Viongozi wawili wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, Josephat Isango- Mwenyekiti wa baraza la Vijana wa CHADEMA, Mkoa wa Singida, na Patrobas Paskali Katambi Mwenyekiti wa Chama wa tawi la St. Augustine University wametishiwa maisha katika matukio tofauti.
Josephat Isango, ameitishiwa kuuawa na Diwani wa kata ya Unyambwa, Shaban Salimu Sattu (CCM), baada ya kutoa taarifa polisi kuwa diwani huyo amesaidia watu mbalimbali akiwemo mke wake na mdogo wake, na mke wa jirani yake ambaye inadhaniwa kuwa ana uhusiano na diwani huyo pamoja na watu kadhaa kujipatia isivyo halali (kwa njia haramu) malipo ya pesa taslimu 54,000,000/-. Pesa ambazoa zilipaswa kuwa za fidia kwa watu watakaohamishwa, Diwani huyo amefikishwa mahakamani Singida mjini leo, amekana shitaka na yupo nje kwa dhamana hadi tarehe 5/June/2012.. Pamoja na kuripotiwa Wizi huo wa Shilingi 54,000,000/- Jeshi la polisi mkoani Singida limenyamazishwa kuhusu wizi huo ulioripotiwa tarehe 30/04/2012, na kuendelea kumlinda Diwani huyo aliyejipatia kitita kikubwa katika sakata hilo.
Kwa upande wa Patrobas Paskali, jana baada ya kutoka katika kipindi cha tuongee asubuhi katika kituo cha televisheni Star Tv. Kilichopo ilemela mwanza, alichukuliwa na gari ya Star TV hadi Nyegezi maeneo ya Nganza, aliposhushwa katika gari ya Star TV, na kuanza kutembea kuingia kwake alitekwa na kushikiliwa na kuhojiwa kwa nusu saaa na Njemba zilizokuwa na gari aina ya Noah , iliyokuwa na namba za Chasis, iliyoanzia na SX 212 . na kuonywa kuwa anachafua serikali, na kusema kuwa Rais ameshindwa kuongoza nchi, watu kadhaa walijitokeza katika njia hiyo na kusababisha Patrobas kuachiwa haraka na hao watu kukimbia na Diary ya Patrobas. Mwenyekiti huyo alinyanganywa Diary tu na kungangania begi lililokuwa na laptop na alishindwa kukariri namba zote za chasis zilizoandikwa katika gari hilo. Tukio hili limeripotiwa leo polisi, mkoani mwanza kwa MW/RB/5207/2012, JALADA LA UCHUNGUZI.
Huku ndiko tunakoelekea?
Josephat Isango, ameitishiwa kuuawa na Diwani wa kata ya Unyambwa, Shaban Salimu Sattu (CCM), baada ya kutoa taarifa polisi kuwa diwani huyo amesaidia watu mbalimbali akiwemo mke wake na mdogo wake, na mke wa jirani yake ambaye inadhaniwa kuwa ana uhusiano na diwani huyo pamoja na watu kadhaa kujipatia isivyo halali (kwa njia haramu) malipo ya pesa taslimu 54,000,000/-. Pesa ambazoa zilipaswa kuwa za fidia kwa watu watakaohamishwa, Diwani huyo amefikishwa mahakamani Singida mjini leo, amekana shitaka na yupo nje kwa dhamana hadi tarehe 5/June/2012.. Pamoja na kuripotiwa Wizi huo wa Shilingi 54,000,000/- Jeshi la polisi mkoani Singida limenyamazishwa kuhusu wizi huo ulioripotiwa tarehe 30/04/2012, na kuendelea kumlinda Diwani huyo aliyejipatia kitita kikubwa katika sakata hilo.
Kwa upande wa Patrobas Paskali, jana baada ya kutoka katika kipindi cha tuongee asubuhi katika kituo cha televisheni Star Tv. Kilichopo ilemela mwanza, alichukuliwa na gari ya Star TV hadi Nyegezi maeneo ya Nganza, aliposhushwa katika gari ya Star TV, na kuanza kutembea kuingia kwake alitekwa na kushikiliwa na kuhojiwa kwa nusu saaa na Njemba zilizokuwa na gari aina ya Noah , iliyokuwa na namba za Chasis, iliyoanzia na SX 212 . na kuonywa kuwa anachafua serikali, na kusema kuwa Rais ameshindwa kuongoza nchi, watu kadhaa walijitokeza katika njia hiyo na kusababisha Patrobas kuachiwa haraka na hao watu kukimbia na Diary ya Patrobas. Mwenyekiti huyo alinyanganywa Diary tu na kungangania begi lililokuwa na laptop na alishindwa kukariri namba zote za chasis zilizoandikwa katika gari hilo. Tukio hili limeripotiwa leo polisi, mkoani mwanza kwa MW/RB/5207/2012, JALADA LA UCHUNGUZI.
Huku ndiko tunakoelekea?