujumla walionyeshana mahaba ya hali ya juu.
Zilipopita dakika chache tu, simu ya yule dada ilianza kuita mara tukamsikia "nakuja niko njiani, nilipitia kwa fulani (alitaja jina la shemeji yake wa kike) nakuja. Walipomaliza tu maongezi na huyo mtu ambaye mimi nilihisi kuwa alikuwa ndio mume wake wa ndoa akampigia simu mdogo wake tulisikia hivi " Mambo? Za leo, Sasa Shemeji yako akikupigia simu kukuuliza kuhusu mimi, mwambie nilikuwa kwako na nimeondoka saa mbili usiku. Haya kwa heri" Basi wote ikabidi tunyamaze kimya naona hapo kila mtu alikuwa akiwaza lake. Walipofika eneo moja baada ya Kibaha Maili 1 kituo sikifahamu kwajina wakashuka sijui walikoelekea. Basi hicho ndio kisa tulichokishuhudia siku hiyo
Zilipopita dakika chache tu, simu ya yule dada ilianza kuita mara tukamsikia "nakuja niko njiani, nilipitia kwa fulani (alitaja jina la shemeji yake wa kike) nakuja. Walipomaliza tu maongezi na huyo mtu ambaye mimi nilihisi kuwa alikuwa ndio mume wake wa ndoa akampigia simu mdogo wake tulisikia hivi " Mambo? Za leo, Sasa Shemeji yako akikupigia simu kukuuliza kuhusu mimi, mwambie nilikuwa kwako na nimeondoka saa mbili usiku. Haya kwa heri" Basi wote ikabidi tunyamaze kimya naona hapo kila mtu alikuwa akiwaza lake. Walipofika eneo moja baada ya Kibaha Maili 1 kituo sikifahamu kwajina wakashuka sijui walikoelekea. Basi hicho ndio kisa tulichokishuhudia siku hiyo