Viongozi wa Bunge na wabunge someni hii kisha mtafakari "Bunge la Hoja Vs Bunge la Kanuni"

Chaimaharage

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
211
78
Hii ni makala iliyo andaliwa na Dr.Kitila Mkumbo(Jembe) kwenye gazeti la Raia Mwema, Toleo la 251, 25 July 2012.


KATIKA siku za hivi karibuni majadiliano katika Bunge letu yamepata ufuasi mkubwa kutoka kwa wananchi wanaofuatilia kupitia luninga na redio. Kuna Mwalimu mwenzetu mmoja Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambaye kwa muda sasa amekuwa akirudi nyumbani kila ifikapo saa nne asubuhi na saa kumi na moja, jioni kwenda kutazama kipindi cha Bunge. Imefika mahala anamshindwa kuacha kwenda kutazama majadiliano bungeni na anaporudi hutusimulia yaliyojiri kwa furaha na hamasa kubwa.

Hata hivyo, katika siku za karibuni ameacha kwenda kutazama Bunge kama ilivyo kawaida yake, kwa sababu anazodai kuwa Bunge letu limegeuka kuwa Bunge la Kanuni badala ya Bunge la Hoja ! Kwamba Bunge letu limekuwa likitumia muda mwingi kulumbana juu ya matumizi ya kanuni za Bunge, badala ya kujadiliana hoja zinazohusu maisha ya wananchi na taifa kwa ujumla. Na kuna wabunge ambao wameamua kubobea katika kutoa miongozo kiasi cha kupachikwa jina la ‘Mbunge wa Mwongozo' mitaani.

Kwa mujibu wa maoni ya wananchi yaliyochapishwa katika magazeti ya Jumapili iliyopita, ni wazi kwamba wananchi wengi wameanza kukosa hamasa na hamu ya kutazama majadiliano bungeni kama ilivyo kwa mwalimu mwenzangu niliyemtaja. Maoni ninayoyatoa katika makala haya yana lengo la kujaribu kuwakumbusha wabunge, na hasa viongozi wa Bunge, juu ya wajibu wao ili warudi katika mstari na kuwapa wananchi kile wanachokitarajia kutoka kwao.
Katika Jumuiya ya Madola, Bunge lina kazi kubwa nne za msingi. Kazi ya kwanza ni kujadili, kutathmini na kusimamia utendaji wa serikali. Kazi ya pili ni kujadili na kupitisha sheria mbalimbali. Kazi ya tatu ni kuiwezesha serikali kupandisha kodi kupitia bajeti za kila mwaka. Kazi ya nne ni kujadili na kutoa mwelekeo juu ya jambo lolote zito lililotokea katika nchi ambalo linaweza kuchukuliwa kama dharura.

Ukiwa mfuatiliaji wa Bunge letu utakubaliana nami kwamba Bunge letu limefanya kazi nzuri sana katika maeneo mawili, ambayo ni kupitisha sheria na kuiwezesha serikali kupandisha kodi mbalimbali kupitia bajeti za kila mwaka. Kwa maoni yangu, Bunge letu halijafanya kazi yake sawa sawa katika kujadili, kutathmini na kusimamia utendaji wa serikali. Hata lugha ambazo wabunge wetu wanazitumia bungeni ni kielelezo cha kutosha juu ya wao kupwaya katika kuelewa au kuzingatia uzito wa mamlaka yao dhidi ya serikali ambayo yapo wazi kikatiba. Kwa mfano, wabunge wengi wanapowasilisha maoni au mahitaji yao kuhusu jambo fulani wana tabia ya kusema kwamba ‘ninaiomba au ‘ninaishauri' serikali. Sasa hata kama mimi nilikuwa ndiye serikali ukishaniambia ‘unaomba' au ‘unanishauri' ni wazi kwamba nina hiari ya kukubali au kukataa ombi au ushauri wako. Serikali ina washauri chungu nzima ambao wameajiriwa kwa ajili hiyo wakifanya utafiti na uchambuzi kwa ajili ya kuishauri serikali kitaalamu, ambao ni muhimu zaidi kuliko ushauri wa mbunge unaotolewa katika dakika 10 anaposimama bungeni.

Kwa sababu wabunge wetu wamekaa kiushauri zaidi kuliko kiuwajibikaji, wamefika mahala hawawezi kujadili jambo lolote zito hadi serikali ikubali kushauriwa. Na ni bahati mbaya kwamba viongozi wa Bunge wanaisikiliza serikali zaidi kuliko wanavyowasikiliza wabunge. Na serikali nao wamebuni mtindo unaowasaidia kukwepesha mijadala mizito kwa kutumia kanuni. Kwa hivyo serikali, badala ya kujiandaa kujibu hoja, inajiandaa kwa kutafuta kanuni ya kukwamisha mjadala ! Matokeo yake ni kwamba Bunge letu lipo ‘busy' kulumbana juu ya kanuni badala ya kulumbana juu ya hoja, na hatimaye upande wa serikali hushinda-kwa kukwamisha mjadala. Ndivyo ambavyo mijadala mizito kama ya utekwaji wa Dk. Steven Ulimboka na kuzama kwa meli ya MV Skagit ilivyozimwa. Kwa kutumia kanuni za Bunge, viongozi wa Bunge wametukosesha fursa muhimu na adimu ya kujua kilichomkumba Dk. Ulimboka na sababu hasa za matukio yanayofuatana ya kuzama kwa meli huko Zanzibar. Bunge letu limeingia katika historia isiyotukuka kwa kukubali kukatazwa kutekeleza kujadili mambo mazito katika jamii.

Ni muhimu viongozi wa Bunge wakazingatia kwamba watazamaji na wasikilizaji wa vipindi vya Bunge hawapo kwa ajili ya kushuhudia umahiri wa kuzijua kanuni za Bunge. Wana hamu na hamasa ya kutazama na kusikiliza jinsi ambavyo wabunge wao wanaibua hoja zinazohusu maisha yao na nchi yao. Na hili ndilo lililoleta hamasa kubwa kwa wananchi kupenda mijadala ya Bunge. Kama viongozi wa Bunge wataendelea kuikumbatia serikali kwa kuiruhusu itumie kanuni kuzima mijadala yenye maslahi mapana kijamii, Bunge litapoteza mvuto na maana katika jamii. Na ikifika hapo Bunge letu litasuswa sio tu na watazamaji/wasikilizaji ,lakini pia hata na wabunge wenyewe kama tulivyoshuhudia hivi karibuni. Tunamshauri Spika wa Bunge atumie kanuni za Bunge katika kufanikisha badala ya kukwamisha mijadala ya wabunge. Tunataka Bunge la Hoja na sio Bunge la Kanuni!

 
hivi huwezi kuandika kwa kifupi na ueleweke mpaka ujaze pumba nyingi? hao wanafunzi mnawaeleweshaje sasa?
 
hivi huwezi kuandika kwa kifupi na ueleweke mpaka ujaze pumba nyingi? hao wanafunzi mnawaeleweshaje sasa?

Hivi unajua kipi ni pumba na kipi siyo? jipi jema, kuandika kwa kirefu watu wakapata ujumbe husika au kuandika kwa kifupi bila kutoa majibu na ufafanuzi wa kile ulicho dhamiria kuwafikishia ujumbe?
Acha uvivu wa kusoma na kufikiri, nyie ndio watanzania tulionao siku hizi na matokeo yake bado tumezidi kukwama kwenye lindi la umaskini na fikra mbovu kama zako. Ili tuendelee inabidi kizazi kama chako kitoweke. Dr kaongea mambo ya msingi lakini mbumbumbu kama wewe bado umeshindwa kuchambua hizo pumba na kuziainisha hapa kwamba hiki na niki ni pumba.

Uvivu huleta umaskini na mwisho wa yote ni wivu kwa kuona wenye fikra za kimaendeleo wakitoa mchango wao kwenye jamii. Jana umelala na hangover nini? make walevi kama wewe ni wengei sana..kodi kwenye kinywaji ndio kiboko yenu.
 
Kama mwalimu uchambuzi wake ni dhaifu, umejaa hisia za kishabiki na propaganda za kuomba huruma.
Kama mwanasiasa amefanikiwa kuonesha picha halisi ya kinachoendelea bungeni, kukigeuza kwa manufaa yake kisiasa na kushambulia mpinzani wake. Inategemea unaitazama kwa jicho lipi.
 
hivi huwezi kuandika kwa kifupi na ueleweke mpaka ujaze pumba nyingi? hao wanafunzi mnawaeleweshaje sasa?

Hiyo ni makala iliyoandikwa gazetini na Dr.Kitila Mkumbo na mleta thread ni Kimbweta ambaye siyo mwalimu sasa kwanini unasema hao wanafunzi mnawaeleweshaje. Uwe makini unapochangia hoja ndugu yangu Technology.
 
Hivi unajua kipi ni pumba na kipi siyo? jipi jema, kuandika kwa kirefu watu wakapata ujumbe husika au kuandika kwa kifupi bila kutoa majibu na ufafanuzi wa kile ulicho dhamiria kuwafikishia ujumbe?
Acha uvivu wa kusoma na kufikiri, nyie ndio watanzania tulionao siku hizi na matokeo yake bado tumezidi kukwama kwenye lindi la umaskini na fikra mbovu kama zako. Ili tuendelee inabidi kizazi kama chako kitoweke. Dr kaongea mambo ya msingi lakini mbumbumbu kama wewe bado umeshindwa kuchambua hizo pumba na kuziainisha hapa kwamba hiki na niki ni pumba.

Uvivu huleta umaskini na mwisho wa yote ni wivu kwa kuona wenye fikra za kimaendeleo wakitoa mchango wao kwenye jamii. Jana umelala na hangover nini? make walevi kama wewe ni wengei sana..kodi kwenye kinywaji ndio kiboko yenu.

kuandika saaana haimaanishi mantiki, wako wabunge wanaongea saana hata zaidi yako lakini mwenyewe unashuhudia kinachotokea leo bungeni. kama wewe ni mwalimu
 
Hiyo ni makala iliyoandikwa gazetini na Dr.Kitila Mkumbo na mleta thread ni Kimbweta ambaye siyo mwalimu sasa kwanini unasema hao wanafunzi mnawaeleweshaje. Uwe makini unapochangia hoja ndugu yangu Technology.
Kwani Dr.Mkumbo sio Mwalimu? hawezi kaundika kwa kifupi??? umakini upi zaidi ya huo. au umakini kwako ni NSSF kutulipa jasho letu baada ya miaka 55?
 
hivi huwezi kuandika kwa kifupi na ueleweke mpaka ujaze pumba nyingi? hao wanafunzi mnawaeleweshaje sasa?

wewe una technology ya mafunzo ya mbwa, kwani mbwa haambiwi sentesi ndefu, (kama, kula, acha, lala n.k) na kwa mtazamo huo upo kitengo kimoja na "rama" kwenye kile kitengo wahusika hurandaranda magogoni kusubiri maelekezo ya jack zoka.
 
Dr. kitila nadhani kubeza kanuni si sahihi, masuala mengine umezungumza yana mashiko kiasi. Nadhani ngezungumzia Bunge kuwa la HOJA NA LENYE KUFUATA KANUNI, kama mtaaluma ningekupa Bigup.

Unaniacha hoi pale unapo refer kwenye magazeti, nilitegemea uzungumzie matokeo ya utafiti nadhani ingesaidia zaidi kuongeza makali ya hoja.
 
Hii ni makala iliyo andaliwa na Dr.Kitila Mkumbo(Jembe) kwenye gazeti la Raia Mwema, Toleo la 251, 25 July 2012.


KATIKA siku za hivi karibuni majadiliano katika Bunge letu yamepata ufuasi mkubwa kutoka kwa wananchi wanaofuatilia kupitia luninga na redio. Kuna Mwalimu mwenzetu mmoja Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambaye kwa muda sasa amekuwa akirudi nyumbani kila ifikapo saa nne asubuhi na saa kumi na moja, jioni kwenda kutazama kipindi cha Bunge. Imefika mahala anamshindwa kuacha kwenda kutazama majadiliano bungeni na anaporudi hutusimulia yaliyojiri kwa furaha na hamasa kubwa.

Hata hivyo, katika siku za karibuni ameacha kwenda kutazama Bunge kama ilivyo kawaida yake, kwa sababu anazodai kuwa Bunge letu limegeuka kuwa Bunge la Kanuni badala ya Bunge la Hoja ! Kwamba Bunge letu limekuwa likitumia muda mwingi kulumbana juu ya matumizi ya kanuni za Bunge, badala ya kujadiliana hoja zinazohusu maisha ya wananchi na taifa kwa ujumla. Na kuna wabunge ambao wameamua kubobea katika kutoa miongozo kiasi cha kupachikwa jina la ‘Mbunge wa Mwongozo' mitaani.

Kwa mujibu wa maoni ya wananchi yaliyochapishwa katika magazeti ya Jumapili iliyopita, ni wazi kwamba wananchi wengi wameanza kukosa hamasa na hamu ya kutazama majadiliano bungeni kama ilivyo kwa mwalimu mwenzangu niliyemtaja. Maoni ninayoyatoa katika makala haya yana lengo la kujaribu kuwakumbusha wabunge, na hasa viongozi wa Bunge, juu ya wajibu wao ili warudi katika mstari na kuwapa wananchi kile wanachokitarajia kutoka kwao.
Katika Jumuiya ya Madola, Bunge lina kazi kubwa nne za msingi. Kazi ya kwanza ni kujadili, kutathmini na kusimamia utendaji wa serikali. Kazi ya pili ni kujadili na kupitisha sheria mbalimbali. Kazi ya tatu ni kuiwezesha serikali kupandisha kodi kupitia bajeti za kila mwaka. Kazi ya nne ni kujadili na kutoa mwelekeo juu ya jambo lolote zito lililotokea katika nchi ambalo linaweza kuchukuliwa kama dharura.

Ukiwa mfuatiliaji wa Bunge letu utakubaliana nami kwamba Bunge letu limefanya kazi nzuri sana katika maeneo mawili, ambayo ni kupitisha sheria na kuiwezesha serikali kupandisha kodi mbalimbali kupitia bajeti za kila mwaka. Kwa maoni yangu, Bunge letu halijafanya kazi yake sawa sawa katika kujadili, kutathmini na kusimamia utendaji wa serikali. Hata lugha ambazo wabunge wetu wanazitumia bungeni ni kielelezo cha kutosha juu ya wao kupwaya katika kuelewa au kuzingatia uzito wa mamlaka yao dhidi ya serikali ambayo yapo wazi kikatiba. Kwa mfano, wabunge wengi wanapowasilisha maoni au mahitaji yao kuhusu jambo fulani wana tabia ya kusema kwamba ‘ninaiomba au ‘ninaishauri' serikali. Sasa hata kama mimi nilikuwa ndiye serikali ukishaniambia ‘unaomba' au ‘unanishauri' ni wazi kwamba nina hiari ya kukubali au kukataa ombi au ushauri wako. Serikali ina washauri chungu nzima ambao wameajiriwa kwa ajili hiyo wakifanya utafiti na uchambuzi kwa ajili ya kuishauri serikali kitaalamu, ambao ni muhimu zaidi kuliko ushauri wa mbunge unaotolewa katika dakika 10 anaposimama bungeni.

Kwa sababu wabunge wetu wamekaa kiushauri zaidi kuliko kiuwajibikaji, wamefika mahala hawawezi kujadili jambo lolote zito hadi serikali ikubali kushauriwa. Na ni bahati mbaya kwamba viongozi wa Bunge wanaisikiliza serikali zaidi kuliko wanavyowasikiliza wabunge. Na serikali nao wamebuni mtindo unaowasaidia kukwepesha mijadala mizito kwa kutumia kanuni. Kwa hivyo serikali, badala ya kujiandaa kujibu hoja, inajiandaa kwa kutafuta kanuni ya kukwamisha mjadala ! Matokeo yake ni kwamba Bunge letu lipo ‘busy' kulumbana juu ya kanuni badala ya kulumbana juu ya hoja, na hatimaye upande wa serikali hushinda-kwa kukwamisha mjadala. Ndivyo ambavyo mijadala mizito kama ya utekwaji wa Dk. Steven Ulimboka na kuzama kwa meli ya MV Skagit ilivyozimwa. Kwa kutumia kanuni za Bunge, viongozi wa Bunge wametukosesha fursa muhimu na adimu ya kujua kilichomkumba Dk. Ulimboka na sababu hasa za matukio yanayofuatana ya kuzama kwa meli huko Zanzibar. Bunge letu limeingia katika historia isiyotukuka kwa kukubali kukatazwa kutekeleza kujadili mambo mazito katika jamii.

Ni muhimu viongozi wa Bunge wakazingatia kwamba watazamaji na wasikilizaji wa vipindi vya Bunge hawapo kwa ajili ya kushuhudia umahiri wa kuzijua kanuni za Bunge. Wana hamu na hamasa ya kutazama na kusikiliza jinsi ambavyo wabunge wao wanaibua hoja zinazohusu maisha yao na nchi yao. Na hili ndilo lililoleta hamasa kubwa kwa wananchi kupenda mijadala ya Bunge. Kama viongozi wa Bunge wataendelea kuikumbatia serikali kwa kuiruhusu itumie kanuni kuzima mijadala yenye maslahi mapana kijamii, Bunge litapoteza mvuto na maana katika jamii. Na ikifika hapo Bunge letu litasuswa sio tu na watazamaji/wasikilizaji ,lakini pia hata na wabunge wenyewe kama tulivyoshuhudia hivi karibuni. Tunamshauri Spika wa Bunge atumie kanuni za Bunge katika kufanikisha badala ya kukwamisha mijadala ya wabunge. Tunataka Bunge la Hoja na sio Bunge la Kanuni!


Niliwahi kutoa tahadhari juu ya mwenendo wa bunge letu na haliya kukosa meno kiasi cha kushindwa kufanya kazi yake barabara katika kuisimamia serikali,nilifika mbali zaidei kwa kutaka kama inawezekana tulivunje bunge na kufanya uchaguzi ambao utawapeleka wabunge makini wenye kuweza kujua majukumu yao ya kibunge.

Naweza kusema bunge limehongwa na serikali ndiyo maana serikali imekuwa juu ya bunge na wabunge wameamua kuisadia serikali kujibu hoja kali za baadhi ya wabunge ambao wamekosa mshikamano toka kwa wabunge wenzao.Ndo maana nimeiunga hoja yako mkono tena umeileta wakati muafaka.

Nasisitiza kuna rushwa ya mazingira kati ya bunge na serikali ndo maana hata wabunge wetu wameona upuuzi wameaamua kula mlungula na kuingiza nchi kwenye giza pasi na sababu za msingi
 
Nakubaliana na mtoa hoja 100%. kwangu mimi wanaoliharibu bunge ni spika na wenyeviti wake kwa kuendesha bunge kwa matakwa ya serikali.Ndio maana hoja yoyote ambayo serikali haitaki ihojiwe bungeni spika et al hawawezi kuruhusu ihojiwe hata kama mbunge atatumia kanuni kwa usahihi wote. mfano, kanuni alivyoitumia Tundu Lisu kutaka uwepo mjadala kwa tukio la kuzama mv skagit na namna jobu ndugai alivyozuia, mpaka unaona aibu jinsi wanavyotumiwa vibaya na serikali.
Kwa suala la DR Ulimboka, serikali ikamtafuta mkenya feki haraka-haraka ikampeleka mahakani ili bunge lifyate mkia, na kweli ikawa hivyo, basi serikali inaendelea na uovu wake bila wasiwasi, huku ikiwa na uhakika wa utetezi wa spika na wenyeviti wake. Kwangu mimi spika et al ni janga la taifa
 
Hivi unajua kipi ni pumba na kipi siyo? jipi jema, kuandika kwa kirefu watu wakapata ujumbe husika au kuandika kwa kifupi bila kutoa majibu na ufafanuzi wa kile ulicho dhamiria kuwafikishia ujumbe?
Acha uvivu wa kusoma na kufikiri, nyie ndio watanzania tulionao siku hizi na matokeo yake bado tumezidi kukwama kwenye lindi la umaskini na fikra mbovu kama zako. Ili tuendelee inabidi kizazi kama chako kitoweke. Dr kaongea mambo ya msingi lakini mbumbumbu kama wewe bado umeshindwa kuchambua hizo pumba na kuziainisha hapa kwamba hiki na niki ni pumba.

Uvivu huleta umaskini na mwisho wa yote ni wivu kwa kuona wenye fikra za kimaendeleo wakitoa mchango wao kwenye jamii. Jana umelala na hangover nini? make walevi kama wewe ni wengei sana..kodi kwenye kinywaji ndio kiboko yenu.
Mkuu umenena. Kizazi hiki ni cha "Multiple choice" kwenye mitihani yao. Mambo ya "discuss", "compare", "define" hayapo tena kwenye syllabus zao!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom