Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Nimekuwa nafuatilia sana ITV ya Mzee Mengi namna inavyo-cover kampeni za uchaguzi na nikagundua kwamba sasa kituo hicho sasa kiko benet na Channel 10 kinachomilikiwa na mafisadi akina RA na Tanil Somaya, na yule mnwingine wa New Africa Hotel.
TV hizo mbili hazitoi kabisa kampeni za Chadema zinaona bora zitoe kampeni za wagombea wa TLP, SAU au Tadea kuliko za Chadema!
Nikawa najiuliza inakuwaje hii, maana haijatulia kabisa hasa ukitia maanani kwamba baadhi ya wamiliki hao aliwataja kama mafisadi papa huko nyuma.
Kwa nini Mzee huyu anaiogopa Chadema wakati viongozi wake hasa Dr Slaa, Zitto etc walikuwa mstari wa mbele kabisa kupinga ufisadi kama alivyokuwa yeye Mengi? Kumetokea nini hapa katikati? Jee yeye na Mbowe hawawivi ingawa wanatoka eneo moja huko Kilimanjaro?
Hata kama yeye Mengi ni CCM hivi hajui wajibu wa chombo chake kwa umma katika kujenga demokrasia halisi. Hivi sasa ITV inaanza kutoa vitangazo vyake kuhusu uchaguzi, kwamba wagombea wafuate maadili etc naona yote hayo ni unafiki tu. Kama chombo hicho hakitoi nafasi sawa kwa wagombea wa vyama vingine, basi ni unafiki mkubwa huo.
Hata hivyo nalipongeza gazeti lake la Nipashe angalau linatoa habari za vyama vyote. Nadhani hii inatokana na umahiri wa Mhariri wake, Jesse Kwayu mtu wa eneo hilo hilo la Kilimanjaro lakini ninavyomjua mimi, yeye na mafisadi ni mbali mbali.