Viongozi wetu Afrika sijui wakoje?

Kigarama

JF-Expert Member
Apr 23, 2007
2,492
1,230
Nimewaangalia viongozi wetu watano wa Afrika wakiwa na Gordon Brown kwenye mjadala wa Uchumi huko Davos, nimeishiwa na nguvu kabisa ya kuamini kwamba hawa viongozi wetu wa Afrika wanao uwezo wa kututoa hapa tulipo. Wote watano hakuna hata mmoja wao aliyeonyesha ni kwa jinsi gani Waafrika tutashiriki kwenye kuleta mabadiliko duniani na kwenye bara letu. Kila mmoja kwa kuhamanika (Desperately) alikuwa anaonyesha ni kwa jinsi gani anahitaji kusaidiwa na "wawekezaji" ili wananchi wake wapate nafuu. Nimemwangalia Kikwete hadi nikajisemea moyoni "huyu jamaa si angebaki ashughulike na mgomo wa Madaktari kuliko hili analolifanya"

Mambo ya ujenzi wa madarasa na kuongeza waalimu haya ni mambo ya kuzungumza kwenye vikao na wazee pale Diamond Jubilee na siyo Davos. Sijasikia Kilimo cha kisasa, ulinganifu wa kibiashara duniani badala yake nasikia watu wazima wakiomba omba hadharani .Sasa nimeelewa ni kwa nini watu kama Jenerali Ulimwengu kila wakiandika makala zao ni lazima jina la Mwalimu Julius Kambarage Nyerere litajwe!! Hawa viongozi wetu wa sasa sijui wakoje?
 
Nyerere na jeuri yake yote lakini na yeye alikua anaomba misaada. Sasa hapa kuna ajabu gani
 
Nyerere na jeuri yake yote lakini na yeye alikua anaomba misaada. Sasa hapa kuna ajabu gani

Nenda kapime bichwa lako mkuu,naona sasa hujuhi kutofautisha kuomba tunakokusemea kwa sasa na kule kwa miaka ya 60's na 70's,ikiwezekana kasome upya historia ya Tanzania.

Hili la sahivi la viongozi wa Afrika linanifanya niwaone kama vile wamegeuzwa malaya ambao sasa wanashindana kujiuza waziwazi,wamegeuzwa nyumba ndogo na wazungu wamekuwa mabwana zao...huyu JK hana tofauti na nyumba ndogo ambaye sasa anatakiwa akomae hata kwa kutembea uchi ili akapewe chochote

Hawa ndo viongozi wetu ambao badala ya kutumia akili zao wameamua wazungu walale kisha waamke waanze kufikiria kwa niaba yao,sasa ukiwaachia wazungu wafikirie kwa niaba yako,wao wafikirie hata jinsi ya kuwalisha watu wako basi tayari umewauza watu wako na nchi yako,tuko Afrika lakini hatuna tofauti na kuwa utumwani kwani tumeuzwa na kufanywa watumwe kwenye nchi zetu wenyewe...Cursed African Leaders
 
Nyerere na jeuri yake yote lakini na yeye alikua anaomba misaada. Sasa hapa kuna ajabu gani
You are missing the point. Am wondering if it is so by design or by fault.Either way you represent degraded mind set
 
Nyerere na jeuri yake yote lakini na yeye alikua anaomba misaada. Sasa hapa kuna ajabu gani
Kuomba ni kuomba lakini staili ya kuomba huku unajidhalilisha inakera. Mwalimu alikuwa anao ujeuri wa kupambana na hii mifumo ya kinyonyaji mpaka siku zake za mwisho, hebu nenda kasome ripoti ya nchi za kusini (South South Commission report)
 
Viongozi wa kiafrika ni walafi tena kama fisi, sijui wanapoenda wanapewa nini Mungu wangu maana wamekuwa kama machangudoa hivi hawajui kuwa wakiwatumia waafrika wenzao wanaweza kulinyanyua bara hili?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom