virusi vya au virusi ya / za???

Kipala

JF-Expert Member
Jan 10, 2009
3,763
699
Jamani neno "virusi" limeingia katika lugha.

Wengi huandika "Virusi vya UKIMWI", "virusi vya kompyuta".

Lakini hii ina matata. Nimeshaona watu wanaoandika "virusi vya kompyuta ni hatari; wiki iliyopita kirusi kipya..."

Hii naona haiwezekani kwa sababu "Kirusi" lamaanisha lugha pekee. Neno ambalo tumepokea kutoka Kiingereza katika Kiswahili ni "virus", si "kirus".

Hapa naona udhaifu wa kawaida hii;: namna gani kutofautisha kati ya virusi 1 (virusi kimoja? virusi vimoja ????) na virusi 100 (virusi vingi?).

Mnaonaje ? Tuseme virusi ya Ukimwi, virusi za hatari sawa na matumizi ya neno "video"?
 
Back
Top Bottom