Viongozi Madikteta Wa Africa Mwisho Ndio Huu

Ndallo

JF-Expert Member
Oct 1, 2010
7,619
4,292
Sasa ndio ule mwisho wa viongozi madikteta Africa kuondoka madarakani kwa aibu umeshawadia, nimeshaamini kila chenye mwanzo hakikosi kuwa na mwisho na huu ndio mwisho wa wale viongozi wanaopenda kutawala milele hakika sasa tunaanza kuyaona na mfano hai ni huu wa Raisi wa Tunisia kukimbilia nchi za Kiarabu tena kaondoka kwa nguvu ya walala hoi bila kujali mitutu wala mabomu, kinachofuata ni Hosni Mubarak naye kuondolewa kwa aibu japokua kavunja baraza lake na kuunda jingine lakini wananchi wameshasema toka na uende zako hatukutaki, na naamini kwa nguvu ya wananchi ataondoka tu, baada ya hapo kitachofuata ni Bagbo naye kuondolewa kibabe, halafu nahisi kuna nchi nyingine zinasubiri zoezi hili liishe nao wataandamana tusishangae hata hapa kwetu endapo serikali ya CCM na utawala wake wakibabe kwa kumtumia Yusuf Makamba pamoja na kuidhinisha malipo ya bilioni 94 kwa Dowans hakika TZ nao moto utawaka! Hizi ni fikra zangu tu, Africa kumekucha hakuna tena wakuonewa na hii inatia hasira kwa kuona walionacho ni asilimia 80 na wasionacho ni asilimia 20 kwakweli haikubaliki.:sad:
 
Ndallo...haka kamsemo kana nguvu sana Mkuu!!

'' Mtu ni Utu sio Kitu'' :yo:

Na niliwahi kusikia kuwa ..mtu ni afya ...

Na utu una nguvu ya kuzima hata bomu la nuklia..una nguvu ..na ccm lazima kujua hilo..

Na Utanzania ni Utu!

Ikitokea tukaunganisha Utanzania wetu ..na kusonga mbele.. hakuna wa kutuzuia kurudisha Utu wa Taifa letu!

CCM... mna utu???
 
Back
Top Bottom