Mchungaji Pentekoste adaiwa kuuza kanisa, atimkia Zambia
2009-03-14 11:14:13
Na Thobias Mwanakatwe, Mbeya
Kanisa la Pentekoste Evangelistic Church lililopo mkoani hapa limeendelea kuandamwa na mikosi baada ya mchungaji wake, Ezekia Mwangomo, kudaiwa kuuza majengo ya kanisa na kukimbilia Lusaka, Zambia.
Mchungaji Mwangomo alikuwa akitoa huduma za kiuchungaji kwenye kanisa lililopo eneo la Sogea Wilaya Rungwe.
Taarifa za mchungaji huyo kudaiwa kuuza majengo ya kanisa zimekuja huku sakata la mchungaji Cosmas Mwasenga wa kanisa hilo lililopo kijiji cha Idiwili wilayani Mbozi, akisota rumande akituhumiwa kukamatwa na viungo vya binadamu.
Askofu Mkuu wa Kanisa la Pentekoste Evangelistic Church, Zebadia Mwakatage, hivi karibuni alisema mchungaji Mwangomo alikimbilia nchini Zambia baada ya kuuza majengo ya kanisa.
Askofu Mwakatage alisema kutokana na mchungaji huyo kuuza majengo ya kanisa yaliyopo Kijiji cha Sogea wilayani Rungwe, tayari huduma za ibada zimesitishwa kwa muda mrefu.
Hata hivyo, Mwakatange alisema kanisa lake limeendelea kutoa huduma za ibara kwenye makanisa yapatayo 15 yaliyopo Mbeya, Mara, Mwanza, Dar es Salaam na nchi jirani ya Zambia.
Juhudi za mwandishi wa habari hizi kumpa mchungaji anayetuhumiwa hazikufanikiwa kwa sababu, yupo nje ya nchi.
Hivi karibuni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Zelothe Stephen, alisema mchungaji Mwasenga na mwenzake Luseshelo Mwashilindi walikamatwa na viungo vya binadamu vinavyosadikiwa kuwa vya albino ambavyo walikutwa wakiviuza kwa Sh milioni 30.
SOURCE: Nipashe
2009-03-14 11:14:13
Na Thobias Mwanakatwe, Mbeya
Kanisa la Pentekoste Evangelistic Church lililopo mkoani hapa limeendelea kuandamwa na mikosi baada ya mchungaji wake, Ezekia Mwangomo, kudaiwa kuuza majengo ya kanisa na kukimbilia Lusaka, Zambia.
Mchungaji Mwangomo alikuwa akitoa huduma za kiuchungaji kwenye kanisa lililopo eneo la Sogea Wilaya Rungwe.
Taarifa za mchungaji huyo kudaiwa kuuza majengo ya kanisa zimekuja huku sakata la mchungaji Cosmas Mwasenga wa kanisa hilo lililopo kijiji cha Idiwili wilayani Mbozi, akisota rumande akituhumiwa kukamatwa na viungo vya binadamu.
Askofu Mkuu wa Kanisa la Pentekoste Evangelistic Church, Zebadia Mwakatage, hivi karibuni alisema mchungaji Mwangomo alikimbilia nchini Zambia baada ya kuuza majengo ya kanisa.
Askofu Mwakatage alisema kutokana na mchungaji huyo kuuza majengo ya kanisa yaliyopo Kijiji cha Sogea wilayani Rungwe, tayari huduma za ibada zimesitishwa kwa muda mrefu.
Hata hivyo, Mwakatange alisema kanisa lake limeendelea kutoa huduma za ibara kwenye makanisa yapatayo 15 yaliyopo Mbeya, Mara, Mwanza, Dar es Salaam na nchi jirani ya Zambia.
Juhudi za mwandishi wa habari hizi kumpa mchungaji anayetuhumiwa hazikufanikiwa kwa sababu, yupo nje ya nchi.
Hivi karibuni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Zelothe Stephen, alisema mchungaji Mwasenga na mwenzake Luseshelo Mwashilindi walikamatwa na viungo vya binadamu vinavyosadikiwa kuwa vya albino ambavyo walikutwa wakiviuza kwa Sh milioni 30.
SOURCE: Nipashe