Godwin Mneng'ene
JF-Expert Member
- Sep 20, 2010
- 215
- 83
Baada ya kujiuzulu Masauni kwenye nafasi ya uenyekiti wa UVCCM taifa nafasi yake imekaimiwa kwa muda mrefu bila kujazwa pamoja na wagombea mbalimbali kujitokeza kuonyesha nia ya kuitaka hiyo nafasi. Sasa hivi naona vijana kibao wamejitokeza kutaka kugombea nafasi ya makamu Mwenyekiti UVCCM taifa. Lakini nafasi ya mwenyekiti imekuwa kimya.
Kwa wadau wa ccm naomba inijuze hii imekaavipi na kwa nini tokea masauni ajiuzulu hajachaguliwa mwingine na kwa sasa mbona vijana wengi wanajitokeza kugombea umakamu na sio uenyekiti? au muda wa kugombea uenyekiti bado. Jamaani naombeni kujulishwa nipate kuelewa haya mambo. Ni mimi Mdau wa Siasa za Tanzania nisiyekuwa na chama.
Natanguliza shukrani kwa kujulishwa vizuri na kwa ufasaha
Kwa wadau wa ccm naomba inijuze hii imekaavipi na kwa nini tokea masauni ajiuzulu hajachaguliwa mwingine na kwa sasa mbona vijana wengi wanajitokeza kugombea umakamu na sio uenyekiti? au muda wa kugombea uenyekiti bado. Jamaani naombeni kujulishwa nipate kuelewa haya mambo. Ni mimi Mdau wa Siasa za Tanzania nisiyekuwa na chama.
Natanguliza shukrani kwa kujulishwa vizuri na kwa ufasaha