Viongozi Chadema - must read

Absolutely Candid scope,

actually kuna mahali nimesema hivi..

I Expected BAVICHA cadres and organs to organize more activities with more appeal to young citizens, and strengthen the youth council's construction to increase the council's influence among Tanzanian's youth.Petty squables are not healthy.

Tarehe 28/5/2012(jumatatu ijayo) Baraza la vijana Chadema Taifa linamaliza mwaka mmoja tangu lichaguliwe.

Nategemea wiki hiii itakuwa ni wiki maalumu kwao katika kujitathmini kwamba ndani ya Mwaka mmoja BAVICHA imefanya nini.

Nilikuwa miongoni mwa watu wa kwanza kabisa kutoa tahadhari.JF haikuwa Hewani lakini waliokuwa wanachama wa JF facebook tulijadili.Nilisema Shibuda hastahili kujibiwa.Anastahili kuachwa tu bila kujibizana nae kwenye media kwani huo ndiyo mchezo anaoutaka.Anataka kupandishwa chati kisiasa(najua kamanda shibuda ni member wa hapa JF unachungulia humu).Ulichungulia humu hata nilipokuwa nakutolea mfano kuhusu mtizamo wangu na cross-carpeting za wanasiasa kutoka chhama kimoja kwenda kingine.Nilisema bila darasa la Itikadi hapa itakuwa kazi kweli kweli.Itabidi kuwe na timua timua za ovyo kwenye vyama vya siasa.

Akiwa CCM alitangaza kugombea Urais kupambana na Jk mwaka 2010.Hakuna mwana-CCM makini aliyemjibu isipokuwa Mzee Makamba aliyeapa kwamba yupo radhi kwenda Jela kuliko kuruhusu upinzani dhidi ya JK,2010.mnalijua hilo,linajulikana

The best way to deal with comrade Shibuda is to ignore him.

Makosa yanafanyika pamoja na kwamba ni demokrasia lakini utani mwingine ni gharama kweli kweli.Huwezi kutangaza kugombea Urais Chadema halafu ukataka meneja kampeni wako awe mwenyekiti wa CCM halafu tukuchukulie mtu serious.Haya ni makusudi kwa kuwa Shibuda ni mzoefu wa michezo ya kisiasa na anajua analenga nini.

Hata mimi ningekuwa mwenyekiti wa vijana nisingevumilia kuona hili.

Sasa naamini hili suala litatauliwa kwa busara.Makamu Mwenyekiti Juliana Shonza ni kiongozi makini na shupavu kweli kweli.Ni kiongozi hodari.ni kiongozi adimu ambaye hawezi kupatikana kwingine isipokuwa ndani ya chadema tu.Anapenda kusema kile anachoamini.Nilipogombea uenyemkiti wa vijana huyu ndiye alikuwa chaguo langu.Aliniunga mkono na nilimuunga mkono.Sijawahi kutilia mashaka uwezo wake wa kuongoza.Kama kuna tatizo la flow of information nadhani tatizo hili litamalizika ndani ya vikao vya chama tu.It's not a big deal at all

Laiti tungekuwa na muundo kama wa ANC-YL ya Afrika Kusini basi leo tungekuwa na msemaji wa kama alivyo comrade floyd shivambu wa ANCYL.Mabaraza yote na jumuiya zote za vijana ndani ya vyama vya siasa Tanzania hatuwa na muundo kama huo kitu ambacho kinaweza kutoa mwanya kwa vijana kujikanganya au kuburuzana katika uendeshaji wa shughuli za kila siku kisaiasa na pengine hata maadui wa demokrasia kutumia mwanya huo kuleta mvurugano.

Naamini Baraza la vijana,litamaliza tatizo hili.Tusiwe na papara za kuhukumu watu.Tuwe na subira,tusikurupuke.Diplomasia na Busara inahitaji kutumika hapa.This is the right time to show leadership.

Malumbano ya watu binafsi yasiharibu taasisi.Shutuma kwamba Baraza la vijana ni wahuni hazivumiliki
Lakini huyu mwana mama nae mwambieni atulize mapepo yake. Kama aliona mwenyekiti amepotoka kwanini yeye azidi kuleta matatizo? Nae ni kicheche tu. Ni kundi moja na wewe na Zitto.
 
Wanajifunza uongozi, muda uliobakia unatosha kabisa kabla ya uchaguzi 2015. Isipokuwa huyo Heche kwa kweli alikurupuka nadhani alikuwa na kinyongo na Shibuda akasahau kufikiri kwanza kabla ya kutoa tamko. Kwa hiyo ajifunze kwamba uongozi hauendi kwa chuki na kuviziana kwenye kona

Mkuu umeongea kitu cha afya sana kama sijakosea HENCHE na SHIBUDA walishashikana mashati siku moja
 
Huyu ni mchumba wa nani kati ya viongozi wa CHADEMA?
0000001anajulia.jpg


Anaonesha ni wa kanda ileile!
 
Absolutely Candid scope,

actually kuna mahali nimesema hivi..

I Expected BAVICHA cadres and organs to organize more activities with more appeal to young citizens, and strengthen the youth council's construction to increase the council's influence among Tanzanian's youth.Petty squables are not healthy.

Tarehe 28/5/2012(jumatatu ijayo) Baraza la vijana Chadema Taifa linamaliza mwaka mmoja tangu lichaguliwe.

Nategemea wiki hiii itakuwa ni wiki maalumu kwao katika kujitathmini kwamba ndani ya Mwaka mmoja BAVICHA imefanya nini.

Nilikuwa miongoni mwa watu wa kwanza kabisa kutoa tahadhari.JF haikuwa Hewani lakini waliokuwa wanachama wa JF facebook tulijadili.Nilisema Shibuda hastahili kujibiwa.Anastahili kuachwa tu bila kujibizana nae kwenye media kwani huo ndiyo mchezo anaoutaka.Anataka kupandishwa chati kisiasa(najua kamanda shibuda ni member wa hapa JF unachungulia humu).Ulichungulia humu hata nilipokuwa nakutolea mfano kuhusu mtizamo wangu na cross-carpeting za wanasiasa kutoka chhama kimoja kwenda kingine.Nilisema bila darasa la Itikadi hapa itakuwa kazi kweli kweli.Itabidi kuwe na timua timua za ovyo kwenye vyama vya siasa.

Akiwa CCM alitangaza kugombea Urais kupambana na Jk mwaka 2010.Hakuna mwana-CCM makini aliyemjibu isipokuwa Mzee Makamba aliyeapa kwamba yupo radhi kwenda Jela kuliko kuruhusu upinzani dhidi ya JK,2010.mnalijua hilo,linajulikana

The best way to deal with comrade Shibuda is to ignore him.

Makosa yanafanyika pamoja na kwamba ni demokrasia lakini utani mwingine ni gharama kweli kweli.Huwezi kutangaza kugombea Urais Chadema halafu ukataka meneja kampeni wako awe mwenyekiti wa CCM halafu tukuchukulie mtu serious.Haya ni makusudi kwa kuwa Shibuda ni mzoefu wa michezo ya kisiasa na anajua analenga nini.

Hata mimi ningekuwa mwenyekiti wa vijana nisingevumilia kuona hili.

Sasa naamini hili suala litatauliwa kwa busara.Makamu Mwenyekiti Juliana Shonza ni kiongozi makini na shupavu kweli kweli.Ni kiongozi hodari.ni kiongozi adimu ambaye hawezi kupatikana kwingine isipokuwa ndani ya chadema tu.Anapenda kusema kile anachoamini.Nilipogombea uenyemkiti wa vijana huyu ndiye alikuwa chaguo langu.Aliniunga mkono na nilimuunga mkono.Sijawahi kutilia mashaka uwezo wake wa kuongoza.Kama kuna tatizo la flow of information nadhani tatizo hili litamalizika ndani ya vikao vya chama tu.It's not a big deal at all

Laiti tungekuwa na muundo kama wa ANC-YL ya Afrika Kusini basi leo tungekuwa na msemaji wa kama alivyo comrade floyd shivambu wa ANCYL.Mabaraza yote na jumuiya zote za vijana ndani ya vyama vya siasa Tanzania hatuwa na muundo kama huo kitu ambacho kinaweza kutoa mwanya kwa vijana kujikanganya au kuburuzana katika uendeshaji wa shughuli za kila siku kisaiasa na pengine hata maadui wa demokrasia kutumia mwanya huo kuleta mvurugano.

Naamini Baraza la vijana,litamaliza tatizo hili.Tusiwe na papara za kuhukumu watu.Tuwe na subira,tusikurupuke.Diplomasia na Busara inahitaji kutumika hapa.This is the right time to show leadership.

Malumbano ya watu binafsi yasiharibu taasisi.Shutuma kwamba Baraza la vijana ni wahuni hazivumiliki

kwahiyo hata hapa bado mwaungana mikono......! nadhani bado kuungana mwili...! umeshajipambanua wazi kuwa HECHE alikubwaga mlipogombea uenyekiti. sasa utamsifia kwa lipi tena....weye siulisema waenda jimboni rombo kucompete na selasini ubunge? huyo bibie ndo meneja campaign wako ee...kaza buti kijana..!
 
Kumbe kuna kundi la Zitto ndani ya CDM? Wana JF wametufumbua akili pale wanaposema huyu dada pamoja na mgombea wa uenyekiti liyeshindwa kuwa wako kundi la zitto hivyo wasubiri CDM itawashughulikia.Nimefurahi sana kujua hilo maana watanzania tunazidi kukifahamu vyema chama chenu CDM kuwa ni cha kikanda na kimejaa ukabila mwanzo mwisho.Mbowe-WA KASKAZINI,SLAA-WA KASKAZINI NA MNYIKA -WA KASKAZINI ndio maana zitto anapigwa zengwe sana ni bola shibuda nae kaingia.Kama ni hivyo CCM tawala milele.

CCM JANA-CCM LEO -CCM KESHO.
 
Leadership is a process... CDM will have to go through it... and this is the time.... Kuongoza Chama ni tofauti na Serikali... in government you can command etc... but not in political party... tuwape muda vijana wajifunze....
 
Lakini huyu mwana mama nae mwambieni atulize mapepo yake. Kama aliona mwenyekiti amepotoka kwanini yeye azidi kuleta matatizo? Nae ni kicheche tu. Ni kundi moja na wewe na Zitto.

zitto kafata nn hapo? Acheni kuweweseka,tafuteni njia sahh ya kutatua migogoro sio kukimbila kumtaja Zitto,kama Zitto anauwezo wa kumkosoa kubwa jinga Mtei itakuwa huyo Heche mpaka amtumie huyo dada? Zittoni next level usimfananishe na hizo takataka za Bavicha!
 
Kukiri makosa ni jambo jema sana na huwa linaonyesha ukomavu wa muhusika katika kukabiliana na matatizo ama changamoto za kuelekea kwenye maendeleo.Chadema kipo kwenye hatua muhimu sana ya mpito hivyo ni vyema wanachama na wafuasi wakajumiaka pamoja katika kusukuma gurudumu sio bora liende bali safari inakuwa ni salama na yenye mafanikio.

Binadamu anatabia ya kuona makosa ya upande wa pili bila kufanya tathmini ya uhalisia wa jambo.Uhalisia wa jambo hupewa nguvu kama kuna uthubutu wa kuvaa uhusika kwa lengo la kujipima kama ingekuwa mimi ningetoa maamuzi gani, wakati gani na kwa hadhira ipi? Pia tukumbuke kuwa katika kipindi cha mpito kunakuwa na mambo mengi ambayo kimsingi yanatakiwa yawe yanafanyiwa marekebisho hususani mfumo wa utoaji maamuzi unaotekelezwa (Hili Comrade Ben ameeleza kiundani kidogo).

Kama wazalendo tuwe na mawazo chanya kwa vijana wenzetu na tufuate njia sahihi za kukosoana pale tunapokosea sio kuanza kutoa mifano kuwa mbona tunakosoa wengine wanapokosea!. Hao wanaokosolewa kwa nguvu zote ni kuwa wanaharibu, kwani kukosea ni utamaduni kwao na wameshaona wananufaika na kuendelea kwao kufanya makosa.
 
kwa hakika Shibuda ni gwiji katika siasa, tamko la utani linawafanya CDM kuweweseka. Sasa wafumua agenda zao za siri na dhambi ya ukanda, udini, ukabila yawsumbua
 
hawa vijana wanatakiwa kuiga mfano wa uongozi wa juu wa chama, hatupendi kusikia malumbano na hayatu saidii hata kidogo! huyu dada alikosea kutoa tamko kama alivyo fanya heche,akutakiwa kurudia makosa ya mwenzake,alitakiwa kutulia na kwenda kulijadili hili jambo! nashindwa kuelewa alifanya vile kutatua tatizo au kuongeza tatizo? kwa sababu ame onesha tofauti yake na mwenyekiti! sikupenda jambo hilo! ndug heche na makamo mwenye kiti kaeni mzungumze siyo kukimbilia kwenye media!
 
Ningekuwa kiongozi wao - Makamu Mwenyekiti angetakiwa kuissue an unqualified public apology. Akikataa ajiuzulu. You have to be very swift and precise. Haya ya kuchekeana ndio matatizo ambayo yatakuja kugeuka baadaye na ambayo yanagharimu CCM tayari.
 
Mara nyingi sana nimekuwa nikilieleza hili jambo na inaonekana ima sioni nahitaji taa au Chadema hawaoni na wanahitaji taa.
Uongozi wa CDM kitaifa bado haujakamilika kiungozi. Kuna viongozi wenye uwezo lakini hilo halitoshi kuwa na uongozi thabiti.Nimewahi sema kuna tatizo katika ngazi ya kitaifa kiuongozi na narudia tena tatizo lipo.

Komredi Ben ameeleza vizuri sana hoja yangu. Ninapotofautiana naye ni pale anaposema uongozi wa vijana hauna msemaji. Hilo tu linashadidia hoja yangu ya kila siku kuwa CDM lazima iwe taasisi iliyokamilika ikiwa na idara na si 'personalities'
Sikutegemea kuwa BAVICHA hawana msemaji na sijui structure yao ya uongozi iko vipi!!

Laiti uongozi wa taifa ungekuwa makini hii 'damage' inayotokea isingefikia hapa. Na labda niseme uongozi umeiga 'template ya CCM' ya kuoneana haya.

Ukiachilia mbali tafrani za siku za nyuma kuhusu Shibuda, na pia ukiachilia mbali malumbano kati ya Heche,Shibuda, Naibu wake na sasa viongozi wa BAVICHA pwani, kuna jambo CDM hawataki kuliona kwa uhatari wake. Kauli ya Shibuda kuwa anahujumiwa kwa usukuma wake inatoa 'reservation' yake juu ya chama. Tuhuma za ukabila na ukanda hazifai kufumbiwa macho hata kwa bahati mbaya. Uongozi wa taifa umeamua 'kumhifadhi' kama CCM ilivyowahifadhi wahalifu wake.

Tatizo linazidi kuwa kubwa pale malumbano yanapoanza ndani ya Chama. Ni wazi Heche na Naibu wake sasa hawaivi hata kama watu hawakubali hadharani. Sina tatizo na kauli zilizotolewa, tatizo nilionalo ni kuwa kuna watu wamemtuma naibu akanushe habari za Mwenyekiti wake. Iwe ni viongozi au kundi bado hilo ni tatizo. Inaonyesha kuna ' hidden power struggle within the party'. Sasa kila kundi linatoka na msimamo wake(mkoa wa pwani wameanza).

Hadi hapo uongozi wa taifa hauoni kuna 'damage' na control ni ya lazima.Hivi utaratibu wa kiungozi unaruhusu Naibu akanushe maelezo ya Mwenyekiti wake hadharani? kuna team work hapo kweli.
Kama ilibidi basi msemaji wa chama angeingilia kati na pengine kuyamaliza haya mambo katika vikao vya ndani.

Hon Mbowe, Dr Slaa et alia as members of this forum my message is, people embrace Chadema en masse across the country north to south, east to west. This is the rare opportunity the party need to seize. Unnecessary distractions derail the mission and defeat the whole purpose. Mutatis mutandis is inevitable at this moment, don't wait to be asked 'who let the dog out'
 
Nguruvi; umesema vizuri sana lakini huyu dada kadokeza kitu kimoja ambacho sidhani kama watu wamekifikiria na ambacho umekisema pia kuwa ni kufuata template ya CCM. Huyu dada alisema maneno ya Heche (mwenyekiti wa taifa) siyo ya Bavicha kwa sababu hakuna "kikao" kilichokaa na kuamua hivyo. Naita hili uongozi wa "vikao" kwamba hakuna lolote linaloweza kufanywa na viongozi au kutendwa bila vikao. Sasa hili ni zuri kwenye kupitisha sera n.k lakini linapokuja suala la kutenda wale waliopewa madaraka ya kutenda ni lazima watende.

Sijui Katiba ya BAVICHA inasema nini kuhusu madaraka ya viongoziwake lakini tunatarajia kuwa kiongozi anapokuwa kiongozi ana madaraka yote ya kiongozi. Kauli ya Heche ilipotolewa ilitakiwa kutetewa na viongozi wengine wote kwa sababu yeye ndiye kiongozi mkuu wa Bavicha na inawezekana ndiye "msemaji mkuu" wa Bavicha kwa mujibu wa katiba yao. Huyu makamu hana madaraka wala uwezo wa kusimama na kusema "ile" siyo kauli ya bavicha!

Lakini tatizo ninalolizungumzia ni hili la 'vikao'. Kwamba, watu wenye madaraka kamili wanashindwa kusema au ufanya jambo lililo ndani ya uwezo wao bila vikao. Hivi, ina maana kila wakati jambo linatokea baraza lazima liitwe liulizwe litoe kauli yake? sasa kuna maana gani ya kuwa na Mwenyekiti? Mbona ni kana kwamba dhana ya madaraka (authority) haijaeleweka? Kama kauli ya Heche ambaye ndiye kiongozi mkuu wa vijana wa CDM haina nguvu yenyewe hadi ipepewe na kufukizwa udi na kikao kuna maana gani ya kuwa na Mwenyekiti? si kamati tu iwe inaongoza na kila jambo lifanywe na kamati hiyo?

Ndio maana naamini ningekuwa na uwezo huyu binti angeomba msamaha kwanza kwa kuingilia mambo yasiyo yake na akikataa anaambiwa ajiuzulu - bila kujali watu watasema nini. Somebody in CDM needs to show leadership. Shibuda anawajaribu na sasa huyu naye mwisho 2015 itafika na tutarudi exactly at status quo ya 2010!
 
Mwanakijiji na Nguruvi mmetoa point nzuri. Mwenyekiti Heche alitoa kauli kutokana na kinga yake ya kikatiba akiwa na kofia ya uenyekiti ikiwa ni kinga yenye uzito stahiki. Kosa lake kutohusisha wachini yake kupata maoni yao. Kilichomsukuma Heche kutoa tamko hili si tamko la Shibuda kugombea urais, bali mazingira aliyotolea kauli na kwamba memeja wake awe Kikwete. Ukichukulia kauli hiyo ni ya utani wa kisiasa, na sasa baada ya kumpa kichwa Shibuda amegeukia upande wa Slaa kuwa awe meneja wake wakati wa kampeni za kuwania urais. Huku ni kuchezea akili na wenye akili zaidi wanampuuzi kwa kutomjibu Shibuda.

Makamu mwenyekiti hana ubavu wa kuitisha vyombo vya habari na kutolea kauli ile, kwani yuko chini ya mwenyekiti wake kiutendaji. Amevuka mipaka vinginevyo anatakiwa afanye hivyo kwa agizo la Mwenyekiti wake. Jambo la kujiuliza nani alimpa msukumo wa kutolea tamko hili Makamu mwenyekiti dhidi ya Mwenyekiti wake? Je ni dalili kuna mpasuko au mgongano katika ofisi yao? Nyuma ya pazia kuna kitu ambacho kinatakiwa kufanyiwa kazi.

Vijana huwa na moto moto kama Mbowe alivyosema kule Arusha hivi karibuni kwamba vijana hulipuka haraka kama moto wa gas. Baadaye tunaweza kushuhudia madhara yake tu ni kwa vile hatuchukui tahadhari ya dalili za awali kama hizi tusipozifanyia kazi. Ndio maana huhitajika uvumilivu fulani vijana kuchangamana na wakubwa, kwani vijana hutaka njia ya mkato wakati wazee huwa na ustahimilivu kwa kuona faida ya mbele zaidi.

Busara ya kawaida viongozi wa BAVICHA kuwa na mawasiliano na viongozi wa Chama kitaifa. Katika safu ya viongozi wa kitaifa tunao vijana wengi tu kama akina Zito Kabwe, Mnyika, nk ambao wana upeo wa kuwasaidia kimawazo kwa busara zao ili kujaribu kufikiria kwanza kabla ya kutoa matamko hayo. Mapokeo yetu vijana huwa tunaomba ushauri kwa wazee kwani tunaamini busara yao inayotokana na kuishi kwingi kwa kuona mengi itasaidia kutupa upeo zaidi. Tukumbuke vijana damu inachemka haraka kama wale wenye vijimelea vya asili vya tabia ya sanguiniki.

Huyu dada ametifua zaidi kwa tamko lake, na kama kuna walio nyuma yake kumsukuma afanye hivyo wamefikiria masilahi binafsi kushindana na mwenyekiti wao bila kuangalia manufaa ya umoja wao na chama chao. Kukosekana kwa busara makamu mwenyekiti ndiko kunaweza kutoa picha mbaya zaidi kwa kuweka bayana kwamba anaenda kinyume cha mwenyekiti wake, na akadai zaidi kwamba hakuombwa ushauri. Angeonyesha busara zaidi kama angemfuata mwenyekiti wake kuongea kwa pamoja na huenda angeweza kusitisha kuitisha kikao cha vyombo vya habari kutolea tamko linalokinzana na tamko la Mwenyekiti wake.

Tamko la Mwenyekiti wake linaungwa mkono na matamko kadhaa yaliyotolewa na wenyeviti wa mikoa kadhaa, ni bayana Makamu mwenyekiti amekurupuka kutoa tamko, na anatakiwa kumwomba radhi mwenyekiti wake kwa kwenda kinyume cha maadili ya kiofisi. Hili ni jambo la kawaida kwa wakomavu wa kisiasa na wala si kujishusha kama wengi wa vijana wanavyofikiria.

Kwa siku za mbele matamko kama hayo yasifanywe kwa papara bila kutuliza nerves na kupata ushauri kutoka kwa viongozi wengine katika kada yao ili kujiridhisha na tamko ambalo haliwezi kukinzana katika ofisi yao. Kama wengi wanavyodokeza kwamba kudharau mtu anayeonekana kuropoka ovyo ovyo kama Shibuda ndiyo silaha pekee, la sivyo ni kumpa kichwa.
 
Mkuu MM, umenikumbusha kitu zaidi. Huyu Dada amesema maneno ya Heche si ya BAVICHA kwasababu hakuna kikao kilichofanyika kutoa kauli hizo. Sijui kama kuna kikao cha BAVICHA kilichokaa ili kutoa kauli ya kuji-dissociate na kauli za Heche kama alivyokanusha Dada yetu. Ndiyo maana nakaandika kuwa huenda ametumwa na sehemu ya uongozi au kundi ndani ya CDM. Je, kama kilikuwepo kikao, ni nani alikuwa mwenyekiti hadi Naibu wa mwenyekiti atoke na kauli ya kumdhalilisha mwenyekiti?

Ukitazama kauli ya Heche kama mwenyekiti haikuwa na maudhui au muundo wa kashfa. Alichokifanya Heche kisiasa kinakubalika'rebut' baada ya chama kudhalilishwa siyo kwa hoja ya kugombea bali hoja za udhaifu wa upinzani Shibuda akiwa mpinzani. Hata bila kauli ya Heche bado wanachama, manazi na mashabiki wa CDM walikereka.

Kauli ya Heche ilipaswa kutetewa kama ulivyonena kwa vile ni kauli ya mwenyekiti iliyolenga kulinda masilahi ya chama isiyo na matusi,kashfa bali majibu. Nimeandika (Duru za siasa) kuwa vyama lazima viwe na 'pundits' kutetea chama katika nyakati kama hizi na athari zake ndizo hizi. Mwenyekiti anaachwa nyikani mwenyewe

Ukisoma bandiko langu la mwisho katika safu ya (Duru za siasa) mara tu baada ya kauli ya Shibuda kumjibu Heche, niliweka wazi kabisa kuwa silaha anayotaka kuitumia Shibuda ni kumwandama Mwenyekiti Heche ili ugomvi uonekane ni kati yake na Heche na siyo CDM kwa minajili ya kujilinda na matokeo anayojua yatamsibu

Nilitahadharisha CDM juu ya hilo kwa bahati mbaya ushauri ukapuuziwa. Leo Shibuda ameibuka Kanda ya ziwa akiwa hana madai ya usukuma wake na kujikosha kuwa hana ugomvi na Chadema bali Heche. Hii imeshadidiwa na kauli ya Naibu BAVICHA mwanadada aliyekitenga chama na kumwacha Heche nyikani kana kwamba alikuwa anatetea familia binafsi.
Chadema wameingia katika mtego wa Shibuda hata pale tulipowapa majibu ya mtihani.

Lakini pia tujiulize kama huyu dada amedai kuwa kauli zile za Heche si za CDM, je ni kauli gani anazodhani Heche amevuka mipaka na nini msimamo wa BAVICHA kuhusu sakata la Shibuda?
Kutoa kauli tu kuwa BAVICHA haihusiki hakujajibu maswali na ni uchanga wa kisiasa usiohitaji ulezi bali kuondolewa

Naungana na MM kuwa Huyu Naibu BAVICHA(Dada) achukuliwe hatua

1. Kama alivyonena MM, aombe radhi kwa kumdhalilisha Mwenyekiti ambaye kiutaratibu ni mkuu wake wa kazi mbele ya vyombo vya habari na umma kwa ujumla

2. Aeleze wapi alipata mwongozo wa kukanusha kauli za BAVICHA na BAVICHA ipi ilimpa ridhaa ya kukanusha.

3. Alazimishwe kuachia ngazi kwasababu zifuatazo:
i] Hajui taratibu za uongozi
ii) Amekiingiza chama katika mtafaruku usio wa lazima na kuondoa mwelekeo wa kampeni zinazoendelea
iii] Anatumiwa na kundi lisilojulikana ndani ya chama kama hakupewa ridhaa na BAVICHA au uongozi
iv] Kushindwa kutetea masilahi ya chama na kuonyesha uoga kwa Shibuda bila sababu za msingi
 
Mkuu MM, umenikumbusha kitu zaidi. Huyu Dada amesema maneno ya Heche si ya BAVICHA kwasababu hakuna kikao kilichofanyika kutoa kauli hizo. Sijui kama kuna kikao cha BAVICHA kilichokaa ili kutoa kauli ya kuji-dissociate na kauli za Heche kama alivyokanusha Dada yetu. Ndiyo maana nakaandika kuwa huenda ametumwa na sehemu ya uongozi au kundi ndani ya CDM. Je, kama kilikuwepo kikao, ni nani alikuwa mwenyekiti hadi Naibu wa mwenyekiti atoke na kauli ya kumdhalilisha mwenyekiti?

Ukitazama kauli ya Heche kama mwenyekiti haikuwa na maudhui au muundo wa kashfa. Alichokifanya Heche kisiasa kinakubalika'rebut' baada ya chama kudhalilishwa siyo kwa hoja ya kugombea bali hoja za udhaifu wa upinzani Shibuda akiwa mpinzani. Hata bila kauli ya Heche bado wanachama, manazi na mashabiki wa CDM walikereka.

Kauli ya Heche ilipaswa kutetewa kama ulivyonena kwa vile ni kauli ya mwenyekiti iliyolenga kulinda masilahi ya chama isiyo na matusi,kashfa bali majibu. Nimeandika (Duru za siasa) kuwa vyama lazima viwe na 'pundits' kutetea chama katika nyakati kama hizi na athari zake ndizo hizi. Mwenyekiti anaachwa nyikani mwenyewe

Ukisoma bandiko langu la mwisho katika safu ya (Duru za siasa) mara tu baada ya kauli ya Shibuda kumjibu Heche, niliweka wazi kabisa kuwa silaha anayotaka kuitumia Shibuda ni kumwandama Mwenyekiti Heche ili ugomvi uonekane ni kati yake na Heche na siyo CDM kwa minajili ya kujilinda na matokeo anayojua yatamsibu

Nilitahadharisha CDM juu ya hilo kwa bahati mbaya ushauri ukapuuziwa. Leo Shibuda ameibuka Kanda ya ziwa akiwa hana madai ya usukuma wake na kujikosha kuwa hana ugomvi na Chadema bali Heche. Hii imeshadidiwa na kauli ya Naibu BAVICHA mwanadada aliyekitenga chama na kumwacha Heche nyikani kana kwamba alikuwa anatetea familia binafsi.
Chadema wameingia katika mtego wa Shibuda hata pale tulipowapa majibu ya mtihani.

Lakini pia tujiulize kama huyu dada amedai kuwa kauli zile za Heche si za CDM, je ni kauli gani anazodhani Heche amevuka mipaka na nini msimamo wa BAVICHA kuhusu sakata la Shibuda?
Kutoa kauli tu kuwa BAVICHA haihusiki hakujajibu maswali na ni uchanga wa kisiasa usiohitaji ulezi bali kuondolewa

Naungana na MM kuwa Huyu Naibu BAVICHA(Dada) achukuliwe hatua

1. Kama alivyonena MM, aombe radhi kwa kumdhalilisha Mwenyekiti ambaye kiutaratibu ni mkuu wake wa kazi mbele ya vyombo vya habari na umma kwa ujumla

2. Aeleze wapi alipata mwongozo wa kukanusha kauli za BAVICHA na BAVICHA ipi ilimpa ridhaa ya kukanusha.

3. Alazimishwe kuachia ngazi kwasababu zifuatazo:
i] Hajui taratibu za uongozi
ii) Amekiingiza chama katika mtafaruku usio wa lazima na kuondoa mwelekeo wa kampeni zinazoendelea
iii] Anatumiwa na kundi lisilojulikana ndani ya chama kama hakupewa ridhaa na BAVICHA au uongozi
iv] Kushindwa kutetea masilahi ya chama na kuonyesha uoga kwa Shibuda bila sababu za msingi

Kosa ni kosa tu, ila kurudia kosa ni udhaifu usiokubalika na huhatarisha. Tukumbuke kwamba vijana bado wadogo na upeo wao katika masuala ya kijamii bado ni mdogo, ndio maana wanaandaliwa wakomae kwa siku za usoni kuwa watendaji wazuri.

Nisingependezwa sana na ibuko la hoja ya kumfukuza Makamu mwenyekiti, kwani kufukuzana si dawa ya kujenga chama, bali kudhoofisha chama. Jambo muhimu ni kumweka kitako Makamu mwenyekiti ajue kosa alilofanya ili asirudie kosa kama hilo tena. Asiposikia na kufuata ushauri hapo hakuna namna nyingine zaidi ya termination from her post. Afundwe namna bora ya utendaji katika ofisi yao kuwa ni mawasiliano, na katu asiwe tayari kutumiwa na wengine kutoa matamko. Tuelewe tamko lile si lake binafsi kuna walio nyuma ya pazia. Akifukuzwa huyu dada atakuwa ameonewa tu kwa vile ametumiwa kama chambo tu. Kuna waliojificha nyuma yake ambao hawataki wajulikane kwamba wako kinyume cha mwenyekiti. Hayo ni makovu ya uchaguzi uliopita ukiangalia kwa jicho la upembuzi.

Angefukuzwa Shibuda tangu alipoanza mizengwe yake huenda kungekuwa na athari zaidi kuliko alivyoachwa. Ndio maana dhana ya ignore imemweka Shibuda katika kapu kisiasa badala ya kuwa jukwaani kama wengine wanavyozidi kuchanja mbuga katika kutangaza magwanda yao. Aanachofanya sasa ni kujikomba upande wa CCM kwa vile ameshapoteza mwelekeo upande wa chama chake alivyotarajia.

Kwa vyo vyote vijana hawa wanahitaji kijana mwenzao kama Zitto au Mnyika kuwasaidia kukaa sawa ofisini mwao, la sivyo matamko yanayokinzana yanatoa mwanya wa kuweka nyufa za kupitisha mende kisha siafu watafuta harufu ya mende na hakutakalika huko ndani.
 
0000001anajulia.jpg
275738_100002659456794_1144001_n.jpg

Matamko ya mmoja mmoja hata kama anakinga ya kikatiba hayakubaliki kwa ajili ya kulinda mshikamano na umoja katika utawala wa kisheria. Ni dalili ya kuwepo ufa katika mfumo wa uongozi na nihatari kutohimili vishindo vya tetemeko la ardhi litokeapo nyumba yenye ufa.

Narudia kauli ambayo nilishawahi kumwambia Katibu Mkuu Dr. Slaa ambaye kwa sasa amefanikiwa kurekebisha kutoka safu ya juu Chadema, lakini tatizo ni kwa Ngazi ya juu Umoja wa Vijana Chadema.

Lazima kuondokana na mlipuko wa kujibu kwenye vyombo vya habari ghafla bila upembuzi wa kutosha, bila kutuliza kwanza nerves, bila kikao cha kushauriana nini cha kujibu na papo kuangalia upande wa pili wa sarafu athari zake kwa tamko litakalotolewa.

Busara inavyoonekana katika uongozi wa juu kwenye Uongozi wa Chadema naheshimu na ndicho kinachotakiwa, ila ipo kazi kuwaweka sawa viongozi wa BAVICHA.
[/QUO

Nakuunga mkono mkuu lakini hata kama viongozi hawa walikosea hasa kwa Heche kutoa tamko pasipo mashauriano ya pamoja na viongozi wenzake bado makamu mwenyekiti wa BAVICHA hakupaswa kukurupuka na kuja kwenye media kumsuta Mwenyekiti wake. Busara ilikuwa yeye kukaa kimya na kusubiri kikao maalum. Kwa ujumla makamu mwenyekiti alikosa busara na hakuzingatia itifaki ya kiuongozi hata kidogo. Wanahitaji kufundwa hawa.
 
Back
Top Bottom