Vioja vya JK: Atunukiwa tuzo ya kimataifa ya Kilimo

Status
Not open for further replies.
Ikulu, Ikulu, Ikulu, hamna sabuni ya kumsafisha huyo jamaa! Fanyeni mfanyalo, mmeishiw na ya kufanya na sasa mmeamua kununua sabuni ya kumuoshea huyo jamaa! Hatari sana! Hasafishiki, nchi inanuka mauaji hata akitabasamu sioni uhalali wa tabasamu lake kwani ameua watu kama Hitler ili abaki madarakani na mifumo yake
 
Sitakuwa na muda wa kukueleza kila kitu hapa. Ila waweza kufunguka macho kwa kusikiliza mara kwa mara RTD na kuangalia TBC1. Kuna vipindi vizuri sana vya mafanikio yetu kwenye kila nyanja ikiwa ni pamoja na kilimo. Utashangaa kwamba tumepiga hatua sana na dunia inasifia maendeleo yetu hususan kwenye kubadilisha kilimo.

Kumbe maendeleo ya kilimo yanasikilizwa redioni na kwenye tv?!
Asante mkuu. Nimeelewa sasa.
 
Ha ha ha ha ha ha ha...kweli JK mpaka amalize ungwe yake atakuwa amejaza vyeti na tuzo nyingi sana ila asilimia 99 ni feki na vioja.
 
Hongera Kikwete kwa kupata hiyo tuzo....sera ya kilimo kwanza ni nzuri sio mbaya na kwa kweli kwa kiasi fulani imeanza kurudisha matumaini ya wakulima. Ingawa ina changamoto zake lakini kama ikitiliwa mkazo uenda ikasaidia mbeleni.
 
Hiki kitaasisis kimeibukia wapi na kina authenticity gani ya kuwapa viongozi wa Afrika tuzo?

Au mradi ni kitaasisi kinataka kumvika kilemba cha ukoka mkuu kinaruhusiwa tu? Kesho kikikutwa na scandal, mkuu anakuwa implicated?

Kimetokea wapi hiki kitaasisi? Nimesoma tamko la Ikulu hawajaeleza hili.
 
Ya ukimya kwenye mambo yanayomhusu na kushindwa kuiongoza serikali yake atatunukiwa lini?
 
Huyo jamaa mtoa tuzo ametoka wapi? Naona alianza na Inkosikati Ntombi kisha akaenda kwa viongozi wa Afrika kusini mwa jangwa la sahara. Asije akawa anainyemelea ardhi au asije akawa ndiyee muuza matrekta yale ya Kihindi.

Hata mimi nina wasiwasi naye. Wahindi kwa rushwa ndiyo umefika
 
Ukiwa kilaza ua rahisi kuchezewa jua utachezewa na kila tapeli.Hili ndilo tatizo tulilo nalo hapa Afrika. Watawala wetu wanapenda sana madaraka na sifa kiasi cha kujikuta wakinaswa na kila aina ya tapeli. Huyu mhindi si angepeleka tuzo yake kwao India kama siyo kutafuta kuwa karibu na Kikwete ili amtumie vibaya?
 
Sera bora za kilimo, halafu utekelezaji zero unapewa zawadi??Kazi ipo
 
hakuna kitu... Raisi wetu amekua jalala la tuzo zisizo na uhalisia...
 
Anastahili kabisa, kwani pale white H anabustani kibao za maua. Kalima kwelikweli
 
Ukiwa kilaza ua rahisi kuchezewa jua utachezewa na kila tapeli.Hili ndilo tatizo tulilo nalo hapa Afrika. Watawala wetu wanapenda sana madaraka na sifa kiasi cha kujikuta wakinaswa na kila aina ya tapeli. Huyu mhindi si angepeleka tuzo yake kwao India kama siyo kutafuta kuwa karibu na Kikwete ili amtumie vibaya?

well said
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom