Viongozi wa Tanzania hawawajali wananchi wao?

Isango

R I P
Jul 23, 2008
295
450
Sitaki kuamini kuwa wagonjwa wanateseka muhimbili, na ocean road kwa ajili ya mgomo wa madaktari. Sitaki kuamini kuwa serikali imeshindwa kuwatekelezea mahtaji yao. Suala la posho kwa madaktari ndio watanzania wanaambiwa hakuna pesa, ila posho bungeni ziliongezwa hata bila ubishi. Kwa wabunge pesa zipo ila taasisi zingine mpaka wagome. Sitaki kuamini kuwa serikali imeshindwa kutatua tatizo hili na kusababisha watu wafe. Siamini zaidi kusikia kuwa mkuu wa nchi naye ameamua kusafiri huku hali hiyo ikiendelea wakati suluhisho likiwa halijapatikana. Mkuu wa nchi anafurahia ziara, wagonjwa katika nchi yake wanakufa........ Siamini. Inakatisha tamaa nchi yetu
 
"Hata kama madaktari wanagoma nani anajali? hata kama sisi tunakufa nani anajali? Wakiugua watanzania walio na maisha bora India watatibiwa, sisi wadanganyika ndo tuishe kabisa. nani anajali? Hata wabunge mnaojidai mna huruma mpaka sasa hamjatoa kauli katika hali hii. Watanzania masikini......... tulikosea!
 
Dunia haimtendei haki mlipa kodi ikiwemo mkulima. madaktari wamesomeshwa bure kwa fedha zetu wakiwemo wananchi wa kipato cha chini sana lakini wakihitimu masomo badala ya kurudisha raslimali zetu kwa njia ya huduma kwa kututibu wao wanasema ni muhimu kuliko jamii yote wakisahau hali ya wagonjwa ambao kimsingi ndio wamewasomesha madaktari hadi wamefika hapo. Hivi na sisi wagonjwa kabla hatujaugua tungegoma kuwalipia ada ya shule wangefika hapo na kuwa madaktari?

jamani twende taratibu mwendo wao ni mdundo mno.
 
unaweza kukuta mtu ni mchafu na mgonjwa kafika hospitali lakini wewe daktari kumbuka hustahiri kumwadhibu mgonjwa kwani kodi yake ndiyo imekusomesha hadi umekuwa daktari. umuhimu wako daktari ni kwa sababu mgonjwa aliye mbele yako alikusomesha. Madaktari hebu tafuteni adhabu zingine za madai yenu sio dhidi ya sisi wagonjwa tuliohangaika kuwasomesha.
 
watu wanapiga dili ya kutafuta wawekezaji wa hiyo muhimbili nyie mnahangaika na madaktari?
subirini wachina wakishauziwa ndipo mdai nyongeza ya mishahara.
 
Yaani kwa sababu waheshimiwa wanatibiwa India wamekaa kimya
wanaopata shida ni walio na kipato kidogo
kweli inasikitisha sana kweli siasa zaidi .... oooh tutawasaidia wananchi
kwenye kutafuta kura maneno kibao utekelezaji .......... sasa hapo si
mkatae posho zenu wapewe madaktari? Tutaona kuwa mnatupenda
na mnajali kazi yao
 
Napata uchungu sana pale mtu anaposhindwa kumsikiliza daktari hebu tafakari ni mangapi anafanya ambayo hatawewe huwezi kufanya jamani tuwe wakweli maana watu wengine ooooh udaktari kazi ya wito . Sasa huo wito unaokosa malipo madhara yake ndiyo migomo ila watu wanapeana hela kama kwenye vikaona posho zisizoisha.Kwa daktari hamtaki kutoa kweli MFUMO MBOVU mbaya zaidi siasa imeingia kwenye sekta muhimu ndiyo madhara haya. Siasa ikiingia kwenye sekta muhimu madhara ni makubwa zaidi kuliko
 
Tuache unafiki humu JF
Madaktari wanagoma, wanakwenda kinyume na kiapo chao, wanaua watu kwa kisingizio cha kudai maslahi bora, badala ya kuwakemea tunajifanya tunawaonea sana huruma, tunaikemea serikali ambayo imeshatuzoweakila siku tunaikashifu wala hatuisifii inapotenda vema. Serikalini kila sekta pako hoi, malamiko ya vitendea kazi na marupurupu kiduchu yametandawaa miongoni mwa watumishi serikalini, je na wengine wagome??Mfano JWTZ, Polisi, TANESCO, Uhamiaji, Magereza, DAWASCO, na wengineo wakigoma, halafu tufikiri kama nasi humu tungebaki salama. Ikumbukwe kila kazi ni muhimu ndiyo maana ikawepo, Rais wetu amesha kubaliana na CHADEMA kuhusu mabadiliko ya katiba, hii ndiyo fursa ya kuweka mambo yote sawa kwenye katiba, fomula ya mishahara/marupurupu ya watumishi wote including wanasiasa iwepo kwenye katiba kuondoa migongano na migomo.
 
Back
Top Bottom