Sitachoka
JF-Expert Member
- Nov 17, 2011
- 3,030
- 1,303
Rushwa, ubadhrifu, wizi na
udokozi wa mali za umma
unaendelea kwa kasi, ari na
nguvu mpya nchini Tanzania.
Wakati mwakyembe
akishanga twiga, pamoja na
urefu wake, kupakiwa
kwenye ndege, huko
bandarini makontena
yanayeyuka kama barafu -
mafisadi wanatia makontena
mifukoni kama vile mwizi
anavyoficha kiberiti mfukoni!
Rais kikwete anashangaa
matumizi makubwa ya
rushwa ktk chaguzi za ndani
za CCM.
Anashangaa tu bila
kuchukua hatua za
kukomesha tatizo hilo. Katika
uchaguzi mkuu uliopita,
rushwa ilikuwa ikitolewa
hadharani bila kificho.
Takukuru hawajawahi
kumkamata hata mtu mmoja.
Wamekuwa wakiwaita
watuhumiwa, wanakaa
mezani wanamalizana na
biashara inaishia hapo.
Matokeo yake, wafanyakazi
wa Takukuru wanafukuzana
na wale wa TRA kwa utajiri.
Kumbe wapo pale kibiashara
zaidi kuliko kikazi.
Kiasha cha Tsh. 32 bilion
zimechotwa kutoka hazina na
kuliwa na wajanja.
Walipoulizwa zile pesa ziko
wapi, wakadai wamezipeleka
Tume ya Ushirika, ambayo
haipo kiuhalisia wala kisheria.
Sisi wananchi yetu macho.
Tunasubiri kufanya maamuzi
sahihi ktk uchaguzi mkuu wa
mwaka 2015.
udokozi wa mali za umma
unaendelea kwa kasi, ari na
nguvu mpya nchini Tanzania.
Wakati mwakyembe
akishanga twiga, pamoja na
urefu wake, kupakiwa
kwenye ndege, huko
bandarini makontena
yanayeyuka kama barafu -
mafisadi wanatia makontena
mifukoni kama vile mwizi
anavyoficha kiberiti mfukoni!
Rais kikwete anashangaa
matumizi makubwa ya
rushwa ktk chaguzi za ndani
za CCM.
Anashangaa tu bila
kuchukua hatua za
kukomesha tatizo hilo. Katika
uchaguzi mkuu uliopita,
rushwa ilikuwa ikitolewa
hadharani bila kificho.
Takukuru hawajawahi
kumkamata hata mtu mmoja.
Wamekuwa wakiwaita
watuhumiwa, wanakaa
mezani wanamalizana na
biashara inaishia hapo.
Matokeo yake, wafanyakazi
wa Takukuru wanafukuzana
na wale wa TRA kwa utajiri.
Kumbe wapo pale kibiashara
zaidi kuliko kikazi.
Kiasha cha Tsh. 32 bilion
zimechotwa kutoka hazina na
kuliwa na wajanja.
Walipoulizwa zile pesa ziko
wapi, wakadai wamezipeleka
Tume ya Ushirika, ambayo
haipo kiuhalisia wala kisheria.
Sisi wananchi yetu macho.
Tunasubiri kufanya maamuzi
sahihi ktk uchaguzi mkuu wa
mwaka 2015.