Vioja Katika Daladala!

Bazazi

JF-Expert Member
Aug 18, 2008
2,806
3,476
Kwa wale wenye magari na kwa kawaida hampandi Daladala;
Hivi ndivyo viroja tunavyopata kwenye Daladala wenzenu tusio na magari




Mlokole: "Nyimbo gani mnapiga?!? Wekeni nyimbo za Yesu.."
Konda: "Vipi wewe, Yesubado hajatoa album..."
********************************
Abiria: "Kuna Kiti auunasema panda tu!?"
Konda: "hao wengine wamekalia ndoo?! "
*******************************
Abiria: "Embu punguzenisauti ya redio..."
Konda: "Sheria za nchi tu zinatushinda, tusikilize na zako!? hebu tupunguzie misheria"
*******************************

Mmama: "Bwana ondoa gari joto sana!!"
Konda: "Usituzingue wewe, shuka upande fridge...."
******************************
Konda: "Anti, kuna siti pale nyuma,ingia...."
Anti: "Siwezi kaa siti za nyuma..."
Konda: "Kwenda zako wewe, Kwani za nyuma ziko nje ya gari?!"
********************************
Sister duu: "Konda unanibana bwana..."
Konda: "mbona nguo ulizovaa huzisemi, kama ulitaka kujiachia ungekodi treni pekeyako!!!"
*******************************
Sharobaro: "Kuna kiti?! Kama hamna sipandi..."
Konda: "Kama unaogopa kukosa kiti si ungebeba chako!!?"
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom