Elections 2010 Viongozi CCM Bado wanaishi karne ya 18?

mozze

Senior Member
Aug 27, 2010
185
28
Nadhani CCM wakiongozwa na Kikwete akili zao zimezimia.
Wewe mtu unawezaje kulazimisha kuwa umetimiza ahadi zako? Kama umejenga barabara si watu wataona, kuna haja gani ya kila siku kesema tumefanya hili au lile?
Miaka ya 70 ndio CCM waliweza kuja na kupiga porojo tu bila wananchi kuhoji, lakini ijapokuwa mfumo ya maisha umebadilika Viongozi na wana CCM wameshindwa kabisa kubadilika na ndio mana wanaonekana kutapatapa bila mafanikio mana ndio wamefikia mwisho wa kufikiria.
Wana CCM wanaishia kufikiria kuwa 1995 = 2010, yani hawawezi kabisa kufikiria. 1995 wanajua watu wangapi walikuwa na access ya radio ambazo ni free from mkono wa government, mawasiliano ya simu, internet, mobility of people etc? Haya mambo wangeweza kuyajua bila shaka wasingeingia kichwakichwa kama sasa bila sera wala utaratibu.
TUNAHITAJI MABADILIKO, NI dhahiri Hawa si watu wa kuitoa Nchi kwenye Umasikini.
Embu fikiria Waziri anasema nchi haiwezi kufanya kitu kwenye kodi kwa sababu ya EAC, huyu kweli ni mzima kiakili? Lets join hands for Changes!
 
Yaani hawa jamaa mpaka wanachosha, ndiyo maana wasaidizi wa JK wanakuja na hii mpya ya kutisha magazeti huru!
 
Nadhani CCM wakiongozwa na Kikwete akili zao zimezimia.
Wewe mtu unawezaje kulazimisha kuwa umetimiza ahadi zako? Kama umejenga barabara si watu wataona, kuna haja gani ya kila siku kesema tumefanya hili au lile?
Miaka ya 70 ndio CCM waliweza kuja na kupiga porojo tu bila wananchi kuhoji, lakini ijapokuwa mfumo ya maisha umebadilika Viongozi na wana CCM wameshindwa kabisa kubadilika na ndio mana wanaonekana kutapatapa bila mafanikio mana ndio wamefikia mwisho wa kufikiria.
Wana CCM wanaishia kufikiria kuwa 1995 = 2010, yani hawawezi kabisa kufikiria. 1995 wanajua watu wangapi walikuwa na access ya radio ambazo ni free from mkono wa government, mawasiliano ya simu, internet, mobility of people etc? Haya mambo wangeweza kuyajua bila shaka wasingeingia kichwakichwa kama sasa bila sera wala utaratibu.
TUNAHITAJI MABADILIKO, NI dhahiri Hawa si watu wa kuitoa Nchi kwenye Umasikini.
Embu fikiria Waziri anasema nchi haiwezi kufanya kitu kwenye kodi kwa sababu ya EAC, huyu kweli ni mzima kiakili? Lets join hands for Changes!
hili hata mimi imenishangaza kuwa hatuwezi fanya lolote kwnye kodi bcs of EAC sasa si bora uvunjike tuu kwa manufaa ya wananchi!
 
Nimeshindwa kuelewa kabisa jinsi gani hawa jamaa wamekosa utashi na wanafanya mambo ya kipuuzi kama vile bado wanaishai 1970s. Inauma zaidi pale wanapowafanya watanzania wajinga, kuwa ni watu wasiojua ukweli na wasioweza kupambanua mambo. wanapowabeza wapinzani mimi hata siwaelewi wao wananongelea mazuri yapi waliyofanya, most ya hawa viongozi wapo kwenye huwa mfumo kwa zaidi ya 40years now na wameshindwa kubadilika.
Kibaya zaidi ni kuona CCM wote wanakubali kukaa kimya, na kusikiliza amri za watu wasiozidi watano, yani wanachama wao hawawezi hata kuhoji na kutoa Changamoto.....I wish wangetokea kama watu wengine hata wawili tu kama Sabondo.

NCHI INAHITAJI UKOMBOZI TOKA KWA HAWA WAKOLONI WEUSI! Tuzidi kuhamasisha watu kwa mageuzi hapo tarehe 31 Oct
 
Back
Top Bottom