vipigo CCM! Jamani vipi?

Msongoru

JF-Expert Member
Apr 16, 2008
306
24
Sophia Simba, Janeth Kahama washambuliana kwa maneno

2008-09-15 09:26:48
Na Simon Mhina


Kikao cha Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Dar es Salaam kilichokutana wiki iliyopita, kiliahirishwa kwa muda baada ya kutokea mzozo kati ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Sophia Simba, na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake ya Chama cha Mapinduzi (UWT) jijini, Janeth Kahama.

Janeth na Sophia wote wanawania nafasi ya Mwenyekiti wa UWT Taifa, ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikishikiliwa na Anna Abdallah.

Chanzo chetu ndani ya kikao hicho kimepasha kuwa kilichoibua mzozo huo ni malalamiko yaliyotolewa na Waziri Simba kwamba siku hizi hashirikishwi katika vikao vya UWT Mkoa wa Dar es Salaam, na malalamiko hayo kumgusa Kahama ambaye ndiye mwenyekiti.

Chanzo chetu kimepasha kuwa Waziri Simba alitoa malalamiko hayo kwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita.

Habari hizo zinasema baada ya Simba kuwasilisha malalamiko yake, Kahama alisimama kujitetea na kusema kuwa, Waziri huyo hapaswi kumlaumu mtu, kwa vile anajifanya ana shughuli nyingi kila wakati anapopelekewa taarifa za mwaliko wa vikao.

Kutokana na majibu hayo, chanzo chetu kimetupasha kuwa Waziri Simba alikuja juu huku akimshambulia Kahama kwa maneno, kwamba ana wivu, yaani anamuonea wivu kutokana na nafasi yake.

Habari hizo zinasema Kahama naye aliamua kujibu mapigo, huku akimrushia makombora mshindani wake kwamba Waziri huyo anatumia madaraka yake katika kampeni za kutaka achaguliwe uenyekiti wa Taifa wa UWT.

``Usifikiri uwaziri wako na kupata ofisi pale Ikulu vitakusaidia, huu ni uchaguzi wa Chama, heshimu taratibu za chama,`` chanzo chetu kilimnukuu Kahama.

Habari zinasema kuwa Mbunge wa Ilala, Mussa Azan Zungu, alisimama na kumuomba Guninita asitishe hoja hiyo, kwa vile haiwahusu.

Imeelezwa kuwa, baada ya Zungu kutoa hoja hiyo, Waziri Simba alimfuata huku akiwa ameweka vidole juu na kuanza kumsuta Mbunge huyo na kumfokea kwamba anajifanya ni mjanja wa CCM jijini Dar es Salaam.

Habari hizo zinasema kuwa Zungu alipoona Simba amefuatwa kwenye kiti chake na kusimama mbele yake, aliamua kutoka haraka haraka na kuacha kikao.

Habari hizo zinaendelea kueleza kuwa baada ya Zungu kuondoka katika kikao, Waziri Simba alielekea alipokuwa ameketi Kahama lakini wajumbe waliwatenganisha ili kuepusha mzozo zaidi.

Akihojiwa na Nipashe jana, Guninita alikiri kupokea malalamiko toka kwa Waziri Simba kwamba hashirikishwi kwenye mambo ya UWT, jambo ambalo alisema analitafsiri kwamba ni njama za kumwangusha katika kinyang`anyiro hicho.

Hata hivyo, alisema hicho kinachoitwa ugomvi siyo kilichosababisha kufungwa kwa mkutano.

``Unajua Waziri Simba alitoa malalamiko yake kwangu wakati mkutano wetu tayari ukiwa umemalizika, hapakuwa na ugomvi mkubwa kama unavyouliza, bali Mwenyekiti wa UWT Mkoa (Kahama) alikuwa akijaribu kutoa ufafanuzi,`` alisema Guninita.

Alipoulizwa na Nipashe kuhusu kutoka katika kikao, Zungu alisema hakukimbia, bali muda wake wa kuondoka ulishafika.

``Mengine yaliyotokea huko nyuma sijui, lakini mimi nilishaondoka,`` alisema Zungu.

Akihojiwa na Nipashe kuhusu kutembeza ubabe kikaoni, awali Waziri Sophia alikana kwamba hajawahi kuhudhuria kikao hicho.

Hata hivyo, alipopigiwa simu mara ya pili, muda mfupi baada ya Guninita kukiri kupokea malalamiko kutoka kwake kikaoni, Simba alikiri kuwepo, lakini akahoji nani aliyevujisha habari za tukio hilo.

``Wewe sijui leo ni mtu wa ngapi kunipigia simu, watu wengi wamenipigia eti wanauliza kulikuwa na masumbwi kati yangu na Janeth. Sasa kwa nini mnaniuliza, huyo aliyeamua kuvujisha siri za kikao basi na awamalizie kilichoendelea,`` alisema.

Kahama alipopigiwa simu na kuulizwa kuhusu madai ya vurumai hizo, alikata simu na hadi tunakwenda mitamboni jana, simu yake ya kiganjani ilikuwa imefungwa.

SOURCE: Nipashe
 
Huyu mama kweli mambo mengi sana!Sophia Simba anajua kuna ulaji lazima agombee kwa vurugu!
Politics Is A Dirty Game!
 
Sophia Simba ubabe utakufikisha pabaya, Uza sera mama siyo kugeuza kikao uwanja wa masumbwi! hao nipashe naona wamekustahi, ukweli ni kwamba makonde alirusha na wanaume walipo jaribu mzuia aliwasukumizia kuleee.....

Ninalo shangaa jamani hivi ni ruksa waziri mwenye dahamana kurusha makonde mbele ya kadamnasi? hakuna 'ethics' hapo zilizo vunjwa?
 
Hii nayo kali ama kweli madaraka ni matamu!mtu waziri bado unataka tena uenyekiti!si ungeridhika tu na nafasi ya uaziri ili ufanye kazi zako kwa ufanisi!sasa UWT nako anataka!
 
ndio hapo mtajua sophia SIMBA ni nani. she is very powerful woman in the system nawaaambieni
 
Sophia Simba, Janeth Kahama washambuliana kwa maneno

2008-09-15 09:26:48

Na Simon Mhina
Kikao cha Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Dar es Salaam kilichokutana wiki iliyopita, kiliahirishwa kwa muda baada ya kutokea mzozo kati ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Sophia Simba, na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake ya Chama cha Mapinduzi (UWT) jijini, Janeth Kahama.

Janeth na Sophia wote wanawania nafasi ya Mwenyekiti wa UWT Taifa, ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikishikiliwa na Anna Abdallah.

Chanzo chetu ndani ya kikao hicho kimepasha kuwa kilichoibua mzozo huo ni malalamiko yaliyotolewa na Waziri Simba kwamba siku hizi hashirikishwi katika vikao vya UWT Mkoa wa Dar es Salaam, na malalamiko hayo kumgusa Kahama ambaye ndiye mwenyekiti.

Chanzo chetu kimepasha kuwa Waziri Simba alitoa malalamiko hayo kwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita.

Habari hizo zinasema baada ya Simba kuwasilisha malalamiko yake, Kahama alisimama kujitetea na kusema kuwa, Waziri huyo hapaswi kumlaumu mtu, kwa vile anajifanya ana shughuli nyingi kila wakati anapopelekewa taarifa za mwaliko wa vikao.

Kutokana na majibu hayo, chanzo chetu kimetupasha kuwa Waziri Simba alikuja juu huku akimshambulia Kahama kwa maneno, kwamba ana wivu, yaani anamuonea wivu kutokana na nafasi yake.

Habari hizo zinasema Kahama naye aliamua kujibu mapigo, huku akimrushia makombora mshindani wake kwamba Waziri huyo anatumia madaraka yake katika kampeni za kutaka achaguliwe uenyekiti wa Taifa wa UWT.

``Usifikiri uwaziri wako na kupata ofisi pale Ikulu vitakusaidia, huu ni uchaguzi wa Chama, heshimu taratibu za chama,`` chanzo chetu kilimnukuu Kahama.

Habari zinasema kuwa Mbunge wa Ilala, Mussa Azan Zungu, alisimama na kumuomba Guninita asitishe hoja hiyo, kwa vile haiwahusu.

Imeelezwa kuwa, baada ya Zungu kutoa hoja hiyo, Waziri Simba alimfuata huku akiwa ameweka vidole juu na kuanza kumsuta Mbunge huyo na kumfokea kwamba anajifanya ni mjanja wa CCM jijini Dar es Salaam.

Habari hizo zinasema kuwa Zungu alipoona Simba amefuatwa kwenye kiti chake na kusimama mbele yake, aliamua kutoka haraka haraka na kuacha kikao.

Habari hizo zinaendelea kueleza kuwa baada ya Zungu kuondoka katika kikao, Waziri Simba alielekea alipokuwa ameketi Kahama lakini wajumbe waliwatenganisha ili kuepusha mzozo zaidi.

Akihojiwa na Nipashe jana, Guninita alikiri kupokea malalamiko toka kwa Waziri Simba kwamba hashirikishwi kwenye mambo ya UWT, jambo ambalo alisema analitafsiri kwamba ni njama za kumwangusha katika kinyang`anyiro hicho.

Hata hivyo, alisema hicho kinachoitwa ugomvi siyo kilichosababisha kufungwa kwa mkutano.

``Unajua Waziri Simba alitoa malalamiko yake kwangu wakati mkutano wetu tayari ukiwa umemalizika, hapakuwa na ugomvi mkubwa kama unavyouliza, bali Mwenyekiti wa UWT Mkoa (Kahama) alikuwa akijaribu kutoa ufafanuzi,`` alisema Guninita.

Alipoulizwa na Nipashe kuhusu kutoka katika kikao, Zungu alisema hakukimbia, bali muda wake wa kuondoka ulishafika.

``Mengine yaliyotokea huko nyuma sijui, lakini mimi nilishaondoka,`` alisema Zungu.

Akihojiwa na Nipashe kuhusu kutembeza ubabe kikaoni, awali Waziri Sophia alikana kwamba hajawahi kuhudhuria kikao hicho.

Hata hivyo, alipopigiwa simu mara ya pili, muda mfupi baada ya Guninita kukiri kupokea malalamiko kutoka kwake kikaoni, Simba alikiri kuwepo, lakini akahoji nani aliyevujisha habari za tukio hilo.

``Wewe sijui leo ni mtu wa ngapi kunipigia simu, watu wengi wamenipigia eti wanauliza kulikuwa na masumbwi kati yangu na Janeth. Sasa kwa nini mnaniuliza, huyo aliyeamua kuvujisha siri za kikao basi na awamalizie kilichoendelea,`` alisema.

Kahama alipopigiwa simu na kuulizwa kuhusu madai ya vurumai hizo, alikata simu na hadi tunakwenda mitamboni jana, simu yake ya kiganjani ilikuwa imefungwa.
• SOURCE: NIPASHE
 
Huyu mama kweli mambo mengi sana!Sophia Simba anajua kuna ulaji lazima agombee kwa vurugu!
Politics Is A Dirty Game!

Labda hela za Zain wanaojenga ofisi kuu zao kwenye kiwanja cha UWT
 
Nanukuu manenokatika gazeti liliandikuwa Bibie bi Sophia Simba alisema kwuwa ameambiwa na Rais kikwete agombanie hiyo nafasi ,hiyo ndiokauli yake sasa hapatujiulize nini kinaendelea na kuwachieni wachambuzi kwamuda huu mtafakari kauli yake bi simba .
 
Akihojiwa na Nipashe kuhusu kutembeza ubabe kikaoni, awali Waziri Sophia alikana kwamba hajawahi kuhudhuria kikao hicho.

Hata hivyo, alipopigiwa simu mara ya pili, muda mfupi baada ya Guninita kukiri kupokea malalamiko kutoka kwake kikaoni, Simba alikiri kuwepo, lakini akahoji nani aliyevujisha habari za tukio hilo.

``Wewe sijui leo ni mtu wa ngapi kunipigia simu, watu wengi wamenipigia eti wanauliza kulikuwa na masumbwi kati yangu na Janeth. Sasa kwa nini mnaniuliza, huyo aliyeamua kuvujisha siri za kikao basi na awamalizie kilichoendelea,`` alisema.

Kahama alipopigiwa simu na kuulizwa kuhusu madai ya vurumai hizo, alikata simu na hadi tunakwenda mitamboni jana, simu yake ya kiganjani ilikuwa imefungwa.
• SOURCE: NIPASHE



Hii mijitu sijui kama inajua kusoma nyakati.



.
 
Sophia Simba ubabe utakufikisha pabaya, Uza sera mama siyo kugeuza kikao uwanja wa masumbwi! hao nipashe naona wamekustahi, ukweli ni kwamba makonde alirusha na wanaume walipo jaribu mzuia aliwasukumizia kuleee.....

Ninalo shangaa jamani hivi ni ruksa waziri mwenye dahamana kurusha makonde mbele ya kadamnasi? hakuna 'ethics' hapo zilizo vunjwa?

Hapo ndiyo muone wenyewe hawa mawaziri wa JK! Amewachagua kwa kuzingatia nini!!!!
 
Nanukuu manenokatika gazeti liliandikuwa Bibie bi Sophia Simba alisema kwuwa ameambiwa na Rais kikwete agombanie hiyo nafasi ,hiyo ndiokauli yake sasa hapatujiulize nini kinaendelea na kuwachieni wachambuzi kwamuda huu mtafakari kauli yake bi simba .

Bwana Black Jesus itakuwa msaada mkubwa kama ukiweka link ya hilo gazeti
 
Akina mama mnatuangusha kwa kweli,mambo ya kususa susa tuu kila wakati hata hamkui.
 
"usifikiri uwaziri wako na kupata ofisi pale ikulu vitakusaidia, huu ni uchaguzi wa chama, heshimu taratibu za chama,`` chanzo chetu kilimnukuu kahama.

Habari zinasema kuwa mbunge wa ilala, mussa azan zungu, alisimama na kumuomba guninita asitishe hoja hiyo, kwa vile haiwahusu.

Imeelezwa kuwa, baada ya zungu kutoa hoja hiyo, waziri simba alimfuata huku akiwa ameweka vidole juu na kuanza kumsuta mbunge huyo na kumfokea kwamba anajifanya ni mjanja wa ccm jijini dar es salaam.

Habari hizo zinasema kuwa zungu alipoona simba amefuatwa kwenye kiti chake na kusimama mbele yake, aliamua kutoka haraka haraka na kuacha kikao. "
wasiwasi wangu haya malengo ya milenia ya kuongeza idadi ya akina mama katika uongozi yakitia hali itakuwaje.
Sijui....
 
Kumbe hawakushambuliana na wka maneno tu. kwa mujibu wa magazeti ya leo, Kahama anasema kuwa alikabwa na kupigwa ngumi na Simba. Anasema hali ilikuwa mbaya kiasi kwamba alikumbuka msalaba! Anasema hata wanaume wenye nguvu walijaribu kumshika Simba lakini walsihindwa kwa jinsi alivyogeuka mbogo
 
Kumbe hawakushambuliana na wka maneno tu. kwa mujibu wa magazeti ya leo, Kahama anasema kuwa alikabwa na kupigwa ngumi na Simba. Anasema hali ilikuwa mbaya kiasi kwamba alikumbuka msalaba! Anasema hata wanaume wenye nguvu walijaribu kumshika Simba lakini walsihindwa kwa jinsi alivyogeuka mbogo



Majina ya magazeti hayo!naomba jina la gazeti
 
Back
Top Bottom