Mongoiwe
JF-Expert Member
- Feb 26, 2008
- 524
- 263
WAZIRI Benard Membe leo alikuwa na wakati mgumu kuwabembeleza viongozi wa madhehebu na Dini za Kikristu pale alipokuwa akifanya nao kikao kuwasii wasimchukue JK na kupuuza uvumi unaoenezwa na kwamba serikali yake inao udini.
Alisema kuwa katika uvumi huo inadaiwa serikali ya Tanzania itajiunga na OIC mwaka 2012 na kuanzisha Mahakama ya kadhi kipindi cha utawala wa JK na kusema hayo siyo kweli na kwamba ametumwa na JK kuja kusafisha hali ya Hewa kwa viongozi wa dini Mwanza.
Katika majibu ya viongozi hao wa dini walimjibu Membe kuwa kama nchi haina Udini kwa nini JK hakemei udini na kwamba kwa nini aibuke na kumtuma Membe wakati huu wa uchaguzi tu kama siyo siasa.
Pili walimueleza kuwa ameshindwa kuwawajibisha mafisadi na kuwanadi jukwaani hivyo kumtamkiwa wazi kuwa hawako tayari kumchagua kuwa kiongozi na kama alitambua jambo hilo alipaswa kuwaona yeye mwenyewe na kutamka wazi mbele yao kuwa Tanzania haijaingia katika Udini na siyo kuwatumia mtu kwani kufanya hivyo ni sawa na kujisafisha katika kampeni.
Membe aliondoka bila muafaka wa viongozi hao wa dini na hata alipofika nje alikataa kuongea na waandishi wa habari.
Alisema kuwa katika uvumi huo inadaiwa serikali ya Tanzania itajiunga na OIC mwaka 2012 na kuanzisha Mahakama ya kadhi kipindi cha utawala wa JK na kusema hayo siyo kweli na kwamba ametumwa na JK kuja kusafisha hali ya Hewa kwa viongozi wa dini Mwanza.
Katika majibu ya viongozi hao wa dini walimjibu Membe kuwa kama nchi haina Udini kwa nini JK hakemei udini na kwamba kwa nini aibuke na kumtuma Membe wakati huu wa uchaguzi tu kama siyo siasa.
Pili walimueleza kuwa ameshindwa kuwawajibisha mafisadi na kuwanadi jukwaani hivyo kumtamkiwa wazi kuwa hawako tayari kumchagua kuwa kiongozi na kama alitambua jambo hilo alipaswa kuwaona yeye mwenyewe na kutamka wazi mbele yao kuwa Tanzania haijaingia katika Udini na siyo kuwatumia mtu kwani kufanya hivyo ni sawa na kujisafisha katika kampeni.
Membe aliondoka bila muafaka wa viongozi hao wa dini na hata alipofika nje alikataa kuongea na waandishi wa habari.