Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
Viongozi wakuu wa nchi sasa kuzikwa Dodoma *wamo Rais,Makamu, Spika, Waziri Mkuu, Jaji MKuu Na Habel Chidawali, Dodoma
VIONGOZI wa juu serikali akiwamo Rais, Makamu, waziri mkuu sasa wataanza kuzikwa katika eneo maalum la ekari 100 lililotengwa kwa ajili ya mazishi ya viongozi hao.
Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Mkurugenzi Mkuu Ustawishaji Makao Makuu (CDA), Martin Kitila, jana zinaeleza kuwa viongozi wataanza kuzikwa katika eneo hilo baada ya kukamilika kwa maandalizi yake.
Alisema viongozi wengine ambao watazikwa katika eneo hilo na wakuu wa mihili ya dola ambo ni Spika na bunge na Jaji Mkuu.
Kitila hakuweza kufafanua mwisho wa mvutano wa Bunge katika pande mbili zinazopingana kuhusu rais wa Zanzibar kuzikwa eneo hilo.
Mchakato wa kupata eneo hilo ulioanza miaka mingi iliyopita, ulilenga kuwa na eneo la pamoja kwa ajili ya mazishi ya viongozi wakuu wa nchi ili kutunza Kumbukumbu zao kwa ajili ya vizazi vijavyo.
Kitila alisema CDA imetenga eneo hilo kwa kushirikiana na ofisi ya Waziri Mkuu na kwamba kuanzia sasa viongozi hao kiongozi yoyote atakayekufa, atazikwa hapo badala ya sasa ambapo kila kiongozi anazikwa eneo lake.
Viongozi wa juu wa serikali waliokufa mpaka sasa ambao wanastahili kuzikwa eneo hilo ni pamoja na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere aliyefariki Oktoba 14, 1999, na kuzikwa nyumbani kwa Butiama mkoani Mara, Waziri Mkuu Edward Soikoine aliyefariki Aprili 20, 1984 na kuzikwa nyumbani kwake Monduli Juu mkoani Arusha, Jaji Mkuu, Francis Nyalali.
Wengine ni Spika wa Bunge, Adam Sapi Mkwawa,Makamu wa Rais, Dk Omar Ali Juma ambaye alizikwa nyumbani kwao Pemba.
Kwa mujibu wa Kitila eneo hilo lililoko Chimwaga karibu na mipaka ya Chuo Kikuu cha Dodoma (DOM),liko chini ya Kitengo cha Maadhimisho kilichopo ofisi ya Waziri Mkuu.
Alisema kazi iliyopo sasa ni kusafisha eneo hilo na kukamilisha mipaka yake baada ya kumalizika kwa michoro na ramani.
"Eneo hilo liko tayari, lipo maeneo ya Chimwaga, kazi tuliyonayo sasa ni kulisafisha na kuweka mipaka vizuri kisha litakuwa chini ya ulinzi kwa hiyo sio kificho tena katika suala
hilo," alisema Kitila.
Eneo hilo ambalo kwa mujibu wa jiografia ya Mji wa Dodoma litakuwa kwenye
miinuko ya upande wa Kusini mwa mji, limekuwa na tafsiri tofauti kwa wakazi wa mji huu.
Baadhi ya wakazi wa mji huo waliozungumza na gazeti hili walihoji mantiki ya serikali kushindwa kuhamishia makao makuu ya Serikali Dodoma badala yake kuweka makao makuu ya makaburi ya viongozi wa serikali.
Mmoja wa watu wanaopinga wazo la kuweka makaburi ya viongozi Dodoma ni Mbunge wa Kibakwe (CCM), George Simbachawene ambaye alihoji mantiki yake wakati serikali imeshindwa kuhamia Dodoma.
Simbachawene ambaye ni mbunge kijana kuliko wabunge wote wa Mkoa wa Dodoma, kimsingi hakupinga kutengwa kwa eneo hilo isipokuwa alikosoa utaratibu wa kuharakisha makaburi badala ya kuharakisha makao makuu ya serikali kama ilivyopitishwa 1973.
Kwa upande wake Balozi Mstaafu Job Lusinde alisema kuwa kutengwa kwa eneo hilo ni hatua moja ya kusonga mbele na kutekelezwa kwa baadhi ya mipango ya serikali katika kuifanya Dodoma kuwa makao makuu.
Hata hivyo, alisema kuwa hatua hiyo imechelewa na kufanya maziko ya Baba wa Taifa yakafanyika katika kijiji cha Butiama mkoani Mara badala ya Dodoma ambako ndiko alikostahili kuzikwa kiongozi huyo wa kwanza wa Tanzania.
"Mpango wa kutenga eneo hilo ni wa muda mrefu sana wala haukuanza leo na kama wangetenga mapema ni imani yangu kuwa hata Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Nyerere angezikwa hapa Dodoma" alisema Lusinde.
Lusinde ambaye ni miongoni mwa Mawaziri wa kwanza katika serikali ya Tanganyika, alisema kuwa kutengwa kwa eneo hilo kusionekane kuwa ni jambo jipya kwani lilizungumzwa miaka mingi iliyopita.
Kulingana na ramani ya CDA ambayo inachukua eneo lote la Manispaa ya Dodoma, eneo hilo kwa siku za usoni litakuwa katikati ya Mji umbali wa hatua chache kutoka zinapotarajiwa kujengwa ofisi mbalimbali Wizara na idara za serikali.
VIONGOZI wa juu serikali akiwamo Rais, Makamu, waziri mkuu sasa wataanza kuzikwa katika eneo maalum la ekari 100 lililotengwa kwa ajili ya mazishi ya viongozi hao.
Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Mkurugenzi Mkuu Ustawishaji Makao Makuu (CDA), Martin Kitila, jana zinaeleza kuwa viongozi wataanza kuzikwa katika eneo hilo baada ya kukamilika kwa maandalizi yake.
Alisema viongozi wengine ambao watazikwa katika eneo hilo na wakuu wa mihili ya dola ambo ni Spika na bunge na Jaji Mkuu.
Kitila hakuweza kufafanua mwisho wa mvutano wa Bunge katika pande mbili zinazopingana kuhusu rais wa Zanzibar kuzikwa eneo hilo.
Mchakato wa kupata eneo hilo ulioanza miaka mingi iliyopita, ulilenga kuwa na eneo la pamoja kwa ajili ya mazishi ya viongozi wakuu wa nchi ili kutunza Kumbukumbu zao kwa ajili ya vizazi vijavyo.
Kitila alisema CDA imetenga eneo hilo kwa kushirikiana na ofisi ya Waziri Mkuu na kwamba kuanzia sasa viongozi hao kiongozi yoyote atakayekufa, atazikwa hapo badala ya sasa ambapo kila kiongozi anazikwa eneo lake.
Viongozi wa juu wa serikali waliokufa mpaka sasa ambao wanastahili kuzikwa eneo hilo ni pamoja na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere aliyefariki Oktoba 14, 1999, na kuzikwa nyumbani kwa Butiama mkoani Mara, Waziri Mkuu Edward Soikoine aliyefariki Aprili 20, 1984 na kuzikwa nyumbani kwake Monduli Juu mkoani Arusha, Jaji Mkuu, Francis Nyalali.
Wengine ni Spika wa Bunge, Adam Sapi Mkwawa,Makamu wa Rais, Dk Omar Ali Juma ambaye alizikwa nyumbani kwao Pemba.
Kwa mujibu wa Kitila eneo hilo lililoko Chimwaga karibu na mipaka ya Chuo Kikuu cha Dodoma (DOM),liko chini ya Kitengo cha Maadhimisho kilichopo ofisi ya Waziri Mkuu.
Alisema kazi iliyopo sasa ni kusafisha eneo hilo na kukamilisha mipaka yake baada ya kumalizika kwa michoro na ramani.
"Eneo hilo liko tayari, lipo maeneo ya Chimwaga, kazi tuliyonayo sasa ni kulisafisha na kuweka mipaka vizuri kisha litakuwa chini ya ulinzi kwa hiyo sio kificho tena katika suala
hilo," alisema Kitila.
Eneo hilo ambalo kwa mujibu wa jiografia ya Mji wa Dodoma litakuwa kwenye
miinuko ya upande wa Kusini mwa mji, limekuwa na tafsiri tofauti kwa wakazi wa mji huu.
Baadhi ya wakazi wa mji huo waliozungumza na gazeti hili walihoji mantiki ya serikali kushindwa kuhamishia makao makuu ya Serikali Dodoma badala yake kuweka makao makuu ya makaburi ya viongozi wa serikali.
Mmoja wa watu wanaopinga wazo la kuweka makaburi ya viongozi Dodoma ni Mbunge wa Kibakwe (CCM), George Simbachawene ambaye alihoji mantiki yake wakati serikali imeshindwa kuhamia Dodoma.
Simbachawene ambaye ni mbunge kijana kuliko wabunge wote wa Mkoa wa Dodoma, kimsingi hakupinga kutengwa kwa eneo hilo isipokuwa alikosoa utaratibu wa kuharakisha makaburi badala ya kuharakisha makao makuu ya serikali kama ilivyopitishwa 1973.
Kwa upande wake Balozi Mstaafu Job Lusinde alisema kuwa kutengwa kwa eneo hilo ni hatua moja ya kusonga mbele na kutekelezwa kwa baadhi ya mipango ya serikali katika kuifanya Dodoma kuwa makao makuu.
Hata hivyo, alisema kuwa hatua hiyo imechelewa na kufanya maziko ya Baba wa Taifa yakafanyika katika kijiji cha Butiama mkoani Mara badala ya Dodoma ambako ndiko alikostahili kuzikwa kiongozi huyo wa kwanza wa Tanzania.
"Mpango wa kutenga eneo hilo ni wa muda mrefu sana wala haukuanza leo na kama wangetenga mapema ni imani yangu kuwa hata Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Nyerere angezikwa hapa Dodoma" alisema Lusinde.
Lusinde ambaye ni miongoni mwa Mawaziri wa kwanza katika serikali ya Tanganyika, alisema kuwa kutengwa kwa eneo hilo kusionekane kuwa ni jambo jipya kwani lilizungumzwa miaka mingi iliyopita.
Kulingana na ramani ya CDA ambayo inachukua eneo lote la Manispaa ya Dodoma, eneo hilo kwa siku za usoni litakuwa katikati ya Mji umbali wa hatua chache kutoka zinapotarajiwa kujengwa ofisi mbalimbali Wizara na idara za serikali.