Msongoru
JF-Expert Member
- Apr 16, 2008
- 306
- 24
Sophia Simba, Janeth Kahama washambuliana kwa maneno
2008-09-15 09:26:48
Na Simon Mhina
Kikao cha Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Dar es Salaam kilichokutana wiki iliyopita, kiliahirishwa kwa muda baada ya kutokea mzozo kati ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Sophia Simba, na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake ya Chama cha Mapinduzi (UWT) jijini, Janeth Kahama.
Janeth na Sophia wote wanawania nafasi ya Mwenyekiti wa UWT Taifa, ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikishikiliwa na Anna Abdallah.
Chanzo chetu ndani ya kikao hicho kimepasha kuwa kilichoibua mzozo huo ni malalamiko yaliyotolewa na Waziri Simba kwamba siku hizi hashirikishwi katika vikao vya UWT Mkoa wa Dar es Salaam, na malalamiko hayo kumgusa Kahama ambaye ndiye mwenyekiti.
Chanzo chetu kimepasha kuwa Waziri Simba alitoa malalamiko hayo kwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita.
Habari hizo zinasema baada ya Simba kuwasilisha malalamiko yake, Kahama alisimama kujitetea na kusema kuwa, Waziri huyo hapaswi kumlaumu mtu, kwa vile anajifanya ana shughuli nyingi kila wakati anapopelekewa taarifa za mwaliko wa vikao.
Kutokana na majibu hayo, chanzo chetu kimetupasha kuwa Waziri Simba alikuja juu huku akimshambulia Kahama kwa maneno, kwamba ana wivu, yaani anamuonea wivu kutokana na nafasi yake.
Habari hizo zinasema Kahama naye aliamua kujibu mapigo, huku akimrushia makombora mshindani wake kwamba Waziri huyo anatumia madaraka yake katika kampeni za kutaka achaguliwe uenyekiti wa Taifa wa UWT.
``Usifikiri uwaziri wako na kupata ofisi pale Ikulu vitakusaidia, huu ni uchaguzi wa Chama, heshimu taratibu za chama,`` chanzo chetu kilimnukuu Kahama.
Habari zinasema kuwa Mbunge wa Ilala, Mussa Azan Zungu, alisimama na kumuomba Guninita asitishe hoja hiyo, kwa vile haiwahusu.
Imeelezwa kuwa, baada ya Zungu kutoa hoja hiyo, Waziri Simba alimfuata huku akiwa ameweka vidole juu na kuanza kumsuta Mbunge huyo na kumfokea kwamba anajifanya ni mjanja wa CCM jijini Dar es Salaam.
Habari hizo zinasema kuwa Zungu alipoona Simba amefuatwa kwenye kiti chake na kusimama mbele yake, aliamua kutoka haraka haraka na kuacha kikao.
Habari hizo zinaendelea kueleza kuwa baada ya Zungu kuondoka katika kikao, Waziri Simba alielekea alipokuwa ameketi Kahama lakini wajumbe waliwatenganisha ili kuepusha mzozo zaidi.
Akihojiwa na Nipashe jana, Guninita alikiri kupokea malalamiko toka kwa Waziri Simba kwamba hashirikishwi kwenye mambo ya UWT, jambo ambalo alisema analitafsiri kwamba ni njama za kumwangusha katika kinyang`anyiro hicho.
Hata hivyo, alisema hicho kinachoitwa ugomvi siyo kilichosababisha kufungwa kwa mkutano.
``Unajua Waziri Simba alitoa malalamiko yake kwangu wakati mkutano wetu tayari ukiwa umemalizika, hapakuwa na ugomvi mkubwa kama unavyouliza, bali Mwenyekiti wa UWT Mkoa (Kahama) alikuwa akijaribu kutoa ufafanuzi,`` alisema Guninita.
Alipoulizwa na Nipashe kuhusu kutoka katika kikao, Zungu alisema hakukimbia, bali muda wake wa kuondoka ulishafika.
``Mengine yaliyotokea huko nyuma sijui, lakini mimi nilishaondoka,`` alisema Zungu.
Akihojiwa na Nipashe kuhusu kutembeza ubabe kikaoni, awali Waziri Sophia alikana kwamba hajawahi kuhudhuria kikao hicho.
Hata hivyo, alipopigiwa simu mara ya pili, muda mfupi baada ya Guninita kukiri kupokea malalamiko kutoka kwake kikaoni, Simba alikiri kuwepo, lakini akahoji nani aliyevujisha habari za tukio hilo.
``Wewe sijui leo ni mtu wa ngapi kunipigia simu, watu wengi wamenipigia eti wanauliza kulikuwa na masumbwi kati yangu na Janeth. Sasa kwa nini mnaniuliza, huyo aliyeamua kuvujisha siri za kikao basi na awamalizie kilichoendelea,`` alisema.
Kahama alipopigiwa simu na kuulizwa kuhusu madai ya vurumai hizo, alikata simu na hadi tunakwenda mitamboni jana, simu yake ya kiganjani ilikuwa imefungwa.
SOURCE: Nipashe
2008-09-15 09:26:48
Na Simon Mhina
Kikao cha Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Dar es Salaam kilichokutana wiki iliyopita, kiliahirishwa kwa muda baada ya kutokea mzozo kati ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora), Sophia Simba, na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake ya Chama cha Mapinduzi (UWT) jijini, Janeth Kahama.
Janeth na Sophia wote wanawania nafasi ya Mwenyekiti wa UWT Taifa, ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikishikiliwa na Anna Abdallah.
Chanzo chetu ndani ya kikao hicho kimepasha kuwa kilichoibua mzozo huo ni malalamiko yaliyotolewa na Waziri Simba kwamba siku hizi hashirikishwi katika vikao vya UWT Mkoa wa Dar es Salaam, na malalamiko hayo kumgusa Kahama ambaye ndiye mwenyekiti.
Chanzo chetu kimepasha kuwa Waziri Simba alitoa malalamiko hayo kwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita.
Habari hizo zinasema baada ya Simba kuwasilisha malalamiko yake, Kahama alisimama kujitetea na kusema kuwa, Waziri huyo hapaswi kumlaumu mtu, kwa vile anajifanya ana shughuli nyingi kila wakati anapopelekewa taarifa za mwaliko wa vikao.
Kutokana na majibu hayo, chanzo chetu kimetupasha kuwa Waziri Simba alikuja juu huku akimshambulia Kahama kwa maneno, kwamba ana wivu, yaani anamuonea wivu kutokana na nafasi yake.
Habari hizo zinasema Kahama naye aliamua kujibu mapigo, huku akimrushia makombora mshindani wake kwamba Waziri huyo anatumia madaraka yake katika kampeni za kutaka achaguliwe uenyekiti wa Taifa wa UWT.
``Usifikiri uwaziri wako na kupata ofisi pale Ikulu vitakusaidia, huu ni uchaguzi wa Chama, heshimu taratibu za chama,`` chanzo chetu kilimnukuu Kahama.
Habari zinasema kuwa Mbunge wa Ilala, Mussa Azan Zungu, alisimama na kumuomba Guninita asitishe hoja hiyo, kwa vile haiwahusu.
Imeelezwa kuwa, baada ya Zungu kutoa hoja hiyo, Waziri Simba alimfuata huku akiwa ameweka vidole juu na kuanza kumsuta Mbunge huyo na kumfokea kwamba anajifanya ni mjanja wa CCM jijini Dar es Salaam.
Habari hizo zinasema kuwa Zungu alipoona Simba amefuatwa kwenye kiti chake na kusimama mbele yake, aliamua kutoka haraka haraka na kuacha kikao.
Habari hizo zinaendelea kueleza kuwa baada ya Zungu kuondoka katika kikao, Waziri Simba alielekea alipokuwa ameketi Kahama lakini wajumbe waliwatenganisha ili kuepusha mzozo zaidi.
Akihojiwa na Nipashe jana, Guninita alikiri kupokea malalamiko toka kwa Waziri Simba kwamba hashirikishwi kwenye mambo ya UWT, jambo ambalo alisema analitafsiri kwamba ni njama za kumwangusha katika kinyang`anyiro hicho.
Hata hivyo, alisema hicho kinachoitwa ugomvi siyo kilichosababisha kufungwa kwa mkutano.
``Unajua Waziri Simba alitoa malalamiko yake kwangu wakati mkutano wetu tayari ukiwa umemalizika, hapakuwa na ugomvi mkubwa kama unavyouliza, bali Mwenyekiti wa UWT Mkoa (Kahama) alikuwa akijaribu kutoa ufafanuzi,`` alisema Guninita.
Alipoulizwa na Nipashe kuhusu kutoka katika kikao, Zungu alisema hakukimbia, bali muda wake wa kuondoka ulishafika.
``Mengine yaliyotokea huko nyuma sijui, lakini mimi nilishaondoka,`` alisema Zungu.
Akihojiwa na Nipashe kuhusu kutembeza ubabe kikaoni, awali Waziri Sophia alikana kwamba hajawahi kuhudhuria kikao hicho.
Hata hivyo, alipopigiwa simu mara ya pili, muda mfupi baada ya Guninita kukiri kupokea malalamiko kutoka kwake kikaoni, Simba alikiri kuwepo, lakini akahoji nani aliyevujisha habari za tukio hilo.
``Wewe sijui leo ni mtu wa ngapi kunipigia simu, watu wengi wamenipigia eti wanauliza kulikuwa na masumbwi kati yangu na Janeth. Sasa kwa nini mnaniuliza, huyo aliyeamua kuvujisha siri za kikao basi na awamalizie kilichoendelea,`` alisema.
Kahama alipopigiwa simu na kuulizwa kuhusu madai ya vurumai hizo, alikata simu na hadi tunakwenda mitamboni jana, simu yake ya kiganjani ilikuwa imefungwa.
SOURCE: Nipashe