Elections 2010 Vipi sasa Mengi anakula sahani moja na mafisadi?

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
234


Nimekuwa nafuatilia sana ITV ya Mzee Mengi namna inavyo-cover kampeni za uchaguzi na nikagundua kwamba sasa kituo hicho sasa kiko benet na Channel 10 – kinachomilikiwa na mafisadi akina RA na Tanil Somaya, na yule mnwingine wa New Africa Hotel.

TV hizo mbili hazitoi kabisa kampeni za Chadema – zinaona bora zitoe kampeni za wagombea wa TLP, SAU au Tadea kuliko za Chadema!

Nikawa najiuliza inakuwaje hii, maana haijatulia kabisa hasa ukitia maanani kwamba baadhi ya wamiliki hao aliwataja kama mafisadi papa huko nyuma.

Kwa nini Mzee huyu anaiogopa Chadema wakati viongozi wake – hasa Dr Slaa, Zitto etc walikuwa mstari wa mbele kabisa kupinga ufisadi – kama alivyokuwa yeye Mengi? Kumetokea nini hapa katikati? Jee yeye na Mbowe hawawivi – ingawa wanatoka eneo moja huko Kilimanjaro?

Hata kama yeye Mengi ni CCM – hivi hajui wajibu wa chombo chake kwa umma katika kujenga demokrasia halisi. Hivi sasa ITV inaanza kutoa vitangazo vyake kuhusu uchaguzi, kwamba wagombea wafuate maadili etc – naona yote hayo ni unafiki tu. Kama chombo hicho hakitoi nafasi sawa kwa wagombea wa vyama vingine, basi ni unafiki mkubwa huo.

Hata hivyo nalipongeza gazeti lake la Nipashe – angalau linatoa habari za vyama vyote. Nadhani hii inatokana na umahiri wa Mhariri wake, Jesse Kwayu – mtu wa eneo hilo hilo la Kilimanjaro – lakini ninavyomjua mimi, yeye na mafisadi ni mbali mbali.
 
Mengi first and foremost ni mfanyabiashara kwa hiyo he is interested in the person who will butter his bread!!! Hayo mambo ya kupiga vita ufisadi ilikuwa geresha yake akituchuhuza kama yule Kiyabo wa CCJ alivyomchuuza Mpendazoe!!
 


Nimekuwa nafuatilia sana ITV ya Mzee Mengi namna inavyo-cover kampeni za uchaguzi na nikagundua kwamba sasa kituo hicho sasa kiko benet na Channel 10 – kinachomilikiwa na mafisadi akina RA na Tanil Somaya, na yule mnwingine wa New Africa Hotel.

TV hizo mbili hazitoi kabisa kampeni za Chadema – zinaona bora zitoe kampeni za wagombea wa TLP, SAU au Tadea kuliko za Chadema!

Nikawa najiuliza inakuwaje hii, maana haijatulia kabisa hasa ukitia maanani kwamba baadhi ya wamiliki hao aliwataja kama mafisadi papa huko nyuma.

Kwa nini Mzee huyu anaiogopa Chadema wakati viongozi wake – hasa Dr Slaa, Zitto etc walikuwa mstari wa mbele kabisa kupinga ufisadi – kama alivyokuwa yeye Mengi? Kumetokea nini hapa katikati? Jee yeye na Mbowe hawawivi – ingawa wanatoka eneo moja huko Kilimanjaro?

Hata kama yeye Mengi ni CCM – hivi hajui wajibu wa chombo chake kwa umma katika kujenga demokrasia halisi. Hivi sasa ITV inaanza kutoa vitangazo vyake kuhusu uchaguzi, kwamba wagombea wafuate maadili etc – naona yote hayo ni unafiki tu. Kama chombo hicho hakitoi nafasi sawa kwa wagombea wa vyama vingine, basi ni unafiki mkubwa huo.

Hata hivyo nalipongeza gazeti lake la Nipashe – angalau linatoa habari za vyama vyote. Nadhani hii inatokana na umahiri wa Mhariri wake, Jesse Kwayu – mtu wa eneo hilo hilo la Kilimanjaro – lakini ninavyomjua mimi, yeye na mafisadi ni mbali mbali.


Nakubaliana nawe. Kuhusu nipashe nadhani Mengi anaogopa likiandika utumbo wa kutetea mafisadi halitauza na hivyo kupoteza mapato. Si unajua tena wakati huu competition kali kutoka kwa T. Daima na Mwananchi? Kuhusu ITV ni different -- hakuna hofu ya kupoteza mapato.
 
Huyo ndiye Mengi halisia! Ukitaka kumfahamu zaidi muulize mpiganaji Mbwambo!!
 
CHADEMA ikiingia madarakani Mengi atabidika kulipa kodi zote, ikiwa ni pamoja na alizosamehewa kinyume cha sheria huko nyuma. Nadhani mnakumbuka habari za vitu kama Mengi kuingiza Mercedes Benz bila ushuru kwa madai kwamba ni la kusaidia vilema.

Kuna wanyonyaji, mabepari na mabwanyeye wengi wanaogopa CHADEMA kuingia madarakani. Wanajua mirija yao itakatwa, na waliovunja sheria wataajibishwa. Akina Mengi wako matumbo moto wakati huu. Wamesahau objectivity inayotakiwa kwenye journalism.
 
Huwezi kuwa CCM kama sio fisadi na huwezi kuwa fisadi kama sio CCM
 
Back
Top Bottom