Viroja: Siku ya kwanza kupanda ndege (ushamba mzigo)

clasi

JF-Expert Member
May 5, 2013
378
683

Nakumbuka ilikuwa Mwaka 2008 mwezi Juni nilikuwa naenda kikazi Lusaka, Zambia basi sijui hili wala lile kwenye tiketi iliandikwa saa ya ndege kuondoka saa 12 asubuhi (ndege ndo inapaa) mimi nikajipa kama dakika 20 kutoka home Tabata mpaka Airport, nikidhani ni kama Mabasi ya Mkoani pale Ubungo stendi duuh ile kufika nikaambiwa muda umeisha daah! Nilichokaje. But taratibu nikajifunza muda wa kufika airport, vitu visivyoruhusiwa kubeba kwenye ndege.

**NEW DEVELOPMENT
Mwezi Juni 2015 nilipata safari ya kwenda CAMEROON (kwa hisani ya Watu wamarekani USAID) sasa tukiwa huko tukalipwa posho kwa hela ya huko Central African Franc sasa nikazibana nije kubadilishia Bongo nafika bongo Bureau De Change zote hawabadilishi hizi pesa yaani nmepagawa sijui nikazitupe Coco maana....

****MPYA ya 2016

Mwezi Januari nilienda NEW DELHI duuh pale airport hakuna sijui kutangaza wala nini ni KIMYA KIMYA tu ukisubiri matangazo utastukia ndege ishakuacha.


HAKIKA USHAMBA MZIGO!
 
Mie mbona sitasahau..
Siku iyo nilijipodoa kama naenda harusini kufika airport parfume yangu ikawekwa kwenye dustibini niliumia sana.

Nilipoingia ndani sijui ni uoga nikaita air host aje kunifunga mkanda kasheshe wakati wa kushuka mkanda ukanishinda kufungua ikabidi jirani yng kk mmoja anisaidie..
 
Tinna cute pole sana. Mimi perfume na dawa za mswaki zilitupwa kwenye waste bin ile kufika kwa jamaa wa uhamiaji wananiuliza vipi mkuu unaenda kufundisha KISWAHILI ughaibuni? Sijui nnimekaa kama mwalimu.

Mwishoni akamalizia kwa kuomba hela ya Chai, UHAMIAJI AIRPORT punguzen njaaa.
 
tinna cute pole sana. mimi perfume na dawa za mswaki zilitupwa kwenye waste bin ile kufika kwa jamaa wa uhamiaji wananiuliza vipi mkuu unaenda kufundisha KISWAHILI ughaibuni? sijui nnimekaa kama mwalimu. Mwishoni akamalizia kwa kuomba hela ya Chai UHAMIAJI AIRPORT punguzen njaaa.

Duh!!
Nimeipenda hii, pamoja na kuwa Airport muda wote lakini hela ya chai inasumbua.!
 
Mie mara ya kwanza kupanda ndege nilitoka Dsm kwenda Mwanza. Process nzima hadi niingie kwenye ndege ilikuwa 'shughuli'. Nilikaa upande wa dirishani, tulipopita Ngorongoro crater eti sikuthubutu kuchungulia nje. Kisa?

Niliogopa eti nikichungulia naegemea upande mmoja hivyo nikaona kama vile ndege italalia upande ule na kuanguka! Ama kweli ushamba ni kazi!
 
Mmh nmefurahi. Mimi ilikiwa mwaka jana mwezi wa tatu(ahsante fastjet)
Niliingia kwa ndege nikiwa na amani, ilipopaa sikujua kuwa kule hewani huwa ni kama inatetema hivi kwenye mawingu sasa ilipokuwa inatikisika roho fyatu najua ndo tunarudi chini.

Halafu siku nasafiri nilisafiri na ile timu toka South Afrika iliokujaga kucheza na yanga kwenye mwez wa pili hivi, sasa nilikaa na mmoja yeye akiwa dirishan tulipoingia nikamuomba nikae dirishani jamaa akatosa..lol

Tatu nilikuwa nahisi tupo palepale mara nikaskia tunatua Dar, mara chache sana nilihisi ina move..na sijui kwanini mpaka leo.

Ushamba duu
 
Mmh nmefurahi. Mimi ilikiwa mwaka jana mwezi wa tatu(ahsante fastjet)
Niliingia kwa ndege nikiwa na amani, ilipopaa sikujua kuwa kule hewan huwani ni kama inatetema hivi kwenye mawingu sasa ilipokuwa inatikisika roho fyatu najua ndo tunarudi chini.

Alafu siku nasafiri nilisafiri na ile timu toka south afrika iliokujaga kucheza na yanga kwenye mwez wa pili hivi, sasa nilikaa na mmoja yeye akiwa dirishan tulipoingia nikamuomba nikae dirishani jamaa akatosa..lol

Tatu nilikuwa nahs tupo palepale mara nikaskia tunatua dar, mara chache sana nilihs ina move..na sijui kwann mpka leo.

Ushamba duu
Hahahaha dah mbavu zinauma kwa kicheko!.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom