Vipindi Maalum vya JF kwenye TV: Naomba Maoni Yako!

Asante Dark City, kwa vile ni kweli, niliendesha kipindi cha 'KitiMoto' na ni kweli kilisitishwa na ni kweli sikuwahi kusema kilichonifanya hadi nisitishe kipindi kile, hivyo pia inaweza kuwa ni kweli nitaendesha kipindi hiki, na ni kweli kinawezxa kusitishwa na ni kweli kabisa sitasema kwanini kimesitishwa.

Kwa wasio jua, walifikiri labda mimi ndiye ninaye rusha kipindi hewani, mimi ndie ninayemiliki hizo stesheni, na mimi ndiye ninaamua nirushe kipindi au nisirushe!. Kwa taarifa tuu, kazi yangu mimi ni kuandaa tuu kipindi na kupeleka kwenye vituo vya TV ambao wao ndio huamua ama warushe, ama wasirushe. Kwa waliosoma attachment nimeeleza majukumu yangu ni kuandaa tuu na sio kurusha. Ili kipindi kirushwe, lazima niwaombe, na watarusha wale tuu watakao kubali. Kunauwezekano wote wasikubali hivyo kipindi hakitarushwa. Watakapo kataa kukirusha, wanaweza kukueleza sababu kwa kwanini wamekataa, ama wanaweza kukataa tuu bila kukueleza sababu. Kiti Moto kilipokufa tulieleza sababu loud and clear, wenye TV zao walikataa kukirusha na hawakutuambia sababu. Hata hiki kipindi kipya kinaweza kurushwa na baadae kikakataliwa kurushwa bila mimi kuambiwa sababu!.Hivyo sababu yako ya kukataa kuniunga mkono kwa sababu hii ni valid!, na kwa sababu kila kipindi kikisimamishwa huwa watazamaji lazima muambiwe!. Funga macho kumbuka vipindi vingapi viliwahi kuwepo na viliposimamishwa kama uliambiwa sababu!.


Kama kuna sheria ya jf kuwa ukishajiunga, lazima upost mabandika kadhaa kwa interval ya siku kadhaa, na baada ya kipindi fulani kupita lazima angalau uwe umefikisha mabadiko kadhaa, hapo naikubali kuwa hii ni sababu valid, kwa nini usiniunge mkono, na pia mwana jf akiadimika, anawajibika kueleza alikuwa wapi, mbona tangu nimejiunga nimekuwa nikiposti from time time, labda mnisaidie na mimi hizo rules ili nizifuate nisije kukosa uungwaji mkono wa Dark City maana michango yako ndio muhimu kweli, ukikataa wewe tuu, baas, kipindi hakiwezekani bila michango yako!.
, kumbe issue ni kuanzisha mtandao wangu?, kusema kweli hili ndilo haswa lengo langu, yaani kuanzisha mtandao wangu, halafu niitumie michango ya watakaochangia mtandao wangu ndio nitumie mawazo yao kwenye hiyo programu yangu, kama utaweza kunisaidia kwa hilo nitakushukuru, hata kunianzishia page tuu kwenye fesibuku, watu watachangia na mimi nitawataja, si unajua tena nilivyo mtupu, hivyo mimi nikiwa mwenyewe, siwezi kutangaza kitu ndio maana nikatafuta humu jf, hivyo kama utanisaidia kuanzisha mtandao wangu, utakuwa umenisaidia sana, please help!.

Kwenye program one hiyo ya mgomo wa madaktari, nimeweka pale script, hata ukiipitia utaona wazi, bila michango ya jf, sitaweza kufanya hivyo program, nisaidieni jamani, niko chini ya miguu yenu!. Tena naombeni niwape siri, nafanya hivi vipindi ili nipate pesa, si nitalipwa na naninihii.. nisaidieni mwenzenu nisife njaa!.

Kusema kweli Dark City, nakuomba ukubali, yaani hata wana jf wengine wote wakikubali na wewe ukataa, then siwezi kutengeneza program bila wewe maana maoni yako ndio yananiletea pesa nyingi!. Ila pia nitauheshimu msimamo wako!.

I wish I had all the powers to say NO...na ikawa hivyo hivyo!

Maoni yangu na msimamo wangu nimeweka wazi...Hata kama wengine watakubali na kukupa ruhusa ya kutumia mabandiko yao....ni sawa tu. Ila mabandiko yangu hapana...Iwe unatengeneza pesa au unatoa offer!

Kwani sina haki ya kukatalia maoni yako??

DC!!
 
Maishapopote, 'Kiti Moto' kilikula rungu la utawala wa Mkapa, jamaa hakupenda critique, ndio maana nimeamua kuiepuka siasa, rungu lile lile lisije likanishukia.

Kusema ukweli, baada ya Kiti Moto kufa, wakati huo nikiwa mtoto wa Ilala, niliishia zangu Italy kutafuta maisha, na huko sio tuu nilikwama bali pia nilipigika na nikapata maswahibu fulani nikaishia hospital, Mfanyakazi fulani wa Ubolozi wetu akiitwa Mchemwa, aliniokoa, habari zikaeneo hapo mjini Rome, Mtanzania mtangazaji wa Kiti Moto amelazwa hospitali fulani, ndipo Balozi Prof. Mahalu na Edward Lowassa wakaja hospital ndipo Lowassa akakiri yeye binafsi kusikitishwa na kufungwa kwa kipindi kile. Hii inamaana japo bosi wake alikerwa na kiti moto, baasdhi ya mawaziri wake walikikubali.

Kwa utawala wa sasa wa JK, umefungua zaidi milango ya uhuru wa habari, hivyo kikianzishwa kipindi kama Kiti Moto, this time kita survive. Acha nianze kuingiza mguu kidogo kidogo kwa talk shows ambazo sio za kisiasa, zikiota mizizi, nitapenyeza hoja muhimu kama mjadala wa katiba kidogo kidoga na kipindi kikisimama, kitu kama kiti moto kitarudi hewani!

Mkuu, kwa huo utenzi hapo juu, especially ushuhuda wako wa jinsi gani ulisaidiwa na EL hata na mimi sasa naanza kukubaliana na AlcoholicSnr, Zee la Pombe kuwa ni kweli wewe Paschal Mayalla = Pasco (wa jf)..., 'll someone prove me wrong!!
 
pasco mayalla you are totally wrong.wanajf hawana tabia ya kinafiki na uwongo.huwezi kutudanganya eti utaongelea masuala mengine na kuiacha siasa pembeni,mambo yote ya kijamii iwe elimu,miundombinu,afya au michezo ni lazima yaathiriwe na siasa sasa unapokuja na longolongo zako za kutohusisha siasa kwenye "vipindi" vyako inaonyesha u mnafiki kwa kiasi gani.nyinyi ndio mliotufikisha hapa tulipo.acha jf iendelee kama ilivyo usituletee madoido hapa!!i insist i hate your idea,it is damn wrong na haina nafasi kwa wakati huu wa uhuru wa habari za kimtandao.endelea kupokea vibahasha na utuache wanajf tushushe vitu hapa jamvini.aaaagrrrrrrrr!!!
 
I wish I had all the powers to say NO...na ikawa hivyo hivyo!

Maoni yangu na msimamo wangu nimeweka wazi...Hata kama wengine watakubali na kukupa ruhusa ya kutumia mabandiko yao....ni sawa tu. Ila mabandiko yangu hapana...Iwe unatengeneza pesa au unatoa offer!

Kwani sina haki ya kukatalia maoni yako??

DC!!
Ni haki yako ila mimi ndio nategemea saana imput yako!, basi tena!.
 
Hakina mshiko, tafuta vya maana vya kufanya. Kama huna ubunifu na kuona haya makorokocho ya JF ndio "idea" unkula huu.

Sioni cha maana kwenye hiyo script na sioni mvuto, mavi ya kale hayanuki. Kipindi kama hicho kinarushwa, "malumbano ya hoja" ni haya haya tunayoongea JF ndio wanayazumgumza humo. Umechelewa jamvini, karamu imeshaliwa.
 
PPR ni independent production house, tunaandaa vipindi mbalimbali (recorded) vya radio na tv from outside na kuvipelekwa kurushwa na vituo mbalimbali vya radio na TV.

Mkuu kuna thread ziliandikwa kuhusiana na wewe, ile ya kusema mapema kwamba wewe uhusiki na chama chochote na siasa na ile ya pili ulikuwa ukitoa ushauri kwa JF juu ya uendeshaji wake.

Sasa mkuu, sitazungumzia kuhusu dhamira na nyenzo unazotaka kuzitumia kupitia JF kufanya unachotaka kufanya lakini hiki unachokisema hapa chini ndicho kinanifanya nikuulize kwanini utumie JF?


Mkuu Paschal, watu kama sisi tupo hapa JF siku nyingi sana na tunaelewa mambo yanavyokwenda.

Sasa inabidi utuelezee kwa kina hasa lengo lako nini unapotaka kutumia JF kwenye kipindi chako cha televisheni?
 
Basically, unachotaka kufanya ni ku-intergrate social media na traditional media. On the paper, it sounds like a good idea, lakini kutokana na the way unavyotaka ku-integrate, implications zake ni far reaching kuliko tunavyojua. Moja ya masuala muhimu ni who is the right person to integrate the two? Pascal Mayalla? I don't think so.

Ni JF na wamiliki wake ndio wanaotakiwa to make it easy for anyone to access the information here either wao wenywe au kwa ku-hire a third party. JF imekua na nadhani labda imefikia stage ya JF kuwa na multiple channels, multiple formats, na ku-embrace multimedia. Lakini ni JF na wamiliki wake ndio wanaotakiwa kuongeza multimedia kwenye habari zake, ili JF iwe iwe na multiple formats, etc.

Tukumbuke social media like JF is often handled by young folks with technical expertise (such as computer folks) or with a journalism background. Traditional media comes from older folks with broadcast and PR expertise. These folks don't speak the same language or understand each other very well. And, they may not work together well. They may even be in different building or cities.

This makes collaboration and integration of social media and traditional media difficult (not impossible) hasa kwenye nchi yetu ambapo views za vijana na za wazee zinatofautiana kwa kiasi kikubwa kwenye masuala muhimu ya nchi. Ndio maana baadhi ya watu wana wasiwasi kuwa kutakuwa na uchakachuaji tuu. For that case, na sababu nyingine zilizotajwa na wachangiaji wengine siungi mkono hoja. Sorry.

BTW, nashangaa Pasco bado hajachangia kwenye huu mjadala japokuwa yuko hapo chini.
 
Mkuu kuna thread ziliandikwa kuhusiana na wewe, ile ya kusema mapema kwamba wewe uhusiki na chama chochote na siasa na ile ya pili ulikuwa ukitoa ushauri kwa JF juu ya uendeshaji wake.

Sasa mkuu, sitazungumzia kuhusu dhamira na nyenzo unazotaka kuzitumia kupitia JF kufanya unachotaka kufanya lakini hiki unachokisema hapa chini ndicho kinanifanya nikuulize kwanini utumie JF?


Mkuu Paschal, watu kama sisi tupo hapa JF siku nyingi sana na tunaelewa mambo yanavyokwenda.

Sasa inabidi utuelezee kwa kina hasa lengo lako nini unapotaka kutumia JF kwenye kipindi chako cha televisheni?


Mkuu Richard kwa kifupi hapa hayaangaliwi maslahi ya JF au members wake, kwa kifupi JF imekuwa maarufu sana miaka ya hivi karibuni na si vibaya ikatumika kwa manufaa ya wajanja wachache, huku wakiidhoofisha, kinachofanyika hapa ni katika kupanua mtandao na wigo wetu wa kampeni za 2015.

Samahani Pasco kama nitakuwa nimeongea mambo ya mbele zaidi kwa kutambua wote tuko kambi moja.
 
Ni haki yako ila mimi ndio nategemea saana imput yako!, basi tena!.

Pascal,

Hutegemei inputs zangu kama mimi ila katika hii project yako yenye utata, unaitegemea JF ambayo mie ni mmoja wa members wake. Ndiyo maana umeleta bandiko lako hapa. That's an irrefutable fact na wewe unaitambua!

Kama kosa ni tabia yangu ya kutopindisha maneno, ya kukueleza kuwa siungi mkono hoja na kwamba niko tayari kubaki peke yangu hata kama members wote wa JF watakukubalia, basi niko tayari kubeba gharama ya hilo kosa.

Uamuzi ni wako na kwa script yako...kipindi kiko kwenye hatua juu kabisa za maandalazi.

Nakutakia kila la heri,

DC!!
 
Mkuu Richard kwa kifupi hapa hayaangaliwi maslahi ya JF au members wake, kwa kifupi JF imekuwa maarufu sana miaka ya hivi karibuni na si vibaya ikatumika kwa manufaa ya wajanja wachache, huku wakiidhoofisha, kinachofanyika hapa ni katika kupanua mtandao na wigo wetu wa kampeni za 2015.

Samahani Pasco kama nitakuwa nimeongea mambo ya mbele zaidi kwa kutambua wote tuko kambi moja.

Mkuu,

Mambo ya uchakachuaji, propaganda, infiltrations na monitoring ndio mambo ya kileo kwahio hata sishangai.

Unapokuwa katika dunia ya kileo ni lazima utaona mambo haya.
 
pasco mayalla you are totally wrong.wanajf hawana tabia ya kinafiki na uwongo.huwezi kutudanganya eti utaongelea masuala mengine na kuiacha siasa pembeni,mambo yote ya kijamii iwe elimu,miundombinu,afya au michezo ni lazima yaathiriwe na siasa sasa unapokuja na longolongo zako za kutohusisha siasa kwenye "vipindi" vyako inaonyesha u mnafiki kwa kiasi gani.nyinyi ndio mliotufikisha hapa tulipo.acha jf iendelee kama ilivyo usituletee madoido hapa!!i insist i hate your idea,it is damn wrong na haina nafasi kwa wakati huu wa uhuru wa habari za kimtandao.endelea kupokea vibahasha na utuache wanajf tushushe vitu hapa jamvini.aaaagrrrrrrrr!!!
Naendelea kupokea maoni, kwa vile mpaka sasa maoni against ni mengi kuliko pro, huu mpango unaweza ukafa.
 
Pascal,

Hutegemei inputs zangu kama mimi ila katika hii project yako yenye utata, unaitegemea JF ambayo mie ni mmoja wa members wake. Ndiyo maana umeleta bandiko lako hapa. That's an irrefutable fact na wewe unaitambua!

Kama kosa ni tabia yangu ya kutopindisha maneno, ya kukueleza kuwa siungi mkono hoja na kwamba niko tayari kubaki peke yangu hata kama members wote wa JF watakukubalia, basi niko tayari kubeba gharama ya hilo kosa.

Uamuzi ni wako na kwa script yako...kipindi kiko kwenye hatua juu kabisa za maandalazi.

Nakutakia kila la heri,

DC!!
Dark City, yote ni kweli, kipindi kiko final stages, on Monday barua za kuomba airtime zinakwenda, shooting can start any moment baada ya kupata airtime, with or without jf imput, kipindi kitapanda.

Kiukweli, very honestly, lengo langu ni kuibeba tuu jf ili hawa great thinkers wake wakibebe kipindi kukipandisha juu, and you were not in my mind kati ya watu niliowatarget. Niko muda wa kutosha humu na kuna vichwa viche vya ukweli na makapi kibao na very very unfortunately kati ya hivyo vichwa in my mind, wamenibonyezea tuu like na wamejinyamazia kimya, hivyo nami ni msoma nyakati mzuri, somo limeshaanza kueleweka.

Pamoja na kutofautiana na mawazo yangu, lazima nikiri wewe Dark City, uu mingoni mwa strong men humu jukwaani, strenght ya kweli ni kusimamia kile unachokuamini no matter what, hata kama utabaki peke yako.

Nauheshimu msimamo wako na asante kunitakia heri.

Thanks.

Pascal
 
Pasco u don't sounds as an intellectual with a pass degree in law
Mwanamtama, I'm not!, ila pia mimi ni Pascal!.
Kuna wafika chuo kusoma na walisoma na kuelewa sasa ni wasomi hawa wako chuo wakiwafundisha wengine.
Kuna waliosoma sheria, japo walisoma hawakuelewa sana, sasa ni wanasheria wanapractice kuelewa zaidi.
Kuna waliopita, chuo ili kusoma, hawakusoma na hawakuelewa, hivyo wao wamepita tuu. Mimi ni mmoja wa hao wapita njia ndio maana bado niko mtaani!, ningekuwa msomi ningebaki chuo, na ningesoma sheria, ningekuwa wakili, au mahakamani. Niko mtaani where I belong!.
 
Basically, unachotaka kufanya ni ku-intergrate social media na traditional media. On the paper, it sounds like a good idea, lakini kutokana na the way unavyotaka ku-integrate, implications zake ni far reaching kuliko tunavyojua. Moja ya masuala muhimu ni who is the right person to integrate the two? Pascal Mayalla? I don’t think so.

Ni JF na wamiliki wake ndio wanaotakiwa to make it easy for anyone to access the information here either wao wenywe au kwa ku-hire a third party. JF imekua na nadhani labda imefikia stage ya JF kuwa na multiple channels, multiple formats, na ku-embrace multimedia. Lakini ni JF na wamiliki wake ndio wanaotakiwa kuongeza multimedia kwenye habari zake, ili JF iwe iwe na multiple formats, etc.

Tukumbuke social media like JF is often handled by young folks with technical expertise (such as computer folks) or with a journalism background. Traditional media comes from older folks with broadcast and PR expertise. These folks don’t speak the same language or understand each other very well. And, they may not work together well. They may even be in different building or cities.

This makes collaboration and integration of social media and traditional media difficult (not impossible) hasa kwenye nchi yetu ambapo views za vijana na za wazee zinatofautiana kwa kiasi kikubwa kwenye masuala muhimu ya nchi. Ndio maana baadhi ya watu wana wasiwasi kuwa kutakuwa na uchakachuaji tuu. For that case, na sababu nyingine zilizotajwa na wachangiaji wengine siungi mkono hoja. Sorry.

BTW, nashangaa Pasco bado hajachangia kwenye huu mjadala japokuwa yuko hapo chini.
EMT, asante kwa objectivity yako kwenye hii issue. Kwa kiasi kikubwa nakubaliana na wewe na sababu zako ni za msingi. Mpaka sasa nimeshaona mwelekeo, najua kusoma alama za nyakati, better be safer than sorry!. The way it is jf is safe the way it is, better it remain safe, kuliko ku venture into something new ikaja kuwa sorry.
Naheshimu msimamo wako.
 
  • Thanks
Reactions: EMT
amzisha bwana,wana JF wamejaaa wivu,wanaona utafaiiidi........mbona magazeti wanatumia JF bila kutoa credit miaka yote na wametulia tuliiiiii siwaoni wakifanya lolote,leo umekuja na hili wazo la kuanzisha program kny tv ndio wanajidai wakaliiiiiiiiiiiiiiiii...washindwe kwa jina la bwana,kama hawataki anzisha watumie michango yao ila usiwataje.....maana unafiki ndio waliozoea!!!!
 
Back
Top Bottom