Vipi tangazo lililo jamiiforums la modem ya Airtel kwa 30,000/- na free internet kwa miezi 6?

Magobe T

JF-Expert Member
Mar 19, 2008
4,619
2,567
Wadau, kuna tangazo hapa jamiiforums linasema: "Buy for only 30,000 Tsh and get free internet for 6 months. Visit any airtel shop." Naona hili tangazo linasema uongo maana jana nilinunua modem kwa 30,000/-, nikalipia bundle ya wiki moja lakini sikupata hiyo "free internet". Badala yake hela nilizolipia kwa bundle ya wiki moja 2,500/- ziliisha muda mchache baada ya kuweka. Sasa hiyo "free internet" kwa miezi sita iko wapi? Je, hawa njemba wanatudanganya ili watulie hela? Pia kuna offer ya Vodacom Tsh 7500 kwa 500MB. Je, waliokwishatumia mnashauri nini hapa? Nihamie Vodacom?
 
Kuna mwanaJF mmoja alishaleta habari hapa kuhusu hizo modem za airtel. Hayo maneno ya internet bure miezi 6 ni changa la macho - hakuna kitu kama hicho - ni lugha ya biashara tu kukuvutia! Wee endelea na bundle zao tu.
Kuhusu bendle za Vodacom, mimi natumia ile ya 2500 ya MG125. Lakini kama unadownload mavitu mengi inaisha kabla ya hizo siku 7. Kwenye hii ya vodacom huwa nabadilishabadilisha na BOMBA7 MB 750 kwa sh 10,000 kwa siku 7.

Ni hayo tu ndugu kwa leo.
 
....ni kwa sababu tu wahusika ni DHAIFU ndio maana makampuni yanaruhusiwa kutangaza uongo wa kuibia watu...!!
 
Vigezo na masharti kuzingatiwa. Kidogo tu namimi niingie mkenge kununua. Ila nikatafakari, kweli ununue kwa alf 30 halafu upewe miezi 6? haiji akilini. Dingi yangu akanunua na anadai bora ile ya zamani. Natumia ya Voda, nanunua BOMBA7 buku ten raha mstarehe.
 
Vigezo na masharti kuzingatiwa. Kidogo tu namimi niingie mkenge kununua. Ila nikatafakari, kweli ununue kwa alf 30 halafu upewe miezi 6? haiji akilini. Dingi yangu akanunua na anadai bora ile ya zamani. Natumia ya Voda, nanunua BOMBA7 buku ten raha mstarehe.
don-oba Wacha kutukosea heshima wazazi tulio humu jamvini hilo neno DINGI unamaanisha kitu gani?
Ebu njoo kwa magoti na ututake radhi wazazi wote humu.
 
Last edited by a moderator:
Wadau, kuna tangazo hapa jamiiforums linasema: "Buy for only 30,000 Tsh and get free internet for 6 months. Visit any airtel shop." Naona hili tangazo linasema uongo maana jana nilinunua modem kwa 30,000/-, nikalipia bundle ya wiki moja lakini sikupata hiyo "free internet". Badala yake hela nilizolipia kwa bundle ya wiki moja 2,500/- ziliisha muda mchache baada ya kuweka. Sasa hiyo "free internet" kwa miezi sita iko wapi? Je, hawa njemba wanatudanganya ili watulie hela? Pia kuna offer ya Vodacom Tsh 7500 kwa 500MB. Je, waliokwishatumia mnashauri nini hapa? Nihamie Vodacom?

.........ndio waliwao! We hujui kuwa hiyo ni biashara ya watu? Funguka mkuu utafilisika...!
 
kila kampuni inafanya itakvyo,hata kusema uongo kwani.hakuna wa kuwauliza.watetezi wa wananchi wote THAIFU.
 
Wao ndo wanatulipia tuwe hewani au tumekosea jamaa wa airtel watajibi
Kubba msemo wa kichama wanatuomba tuhamie
 
Kuna mwanaJF mmoja alishaleta habari hapa kuhusu hizo modem za airtel. Hayo maneno ya internet bure miezi 6 ni changa la macho - hakuna kitu kama hicho - ni lugha ya biashara tu kukuvutia! Wee endelea na bundle zao tu.
Kuhusu bendle za Vodacom, mimi natumia ile ya 2500 ya MG125. Lakini kama unadownload mavitu mengi inaisha kabla ya hizo siku 7. Kwenye hii ya vodacom huwa nabadilishabadilisha na BOMBA7 MB 750 kwa sh 10,000 kwa siku 7.

Ni hayo tu ndugu kwa leo.
Nilishaleta hii mada pia lakini post yangu ikaishia kuhamishwa kwenye Jamvi la malalamiko na hakuna kilichofanywa na wahusika. Mleta mada ni mmoja wa wadau waliopigwa changa la macho kwa kununua hiyo modem kwa tangazo hili..it's a shame kwa wizi unaofanywa na AIRTEL huku wakipata hifadhi humu Jamii Forum.
 
hawa jamaa wa airtel ni wezi tu kama wezi wengine nimenunua modem yao hadi leo ni siku 50 hivi zaidi ya mwezi wanodai wanatoa offer ya 6 miezi sijapata kitu
 
kuna jamaa yangu nilijaribu kumuulizia kuhusu hizi modem akaniambia kua hiyo ofa ya miezi sita inaanza kila ikifika saa sita za usiku nikaudhika sikufatilia kama ni kweli labda mjaribu.
 
jf ipo juu,hilo tangazo safi sana linaendana na hali halisi ya mtanzania hahahahahahahahahahahhaahha,



Du! Hwa njemba kiboko!Ni kama anayeenda baa kupta huduma na kukuta pombe bei Sh2,500 kwa halafu mhudumu wa luringa na choo hakivisafishwa karibia mwezi na bado wateja wanamiminika kuchapa maji na kumpa mwenye baa picha kuwa baa yake ina huduma nzuri. Ni kama daladala pia - gari chafu, konda mchafu na hajawahi kuoga kwa sababu ya kukosa nafasi kwa vile anatafuta 'chenji' ya mwenye gari na anapakia watu wanajaa mpa hakuna anayeweza kupimua vizuri. Halafu akisema: "wewe mwenye miwani sogea nyumba" unakuta mtu anasogea hata kama anajua hakuna nafasi. Hivi Watanzania tukoje? Tuna tatizo kichwani?
 
Pole Mkuu Magobe, airtel ni wezi!. Nashauri tupeleke rasmi malalamiko yetu TCRA kwa huu sio tuu ni wizi, bali ndani yake kuna ujambazi na utapeli!.

1. Kwanza unaambiwa "nunua moderm kwa 30,000 utapata internet bure kwa miezi 6!".
2. Ukishalipia, unakutana na 1st surprise eti kumbe hiyo 30,000 ni moderm tuu!, lazima ununue bundle!, nikadaiwa 14,000!. Nikalipa nikijiaminisha kama kweli ni miezi 6, bado inalipa!.
3. Kwanza iko slow, pili within a week, hakuna cha bundle wala miezi 6!.

Nimetumia moderm mbalimbali!.
1. Vodacom wako expensive na sio fast sana!.
2. Sasatel unalipa 30,000 wanakupa moderm bure with 4 GB tatizo hawajaenea sana!.
3. TTCL ndio fastest, unalipa bundle ya 8 kwa wiki wanakupa 2GB, tatizo recharge voucher zao ni issue na ukisafiri hawana mtandao uliosambaa ni makao makuu ya mikoa tuu!.
4.Zentel pia wako fast, cheap ila nao hawasambaa sana.
5. Airtel ndio cheapest kwa ile bundle yao ya 2,500 kwa wiki, mimi nimewanunulia watoto wangu wakubwa 4, nikifikiri ndio nawasaidia kumbe kwao hata siku hawamalizi na hawa wadogo wawili nao wanajisogeza kwenye laptops za kaka zao kuzama kwenye net games hivyo naumizwa sana.

ushauri kama uko fixed dar tumia TTCL au Zantel, ukisafiri njiani tumia Voda iko kote ila lazima utoboke au zain ila utasuasua!.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom